Kesi ya Mbowe: Kibatala na Mallya wameiondolea Mahakama uwezo wa kumfunga Mbowe hata ikishinikizwa

Kesi ya Mbowe: Kibatala na Mallya wameiondolea Mahakama uwezo wa kumfunga Mbowe hata ikishinikizwa

Kisanduku

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2009
Posts
284
Reaction score
483
Jana tumesikia polisi akitoa ushahidi wake kwenye kesi ya Mbowe. Tumesikia na siyo mara ya kwanza wakijitetea kwamba maelezo waliyoandika wamejisahau wakakosea yaani "typographical error".

Je, sheria na mahakama zinasema kuhusu hiki kinachoitwa "typographical error"?

Ukweli ni kwamba mtu unaweza kukosea kuandika kitu tofauti na ulivyotarajia. Ila wakati wa kusahihisha "typographical error"? jaji hajaanza kusikiliza kesi.

Bahati nzuri kesi hii imeenda hivyo upande wa akina Mbowe. Kama mnakumbuka wiki mbili zilizopita akina Kibatala, Mallya na wenzao waliomba kuwe na kesi ndogo yaani "trial within trial".

Msingi wa kesi ile ndogo ilikuwa maandishi au maelezo ya mtuhumiwa mmoja yasipokelewe kama ushahidi. Sasa hivi kidogokidogo tutaanza kuona akina Kibatala, Mallya walitumia akili ya ziada ambayo wote hatukuiona.

Pamoja na polisi kuendeshwa sana kwenye ile kesi ndogo hadi nchi nzima tukajua PGO polisi hawajui PGO bado ilikuwa ni vigumu kina Kibatala kushinda. Naamini hata akina Kibatala walijua wasingeshinda lakini kuna kitu walikuwa wanakiweka

Kwa nini hawakushinda na walijua hawatashinda? Hoja pale si polisi kuijua au kutoijuaPGO . Hoja kubwa pale ilikuwa kwamba kama mtuhumiwa aliandika maelezo kwa hiari yake au aliteswa ndipo akalazimishwa kuyaandika baada ya mateso.

Maadam mtuhumiwa alikiri kwamba ameandika lakini kwa mateso jaji hakuwa na namna ila kuitupilia mbali kesi ile. Ni vigumu kwa jaji au mtu yeyote kuthibitisha kwamba mtuhumiwa aliteswa ndipo akaandika maelezo.

Hapa msingi ni uleule kwamba huwezi kuandika maelezo halafu mbele ya jaji uyaruke kwa kisingizo cha "typographical error" au cha kuteswa kabla ya kuyaandika.

Hivyo, polisi, serikali na mahakama hawakujua wanachokitaka akina Kibatala na kimsingi walitaka ile hukumu ije vilevile kama ilivyokuja, yaani washindwe. Na akina Kibatalla walishindwa kama walivyotaka.

Sasa kushindwa kwa akina Kibatala kuna msaada gani kwako?

Ukiangalia kesi inavyokwenda sasa ndiyo utajua kwa nini walitaka washindwe kesi.

Hebu angalia wanachokifanya sasa hivi. Huwasikii tena wakiuliza maswali ya PGO. Wanajikita sana kushambulia ushahidi wa polisi unaoletwa mahakamani.

Wanasoma maelezo ya shahidi wa serikali aliyoyaandika kisha wanalinganisha na anachosema mahakamani. Kwa kufanya hivyo wamefaulu kukuta ujinga mwingi kwenye ushahidi wa polisi na mashahidi wote wanaoletwa na serikali

Mwisho wa siku ni kwamba kila polisi (shahidi) mmesikia akisema "hapo nilikosea kiandika" au wakisema hilo kosa ni "typographical error" kama alivyosema wa jana.

Hii maana yake akina Kibatala, Mallya na wenzao wameshafaulu kuiweka mahakamani katika kitanzi. Maana yake ushahidi wote wa maandishi jaji sasa hana mamalaka ya kuukataa. Hana mamlaka ya kuona kwamba hiyo ni "typographical error".

Mahakama hiyohiyo ilikataa mtuhumiwa kubadili ushahidi wake kwa kisingizo cha kuteswa hivyo ushahidi huo utaingia mahakamani.

Sasa polisi nao ushahidi wao hautaruhusiwa kubadilishwa. Alichoandika mtuhumiwa kitahesabika kama ushahidi na alichoandika polisi kitatumika kwenye hukumu. Hapa akina Kibatala wamecheza kama Pele na ilikuwa vigumu kugundua.

Kimsingi kama mahakama ilinuia kumfunga Mbowe kwa mbinu hii ya kina Kibatala imewashinda na inawezekana serikali inaweza isilete mshahidi wengi kama tulivyodhani

Vilevile mojawapo ya kesi muhimu kwa kesi hii ni ile ya Mahakama ya Rufani ya "Harish Ambaram Jina (By His Attorney Ajar Patel) v. Abdulrazak Jussa Suleiman".

Katika kesi hii mahakama iligundua tatizo kwenye malezo ya Patel yeye akajitetea kwamba alikosea kuandika yaani "typographical error".

Mahakama ya Rufani ikakataa utetezi huo ikamwambia "kama ulikosea kuandika "typographical error" basi ulitakiwa kurekebisha kabla ya siku ya kusikilizwa kesi". Kipindi cha jaji kusikiliza kesi siyo cha kurekebisha document.

Hivyo, akina KIbatala, Mallya naamini kesi hii wanaijua lakini kama hawaikumbuki basi iko kwenye ukurasa wa 134 wa ripoti za kesi Tanzania za mwaka 2004 yaani [2004] T.L.R. 134.

Wasalaam
 
Wakati mwingine nikisikia watu wasio wanasheria wanavyojadili mambo ya kisheria huwa nawaonea huruma sana kwasababu it will take them 100 years to know the truth. hapo hakuna wanasheria, tafuteni wengine, fuateni ushauri huu mtakuja kunishukuru.

Hao sio criminal lawyers, kuna mawakili wa jinai wazuri na wanajua techniques kuliko hao, wao faida yao ni kwamba wanajipublicise na kupata wateja na kujulikana zaidi nchini ila sio kuwasaidia kwenye hiyo kesi.
 
Wenye nchi yao wanaiita Serikali sikivu ya CCM, ila inavuliwa dera kwa sababu ya kutosikia.
Screenshot_20211028-105801.jpg
Screenshot_20211029-151136.jpg

Namkumbusha tu IGP Sirro ajiandae na yeye kusimama kizimbani kwaajili ya kutoa ushahidi wake dhidi ya alichoongea kwenye Press.
 
Serikali sikivu ya CCM inavuliwa dera kwa sababu ya kutosikia.View attachment 1992680View attachment 1992681
Hayo hapo juu yanaathiri nini ushahidi wa prosecution hasa ikizingatiwa shahidi hajui kiingereza, ameulizwa kwa kiswahili, maelezo yaliandikwa kwa kiswahili, na wapo mashahidi wengine wanatarajiwa kuitwa pengine kana kwamba ushahidi wa mtu mmoja tu huyo hata ukiwekwa pembeni utaangaliwa ushahidi wa wengine?

Kujua kiswahili cha terrorist/terrorism au kutojua kunafifisha charge aliyosomewa? wakati pengine ameshaeleza maelezo ya nini maana ya ugaidi?.....je? wamejua nini lengo la prosecution kumwita shahidi huyo?

Kwamba walimwita kuja kuthibitisha nini among others kwasababu kuna wakati prosecution wanaweza kuita shahidi kuja kuthibitisha kitu kimoja tu miongoni mwa vingi na vingine vitathibitishwa na mashahidi wengine na akishathibitisha kile wanachokitaka tu wanakuacha tu wewe uulize maana za terrorism na matakataka yako yoote na kesi yao inabaki imesimama.

Ndio maigizo wanayoyafanya hao mawakili wenu. kwa bahati nzuri nilishawahi kuwa prosecutor na ninawaonea huruma chadema kwasababu kwa wanachokifanya mawakili wenu mtakuja kulia.
 
Hakuna kitu kibaya Kama kuwaamini watumishi wa chini yako halafu wao wakakudanganya!!
Najisikia vibaya Sana kwa Rais wetu kudanganywa na wasaidizi/washauri wake
Amedanganywa nini mzee? kwamba wewe unajua mambo yote yanayotendeka hapa nchini? una tiss? una polisi? una vyombo vya uchunguzi?

Utasemaje waongo wakati wewe mwenyewe hapo ulipo upo kiganjani mwa vyombo hivyo vinavyojua unaishije na unatakiwa kuishije kila siku? usilolijua ni kama usiku wa giza.
 
Subiri umbuko.

wakati mwingine nikisikia watu wasio wanasheria wanavyojadili mambo ya kisheria huwa nawaonea huruma sana kwasababu it will take them 100 years to know the truth. hapo hakuna wanasheria, tafuteni wengine, fuateni ushauri huu mtakuja kunishukuru. hao sio criminal lawyers, kuna mawakili wa jinai wazuri na wanajua techniques kuliko hao, wao faida yao ni kwamba wanajipublicise na kupata wateja na kujulikana zaidi nchini ila sio kuwasaidia kwenye hiyo kesi.
 
hayo hapo juu yanaathiri nini ushahidi wa prosecution hasa ikizingatiwa shahidi hajui kiingereza, ameulizwa kwa kiswahili, maelezo yaliandikwa kwa kiswahili, na wapo mashahidi wengine wanatarajiwa kuitwa pengine kana ninawaonea huruma chadema kwasababu kwa wanachokifanya mawakili wenu mtakuja kulia.
Prosecutor kama prosecutor
 
Kwa hiyo shahidi alikuja kutoa ushahidi wa Utalii?? mahakamani sio chumbani kwa demu wako. Chochote unachoongea kina matter
wakati mwingine nikisikia watu wasio wanasheria wanavyojadili mambo ya kisheria huwa nawaonea huruma sana kwasababu it will take them 100 years to know the truth. hapo hakuna wanasheria, tafuteni wengine, fuateni ushauri huu mtakuja kunishukuru. hao sio criminal lawyers, kuna mawakili wa jinai wazuri na wanajua techniques kuliko hao, wao faida yao ni kwamba wanajipublicise na kupata wateja na kujulikana zaidi nchini ila sio kuwasaidia kwenye hiyo kesi.
 
wakati mwingine nikisikia watu wasio wanasheria wanavyojadili mambo ya kisheria huwa nawaonea huruma sana kwasababu it will take them 100 years to know the truth. hapo hakuna wanasheria, tafuteni wengine, fuateni ushauri huu mtakuja kunishukuru. hao sio criminal lawyers, kuna mawakili wa jinai wazuri na wanajua techniques kuliko hao, wao faida yao ni kwamba wanajipublicise na kupata wateja na kujulikana zaidi nchini ila sio kuwasaidia kwenye hiyo kesi.
Wataje basi mkuu tuwajue hao mawakili wa jinai wazuri wanaojua techniques kuliko hao.
 
Mkuu Mbowe na wenzie hawana hatia lakini mahakama zetu ziko chini Majaji na Mahakimu MAZUZU walioamua kuigeuza mahakama kuwa kitengo cha maccm kinachoendeleza dhuluma na udhalimu dhidi ya raia, vyama vya siasa na vyombo vya habari.

Kwa hiyo shahidi alikuja kutoa ushahidi wa Utalii?? mahakamani sio chumbani kwa demu wako. Chochote unachoongea kina matter
 
hayo hapo juu yanaathiri nini ushahidi wa prosecution hasa ikizingatiwa shahidi hajui kiingereza, ameulizwa kwa kiswahili, maelezo yaliandikwa kwa kiswahili....
Ndugu unazunguka zunguka kote huko kwanini? HAPO HAKUNA KESI, kilichopo mahakamani ni mgogoro wa kisiasa kati ya Freeman Mbowe/CHADEMA na serikali/CCM.

Ni CCM wamegaragazwa kwa hoja ktk uwanja wa siasa, na kwa kuwa wana dola, basi wameamua kuitumia kunyanyasa na kuonea wapinzani wao. Lakini kumbuka hili, kwamba, the LINE HAS BEEN DRAWN because THAT CAN'T WORK ANYMORE.

KUMBUKA HILI; Hakuna shahidi mwingine yeyote wa JAMHURI anayeweza kuja ku - repair uharibifu wa ushahidi wao wa uongo uliokwisha kufanywa na mashahidi wao hususani Kingai na wale wajinga na waongo wengine wawili.

Yaani yule wa Longido, Kaaya a.k.a Power Tiller na Koplo Hafidhi wa Forensic Police Investigation Department aliyetoa tafsiri ya "terrorism" kuwa hayo ni "mambo ya utalii."

Kama mpaka hapo hujatambua tu kuwa hawa watu waleta mashitaka haya ni waongo na ni wanabambikia kesi watu, basi wewe utakuwa mjinga wa mwisho katika dunia hii.
 
Back
Top Bottom