aliye - engineer haya yote ni Mzee wa kutoboa watu misumari chini na ulinzi wa mwendazake. hii nchi kuna watu wameumizwa saaaana.nimewahi kusema humu only in Tanzania unaona Komandoo anafukuzwa kazi tena mtu anauzoefu mkubwa wa vita ,then anajitafutia ajira binafsi anakamatwa na kuteswa na polisi.ukiangalia kilichomfukuzisha kazi ni mausuala ya kisaikolojia kutokana na kazi yake .
Siro asipokuwa makini ataastafu vibaya sana... hili ni shimo limewekewa nyasi juu awe makini anaweza asitoboe.Siro an aushaushshidi. Mbowe sio malaika. As per Siro
Hili ni jambo baya mno !Mtoa mada hivi una taarifa ndugu yako akikamatwa anaweza asipatikane kituo chochote kwa kuwa polisi wanawapa watuhumiwa majina bandia..
Kazi ipo
You are very right...Polisi wanaposhughulika na muhalifu hawaangalii wewe ni nani bali wanafuata sheria inavyoelekeza.
RIP Ole Nasha
nimejifikirisha sana humu ,ndiomaana gazeti moja limeripoti leo waliofaulu vizuri wakataliwa ajira polisialiye - engineer haya yote ni Mzee wa kutoboa watu misumari chini na ulinzi wa mwendazake. hii nchi kuna watu wameumizwa saaaana.
Kama ndipo ilipofikia na hatujui yajayo, itoshe kusema umetoa ushauri/maoni mazuri yanayohitaji kufanyiwa kazi na wahusika iwapo kama ni kesi isiyokuwa na mashiko na labda haikustahili kuwepo.Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mkubwa mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu. Nafuatilia kwa kwenda mwenyewe Mahakamani. Hata sasa nipo Viunga vya Law School of Tanzania ilipo Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuhudhuria kesi ya akina Mbowe. Sitaki kupitwa wala kusimuliwa. Najionea na kusikia mwenyewe moja kwa moja.
Yanayozungumzwa Mahakamani hapa yanashtua, yanaogofya na kuanika hata visivyofaa kuanikwa. Wengi wanaofuatilia wanajua kuwa kesi hiyo sasa imezaa kesi ndogo. Kesi ndogo ni imezaliwa baada ya Maelezo ya Mshtakiwa wa pili (Adamoo) kupingwa na upande wa Utetezi Mahakamani hapa. Ndipo Jaji Siyani anayeisikiliza kesi kuu alipotoa amri ya kuendeshwa kesi ndogo ndani ya kesi kuu kuhusu pingamizi hilo.
Mwisho wa kesi ndogo inayoendelea kutolewa ushahidi sasa ni kukubaliwa au kukataliwa kupokelewa kwa maelezo ya Adamoo yanayodaiwa aliyatoa huko Polisi alipokamatwa na kuhojiwa/kuchukuliwa maelezo. Yeye mwenyewe Adamoo kwenye ushahidi wake ameyakana Maelezo hayo akisema aliletewa yakiwa yameshaandikwa na kusainishwa chini ya vitisho vikubwa vya polisi (ACP Kingai). Jana shahidi wa pili (Bwana Ling'wenya) alianza kutoa ushahidi wake na anaendelea leo hii.
Kuna mambo yameshasemwa hapa Mahakamani na mashahidi wa Utetezi yanaogofya sana. Kwanza, kuna idadi kubwa ya wanajeshi wamekamatwa na wanateswa kwenye vituo vya polisi. Kuna nini na kumetokea nini jeshini huko hadi kufikia hapo? Pili, aliyetajwa na ACP Kingai kama mtoa taarifa za uhalifu wa Mbowe na wenzake (Luteni Urio) naye alishakamatwa na kuteswa na polisi. Je, aliteswa ili 'amchome' Mbowe na wenzake?
Kuna jambo linaogofya zaidi. Ushahidi wa kwamba wanajeshi wanakamatwa na kuteswa na polisi waweza kupika chuki na hasira kwenye mioyo ya wawili hao na kuzua suitafahamu ambayo itashindikana hata kusemeka huko mbeleni. Yaani, kunaweza kukachemka 'bifu' kati ya wapambanaji hao. Ikifika hapo, hali itakuwa tete. DPP, hujachelewa kuzuia kuvuja zaidi mambo ya ndani kuliko maini ya nchi na kuzuia taharuki isiyo na hata mkuki.
Buriani Ole Nasha!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Kulingana na ushahidi unaoendelea mahakamani ni wazi Moses ameshauwawa.usisahau issue ya Moses Lijenje ndugu zake wamekuja juu wanataka kujua alipo.
sasa si awachukue na hao wengineNi mpango wa Mungu y yaliyo maovu ya sirin yajulikane.Mungu anaipenda sana Tanzania ndo maana alimchukua jiwe wakati sahihi kabisa.
Wandaaji wote wa mpango huu wawajibishwe haraka iwezekanavyo. Tukianza na Kingai pamoja na Mahita. Vinginevyo kesi iendelee wazidi kuanikwa.Kama ndipo ilipofikia na hatujui yajayo, itoshe kusema umetoa ushauri/maoni mazuri yanayohitaji kufanyiwa kazi na wahusika iwapo kama ni kesi isiyokuwa na mashiko na labda haikustahili kuwepo.
Jumanne ni mnoma alishafanya ya kwake kitambo!!Tuliambiwa watuhumiwa waliongozwa ili wasaidie upatikanaji wa Moses Lijenje, kumbe alishatupwa..!!
Jwtz imekuwa ya wachumba?Yaani vijana wa Sirro wanawashughulikia vijana wa Mabeyo?
Maisha yanaenda kwa kasi sana..
Enzi zetu tulishuhudia Polisi wakijishusha mbele ya JWTZ.
Kama haya yametokea kweli, sasa naamini kinachosemwa kwenye kuchelewesha taarifa za msiba wa Meko.... lazima kuna jambo lilikuwa linapangwa
Subiri waaibike kwanzasasa si awachukue na hao wengine