Kesi ya Mbowe: Umuhimu wa Ushahidi wa CPL. Abdallah ni Upi?

Mwalimu Nyerere alitupatia 'mateso' kama vile kocha anavyowafanyisha wachezaji mazoezi magumu. Hakuwa na nia ya kukomoa mtu bali alikuwa na visions zake za miaka 100 mbele wakati waliomzunguka walikuwa na vision za mwezi mmoja mbele. Sio ajabu yeye aliliangalia taifa kwa ukubwa wake lakini huwezi amini waliomfuatia (wengi walimzunguka) mtu mwenye hadhi ya uwaziri unakuta upeo wake si kuangalia hata watu wa mkoa wake bali familia yake na mkewe tu.

Katika maadui alopambana nao mmoja alikuwa ni UJINGA, waliomfuatila walidharau na matokeo yake wajinga wamekuwa wengi na kwa vile mfumo ni wa 'wengi wape' sasa wamejipenyeza hadi kwenye nafasi za maamuzi na kuzaa haya, Dunia inatuangalia na kutucheka
 
aliyeweka sera ya kuajiri polisi walioishia div 4 anatumia nini kufikiri.
Hujui tu, vyeti vilivyokwenye mafaili wanavyojua mabosi wao nitofauti na elimu zao hao form iv kazi zao zinajulikana ila wenye vyeti venye elimu zaidi ndo wanapandishwa daraja tatizo ndo linaanzia hapo.
 
Vuta subira. Umuhimu wake utauona muda utakapofika. Bado mashaidi 20 upande wa serikali. Mambo ya ku connect dots ni wachache tunayoyaweza ila hairuhusiwi kujadili maswala ambayo yako mahakamani.
Usipotoshe, kinachojadiliwa hapa tayari shahidi amekwisha maliza kazi yake hivyo kiko wazi kwa jamii na kinaweza kijadiliwa.
 
Mahakimu na majaji wanatakiwa wawe ni wazoefu wa utani na mizaha, vinginevyo kila mara wangekuwa ni wa kuangua vicheko mahakamani.
... pamoja na kwamba kuna kanuni ya kuzuia kucheka mahakamani ila kuna wakati inafika wote hadi jaji mnacheka hivyo inakuwa ni kosa la population yote hakuna wa kuadhibiwa.
 
Hadi hapa si bunduki wala risasi alizopewa Cpl. Abdallah wala alizowasilishwa mahakamani zinaweza kufungamanishwa na mshitakiwa yeyote pasipo kuwa na kuacha shaka yoyote.
... ni rahisi sana tena sana ushahidi na vielelezo vya Cpl. Abdallah kufungamanishwa na Kingai na timu yake kuliko kuufungamanisha na Mbowe na timu yake.
 
... ni rahisi sana tena sana ushahidi na vielelezo vya Cpl. Abdallah kufungamanishwa na Kingai na timu yake kuliko kuufungamanisha na Mbowe na timu yake.

Hapo ndipo penye maajabu Mussa, Siyani na Kaaya 😁😁.
 
Hiki kikesi ni kumtesa FAM na wenzake pia kuhamisha akili toka mjadala wa katiba mpya na kujadili kesi.
Msidhani hawawatu hawana akili kabisa!!!
Waliobaki wachochee katiba mpya ipatikane au nao wanaogopa kubambikwa 'consiparancy' to commit 'terrolist'
 

Mkuu umeangazia hoja muhimu.

Hapa ndipo Viongozi Madarakani waliopo hasa pale ufipa wanapo tuangusha:

CHADEMA: Bila kuwapa Makavu hakuna Katiba Mpya

Tayari kumekuwa na miito ya kuwahimiza kama vipi watupishe tukamate hatamu za chama na kukimalizia kiporo kilochobadilika.

Adui anajulikana:

Kama CCM siyo adui, mchawi wetu ni nani?

Haya mambo ya kusema wananchi wakinukishe kwanza, wananchi gani bila uongozi?

Cc: mnyika, Lema, Erythrocyte, Salary Slip, BAK, technically na wote wakiwamo pale ufipa
 
Vuta subira. Umuhimu wake utauona muda utakapofika. Bado mashaidi 20 upande wa serikali. Mambo ya ku connect dots ni wachache tunayoyaweza ila hairuhusiwi kujadili maswala ambayo yako mahakamani.
Lakini wakubwa wanaruhusiwa kusema huyu tayari wenzake walishahukumiwa na kufungwa? Ninavyojua mimi jaji amekula kiapo kutenda kwa haki na kwa kuzingatia sheria na ushahidi ulio mbele yake, na kamwe si kwa kusikiliza mijadala ya pembeni... Refarii uwanjani hafanyi maamuzi kwa kusikiliza sauti za mashabiki!!!
 
Hakuna sheria inayozuia kujadiliwa kwa mambo yaliyo mahakamani, ni propoganda ya wanasiasa na wanahabari uchwara tu wanapotaka kukwepa kuzungumzia jambo.
Hiyo sheria ipo mkuu na jana kwenye space kaka yake Lissu aliwakumbusha wachangiaji kwamba sheria inakataza kujadili kesi inayoendelea. Hata hivyo mdogo wake (Lissu) alimpinga vikali sana kwamba hicho kitu, pamoja na kuwepo kisheria watu wapuuze kwa sababu mfumo wetu wa mahakama tayari umekuwa compromised na wa tawala hivyo kuwaachia eti wasubiri mahakama kutenda haki ni muujiza. It was very interesting and hot debate kwa kweli sijui walihitimishaje maana mimi simu ilikata chaji baada ya vijana wa Mhe Makamba (Tanesco) kufanya yao...
 
Pia kwa kuongezea : Moja ilitakiwa huyu mtaalamu wa silaha aionyeshe mahakama kwamba amefanya finger prints hiyo silaha na kuonekana ina match na alama za mshtakiwa. Pili kuonyesha kwamba hiyo bastola kweli mmiliki wake through documents ni huyo mshtakiwa. Sijui ni kwa nini ametumia muda mwingi kuelezea kwamba ameitest bunduki na iko OK. Kingine pamoja na maelezo mengi aliyotoa ameshindwa kuoanisha aina ya hiyo bastola na ile waliyozungumza akina Kingai...
 
Hey Mkuu!; Kwanii .... ee.. "Kiswakingi" ni cha wapi vile?🤣
 
Vuta subira. Umuhimu wake utauona muda utakapofika. Bado mashaidi 20 upande wa serikali. Mambo ya ku connect dots ni wachache tunayoyaweza ila hairuhusiwi kujadili maswala ambayo yako mahakamani.
Hakuna shahidi mwingine wa maana atakayekuja tena kwa upande wa jamhuri....

HEBU CHEKI HII;

1. Yaani "Sterling" wao shahidi No. 1 aliyepaswa kuweka msingi mzuri wa ushahidi wake, Polisi Kingai, kaboronga big time...!

2. Akaja No. 2 polisi mwingine Mahita, aka - cement uharibifu (damage) ya ushahidi wao kaa kiwango cha kufa mtu....!

2. Kaja yule mwingine wa Loliondo, [Kaaya au Power Tiller] yeye ndiye mwongo kabisa wa waziwazi, akaharibu kisawasawa...!

3. Huyu wa Jana akamalizia week end ya Kingai kwa uongo mwingine wa mchana kweupe utadhani wanaomtazama na kumsikiliza ni wajinga kama yeye....!

##Sasa hebu fikiri. Hawa waliobaki 20 watakuja na uongo gani mpya kugeuza ukweli ambao dunia inao uwe UONGO wao....???
 

Hata kama bastola ingekuwa na finger prints za yeyote kusingekuwa na maana yoyote.

Sekeseke la kutokea RAU, Moshi Central, central Dar hadi Mbweni kwa maelezo ya Kingai. Bado tunaongelea fingerprints za nani kwenye hiyo bastola?
 
Hakuna dots hapo.
Dots zipo. Bado hujaambiwa hizo silaha ni nani alikuwa akiwapa hao makomando wa kikosi cha vip protection squard. Nani hasa mmiliki wa hizo silaha za Luger 9mm pistols aliyesajiliwa na kadhalika. Hivyo vuta subira uhondo utajulikana taratibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…