Kesi ya Mbowe: Umuhimu wa Ushahidi wa Kaaya ni upi?

Kesi ya Mbowe: Umuhimu wa Ushahidi wa Kaaya ni upi?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Shahidi #2 wa upande wa mashtaka Justine Kaaya katika ushahidi wake kaeleza ya kwake:

1. Alivyokutana na Mh. Mbowe
2. Alivyompa Mbowe taarifa za washirika wa Sabaya.
3. Alivyosafiri Longido, Arusha, Moshi.
4. Malipo aliyopata kutoka kwa Mh. Mbowe.

Shahidi anathibitisha kuwa, hakuwahi kusikia jinai yoyote ikijadiliwa kwenye mahusiano yake na Mh. Mbowe. Kwamba hakuwahi kuhusishwa katika mpango wala mkutano wowote wa kumdhuru mtu yeyote.

Shahidi anathibitisha kuwa hakuwahi kudhulumiwa au kujisikia kutokutendewa haki popote na Mheshimiwa Mbowe. Kwamba wala hakuwahi kusikia wala kuona Mh. Mbowe akipanga au kumtendea yeyote ndivyo sivyo.

Shahidi anathibitisha kuwa hakuwa na shaka yoyote na Mheshimiwa Mbowe au washirika aliokuwa nao. Ndiyo maana hakuwahi kutoa ripoti au taarifa popote ikiwamo polisi.

Hakuwahi kutoa onyo lolote la tahadhari au vyovyote kwa Sabaya, Jesca au washirika wa Sabaya kwa kuwa hakukuwa na sababu hiyo.

Zaidi sana kwa mukthadha wa kesi hii, Justin Kaaya hakuwahi hata kukutana na Adamoo, Ling'wenya, wala Lijenje kabla ya kukamatwa kwao.

Kwenye mazingira haya Justin Kaaya alikuwa na umuhimu gani kwenye kesi hii?

Au ni mwendelezo ule ule wa kustajaabu vigezo vya hukumu kama zile za mapingamizi?

Kesi ya Mbowe: Ushahidi upande wa Mashtaka unapochukuliwa kuwa ndiyo Dhahiri
 
Umuhimu wake ni kwa sababu ya weledi wa kitanzania.

Wachawi nao wote wametokomea kizani:

IMG_20211016_132442_593.jpg


Utadhani si wao waliokuwa wakishadadia ya Joyce kabla ya kuyasikia ya Mario wa ukweli, msaka fursa 😁😁.

Hiiiiii bagosha!
 
Hii kesi ushahidi wake mwingi ni wa kinadharia zaidi! Haihitaji uwe wakili msomi kugundua ni ya kubambikia! Na mbaya zaidi ubambikiaji wenyewe ni wa kukurupuka.
Upo sahihi. Nafikiri kuna tatizo kwa wale wachoraji wa kesi nzima na maelezo pamoja na ushahidi utakavyokuwa.

Kesi kama hizi wapo watu unawakodi wanakutengenezea kila kitu...mnakaa miezi miwili mna practice mkimaliza mahakamani mtu hachomoki.

Sasa haya mambo ya
Lete hiki..hakipo
Lete hiki ..hakipo.
Tiket ya bus sina...mara tarehe unazotaja muhusika kumbe alikuwa gelezani ha ha ha

Sasa namna hii ni aibu tupu..sema ni woga tu wa Serikali ila ukiwa shahidi kwa namna hii unagoma kwenda mahakamani kuaibika mbele za watu kama power kaaya jana na leo.
 
Ndugu brazaj, kesi hii kuna mambo mawili yako dhahiri shahiri;

1. Kuna uwezekano mkubwa kuwa hukumu ya "kumkomesha Freeman Mbowe" ilishaandaliwa na;

2. Kinachofanyika ni kuitafutia uhalali wa kisheria hukumu hiyo kwa kutumia mchakato wa kimahakama...

##BAHATI MBAYA sana kwa waandaa mkakati huu ni kuwa;

å 100% ya mambo yao yanawaendea kombo kwani kila walifanyalo linaendelea kuthibitisha pasipo shaka yoyote kuwa HII KESI NI YA UONGO WA KUTUNGWA na watu wenye dhamana ya umma wakubwa serikalini. This is truly TOO BAD ...!!

å Kama nilivyosema kuna possibility ya 100% kuwa hukumu dhidi ya Freeman Mbowe imeshaandaliwa, lakini ushahidi wa kisheria kui - support hukumu hiyo mpaka dakika hii umeshagoma beyond curable...!

Hapa ndipo kila Jaji atakayekuja (maana hata huyu atajitoa tu) anapopata taabu...

å Ushahidi wa songombingo hili ni mpishano wa majaji KUTOKA na KUINGIA kusikiliza kesi hii. Ni kwa sababu hawa majaji WANAOGOPA kunajisi professions zao kwa kulazimishwa kuhukumu damu ISIYO NA HATIA inayoweza kugharimu integrity yao na ya vizazi vyao vyote vijavyo..!

Ikienda hivi na huyu Jaji alazimishwe kuhukumu kulingana na matakwa ya MADHABAHU YA IBILISI, nakuhakikishia jambo moja kuwa kabla hajafika huko, huyu naye atatengeneza mazingira ya sababu za KUJITOA...!!

You just wait and see. Hizi ndizo dalili halisi za utawala ULIOFITINIKA WENYEWE..
 
Upo sahihi. Nafikiri kuna tatizo kwa wale wachoraji wa kesi nzima na maelezo pamoja na ushahidi utakavyokuwa.

Kesi kama hizi wapo watu unawakodi wanakutengenezea kila kitu...mnakaa miezi miwili mna practice mkimaliza mahakamani mtu hachomoki...
Labda hao mashahidi wanaofuata watakuwa na ushahidi mzito alio tuahidi Afande IGP! Ila kwa hawa mashahidi wawili; Kingai na huyu Kaaya, kiukweli hakuna kitu!

Yaani shahidi anagongwa nyundo na Mawakili Wasomi wa upande wa utetezi, mpaka wanajikuta kuchanganyikiwa na kufedheheka!
 
Ndugu brazaj, kesi hii kuna mambo mawili yako dhahiri shahiri;

1. Kuna uwezekano mkubwa kuwa hukumu ya "kumkomesha Freeman Mbowe" ilishaandaliwa na;

2. Kinachofanyika ni kuitafutia uhalali wa kisheria hukumu hiyo kwa kutumia mchakato wa kimahakama....
Mdogo mdogo tutafika tu.

Ila ni vyema wajue tunafuatilia kweli kweli. Records walizo nazo tunazo na ziko duniani kote.

Ni vizuri wajue tunapenda haki itendeke na ni vyema tuione haki ikitendeka.

Wala hatuna ugomvi na mtu.

Sidhani kuwa tuna matakwa yasiyoweza kutimilizika.
 
Shahidi anasema mbunge kazi yake ni kutunga sheria na anaweza kushughulika na uhalifu, kumbe kwa mujibu wa shahidi wetu wa jamhuri leo kuna wakati mbunge anaweza kujigeuza polisi, aisee na bado hawa jamaa watashinda kesi!

Tuna taifa limejaa mazombi sana.
 
At the very least, kama ushahidi huo ni wa kweli, unampa picha mbaya tena mbaya sana Mbowe. Kwanini atende hayo yaliyodaiwa? Kwa nia gani nzuri?
 
Back
Top Bottom