“Ninaomba mahakama yako Tukufu, kuruhusu na kuridhia kurushwa kwa matangazo ya moja kwa moja au mubashara (live) ya mwenendo wa shauri hili tangu siku ya kwanza ya shauri hili litakapotajwa na kuanza kusikilizwa,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.
Hata hivyo, anabainisha lengo la kuomba kesi hiyo iendeshwe mubasahara kuwa ni ili kutoa fursa kwa ndugu, marafiki na jamaa zake waishio nje ya nchi washriki kwa nji ya mtandao na vyombo vya habari kushuhudia yanayojiri katika shauri hilo.
Amezitaja baadhi ya nchi hizo waliko ndugu marafiki na jamaa zake hao kuwa ni pamoja na ngu waishio Marekani, Sweden, Lebanon na Afrika Kusini.
MWANANCHI