Khaligraph Jones vs Tanzania rappers, Je Khaligraph atawaweza Wabongo?

Khaligraph Jones vs Tanzania rappers, Je Khaligraph atawaweza Wabongo?

Kaligraph Jones ni Rapper mkali na amefanikiwa kufika mainstream kwa Africa mashariki, ila uwezo wake ukilinganisha na Rappers kama Nikki mbishi, One the incredible na Mex cortez bado ni mdogo, nimechagua hao rappers watatu kutoka TZ kwa sababu ya uwezo wao mkubwa kwenye ku flow vitu vyenye tija ama kushambulia mpinzani kwa ufanisi kupitia lugha ya kiswahili na Kiingereza (Bi Lingual) kitu ambacho kaligraph anajivunia nacho, tofauti ni kwamba hao watatu hawajafanikiwa kwenda mainstream, ila kama anataka battle atagaragazwa vibaya sana na hao ndugu watatu na ndio inawezekana ikawa nafasi ya kuwapeleka mainstream east Africa. BTW Nyashinski akiamua kurudi zama zake za ku Rap anaweza kumkalisha Kaligraph Round ya kwanza na kuiteketeza kabisa career ya Kaligraph.
 
Hii kazi tumuachie P the mc amnyoshe Kama alivyonyishwa mbishi kwenye futi 6 chini

Alafu dizasta aje kumpa darasa la hip-hop, Kama alivyofundishwa rapcha kwenye best friend
Battle rap inahitaji ma mc vichaa wa ku flow na kushambulia, P the mc anaweza akashambulia lakini Flow ya kiswakinge inaweza ikamuangusha.
 
Mawenge alivyotoa Ile diss track iliyojulikana kama futi 6, kwa Niki Mbishi unahisi kwanini hakukuwa na comeback
Yawezekana Niki alipuuzia kwa sababu aliona haina financial impact yoyote, itaishia kwenye kurushiana maneno matupu tu kitu ambacho nikki ameshavuka huko. Ila kumbuka hapa nawalinganisha Nikki, Mex, One VS Kaligraph kwenye uwezo wa ku rap sio uwezo wa ku dis kitu ambacho Kaligraph atazidiwa pia
 
Yawezekana Niki alipuuzia kwa sababu aliona haina financial impact yoyote, itaishia kwenye kurushiana maneno matupu tu kitu ambacho nikki ameshavuka huko. Ila kumbuka hapa nawalinganisha Nikki, Mex, One VS Kaligraph kwenye uwezo wa ku rap sio uwezo wa ku dis kitu ambacho Kaligraph atazidiwa pia
Niki sio msanii wa hivo, rudia kusikiliza futi 6, jamaa alizikwa mzima mzima.
Wasanii bongo wako wengi sana wakali ingawa sio wote wanapenda battle
 
Niki sio msanii wa hivo, rudia kusikiliza futi 6, jamaa alizikwa mzima mzima.
Wasanii bongo wako wengi sana wakali ingawa sio wote wanapenda battle
Futi sita kiasi fulani ni diss track nzuri, ilipata attention kwa sababu kwanza aliye mdiss nikki ni mtu wa karibu i.e wanajuana vizuri pili ni kama P alijitoa muhanga so ikawa na hype watu wakisubiri nini kitajiri, kwa mtizamo wangu ki ukweli haikuwa diss track bora kwa sababu ili address issue ambazo tayari zinajulikana kuhusu nikki, ni sawa na wewe uwe na tabia ya kiburi alafu kwenye ku diss nakuchana Kevin complex unakiburi, ok tunajua Kevin complex anakiburi then what?? Nadhani ndio maana nikki aliamua kuamuambia kuwa ulivyonidiss ni marudio ya vitu ambavyo nimewahi kujidiss mwenyewe kwenye ngoma ya maneno ya mashabiki. BTW namkubali sana P kwenye uandishi wa Usimuliaji, ni jamaa mnoma upande huo.
Unaweza ukawa mkali wa Kuchana sana ila ukashindwa ku battle. Battle rap ni sanaa nyingine
 
Back
Top Bottom