Kiarabu ndio lugha ya asili ya sayansi, tiba, biashara na elimu kwa ujumla

Kiarabu ndio lugha ya asili ya sayansi, tiba, biashara na elimu kwa ujumla

Hakuna anaye ogopa nguruwe, kama majini ni sehem ya uislam hata nguruwe pia angekuwa mdau wa uislam...

Ila dini imetupa vitu vzur na vbaya hata kwa afya imekataza.. Nguruwe sio mzuri kwa afya yako..

yesu wa kizungu alikuwa anafuga majini na kuongea nayo kama kawaida na hata yeye mwenyewe alikuwa sio mdau wa nguruwe ila nyie yesu weusi Ndio mnaishobokea
Hospitali ya wapi? Kupitia hiko kitabu kilifanya uchunguzi
 
Hospitali ya wapi? Kupitia hiko kitabu kilifanya uchunguzi

Kipande cha nyama ya nguruwe kwa siku 'chaweza kusababisha saratani '​


Source Chuo kikuu cha Oxford kupitia BBC news
 
Very myopic Uislamu kwako unaoujua ni wa Tanzania tuu.
Narudia, uislam na elimu wapi na wapi? Hata waislamu wenye itikadi kali lakini wanapenda elimu, huwezi kuwakuta wakienda kusoma nchi za Kiarabu, wote safari ni kwa makafiri. Hilo nalo unataka tubishane? Mwenye amekwenda kusoma uarabuni, akirudi hapa huwezi kumkuta ana practice professional yake, atakwenda kwenye siasa, ushehe au uganga wa kutabiri nyota tu. Nasisitiza, "Uislam na elimu wapi na wapi"?
 
Uongo taslimu. Uislamu na elimu wapi na wapi, miaka na miaka Kigiriki kinajulikana kua ni lugha ya sayansi. Hata Isack Newton pamoja na kwamba alikua Myahudi aliyezaliwa na kukulia hadi kufia Uingereza but zile kanuni zake za motion alilazimika kuziandika kwa Kiyunani/Kigiriki. Uislamu na elimu wapi na wapi kaka? Msukumo wa Waislamu kwenda shule umeanza miaka ya juzi juzi tu, labda watu kama wa Iran hawa wamekua na mwamko wa elimu kabla hata ya Uislamu kuja
Wanavyofanya hivi ni kama kuutangaza uislamu lakini uislamu na elimu mbalimbali.
Waarabu walipokuja Tanganyika walikuwa wanajenga msikiti, kisima cha kujitawazia na madrasa (kusoma kiarabu na elimu ya dini ya kiislamu).
 
Uongo taslimu. Uislamu na elimu wapi na wapi, miaka na miaka Kigiriki kinajulikana kua ni lugha ya sayansi. Hata Isack Newton pamoja na kwamba alikua Myahudi aliyezaliwa na kukulia hadi kufia Uingereza but zile kanuni zake za motion alilazimika kuziandika kwa Kiyunani/Kigiriki. Uislamu na elimu wapi na wapi kaka? Msukumo wa Waislamu kwenda shule umeanza miaka ya juzi juzi tu, labda watu kama wa Iran hawa wamekua na mwamko wa elimu kabla hata ya Uislamu kuja
Papa Sylvester ndio mkristo wa mwanzo wa ngazi za juu kupenda elimu.Alisoma madrasa na kufuzu hesabati ndio akazifundisha kanisani kwake..Hapo ni mwaka 1095 wakati waislamu washajenga vituo vya kuratibu mienendo ya nyota na sayari.
 
Huu ni ukweli ambao wengi hawaujui kwani umejificha ya kuwa lugha ya kiarabu ndio lugha iliyotumika kuufikishia ulimwengu elimu karibu zote.

Lugha ya kiarabu ambayo ndiyo lugha iliyoteremshiwa Qur'an imetoa fursa za wazi kwa walimwengu dunia nzima na kuwapa ujanja wa kuishi na kuifaidi dunia.

Kwa ufupi kabisa ufunguzi wa ulimwengu kielimu ulianzia Baghdad wakati wa utawala wa bani Umayya na baadae utawala wa Abbasiya chini ya utawala wa Haroun Alrashid.

Tawala hizo ndizo zilijenga maktaba kubwa sana iliyoitwa baitul Hikma ambayo ilidumu kwa karne nyingi kabla kubomolewa katika vita kutoka watawala wa kikristo waliopitia bara hindi.

Chanzo cha maktaba hiyo ilikuwa ni wakuu wa koo za kiarabu waliopenda kuhifadhi Qur'an na hadithi za mtume Muhammad saw pamoja na mashairi mazuri ya koo zao.

Mara maktaba hiyo ikaanza kuweka vitabu vyengine vilivyopatikana katika tawala ambako majeshi ya waislamu yalikuwa yakienda wakati wa vita na kutoka misafara ya kawaida ya kibiashara.

Maandishi hayo hayakuwa katika mfumo wa vitabu vya kisasa yalipatikana kutoka tawala za kirumi,kigiriki na kihindi.Maandishi hayo yailetwa hapo na kutafsiriwa kuingizwa lugha ya kiarabu.

Maktaba hiyo kila miaka ilivyoongezeka ikapanuliwa na kuongezwa vitengo vya matawi mbali mbali ya kielimu ukiongezea na kitengo cha uchapishaji.

Hatimae teknolojia ya uchapishaji na uandishi kwa njia nyepesi uliochukuliwa kutoka mbali kama vile China ukaingizwa kwenye maktaba hiyo na kuongeza kasi za uandishi na tafsiri.

Vitengo vilivyonawiri zaidi katika kituo hicho ni vile vya elimu ya tiba,elimu ya anga na hesabati chini ya mwanahesabati Alkhwarizm ambaye ndiye mwandishi wa kitabu cha aljebra alichokiandika katika kutafsrii mahesabu yaliyomo ndani ya Qur'an juu ya mirathi.

Umaarufu wa maktaba hiyo ambao uligeuka kuwa kama chuo cha elimu uliwavuta watu wengi sana kutoka maeneo ya jirani ikiwemo Iran na majimbo ya Urusi kuja kujisomea au kwa kazi maalumu. Kulikuwa na wafanyakazi wa kila fani na kutoka maeneo mbali mbali.Walikuwepo waliokuwa na asili za kiyahudi na makabila mengineyo ya jirani.

Kituo hicho kilipobomolewa na kuchomwa moto,mto wa dijla ambao unajulikana sasa kama euphrates uligeuka rangi kuwa mweusi kutokana na wino wa vitabu hivyo.

Wakatokea baadhi ya wasomi na waliokuwa wafanyakazi wa kituo hicho wakachagua baadhi ya nakala walizoweza kuziokoa na kwenda nazo maeneo yao.Miongoni mwa hao ni Nasrudin Al tulsi wa Azerbajan ambaye alikwishajenga kituo chake cha anga huko kwao.Yeye alifanikiwa kuokoa vitabu zaidi ya 40,000 ambavyo alikuwa akivibeba kidogo kidogo kwa kutumia farasi na ngamia.

Pamoja na kupigwa vita,waislamu nao kwa fitna walikuwa na ugomvi baina yao wenyewe.Wako walionusurika vifo na kuamua kukimbilia maeneo ya mbali ambako tayari athari za tawala za kiislamu zilikwishatangulia.
Maeneo hayo ni kama vile kaskazini ya Afrika,Libya,Tunisia,Aljeria na Morocco mbali na maeneo ya ndani ya kama vile MalimChad na Niger.

Kwa upande wa Ulaya ya sasa waislamu walikwishatangulia Spain zamani. Mmoja ya waliofanikiwa kuhama na kuendeleza mfano wa tawala za Baghdad ni Abulrahmaan ambaye alikwenda kufanya makazi yake Cordoba chini ya himaya ya Ummawiyah. Miji mingi sana ndani ya Spain iliyojulikana wakati huo kama Andalus ilijengwa kwa nidhamu za tawala za kiislamu ambapo lazima kuwe na maktaba.Miji michache kati ya hiyo ni Granada,Sevile na Toledo.

Kwa mfano papa Sylvester (Gerbet) ni miongoni mwa wakristo wa mwanzo kusoma kwenye chuo kikuu cha kiislamu cha Granada na aliwahi kuhudhuria mafunzo chuo kikuu kikongwe zaidi duniani cha Alqarawiney ambacho kiko Fez nchini Morroco ambacho bado kinaendeshwa kwa mfumo ule ule maarufu kama madrasa.

Papa Syvester ambaye alivutiwa sana na utamaduni wa waislamu na elimu zao alipenda sana somo la hisabati na ndiye wa mwanzo kuingiza elimu hiyo nchini Italy wakati wa utawala wake ambapo mwenyewe alikuwa ni mwalimu pia pamoja na kazi za upapa (1095).

Maktaba ya Toledo ndiyo maarufu zaidi kwani hapo ndipo makabila mengi ya Ulaya kuanzia Ureno, Ufaransa,Italy na kote kwengineko walisoma na kutafsiri kazi hizo kutoka lugha ya kiarabu na kuingiza kwenye lugha zao za asili. Katika maktaba hiyo pia walikuwepo wafasiri walioweza kuingiza elimu hizo kwenye lugha ya kiyahudi ya kiebrania.

Ikumbukwe wakati ulimwengu wa kiisalamu ukiwa unairithisha dunia elimu kwa lugha zao kutoka kiarabu lugha maarufu za sasa kama vile kiiengereza na kifaransa hazikuwepo au ndio muda zilikuwa zinazaliwa na kuanza kujulikana.

Vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya kiarabu na kutumika kwenye vyuo vikuu vingi vya ulaya walivyojenga wenyewe ni vingi sana.Ngoja tutaje baadhi tu ya vitabu hivyo.

1. AL HAW. Ni kitabu cha tiba kiliandikwa na Abubakr Al Razi (864 -935)AD.Kinajumuisha vitabu vidogo (volumes) 23.Kilitafsiriwa kuingizwa lugha ya kilatin na myahudi aitwaye Faraj ben Salim kutoka visiwa vya Sicily mnamo mwakka 1276.

2. AL QANON FIY TTIB cha tiba kwa kiiengereza kinajulikana kama The canon of medicines. Kiliandikwa na Ibn Sina (980 -1037)AD.Kitabu hicho kimetumika kama rejea kubwa kwenye vyuo vikuu vya Ulaya mpaka mwaka 1650.Kilikuwa kikitoa ufafanuzi wa tiba na madawa kwa kutumia michoro kufahamisha vizuri.

3. KITAB AL TASIF cha Abul Qassim (936-1013)AD.Ni mkusanyiko wa vitabu vidogo 30.Abulcasis ndiye mvumbuzi wa vifaa zaidi ya 200 vinavyotumika mpaka leo kwenye vyumba vya upasuaji na vitabu vyake vimetumika kufundishia Ulaya kwa zaidi ya miaka 500.Aliishi na kufia mjini Cordoba ndani ya Spain.Nyumba yake mpaka leo ipo na imepewa thamani ya juu katika utalii wa majengo.

4.AL KITAB AL MUKHTASAR FIY HISAB ALJABR WAL MUQABALA.Kiliandikwa na Muhammad bin Mussa Alkharizm (780-850).Alikuwa ni mmoja ya wafanyakazi mashuhuri wa kitengo cha kutafsiri maandishi kwenye jengo la Baitul Hikma na baadae akawa ndiye mkurugenzi wa kituo hicho.

Pamoja na kazi nyingi alizozifanya alisoma na kutafsiri maandishi ya Euclid, mwanafalsa wa zamani wa kigiriki.Hata hivyo maandishi na hesabu zake za Aljebra ambazo ndizo zilizozalisha ujanja wote wa hesabu duniani haujaonekana kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na michoro ya maumbile ya Euclid.

Nakala halisi ya kitabu cha Alkhwarizm katika hati zake za kiarabu kinapatikana kwenye maktaba ya chuo kikuu cha Oxford nchini Uiengereza.
Mwanafalsafa Aristotle wa Ugiriki ya kale aliandika mambo mengi ya sayansi miaka kama 1,100 kabla ya kuzaliwa Muhammad, kabla ya hao bani Ummayad.

Aristotle hakujua Kiarabu.

Acheni ujinga nyie.

20250203_123218.jpg
 
Meanafakdafa Aristotle wa Ugiriki ya kale aliandika mambo mengi ya sayansi miaka kama 1,100 kabla ya kuzaliwa Muhammad, kabla ya hao bani Ummayad.

Aristotle hakujua Kiarabu.

Acheni ujinga nyie.

View attachment 3223881
Ukimtaja Aristotole lazima uongeze kwa hisani ya waislamu.Kwani taarifa zake na kazi zake kwanzo zilikushanywa kule Baghdad na kutafsiriwa kwa lugha ya kiarabu.Hatimae zikafika Toledo na Cordova kule Uhispania ndipo hao lugha ndogo ndogo za Ulaya na makabila yakanukuu kazi zake mpaka zikawafikia hao Britanica.lugha ya kiiengereza ilikuwa ni miongoni mwa lugha ndogo ndogo ambayo baadae ikakuwa wakati huo kiarabu kimshawazomesha wazungu. kwa karne kadhaa.
Kigiriki ilikuwa ni moja ya lugha zilizotumiwa na wataalamu wa Baghadad kufahamu aliyofanya Aristotle na wenzake.
Waislamu wana maelekezo mengi ndani ya dini yao ya kutodharau elimu na lugha za watu wengine.
 
Ukimtaja Aristotole lazima uongeze kwa hisani ya waislamu.Kwani taarifa zake na kazi zake kwanzo zilikushanywa kule Baghdad na kutafsiriwa kwa lugha ya kiarabu.Hatimae zikafika Toledo na Cordova kule Uhispania ndipo hao lugha ndogo ndogo za Ulaya na makabila yakanukuu kazi zake mpaka zikawafikia hao Britanica.lugha ya kiiengereza ilikuwa ni miongoni mwa lugha ndogo ndogo ambayo baadae ikakuwa wakati huo kiarabu kimshawazomesha wazungu. kwa karne kadhaa.
Kigiriki ilikuwa ni moja ya lugha zilizotumiwa na wataalamu wa Baghadad kufahamu aliyofanya Aristotle na wenzake.
Waislamu wana maelekezo mengi ndani ya dini yao ya kutodharau elimu na lugha za watu wengine.
Waislamu gani mkuu nimekwambia Aristotle kaandika habari zake miaka 1,100 kabla Quran haijaandikwa.

Waislamu gani?
 
Waislamu gani mkuu nimekwambia Aristotle kaandika habari zake miaka 1,100 kabla Quran haijaandikwa.

Waislamu gani?
Waislamu wa Baghdad ndio waliozileta kazi za Aristotle hizo za miaka unayosema na hizo tarehe zale wakazidhibiti.
Sasa sijui ni kipi unachokipinga.
Waislamu waliziweka sawa kazi za watu wengine wa jamii ya kihindi halafu kuzichanganya na kutoa maarifa makubwa yaliyofika Ulaya kupitia Spain.
Kwa mafunzo ya uislamu tunaamini uislamu ndio dini ya mwanzo ya binadamu kabla hata Quran haijaanza kuandikwa kwa lugha ya kiarabu ambayo ndiyo Mungu kwa hekima zake aliyoichagua iandikwe kwayo.
Hivyo dini ya Aristotle na wenzake hatuwezi kukanusha kuwa haikuwa Uislamu.Ba kama walikuwa dini tofauti na Uislamu basi bado walikuwa ndani ya muongozo wa Mwenyezi Mungu.
 
Waislamu gani mkuu nimekwambia Aristotle kaandika habari zake miaka 1,100 kabla Quran haijaandikwa.

Waislamu gani?

Mkuu kiranga usipate tabu mimi nimesoma andiko la jamaa nikaishia Kusikitika.

Naomba unisaidie Kusikitika.
 
Waislamu wa Baghdad ndio waliozileta kazi za Aristotle hizo za miaka unayosema na hizo tarehe zale wakazidhibiti.
Sasa sijui ni kipi unachokipinga.
Waislamu waliziweka sawa kazi za watu wengine wa jamii ya kihindi halafu kuzichanganya na kutoa maarifa makubwa yaliyofika Ulaya kupitia Spain.
Waislamu wa Baghdad kina nani hao wasio na majina? Taja majina yao tuchunguze habari zao, tujue kama ni Waislamu kweli ama ni uzushi tu. Tujue ni wa mwaka gani.

Mbona unaongelea kivivuvivu na kijuujuu jambo la usomi?

Huoni hapo mimi nimekuwekea jina la mtu, nimekuwekea sehemu, nimekuwekea mwaka.

Sasa hao Waislamu wa Baghdad wa mwaka gani? Kina nani?

Baghdad imeanzishwa July 30, 762 CE.

Aristotle kaandika habari zake 500 BCE. Miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa.

Sasa Aristotle aliyeandika sayansi miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa itakuwaje awe kafundishwa sayansi na Waislamu wa Baghdad?

Wewe hata historia unaijua?
 
Mkuu kiranga usipate tabu mimi nimesoma andiko la jamaa nikaishia Kusikitika.

Naomba unisaidie Kusikitika.
Mtu anakwambia Waislamu wa Baghdad walimfundisha Aristotle sayansi.

Hata hajui kuwa Aristotle aliandika sayansi miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa.

Ukimsoma unaona huyu hata historia ndogo tu ya Baghdad haijui.
 
Waislamu wa Baghdad kina nani hao wasio na majina? Taja majina yao tuchunguze habari zao, tujue kama ni Waislamu kweli ama ni Wababeli tu. Tujue ni wa mwaka gani.

Mbona unaongelea kivivuvivu na kijuujuu jambo la usomi?

Huoni hapo mimi nimekuwekea jina la mtu, nimekuwekea sehemu, nimekuwekea mwaka.

Sasa hao Waislamu wa Baghdad wa mwaka gani? Kina nani?

Baghdad imeanzishwa July 30, 762 CE.

Aristotle kaandika habari zake 500 BCE. Miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa.

Sasa Aristotle aliyeandika sayansi miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa itakuwaje awe kafundishwa sayansi na Waislamu wa Baghdad?

Wewe hata historia unaijua?
Kichwa chako ni kigumu kuelewa au umeamua kupinga ukweli uliokuwa hukuujua hapo zamani.
Hatupingi habari za Aristotle isipokuwa tuanchosema Aristotle habari zake zisingejulikana kama si kazi ya Alkindi kwenye jumba la hikma la Baghad ambaye ni miongoni mwa waliozitafsiri kazi hizo.
Kwa ujumla wake walichofanya akina Aristotle na Socrates vilikuwa na kasoro kadhaa ambazo baada ya tafiti waislamu walikwenda mbali sana.
 
Mtu anakwambia Waislamu wa Baghdad walimfundisha Aristotle sayansi.

Hata hajui kuwa Aristotle aliandika sayansi miaka 1262 kabla Baghdad haijaanzishwa.

Ukimsoma unaona huyu hata historia ndogo tu ya Baghdad haijui.
Sayansi ni maneno yatokanayo na hao waislamu wa Baghdad na wenzao na hatusemi kuwa walimfundisha Aristotle bali walithamini kazi zake na kuzifanyia kazi wakaacha alichokosea na kuchukua walichoona kapatia.
Huo ndio ubora wa uislamu katika elimu.
Kwanini ungangangania kuonesha kuwa Aristotle ni bora kielimu kuliko waislamu waliomtambulisha kwa ulimwengu.Kilichofanywa ni kuthamini elimu na kutunza historia kama tunavyofanya hapo kuhusiana na mchango wa uislamu na lugha ya kiaarabu katika maendeleo ya dunia
 
Kichwa chako ni kigumu kuelewa au umeamua kupinga ukweli uliokuwa hukuujua hapo zamani.
Hatupingi habari za Aristotle isipokuwa tuanchosema Aristotle habari zake zisingejulikana kama si kazi ya Alkindi kwenye jumba la hikma la Baghad ambaye ni miongoni mwa waliozitafsiri kazi hizo.
Kwa ujumla wake walichofanya akina Aristotle na Socrates vilikuwa na kasoro kadhaa ambazo baada ya tafiti waislamu walikwenda mbali sana.
Mji wa Baghdad umeanzishwa mwaka gani na Aristotle kaishi mwaka gani mpaka mwaka gani?

Tuanzie hapo kwanza.
 
Sayansi ni maneno yatokanayo na hao waislamu wa Baghdad na wenzao na hatusemi kuwa walimfundisha Aristotle bali walithamini kazi zake na kuzifanyia kazi wakaacha alichokosea na kuchukua walichoona kapatia.
Huo ndio ubora wa uislamu katika elimu.
Kwanini ungangangania kuonesha kuwa Aristotle ni bora kielimu kuliko waislamu waliomtambulisha kwa ulimwengu.Kilichofanywa ni kuthamini elimu na kutunza historia kama tunavyofanya hapo kuhusiana na mchango wa uislamu na lugha ya kiaarabu katika maendeleo ya dunia
Kwa hiyo unakubali kuwa sayansi ilikuwepo kabla ya hao Waislamu wa Baghdad na wao ndio walijifunza kwa Aristotle?
 
Back
Top Bottom