Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

Sifa ya mtu aliyekosa tumaini au kukataa tamaa ni kumkufuru Mungu, tuendelee kumwomba Mungu apambane na huu wizi wa binadamu na mtandao wake ambao naamini unaanzia juu kabisa kwa wazee wa mitano tena au wapambe wao
kwahiyo mkuu una amini mungu anaweza kupambana na wezi?
 
Sifa ya mtu aliyekosa tumaini au kukataa tamaa ni kumkufuru Mungu, tuendelee kumwomba Mungu apambane na huu wizi wa binadamu na mtandao wake ambao naamini unaanzia juu kabisa kwa wazee wa mitano tena au wapambe wao
Kukata tamaa kivip ? Na kwenye nini na kwanini unalazimisha kila mtu aamini uwepo wa Mungu na unataka akishaamini, aamini Mungu yupi kati ya hawa zaidi ya 1000 wanaoaminiwa na jamii tofauti humu duniani?
 
Washikwe na kutumbukizwa makaburin ili liwe somo. Nashukuru mheshimiwa rais kwa hili.
kwahiyo mkuu una amini mungu anaweza kupambana na wezi?
 
Ndio, fanya utafiti wa wezi maarufu miaka 30 iliyopita, angalia hatma zao
Binadamu ndiyo atapambana na wezi mkuu na siyo Mungu.
Ndiyo maana kuna Askari Polisi, Mahakama na Jela.
Mungu hawezi kufanya chochote pindi mtu anapofanya wizi.
 
Watu ambao hawajafahamika wamevamia nyumbani kwa mkazi wa Kibaha kwa Mfipa Mkoa wa Pwani, Melkisedeck Sostenes na kupora gari, pesa na vitu mbalimbali kisha kuwatumbukiza wanandoa kwenye chemba za vyoo.

Watu hao wanaodaiwa kutekeleza tukio hilo saa 12 asubuhi pia wanadaiwa kuondoka na mtoto mchanga mwenye umri wa miezi saba.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Alhamisi Januari 16, 2025 Sostenes amesema kuwa watu hao walifika nyumbani kwake jana saa 12 asubuhi na walimvizia alipokuwa akitoka ndani kwenda kulisha kuku bandani.


========

My Take
Kuna Baadhi ya Matukio binadamu wenzetu wanafanya unashindwa uanzie wapi kuduwaa.

Lakini nawashangaa zaidi wanaosema hukumu ya kifo Ifutwe badala ya kuangalia aina ya matukio ya kuyapa hiyo hukumu.

Ndio maana wakati mwingine Huwa napata kigugumizi sana kuwaonea huruma watu walioko jela licha ya usemi kwamba sio wote walioko jela Wana makosa lakini ni zaidi ya 90% wanakuwa na makosa tena ya Ukatili,hapo kiukweli Huwa inaniwia vigumu kumhurumia mfungwa.

Poleni sana mliofikwa na haya.
 
Hio hukumu ni nzuri ikiwa kwa mwenzio sio mwanao wala familia yako
Hakuna hukumu iliwahi kuwa nzuri ikiwa anayehukumiwa ni ndugu au mwanao.
Kuna watu wanafanya makosa yanayostahili hukumu hiyo.
Wanaoua watoto kwa ajili ya ushirikina, wanaovuna viungo, wanaua watu kwa ajli ya ujambazi, ugaidi. Kama umechukua maisha ya mtu kwa makusudi, nawe yako yachukuliwe. A life for a life.
Kuna bahati mbaya mfano ajali, au kuua pasipo kukusudia, lakini umeua ukiwa kwenye shughuli za kijambazi, umeteka mtoto ukaenda kumuuza kwa mganga kwa ajili ya viungo, hiyo hukumu inafaa.
 
Mi binafsi hukumu ya kunyongwa iendelee
Hukumu ya kifo yafaa iendelee kuwepo.

Hio hukumu ni nzuri ikiwa kwa mwenzio sio mwanao wala familia yako

Hukumu ya kifo ni muhimu sana kuwepo regardless Hukumu hiyo inatolewa kwa Mtu gani. Isipokuwa Kitu Cha muhimu zaidi cha kuzingatiwa kwenye suala hili ni kuwepo kwa sababu za msingi kabisa za Mtu kuweza kuhukumiwa adhabu hiyo. Wanaohukumiwa adhabu hiyo wawe ni wale Watu ambao tu kimsingi na kwa uhakika wanastahili na inalazimu mhalifu kuhukumiwa adhabu hiyo kali ya kuuawa kutokana na wao kufanya uhalifu mbaya sana ambao unastahili kuhukumiwa adhabu ya kifo
 
Mafanikio ya na mengi nyuma yake ikiwemo dhuluma...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…