Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

Kibaha: Waiba gari, kichanga na kuwatumbukiza wazazi kwenye shimo la choo

rais ndo anasaini hukumu ya kifo ila sikuhizi sidhani kama wana saini!, wanahofia imani/dini
 
Watu ambao hawajafahamika wamevamia nyumbani kwa mkazi wa Kibaha kwa Mfipa Mkoa wa Pwani, Melkisedeck Sostenes na kupora gari, pesa na vitu mbalimbali kisha kuwatumbukiza wanandoa kwenye chemba za vyoo.

Watu hao wanaodaiwa kutekeleza tukio hilo saa 12 asubuhi pia wanadaiwa kuondoka na mtoto mchanga mwenye umri wa miezi saba.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Alhamisi Januari 16, 2025 Sostenes amesema kuwa watu hao walifika nyumbani kwake jana saa 12 asubuhi na walimvizia alipokuwa akitoka ndani kwenda kulisha kuku bandani.
View attachment 3204158
========

My Take
Kuna Baadhi ya Matukio binadamu wenzetu wanafanya unashindwa uanzie wapi kuduwaa.

Lakini nawashangaa zaidi wanaosema hukumu ya kifo Ifutwe badala ya kuangalia aina ya matukio ya kuyapa hiyo hukumu.

Ndio maana wakati mwingine Huwa napata kigugumizi sana kuwaonea huruma watu walioko jela licha ya usemi kwamba sio wote walioko jela Wana makosa lakini ni zaidi ya 90% wanakuwa na makosa tena ya Ukatili,hapo kiukweli Huwa inaniwia vigumu kumhurumia mfungwa.

Poleni sana mliofikwa na haya.
Visasi visivyokuwa na Ubinadamu!
 
Hio hukumu ni nzuri ikiwa kwa mwenzio sio mwanao wala familia yako
Mimi kama nikiua ninyongwe tuu. Mwanangu akihusika kuua na kufanya ukatili uliopitiliza atangulizwe kuzimu tuu maana amekuwa disgrace to the World.

By the way, niliwahi kumsikia mzazi anayejitambua (Mama) wa JOSEPH KONY akisema hatoumia siku mwanae akikamatwa na kupewa hukumu ya kifo, kwasababu aliyowafanyia raia wa Uganda wasio na hatia hayavumiliki, na yeye kama Mzazi anajuta kwanini alimzaa.
 
rais ndo anasaini hukumu ya kifo ila sikuhizi sidhani kama wana saini!, wanahofia imani/dini
Ni unafiki tu wanafanya.

Ndo yale ya Magufuli kuona huruma (au kwa sababu za kidini) kusaini hati ya mashtaka ya kifo kwa waliokutwa na hatia makahamani, kisha anaenda kumuua Ben Saanane kwa mikono yake (kwa mujibu wa Eric Kabendela). Unafiki wa hali ya juu sana huu.
 
Mbona umepaniki sana? Nadhani kama kuna mtu mkubwa wa muhimu kwako alishawahi patwa na hii hali umeathirika nayo. Bado una hasira. Mimi nampigia samia kampeni wewe unaumia? Samia mitano tena
Dada, utatokwa na hedhi kwenye daladala ulilosimama hilo bila kutarajia kutokana na chuki na wivu. Kwahiyo hili ni makosa ya Samia? Nyumbu wa lissu na mbowe bwana........umakumaku tu muda wote!!
 
Hio hukumu ni nzuri ikiwa kwa mwenzio sio mwanao wala familia yako
Ni kweli, ndiyo maana ni jukumu letu wazazi kuwafundisha maadili mema hao wanetu ili wakawe raia wema wenye kufuata sheria. Zaidi ya hapo kila mtu anabeba msalaba wake
 
Back
Top Bottom