Kibajaji amvaa vikali Zitto Kabwe kumsema Magufuli, amuita muoga kwani wakati yupo hakusema?

Kibajaji amvaa vikali Zitto Kabwe kumsema Magufuli, amuita muoga kwani wakati yupo hakusema?

Kwanza kusemwa vizuri/vibaya, uwe hai/umekufa ni lazima. Swali ni unasemwa kuh. nn.
Lkn pia kna watu wana ugonjwa wa kumwagia misifa kupitiliza, hao pia ni wa kuwavumilia ingawa inakerehesha.
Kitu kinachonikwaza ni hiki - kuyafanya hayo ukiwa bungeni. Wamepelekwa huko kwa lipi? Wangezungmzia zaidi ya waliomtuma badala ya kuwa wakili wa kumtetea marehamu, wkt wala hajalipwa. Au labda waliompeleka ndo wanalotaka. Kina nani hao?
Mwisho wa yote kuna haja ya kushughlikia ubora wa wabunge wetu. Hakuna namna, ni Katiba Mpya
 
Tuelewane hapa kwamba Mbowe na Lissu hawakuacha kumkosoa Magufuli waliendelea. Et asingekuwa Samia! Mara ya kwanza huyo Samia alipoulizwa kuhusu kesi ya Mbowe alijibu? Msinge mshinikiza mngemuacha atende haki pasina kushinikizwa kama alivyowaachia wazanzibari wenzie.
Haki ni asili ya Samia,ile ilikuwa kesi ya mchongo ya sukuma gang usijifanye huelewi.
 
Ila Lissu hakuacha kumsema Magufuli.

Sasa ukijakumsema wakati kafa ndio tutegemee atajirekebisha huko kaburini au ndio kupunguza hasira tu?

Sio kila mtu ni jasiri kama Lisu, hawa wengine walingoja atoke madarakani wateme nyongo. Kwa bahati mbaya kafia madarakani. Hivyo kwakuwa hakuwa mstaarabu acha ukweli wake apewe akiww huko huko motoni.
 
Hayati aliwanyima watu haki ya kusema kipindi angali hai, wacha asemwe akiwa mfu. Ulikua ukimkosoa lazima ushughulikiwe.

Ukiwanyima watu haki ya kusema ukiwa hai, utasema ukiwa kaburini. Ili uwe binadamu sharti usemwe.

Ni wapumbavu pekee wasiotaka kusemwa.
Sasa hata akimsema JPM sasa atamsikia? .Hizo ni dalili za upunguani ni sawa kuongea na mawe ukidhani yanakusikia.lazima aliye sanaa aliporwa hela alizopata kiharamu alipokuwa PAC
 
Kwahiyo kwa wale walisoma logic
Zito anasema waliopenda Jpm wakazikwe chato.
Je Yeye hakuwa anampenda mama yake?
Hakumpenda Maalim
Ndio maana hajazikwa nao.
She is stupid. Narudi she is stupid
Nakazia Shiiiis stupid. Period
Jamani Zito ni He wala si She [emoji1787][emoji1732]
 
Aliogopa Kwa kuwa wasiojulikana na vikosi kazi walikuwepo
Ni tabia ambayo ameridhika kwa mzazi wake Mama ake aliishi kwa musaada alikuwa kilema na yeye amekuwa dalali wa siasa na anaishi kwa misaada ya siasa ya JPM alimmwaga akawa anahaha hana kazi yakufanya sasa karudushwa kwenye udalali na ombaomba huruma ya viongizi apewe ulaji
 
Kwa hiyo sisi tunaomsema unadhan hatujui hatusikii???? Tunajua tukimsema kina nani inawauma sisi kazi yetu ninkumsema mpaka wajiue tutaendeleankumsema hadi 2050
Sekunde 1 yenyewe kuimaliza ni neema zake Mungu pekee, ndiyo uwe na uhakika kama utafika 2050, kweli kuvimbirwa makande ni raha sana [emoji23]
 
Si yeye zao la huyo mbaguzi, mbambikaji, mtekaji, mpotezaji watu na mwenye roho mbaya.
Kibaya kinazikwa na wabaya.
Hata nawe ungepotezwa tu maana unaropoka hapa ilihali haujapotezwa uko hai na huenda ukawa na roho mbaya hata zaidi ya shetani lakini unajificha tu nyuma ya keyboard [emoji34]
 
Leo bungeni mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde amemvaa vikali kiongozi mkuu wa ACT, Zitto Kabwe kwa kumsema Hayati Magufuli. Kibajaji amemuita Zitto muoga kupitiliza kwani wakati Magufuli yupo hai hakusema mpaka ameondoka.

Pia Kibajaji amesema wote wanaomsema Magufuli ni wanafki na hata Samia akiondoka nae watamsema vilvile. Amemsifu Nyalandu kwa kusema kwa vitendo hawezi kufanya kazi na Magufuli wakati yupo hai na kuachia nafasi yake ya ubunge.

========

Kibajaji: Nchi yetu imeweka vizuri sana masuala ya utawala bora kisheria lakini kuna baadhi ya vyama kwa mfano pale Zanzibar, ACT tunashirikiana nacho kwenye utawala bora, sisi tuna Rais, tuna Serikali wao wana makamu wa kwanza wa Rais lakini mmesikia kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto anamnanga mheshimiwa Magufuli kana kwamba Zitto hashiriki kwenye Serikali.

Magufuli aheshimiwe, Zitto aelewe kwamba suala la kufiwa ni suala kubwa. Haiwezekani kwenye utawala bora tuache suala la Magufuli kuzungumzwa vibaya na mimi sitaacha.

Leo nnapoongea Waislamu mmefunga, dini inawakataza kuwasema vibaya marehemu, Zitto ni muislamu anajua.

Mheshimiwa Zitto anatutaka tunaompenda mheshimiwa Magufuli tukazikwe nae. Zitto amewahi kufiwa na mama yake, mimi sitaki kufika huko, mama wa Zitto ni mama yangu mimi. Mimi nimewahi kufiwa na baba yangu lakini ACT wamewahi kufika na makamu wa kwanza wa Rais, Zitto anatulazimisha sisi tuanze kumsema vibaya Maalim Seif, hatuwezi.

Inakuwaje watu mnakuwa waoga, viongozi wakiwepo hamsemi wakiondoka ndio mnasema, huu ni uoga uliopitiliza. Mtu mmoja tu alisema kwa vitendo kwamba yeye hawezi kufanya kazi na Magufuli, Nyalandu.

Aliachia ubunge akaondoka lakini watu tuliobaki hapa ni watu wa Magufuli na tumefanya nae kazi na tulikuwa tunamsifu.

Hawa watu ambao sasa wanamsema Magufuli na kumsema Samia na wanafiki wakubwa, Samia akiondoka watamsema vibaya hivyohivyo, ni bora mimi Lusinde ambae niko wazi na siwezi kuacha.

Pia, soma=> Zitto: Wanaompenda Magufuli wakazikwe naye Chato, alikuwa Rais fisadi zaidi kuwahi kutokea Tanzania
Mwambieni Lusinde hatuwezi kupowa kuanika UFEDHULI alioufanya huyo mungu wenu wa Chato kwa Watanzania. Zitto kabwe alisema this week, na Mwingira kasema miezi 3 iliyopita. Hatupoi mpaka dunia nzima ijuwe kuwa tulikuwa kwenye himaya ya shetani kwa mwaka 2015-20.
 
Sekunde 1 yenyewe kuimaliza ni neema zake Mungu pekee, ndiyo uwe na uhakika kama utafika 2050, kweli kuvimbirwa makande ni raha sana [emoji23]
Uzuri yy ndo kafa (naenjoy) ,ila usijar tusiompenda ninidadi ya kura za chadema za uongo za 2020 mpaka tufe wote ,tunavikao na kamati za kumsema na tunahakikisha hii haiishi walau 2100 itakiwa anasemwa na wajukuu wangu hard than me na wanae wasirelax urithi ni toa hela za kodi zetu alizoiba na doto
 
Back
Top Bottom