Kibiti mpaka laana ya Cabo Delgado: Part II

Kibiti mpaka laana ya Cabo Delgado: Part II

Makala murua kabisa. lakini wenye uwezo mdogo wa akili wataendelea kuishutumu dini badala ya mzizi halisi wa tatizo. Utawala mbovu wa serikali zetu na mgawanyo wa huduma usiojali wananchi, rushwa na ukandamizaji huzaa haya yote. Watu katika mazingira haya ni rahisi sana kurubuniwa na mabeberu ili tu msitulie na wao waendelee kuchota mali.
Mbona wanashambulia raia badala ya viongozi wanaosababisha hayo matatizo?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Tanzania inapoelekea naionea huruma sana.

Wao wanasema JKT haitoi ajira 😀 ila cha kusikitisha wanawapa mafunzo halafu wanawarudisha mitaani mikono mitupu.

Tunapanda mahindi tunategemea tutavuna mpunga😀.

Kila mwaka unamwaga tu mitaani JKT waliokosa matumaini unategemea nini sasa ? ila walio kwenye connection mnawaajiri mnafikiri hawa wengine wanawatazama tu.

JWTZ NA JKT MNATENGENEZA MAGAIDI NA WAASI WENDA KWA KUJUA AU KWA KUTOKUJUA.
Ndio maana kwenye graduation zao husisitizaga uzalendo na kuto tumia mafunzo vibaya..

Raia wa kawaida wa Tz 'layman & women' Ni waoga Sana wa bunduki na vurugu for sure watu walio pitia mafunzo ya JESHI hawaogopagi bunduki na waki be manipulated ndio balaa.
 
Kuna uzi wa part 1 alianza nao. Sasa badala ya kuendelea kwenye uzi ule ule kaanzisha uzi mwingine wa part 2 ina maana part 3 ataanzisha uzi mwingine.

Sorry nilidhani unaujua uzi wa kwanza ukaamua kunizingua.
Kutokana na andiko lako hili imebidi niutafute nimeukuta jukwaa tofauti na hili
upo jamii intel kule.
 
Ndio maana kwenye graduation zao husisitizaga uzalendo na kuto tumia mafunzo vibaya..

Raia wa kawaida wa Tz 'layman & women' Ni waoga Sana wa bunduki na vurugu for sure watu walio pitia mafunzo ya JESHI hawaogopagi bunduki na waki be manipulated ndio balaa.
Uko ndio tunapoelekea unafikiri vijana wanapenda kukalishwa bila ajira zozote za kueleweka.

Vijana wa JKT wanarudishwa majumbani wale wasio na watu wa kuwashika mkono lakini watoto wa wakubwa ni mwendo wa kupigiwa simu tu za maelekezo na kuitwa.

Maafande wanajibu shit kuwa jeshi halitoi ajira etii muwe wazalendo hakuna uzalendo kwenye njaa.

Watoto wao wanawaweka kwenye system chap madogo wengine wanarudishwa kwao, madogo wengine wenye mioyo mepesi huishia kujinyonga.

Ubaya JKT wanaorudishwa kitaa wanazidi kuwa wengi na kitaa pakavu balaa life lime tight.

Hawa watu wanahitaji tu supplier wa silaha kuanzisha vikundi vya kiasi na ubaya nchi yetu rasilimali inazo tena za kutosha za kupigania.

Huwezi wapa vijana mafunzo utegemee watakuwa humble maisha yao yote huku wakiona viongozi wa chama na serikali na maafande wao pekee wakila mema ya nchi na kulindana.

JKT wanatengeneza bomu la vikundi vya kiasi sio vya kigaidi ni suala la muda serikali ijitafakari sana namna wanavyo iongoza hii Tanzania.

Watu wanaumia ndani kwa ndani tena hasa vijana kitu ambacho ni kibaya sana.

Hawa watu wanahitaji supplier tu wa silaha maana kama chuki dhidi ya serikali wanazo hawaitaji wa kuwaambia hiki na hiki kibaya serikali imefanya na inafanya.
 
Makala murua kabisa. lakini wenye uwezo mdogo wa akili wataendelea kuishutumu dini badala ya mzizi halisi wa tatizo. Utawala mbovu wa serikali zetu na mgawanyo wa huduma usiojali wananchi, rushwa na ukandamizaji huzaa haya yote. Watu katika mazingira haya ni rahisi sana kurubuniwa na mabeberu ili tu msitulie na wao waendelee kuchota mali.
hakika
 
Yah hiyo ndio ilikua maana yangu tunakosa mtitiriko mmoja. Kule kuna wadau nao wamechangia. Sasa angeweka nyuzi moja mtitiriko ungekua mzuri.

I hope Moderator watamsaidia kwa hili.
Kuweka nyuzi jamii intelligence ni kama kuomba kazi Utumishi. Unapost then unakaa kungoja watakapojisikia.
 
Tanzania inapoelekea naionea huruma sana.

Wao wanasema JKT haitoi ajira 😀 ila cha kusikitisha wanawapa mafunzo halafu wanawarudisha mitaani mikono mitupu.

Tunapanda mahindi tunategemea tutavuna mpunga😀.

Kila mwaka unamwaga tu mitaani JKT waliokosa matumaini unategemea nini sasa ? ila walio kwenye connection mnawaajiri mnafikiri hawa wengine wanawatazama tu.

JWTZ NA JKT MNATENGENEZA MAGAIDI NA WAASI WENDA KWA KUJUA AU KWA KUTOKUJUA.
Hii nimekumbuka mwanzoni mwa 2010s kuna Vijana waliajiriwa JWTZ kama Wanajeshi wakapangwa kambi tofauti tofauti Nchini baadae likatoka tangazo kuwa Vijana wote walioajiriwa wapya ambao hawakufika form 4 yaani walioishia Darasa la Saba wote wapigwe chini. Kuna jamaa fulani alitokea Temeke Mikoroshini yeye alipangwa kambi moja kule Kigoma akarudi zake home.

Baada ya muda fulani akapata dili la kuwa Mzee wa Chuma,anapewa dili na location pamoja na chuma anaenda kupiga kazi,aisee baadae akanogewa akawa anafanya peke yake kwa kushirikiana na baadhi ya Polisi wa Temeke na Ilala,jamaa alikuwa Master hatari shabaha imelala akafikia hatua akawa anafanya matukio mchana kweupe kabisa kwa kutumia boxer akiwa na dereva wake mpaka Kariakoo alifanya matukio mchana kweupe na halamatwi,baadae ikafikia akijua unamfuatilia tuu analamba shaba,polisi ukijependekeza unakula shaba,aliwahangaisha sana Kanda maalumu ya Dar mpaka kuja kumtageti na kumuua kule Mbagala akiwa kwa Maganga Polisi wa Chang'ombe na Kanda maalumu Dar jasho liliwatoka.
 
Back
Top Bottom