Kichuya:Niliua off-side,ni mechi ya Mbeya City

Kichuya:Niliua off-side,ni mechi ya Mbeya City



Mchezaji wa Simba aliyefunga bao pekee katika mechi ya jana akiifungia timu yake ya Simba dhidi ya wenyeji Mbeya City ametolea ufafanuzi goli alilofunga jana

Goli hilo limezua mjadala katika mitandao ya kijamii baada ya uongozi na mashabiki wa Yanga kutuhumu kwamba mfungaji aliotea

Kichuya ambaye amekuwa akiifunga Yanga katika mechi tano mfululizo amesema kuwa refa alijiridhisha kuwa hakuotea

Akizungumza na Azam TV mara baada ya mchezo anasema aliwazunguka mabeki wa Mbeya City kwa mbele huku wao wakibaki kumtazama tu. Amefafanua kuwa kama angewazunguka mabeki kwa nyuma ilikuwa ni off-side dhahiri lakini trick aliyoifanya iliwachanganya mabeki

Anasema angeshangaa kama refa angekataa goli lake

Golikipa wa Mbeya City aliweka wazi kuwa Simba ni timu kubwa nchi hii ni lazima iheshimiwe

Kipa amesema simba ni timu kubwa....so yanga tulieni
 
Ndio takwimu gani hizo! Mbona mnazungumzia takwimu za Yanga akiwa hana akina Kamu, Ngoma na Tambwe?
Jisikie aibu,ina maana Yanga ni kubwa kuliko Kamusoko!bila hao timu haiendi?wasiporudi bahati mbaya je
 
mkuu suala la off-side mpaka leo linasumbua hata ulaya sio sisi tu, ko suala la kugusa madaraja yote halifanyi kuwa sahihi kuitafsiri ile off-side.

off side ni kweli hutafsiriwa toka pigo la mwisho la mtoa pasi (mkude) kwenda kwa mpokeaji (kichuya). tayari alikuwa yuko mbele

kwanza niseme azam hawakuwa na camera ya pembeni kuonesha vizuri ndo maana imeleta utata.maelezo ya kichuya anakwambia aliua off-side (kwa maana ya kutoka nafasi ya kuotea kurudi nyuma) kitu ambacho si kweli. hakuna sehemu amerudi, tangu anapokea (angalia video) alikuwa ana move kwenda mbele.
Kama hukuwepo uwanjani basi hupaswi kukataa maelezo ya kichuya maana kwa tuliongalia mpira kwenye luninga hatukuona mwanzo wa move ispokuwa tumekuja kuona kichuya kachomoka na beki mmoja nyuma ndo analilia offside

ila kama camera zingekuwa kwenye angle nzuri basi wote tungeongea lugha moja, kwa upande wangu mimi hadi leo sijui kama lile goli la offside au onside hivo tuache ushabiki wa kitoto, kutolea ufafanuzi kitu ambacho hujakiona
 
Kama hukuwepo uwanjani basi hupaswi kukataa maelezo ya kichuya maana kwa tuliongalia mpira kwenye luninga hatukuona mwanzo wa move ispokuwa tumekuja kuona kichuya kachomoka na beki mmoja nyuma ndo analilia offside

ila kama camera zingekuwa kwenye angle nzuri basi wote tungeongea lugha moja, kwa upande wangu mimi hadi leo sijui kama lile goli la offside au onside hivo tuache ushabiki wa kitoto, kutolea ufafanuzi kitu ambacho hujakiona
mkuu mara ngapi una ona kwenye kideo mchezaji anajaribu ku epuka mchezo wa offside trick na anafeli. ila hapa unataka niyachukue maelezo ya kichuya (mtuhumiwa) kwamba ni sahihi.

ko kwa akili yako kubwa unadhani kichuya anaweza sema aliotea.
 
mkuu mara ngapi una ona kwenye kideo mchezaji anajaribu ku epuka mchezo wa offside trick na anafeli. ila hapa unataka niyachukue maelezo ya kichuya (mtuhumiwa) kwamba ni sahihi.

ko kwa akili yako kubwa unadhani kichuya anaweza sema aliotea.
Watanzania sijui tukoje hujajibu swali unaanza kuingiza mambo ya akili kubwa, ndio nina akili kubwa wala hujakosea ndomana nauliza ulikuwepo uwanjani? Kama uliangalia kwa luninga kama sisi basi huna uhakika na unachosema maana video inayoonesha goli haikupi % kusema kuwa ile ni offside labda kama ufate mapenzi ya moyo wako tu
 
Waamuzi wa mechi kama hizi huwa Hadija Manara anawapenda sana//
 
Tambwe akichukua mpira kimbinu viti vyoote vikang'olewa
Mkuu huwa napita tu humu kusoma comments za watu, ila hii yako nimecheka sana kwa sauti hadi daladala nzima wamenishangaa..... Offside fc wabishi sana.
 
Back
Top Bottom