Kichwani kwa Bondia Mwakinyo kupo sawa sawa? Amuombe Radhi upesi sana ' Legend ' Rashid Matumla kabla hajatuudhi zaidi

Waliomzunguka ndio washenzi, wanamdanganya sana, huwezi kuwa bondia mkubwa Tanzania halafu unampuuza mtu kama Rashid Matumla, huyu dogo ni mpuuzi sana, nilikuwa namuunga mkono naona atafika mbali kumbe akili hana kabisa, mabondia wakubwa kuwa wanajifunza kabisa namna ya kufanya mahojiano, huwezi kukuta wameongea utumbo kama huyu dogo.
 
Dogo mwakinyo omba radhi haraka sana!!!!!

Tena afanye hivyo ndani ya Saa 24 au 48 au 72 kabisa vinginevyo Moto aliouwasha unaenda Kumuunguza na hatoamini Macho na Masikio yake.
 
Siyo huko tu,clip yake imesambaa mitandao ni,huyu atakuwa anatumia kitochi 4G
 
Namì nasema matumla ni mpuuzi! Hana kitu cha kujivunia zaidi ya jina snake boy. Hajui hata uchambuzi. Mwakinyo baba lao.
 
Wote hawajielewi.
Kama kweli Matumla anajiheshimu,hakupaswa kusema kinyume na mwenzake.Kajibiwa kwa kadri ya alichokisema
 
Tatizo Watanzania tuna Wivu sana Mtu akishaanza kupata mafanikio tuna mkalia kooni, Hassan Mwakinyo jr ana displin kubwa sana kuliko mnavyo mchukulia.

Nakumbuka Pambano lake la kwanza nje ya Nchi nilimrecord na kuwarushia baadhi ya Media na Watu Mashuhuri wengi ikiwemo Mpaka tajiri namba moja hapa Tanzania nikiamini anaweza kufanya jambo maana niliona uwezo wake.

Dogo alinitafuta na kunishukuru sana hakika ni Mtu ambae kalelewa katika Misingi ya nidhamu, Shida yetu baadhi ya Watanzania ni WIVU na pia NEGATIVE sana.

Huyo Matumla NEGATIVE zake ndio zimemperekea kujibiwa hivyo, na kajibiwa UKWELI.. kama aliona kuna Mapungufu asinge shindwa kumtafuta Cocha wa Hassan Mwakinyo Jr na kutoa ushauli wake kama Legendary.. Matokeo yake anaongea upuuzi uliojaa WIVU.

Ndugu Hassan Mwakinyo Jr naomba ujue kabisa kuwa sisi Watanzania tunataka ila atujui tunataka nini!! Naomba uongeze Mazoezi sana na ukae kimya wengine walikuwa hawasikiki wamefulia sasa wanataka kusikika kupitia wewe, kaaa kimya piga zoezi natumaini siku moja watakaa kimya.

One love na hongera kwa kuleta hamasa kubwa za Ndondi Nchini wewe ni Champion Man Big up sana na utafika mbali trust Kanyeeeela Mumo.
 
acha kubishana na bondia utapingwa ngumi ya matako
 
hata kama matumla kafanya vizuri kiasi gani hana haki ya kumtukana mwakinyo.
Alichokifanya mwakinyo ni sahihi wala asilaumiwe , Matumla ni mpuuzi tu.
 
Wote hawajielewi.
Kama kweli Matumla anajiheshimu,hakupaswa kusema kinyume na mwenzake.Kajibiwa kwa kadri ya alichokisema

' Wapumbavu / Mapopoma ' wanazidi Kuongezeka kila Kukicha nchini Tanzania.
 
Anawazee wake waganga wakienyeji anakuanao Marakwamara ndowanamjaza huo ujinga.
 
hata kama matumla kafanya vizuri kiasi gani hana haki ya kumtukana mwakinyo.
Alichokifanya mwakinyo ni sahihi wala asilaumiwe , Matumla ni mpuuzi tu.

Unaweza ukaweka Ushahidi wako kuwa Rashid Matumla alimtukana Bondia Mwakinyo alipokuwa akifanya ' Live Game Analysis ' yake Juzi? Hivi Kumbe Bondia Mwakinyo kuambiwa kuwa aache Kucheza Ngumi Kitoto Kitoto na abadilishe ' Trainer ' wake kama kweli anataka Kufika mbali Kimchezo ndiyo Kutukanwa? Hivi ni kwanini baadhi yenu hapa Jamvini hamna Akili kama Wewe hivi? Kwani kama unajijua huna Akili na huna ' Facts ' za Kutosha juu ya Jambo / Suala husika ni lazima nawe uchangie? Ukikaa Kimya uwaache wenye IQ Kubwa wachangie na Wewe kwa ' Upopoma ' wako uweze Kujifunza na Kuokotezaokoteza Madini yao utapungukiwa na nini?
 

Ninalolisema / Ninaloliona Mimi jua hata Mwenyezi Mungu nae pamoja na Malaika wake Jibril na Mikaela nao wameliona vile vile.
 
Bahati mbaya sana hajui kukosolewa kama alivyofanya Matumla ni namna tu ya kumsaidia ajirekebishe wapi ajipange vipi kama kijana. Mwakinyo amelewa sifa mapema wakati bado ana safari ndefu,kwa shombo anazoendelea nazo,ataishia Lushoto tu hapo hapo. Nimesikia vile vile akiponda Azam kwamba hatafanya nao kazi,ujinga wa kiwango cha juu. Bila kukosolewa huwezi kuwa mzuri ktk fani uliyopo. Asione akina Diamond wanapiga mpunga mrefu mpaka sasa,wamevumilia na kurekebishwa sana. Wala hakuna anaojibishana nao kwa jeuri hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…