KIDATO CHA NNE KULIPIA CHETI NI SAHIHI?

KIDATO CHA NNE KULIPIA CHETI NI SAHIHI?

Hypersonic

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2012
Posts
829
Reaction score
1,564
Wadau Eid Mubarak,
Niende kwenye mada nina mtoto wa mdogo wangu ambaye nimekuwa nikimsuport katika elimu yake ya Sekondari. Huyu binti anasoma shule moja SIJUI niite ya serikali au ya kijamii, ni shule zile amabazo zilijengwa mahususi kwa ajili ya jamii za kifugaji ili kuisaidia ukuaji wa elimu kwenye maeneo husika.
Binti huyu mwanzo alifaulu kwenda shule ya kata maeneo ya kijijini kwetu kutokana na mazingira nikaona nifanye ninavoweza kumtoa maeneo yale na akiwa kidato cha kwanza nilifanikiwa kumuamishia shule ya bweni, ilikuwaje hii si mada ya leo.
Kifupi hii shule ina michango mingi sana nadhani Headmaster anakula kutokana na urefu wa kamba. Sasa shule zilivofungwa kwa ajili ya likizo fupi kidato cha nne hawakufunga. Leo ndo nimetumiwa mahitaji kwa ajili ya kumalizia miezi michache iliyobaki. Mojawapo ya michango iliyonistua ni kama ifuatavyo:-
1. Kitambulisho shilingi 10,000/= (Hiki wakati mtoto anaanza fomu one alilipa na hakijawahi tolewa mpaka leo)
2. Project ambayo haitajwi shilingi 30,000/=
3.Remedial 20,000/=
4. Cheti shilingi 8,000/=
5. Mahafari ya shule 20,000/=
6. Mahafari ya dini 10,000/=
7. Bima ya afya 10,000/= hii bima nikauliza kuna bima ya elfu 10? jibu nikwamba wanaunganishwa watoto watano. Hapo pia sijaelewa.
 
Wadau Eid Mubarak,
Niende kwenye mada nina mtoto wa mdogo wangu ambaye nimekuwa nikimsuport katika elimu yake ya Sekondari. Huyu binti anasoma shule moja SIJUI niite ya serikali au ya kijamii, ni shule zile amabazo zilijengwa mahususi kwa ajili ya jamii za kifugaji ili kuisaidia ukuaji wa elimu kwenye maeneo husika.
Binti huyu mwanzo alifaulu kwenda shule ya kata maeneo ya kijijini kwetu kutokana na mazingira nikaona nifanye ninavoweza kumtoa maeneo yale na akiwa kidato cha kwanza nilifanikiwa kumuamishia shule ya bweni, ilikuwaje hii si mada ya leo.
Kifupi hii shule ina michango mingi sana nadhani Headmaster anakula kutokana na urefu wa kamba. Sasa shule zilivofungwa kwa ajili ya likizo fupi kidato cha nne hawakufunga. Leo ndo nimetumiwa mahitaji kwa ajili ya kumalizia miezi michache iliyobaki. Mojawapo ya michango iliyonistua ni kama ifuatavyo:-
1. Kitambulisho shilingi 10,000/= (Hiki wakati mtoto anaanza fomu one alilipa na hakijawahi tolewa mpaka leo)
2. Project ambayo haitajwi shilingi 30,000/=
3.Remedial 20,000/=
4. Cheti shilingi 8,000/=
5. Mahafari ya shule 20,000/=
6. Mahafari ya dini 10,000/=
7. Bima ya afya 10,000/= hii bima nikauliza kuna bima ya elfu 10? jibu nikwamba wanaunganishwa watoto watano. Hapo pia sijaelewa.
Yani anaitishwa michango yote hiyo akiwa mwaka wa mwisho?
 
Cheti kipi? Cha Dini au Cha Form 4?
Dini hawana utaratibu wa vyeti kwa imani yangu na endapo kuna cheti ni cha ubatizo ambacho ni bure, cheti cha pili ni cha ndoa kinalipiwa kwa kuwa ni mali ya serikali.
 
Leaving certificate hata cha dini alipie pia
Kuna haja gani kulipia cheti ili hali hii tuzo kutokana na gharama ambazo mwanafunzi anakuwa ameshalipia ikiwa ni pamoja na kukaa darasani miaka minne, nakumbuka kipindi cha nyuma kulikuwa na hela ya mtihani wa taifa kwa sasa sina uhakika kwa kuwa nimesomesha zaidi private ambako nadhani hizo gharama hujumuishwa huko huko
 
Aisee, kama ndo hivyo waseme tu HAKUNA ELIMU BURE YAANI UNATAKIWA KULIPA ADA.
 
Nadhani shuleni leaving certificates zipo softcopy, so, walimu hujaza details za mtoto, wanaprint na kugonga muhuri.

Sasa hapo kwenye kuprint na kujaza details za mwanafunzi ndo unakuta watu wanakula cha juu.

So, kaa kwa kutulia.
 
Back
Top Bottom