Kidini Israel na Trump wapo sahihi, kisheria Wapalestina wapo sahihi

Kidini Israel na Trump wapo sahihi, kisheria Wapalestina wapo sahihi

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Madai ya Waisraeli yanaanzia katika misingi ya kidini ambapo katika Biblia (kitabu kitakatifu wa Wakristu na Wayahudi), Kitabu cha Kwanza cha Nabii Musa kiitwacho Mwanzo (sura ya 12), kinaonesha jinsi Ibrahim alivyoitwa na Mwenyezi Mungu ili kumtumikia. Eneo hilo la Palestina ambalo zamani lilijulikana kama Kaanani, ndipo chimbuko la dini tatu kuu zenye msingi wa Ibrahim zilibuka. Dini hizo ni Uyahudi, Ukristu na baadaye Uislamu. Dini ya Wayahudi yenye misingi ya Biblia ya Agano la Kale, likianza na vitabu vitano vya Musa: Mwanzo, Kutoka, Hesabu, Mambo ya Walawi na Kumbukumbu la Torati. Ukristu ukianzia misingi kwenye Agano la Kale hadi Agano Jipya na Uislamu ukishika vitabu vinne vya Tourat ya Nabii Musa (a.s), Zabur ya Nabii Dawood (a.s), Injili ya Issa bin Mariam (a.s.) au Yesu na Kurani ya Muhamad (s.a.w).

Ibrahim, mwenyeji wa Uru wa Ulkadayo (Mesopotamia), leo Iraq, wa kabila la Waebrania anahama kutoka Iraq na kwenda Haran, Syria, na baadaye kuingia Kaanani (Uyahudi), ambapo Mwenyezi Mungu anamtokea katika njozi na kumwapia Ibrahimu kuwa, ardhi yote hiyo amepewa yeye na uzao wake na kuahidiwa Baraka. Yaani, kubarikiwa kwa kila atakaye mbariki na kwamba jamaa zote za dunia zitajibarikia. Pamoja na ahadi hiyo, Mungu anamwambia nabii Ibrahimu kuwa uzao wake utakwenda utumwani, Misri, kwa miaka mia nne (400) hadi kizazi cha nne, ndipo watakapookolewa na kupandishwa Kaanani.

Mizizi ya ugomvi huo inaanzia mnamo Karne ya Kumi na Tisa (19), wakati wa vuguvugu la utaifa la Uzayuni na Uarabu. Vuguvugu la Wayahudi lilianzishwa kuwa la kisiasa, mwaka 1892, dhidi ya Urusi na Ulaya. Mkakati ulianza kwa Wayahudi wote, popote walipo, kurejea katika nchi ya Palestina ambapo walipachukulia kuwa ndipo nchi yao ya asili. Katika kutimiza azma yao, Muungano wa Kizayuni na Taasisi za Fedha za Kiyahudi walihimiza uhamiaji na kufadhili ununuzi wa ardhi Palestina, chini ya utawala wa Ottoman na Uingereza. Mgongano huo ukianzishwa na Uingereza, kupitia Mikataba mitatu: Mkataba wa McMahon (chini ya Sir Henry McMhaon-Hussein); Azimio la Balfour la Novemba 2, mwaka 1917; na Mkataba wa Sykes-Picot, chini ya mwanadiplomasia wa Uingereza, Mark Sykes na Mfaransa, Frncois George-Picot.

Aidha, tangu hapo kulifuatiwa na milipuko ya mapigano ya mara kwa mara, kati ya Wayahudi na Waarabu, katika eneo la Palestina. Hakuna asiyekumbuka jinsi kiongozi wa Chama cha Nazi, Adolf Hiltler alivyowafanyia Wayahudi maangamizi makuu ya kupitia angamizo la Holocaust, ikiwa ni jitihada ya kulifuta taifa hilo. Azimio la Umoja wa Mataifa la mwaka 1947, liliridhia kugawanywa kwa nchi ya Palestina kwa Wayahudi na Wapalestina, ambapo Wayahudi walikubali na Wapalestina wakiungwa mkono na Umoja wa Nchi za Kiarabu, wakikataa na kusababisha kuzuka vita baina yao. Vita hivyo viliwafanya Wapalestina kuhama na kukimbilia nchi jirani za Kiarabu wakiwa wakimbizi yaani Al-Naqba. Makundi kwa makundi ya Wazayuni kutoka Ulaya Magharibi na Marekani walihamia Israeli. Zikabuniwa propaganda kuwa Wazayuni walikuwa katika mateso makali, chini ya utawala wa Adolf Hitler.

Miongoni mwa vitengo vilivyoundwa kuilinda Israeli, kilikuwa ni kikundi cha ulinzi na ujasusi, maarufu kikijulikana kama Shay ambacho wakati wa utawala wa Waingereza, wanachama wake walikuwa mkono muhimu wa harakati za chinichini za Mazayuni dhidi ya maeneo ya wenyeji wa asili ya Palestina. Wakazi asilia wa maeneo hayo ni Wafilisti na Wayahudi. Kitengo hiki kilipata msaada mkubwa, kutoka kwa wakala mkubwa wa Mazayuni, Zionist Congress, idara iliyoanzishwa mjini Zurich mwaka 1929.

Mara baada ya kuundwa taifa la Israeli, wahamiaji kutoka Ulaya na Marekani (Wazayuni) wakiongozwa na Shay walisuka mipango na kuendesha shughuli za kijasusi sehemu mbalimbali ulimwenguni. Kabla ya hapo, tokea mwaka 1923 hadi ilipofanikisha mpango wake, mwaka 1948, Shay ililenga kuanzisha taifa huru la Kizayuni katika maeneo ya Waarabu.

Na, mbinu iliyotumika wakati ule, ilikuwa kupandikiza watawala wa Kizayuni kimya kimya, ambao kwa taswira ya nje walionekana kama watumishi wa utawala wa Kiingereza, ambapo, wakati huo huo, walitumia fursa ya utawala kuandaa programu na kupanga mikakati dhidi ya Waarabu hasa wakazi wa maeneo hayo. Kwa ajili hiyo, taarifu za kijasusi zilikusanywa ili kutumika katika udanganyifu au propaganda na mipango ya utekaji nyara maeneo hayo.


Makala hii ni kutoka katika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi Sura ya 1, Uk 10.

0715865544/0755865544

IMG_20171212_212829.jpg
 
Kisheria wapalestina wapo sahihi!? How!? Sijaona popote ktk andiko lako ukiainisha ni sheria ipi hyo inayo itanabaisha Palestine kwa kile wanachokipigania ukiachilia mbali mkataba wa Montevideo

Angesema kidiplomasia sio kisheria. Yaani kwa hisani tu. Jerusalem ya Wayahudi. Yesu atatawala pamoja na Kanisa miaka elfu kutokea hapo. Lazima hili lianze kuandaliwa tokea sasa.
 
Diplomasia haina sheria?
Diplomasia huendeshwa na mikataba na sheria za kimataifa. Hakuna mkataba pale Jerusalem. Kama Sheria juu ya Jerusalem ingekuwepo ambaye angedai haki hapo ni Jordan sio Wapelistina. Mji huo ulikuwa makao makuu ya Jordan hadi vita vya Juni 67. Ukatekwa nusu.Vita vya 1973 ukakombolewa wote. Wapalestina wanadai wasichokistahili. Gaza na Ramallah vinawatosha.
 
so tufate dini au sheria ili tuone nani mkorofi??
 
Tatizo huu mgogoro wanatajwa waislam na wayahudi tu ila wakristo hawatajwi sijui ni kimkakati au bahati mbaya, nataka kujua wakristu walioa maeneo hayo ya Jerusalem wapo upande upi, wa Israeli au Palestinia?
 
Wanasema israel ni kitovu cha dini tatu uyahudi, ukristo na uislam, kwani uislam ulianzia israel?
 
Kiukweli hakuna sheria yoyote inayotoa nguvu kwa madai ya Wapalestina: Madai yao hayana nguvu wala ushahidi wa kihistoria! Sana sana wanalilia huruma ya umoja wa mataifa na mkataba wa amanj kati ya Misri na Israel wa mwaka 1973.
Hakuna kipindi chochote katika historia ambapo wapalestina waliwahi kuumiliki mji wa Yerusalemu! Yordan ndiyo ilikuwa inaumiliki kabla ya kupokonywa kwa nguvu na Israel
 
Uislamu umekuja miaka ya 600 AD , sasa wakajipendekeza kwa wayahudi na kudai ibrahimu alikuwa muislamu, kitu ambacho sio kweli, before 600AD hakuna historia,wala mabaki ya chembe ya historia yanayoonesha paliwahi kuwepo din inaitwa uislamu,

Waarabu walikuwa. Wanaabudu jiwe jeusi na kufanya ibada kwa mungu allah,
Ndio tamadun alizokuja kuzichukua muhamad na kuziboresha kisha kusema huu utakuwa UISLAMU

lakin uislamu hauhusiani hata kidogo na MANABII WAYAHUDI ,

HATA QURAN inataja neno ISRAEL lakini haijui nini maana ya israeli, lkn BIBLIA inakuambia mwanzo na chimbuko la neno ISRAEL,

Quran haitaji neno YERUSALEM , Lakin biblia imelitaja mara 5000 ,

Waislamu wanaongopewa kuwa YERUSALEMU NI YAO , wakati hapo Yerusalemu palijengwa HEKALU NA MFALME SULEMAN, hilo hekalu muundo wake , na vitu vilivyokuwepo ndani haviendan na UISLAMU hata kidogo,


Leo pamejengwa msikit wa Al aqsa, miaka ya karibuni, lakin bado kuna waislamu wanadanganywa HUO MSIKITI ALIJENGA SULEMAN
 
Usijitoe ufahamu wewe! Rejea vita ya Wafilisti na Wana wa Israeli Daudi alipomuuwa Goliath.
Kiukweli hakuna sheria yoyote inayotoa nguvu kwa madai ya Wapalestina: Madai yao hayana nguvu wala ushahidi wa kihistoria! Sana sana wanalilia huruma ya umoja wa mataifa na mkataba wa amanj kati ya Misri na Israel wa mwaka 1973.
Hakuna kipindi chochote katika historia ambapo wapalestina waliwahi kuumiliki mji wa Yerusalemu! Yordan ndiyo ilikuwa inaumiliki kabla ya kupokonywa kwa nguvu na Israel
 
Uislamu umekuja miaka ya 600 AD , sasa wakajipendekeza kwa wayahudi na kudai ibrahimu alikuwa muislamu, kitu ambacho sio kweli, before 600AD hakuna historia,wala mabaki ya chembe ya historia yanayoonesha paliwahi kuwepo din inaitwa uislamu,

Waarabu walikuwa. Wanaabudu jiwe jeusi na kufanya ibada kwa mungu allah,
Ndio tamadun alizokuja kuzichukua muhamad na kuziboresha kisha kusema huu utakuwa UISLAMU

lakin uislamu hauhusiani hata kidogo na MANABII WAYAHUDI ,

HATA QURAN inataja neno ISRAEL lakini haijui nini maana ya israeli, lkn BIBLIA inakuambia mwanzo na chimbuko la neno ISRAEL,

Quran haitaji neno YERUSALEM , Lakin biblia imelitaja mara 5000 ,

Waislamu wanaongopewa kuwa YERUSALEMU NI YAO , wakati hapo Yerusalemu palijengwa HEKALU NA MFALME SULEMAN, hilo hekalu muundo wake , na vitu vilivyokuwepo ndani haviendan na UISLAMU hata kidogo,


Leo pamejengwa msikit wa Al aqsa, miaka ya karibuni, lakin bado kuna waislamu wanadanganywa HUO MSIKITI ALIJENGA SULEMAN

Jackwillpower
Umesema yote na ziada na ushahidi wa hali ya juu sana ila atakuja mtu na mapovu bila ushahidi ila maneno mengiiiii
 
Hivi unajua document Wayahudi wanayoitumia kisheria kuonesha umiliki na mipaka ya nchi yao huko UN ni hicho kitabu kitakatifu cha Mussa.
Nilisoma sehemu kuwa jamaa alisimama na biblia UN akaitaja mpaka yote ya Israel kutoka katika biblia kisha akasema kuwa baba yao Ibrahimu hakuwai kuuza kwa mtu yyte
 
Back
Top Bottom