Kidonda kina siku 12 hakikauki na kupona, natumia dawa

Kidonda kina siku 12 hakikauki na kupona, natumia dawa

Anachoma..... hio ni njia ya zamani sana ili kuua bacteria
Mh!
Basi ndio maana hakijapona mpaka leo siku 12, bacteria hawauwawi kwa kuchoma bali kwa dawa za kupaka au za kumeza.

Ukikichoma ina maana unaweka jeraha jipya na hata uchafu unaingia. Hata kinapokauka haishauriwi kulibandua lile gamba mapema kabla halijaanza kujiachia lenyewe.

Kama mbinu hiyo ya kuchoma ndiyo anayoitumia (kukichoma) kwa kweli safari itakuwa ndefu sana. Hakuna haja ya kukichoma ni usafi tu ndiyo ilihitajika basi, lakini kwa sasa inabidi akisafishe na kupaka hiyo dawa aliyopewa na kukifunika kwa pamba safi wala asisumbuke kuchoma.
 
Kuna hii dawa pia ni nzuri ukipaka kwa kidonda
IMG-20241113-WA0000.jpg
 
Mungu mkubwa sana aisee
Yaani nilivyokua mdogo vidonda vyote nilikua navitupia mchanga tu kwisha habari yake kummmqe

Hakuna cha hospitali wala nini.

Sasa hv sasaaa ni miyeyu tu,maelekezo ya kina Janabi ni meeengiiii
 
Mungu mkubwa sana aisee
Yaani nilivyokua mdogo vidonda vyote nilikua navitupia mchanga tu kwisha habari yake kummmqe

Hakuna cha hospitali wala nini.

Sasa hv sasaaa ni miyeyu tu
😂😂Daa! Umenikumbusha mbali sana. Utoto una raha na karaha zake
 
Wakuu nauliza Kuna dawa ya kukausha kidonda?
Kifungeeeeeeeeeee na kitambaa cha mkononi au bandage hakikisha hakiingii maji kwa siku 3/4/5 mfululizo kitajifunga chenyewe wewe wa wapi? Yaan upo wapi muda huu?
 
Habari wakuu

Nina kidonda kwenye kidole kina siku 12, nilikipata baada ya kwenda kutibiwa Bawasiri clinic za Wakorea.

Unakiwekea dawa ya kuchoma moto ktk kidole mara Saba nichome kwa siku tano mfululizo Kila siku mara Saba.

Unaweka dawa ktk kidole hapo Kisha inachomwa inaungulia kidolea hadi iishe. Ilichomwa siku moja tu nikakataa kurudia Tena.

Sasa eneo hilo limeacha kidonda sasa naona hakiponi maana nilikuwa siweki dawa ya aina yoyote, mpaka kufika juzi nikaenda hospitali wakanipa dawa ya FLUCAMOX na tupe ya MUPIROCIN OINTMENT bp 2%

Leo siku ya tatu Sasa kidonda kama kinataka kukauka ila kinakua na usaha kidogo

Wakuu nauliza Kuna dawa ya kukausha kidonda?

View attachment 3151499
Mkuu chukua jani la huu mmea ufikiche kisha dondoshea hapo maji yake, au fikicha kisha fungia hapo kwenye kidonda.

Ukiweza fungia hapo kwa usiku mmoja alafu asubuh utoe utaona siku ya kwanza panaanza kukauka penyewe
images (9).jpeg
images (8).jpeg
images (10).jpeg
 
Mkuu chukua jani la huu mmea ufikiche kisha dondoshea hapo maji yake, au fikicha kisha fungia hapo kwenye kidonda.

Ukiweza fungia hapo kwa usiku mmoja alafu asubuh utoe utaona siku ya kwanza panaanza kukauka penyewe
View attachment 3151560View attachment 3151561View attachment 3151562



Hii Dawa huitwa kakulula Kwa watu wa Bukoba.

Kuhusu kidonda , Tumia vidonge vya kumeza na uzingatie Usafi Sana

Ni vizuri ukiweza ukawa unakifunika ili kuzuia kujitonesha.

Na kuna mdau kauliza kuhusu sukari matumizi ya sukari jaribu kuyapunguza.
 
USHUHUDA JINSI NILIVYOPONA KIDONDA CHANGU
Yalishawahi nikuta. Kwanza
Pole sana kwa changamoto ya kidonda. Mi binafsi nilipata jeraha kubwa kidoleni, kiasi nilikwenda hospital ya serikali mwenge Dsm lakini wakasema napaswa kushonwa sababu kidole kimechanika sana nyama zipo wazi, niliandikiwa sindano 5 za antibiotics na tetenasi gharama ikaea Kama elfu 50,
Nikawaza nikaona hapana nikaenda maabara ndogo nikaandikiwa vidonge vya antibiotics, nikachomwa sindano ya tetenasi na nikapakwa dawa ya chenga chenga ili kukausha kidonda ila nilimuuliza dokta "dawa gani kama chenga chenga umenifunga kwa bandeji"? Akanijibu kuwa ni dawa inayotumika kumtibu kidonda haraka mtoto akitahiriwa basi nikalipiwa elfu 3. Tu + dawa jumla kama elfu 5 tu.
Nilirudi home nilikas siku 4 tu kidonda kikafunga na kukauka kabisa mpaka Sasa Nipo vzuri naendelea na ujenzi wa taifa
NB TUMIA NJIA YA HOSPITAL achana na kienyeji usije jitafutia matatizo makubwa

nitakupa maelekezo uende mahali utibiwe kwa maabara nicheki au nipatie no zako
 
Kapime sukari kwanza. Kama hauna sukari tafuta asali halisi. Pakaa asali hapo,chukua pamba ipake asali iweke hapo kwenye kidonda,kisha funga bandeji.Pisiloweshwe maji kwa muda wa siku tatu.Baada ya siku tatu fungua bandeji halafu tuletee majibu.
 
Hii Dawa huitwa kakulula Kwa watu wa Bukoba.

Kuhusu kidonda , Tumia vidonge vya kumeza na uzingatie Usafi Sana

Ni vizuri ukiweza ukawa unakifunika ili kuzuia kujitonesha.

Na kuna mdau kauliza kuhusu sukari matumizi ya sukari jaribu kuyapunguza.
Nje ya vidonge akiweka haya majani ni mara 1 tu ataona mabadiliko ya haraka kesho yake
 
Una shika sana maji
Ndio...maana nimkono wakushoto kujisaidia haha kubwa lazima nitumie mkono wakushoto Sasa naufunga na nailoni ila maji kidgo sana yapenya najoto pia la nailoni joto linakuepo kidonda kinakua kibichi bichi
 
Back
Top Bottom