Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Raia wema wanaochukia vitendo vya kinyama baada ya msako mkali kuanzia May 31, 2024 hadi usiku wa kuamkia leo June 19, 2024 wamefanikisha kukamatwa kwa Watu tisa wakiwa na viungo vinavyodhaniwa ni vya Mtoto Albino Asimwe Novart (aliyeuawa Wilayani Muleba Mkoani Kagera) wakiwa wamehifadhi katika vifungashio vya plastiki wakitafuta Mteja Mkoani Kagera.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Polisi, David Misime imesema Watuhumiwa waliokamatwa ambao wameeleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hili ni pamoja Baba mzazi wa Mtoto huyo aitwaye Novart Venant, Desideli Evarist ambaye ni Mganga wa jadi Mkazi wa Nyakahama, Elipidius Rwegoshora Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bugandika ambaye anadaiwa kumfuata na kumshawishi Baba mzazi wa Mtoto ili wafanye biashara ya viungo vya binadamu na pia anatuhumiwa kuwa ndiye aliyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga.

Watuhumiwa wengine ni Dastan Kaiza Mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman Mkazi wa Nyakahama, Gozibert Alkadi Mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Rwenyagira Burkadi Mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Ramadhani Selestine Mkazi wa Kamachumu na Nurduni Hamada Mkazi wa Kamachumu.

“Jeshi la Polisi linatoa kutoa onyo kali kwa Watu wanaoendekeza imani za kishirikina ikiwemo kupiga ramli chonganishi wakiaminishana kwamba wanaweza kupata utajiri kwa njia za kishirikina kuacha tabia hizo”
#MillardAyoUPDATESView attachment 3020915
Paroko?
 
Mimi kuna jambo sjaelewa yaaani wameua mtoto kwa imani za kishirikina na kuanza kutafuta wateja wa kuwauzia viungo vya huyo mtoto Inamaana waliua kabla hawajapata mteja?,Lingine mbona wahusika ni wengi sana kiasi hicho?.
Ishu ya kukosea kutaja cheo cha mtu kumbe sio chake mbona kawaida tu,Mbona Samia Suluhu aliteua mtu kumbe alishafariki?.
 
Watu kama hawa wakikamatwa inapaswa wawe wananyongwa kihadhara tena tukio likirushwa live na television ya taifa.

Inatia ukakasi sana
 
Msemaji wa jeshi la Polisi kachemka na kwenye hili litamgharimu.
Aliyekamatwa siyo Paroko msaidizi na wala siyo Padre.
Ni mraibu ambaye Paroko msaidizi alisoma naye na aliamua kumchukua Parokiani ili aweze kusaidiwa.
Hivyo kumtaja kama Baba Padre ni watu kutokutimiza majukumu yao katika kufuatilia mambo .
Paroko anaitwa Deodatus Tibakwasa na msaidizi ni Fr.Mathias.
Kifupi.
Nilijua tu kanisa haliwezi kukubali aibu hii lazima watafute njia ya kujinasua
 
Kuwakamata hao wahalifu ilikuwa ni kazi nyepesi sana kwa polisi.

Watu wanaoamini ushirikina huwa ni wajinga hawanaga akili ya kupanga tukio bila kuacha trace.

Nina uhakika kipindi wanamuiba mtoto walikuwa na simu zao mfukoni. Na hata kipindi wanamuua mtoto simu zilikuwepo.

Polisi hawajatumia hata nguvu ya kuwajua na hata kuwatafuta. Wamecheza na simu zao tu
Jidanganye kuwa we ni Bingwa muuaji utayeua bila kukamatwa, dola haisinzii na damu ya Mtu ni nzito kuliko maji.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
mama-pic.jpg
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi limewakamata watu wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya mtoto mwenye ualbino Asimwe Novath (2).

Mei 30, 2024 Asimwe anadaiwa alichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Muleba mkoani Kagera na juhudi za kumtafuta hazikuxzaa matunda hadi hapo Juni 17, 2024 mwili wake ulipopatikana ukiwa katika mfuko wa sandarusi huku baadhi ya viungo vikiwa vimenyofolewa.

Waziri Masauni amesema watuhumiwa hao wamekamatwawakiwa na vithibiti vya kutendea kosa hilo na kufafanua kuwa hawajabahatisha katika kuwakamaa watu hao.

“Hakuna hata mmoja ambaye amehusika na mauaji ya binti huyu malaika wa Mungu atakayrepona, tumefikia pazuri na kitakachofanyika itakuwa fundisho kwa wahalifu wengine, tupo vizuri katika kukabiliana na uhalifu na ndiyo maana hakuna mtu atakayefanya uhfifu asipatikane,” amesema Masauni

Credit: Bongo 5

___
Kupitia taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime imewataja watuhumiwa waliokamatwa ambao walieleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hilo ni pamoja Baba mzazi wa mtoto huyo aitwaye Novart Venant, Desideli Evarist ambaye ni mganga wa jadi mkazi wa Nyakahama, Elipidius Rwegoshora Paroko Maidizi wa Parokia ya Bugandika ambaye anadaiwa kumfuata na kumshawishi Baba mzazi wa mtoto ili wafanye biashara ya viungo vya binadamu.

Paroko huyo pia anatuhumiwa kuwa ndiye allyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga.

Watuhumiwa wengine ni Dastan Kaiza mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman mkazi wa Nyakahama, Gozibert Alkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Rwenyagira Burkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Ramadhani Selestine mkazi wa Kamachumu na Nurduni Hamada mkazi wa Kamachumu.

Pia soma:
ukiona hadi polisi wametangaza hivyo, jua wana uhakika, na paroko atakuwa ameminywa maeneo fulani akafunguka hadi kuonyesha ushahidi mwingine.hawawezi kukurupuka kugusa dini.

huwa nasema, ukiona mtu ana ujasiri wa kuua albino, jua sio mara yake ya kwanza, jua alishawahi kufanya na akapona, kwasababu hakuna mwenye akili timamu anayeaminikwamba atafanya hicho kitendo halafu asikamatike. hata wanaopona ni basi tu ila hakuna anayeweza kuua albino halafu polisi wasimkamate, hayupo. na wanaofanya hivyo jua walishawahi kufanay wakapona hivyo wanafikiri hawatajulikana kama walivyokwepa mkono wa sheria awali.
 
Mahakama itachunguza ukweli wote
Mahakama isiishie kwa hawa watuhumiwa tu wakibanwa korodani list inaweza kuongezeka, kawaida biashara yoyote huwa na mtandao, hapa ndo pa polisi kuanzia, hasa wakimning'iniza mganga wa jadi kichwa chini miguu juu huku korodani zimefungwa kilo kumi kumi kila moja mganga atataja wateja na waganga wenzake wote wenye madili hayo ya kuua albino. Waganga lazima wanajuana na kukutana.

Hapa inabidi mtandao mzima utafutwe na polisi tukio kama hili lisijirudie tena maana kuua albino ni laana na fedheha kwa nchi nzima. Hii dhambi hufika mbali hata tukienda uzunguni kuomba mikopo wazungu hawatavunga watasema ooh wewe unatoka Tanzania? Utasema ndiyo, kisha watasema, ile nchi inayoua albino kwa ujinga kama wa watu wa old stone age , utabaki kimya jicho litakutoka kodooo! Mikopo na safari za uzunguni bye bye!!
 
Back
Top Bottom