Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Msemaji wa jeshi la Polisi kachemka na kwenye hili litamgharimu.
Aliyekamatwa siyo Paroko msaidizi na wala siyo Padre.
Ni mraibu ambaye Paroko msaidizi alisoma naye na aliamua kumchukua Parokiani ili aweze kusaidiwa.
Hivyo kumtaja kama Baba Padre ni watu kutokutimiza majukumu yao katika kufuatilia mambo .
Paroko anaitwa Deodatus Tibakwasa na msaidizi ni Fr.Mathias.
Kifupi.
Acha kutoa ufafanuzi uchwara hapa.

Huyo paroko msaidizi ajitokeze mwenyewe hadharani.

Kwani wanaparokia si wanamjua paroko wao msaidizi ni nani?

Je jeshi la polisi limekurupuka kusema kwamba huyo mtuhumiwa ni paroko msaidizi?
 
Mahakama isiishie kwa hawa watuhumiwa tu wakibanwa korodani list inaweza kuongezeka, kawaida biashara yoyote huwa na mtandao, hapa ndo pa polisi kuanzia, hasa wakimning'iniza mganga wa jadi atataja na waganga wenzake wenye madili hayo ya kuua albino.

Hapa inabidi mtandao mzima utafutwe na polisi tukio kama hili lisijirudie tena maana kuua albino ni laana na fedheha kwa nchi nzima.
Police wanajua jinsi ya kufanya kazi.
Kuwa na subra , kuwa na amani na vyombo vya usalama ukweli utadhiri muda sio kitambo
 
Hii comment nimeikuta sehemu nyingi sana, lakini inafikirisha. Taarifa ya polisi imetaja "Paroko msaidizi" na ili awe Paroko msaidizi lazima awe padri tena mwandamizi. Nyie mnaosema "ni kijana aliyekuwa nalelewa tu" mnataka kusema polisi wamekurupuka?? Kwasababu wao ndio waliomtaja kwenye taarifa yao.

Kama wamekurupuka maana yake tusubiri waje kuomba radhi na kusahihisha makosa yao lakini kwasasa kinachosomeka ni paroko msaidizi
Face saving mkuu,hawataki kanisa moja takatifu la mitume lichafuke,maana uchafu huko ni mwingine,kuanzia kulawiti watoto mpaka kulawatiana wao na Sasa wanahalalisha ndoa kabisa,Sasa ukiongeza na hili la albino,doh!!!..jk aliwachana 'baadhi yenu mnauza unga'..wakanuna,wakaitisha kongamano la vijana Koko bichi
 
KUna tetesi
Aliyekamatwa siyo Paroko msaidizi na wala siyo padre.
Ni mraibu ambaye paroko msaidizi alisoma naye aliamua kumchukua parokiani ili aweze kusaidiwa.
Hivyo kumtaja kama baba padre ni watu kutokutumiza majukumu yao katika kufuatilia mambo .
Paroko anaitwa Deodatus Tibakwasa na msaidizi ni Fr.Mathias.



Nimeitoa group Fulani huko.
 
Baba Asimwe alikuwa na njaa kali kama ya Sudan au Gaza mganga na paroko badala ya kumpa msosi, labda walimpa "cha Arusha" , advance payment na dili la kuua mwanae, yaani I can not imagine, jinsi I love my
kids na ninavyowanunulia majezi ya timu yao pendwa ya Azam wakavaa na kupendeza, bora nife maskini kuliko utajiri wa shetani.

Haya majitu yasiuwawe maana kifo kipo, dawa yao yakishahukumiwa life sentence yafungwe plau na kulimishwa kama ng'ombe kila siku hadi siku yatakufa natural death.
Hata mimi siamini, alafu taarifa zinasema waarifu wamekamatwa wakitafutq mteja means pesa bado haijapatikana sasa Umtoe mtoto wakamuue kweli ni jambo gumu sana
 
Hata mimi siamini, alafu taarifa zinasema waarifu wamekamatwa wakitafutq mteja means pesa bado haijapatikana sasa Umtoe mtoto wakamuue kweli ni jambo gumu sana
Wapuuzi sana hao. Tamaa na roho mbaya za kibinafsi zitawapoteza. Hawa haina haja ya kwenda kula ugali jela.
 
Kuua mtu inahitaji uwe na roho ya ibilisi.

Mimi hata kuku napata shida sana kuchinja.
Aisee hata mimi kuchinja hata bata napata tabu.
Hao watu waliofanya hicho kitendo kila adhabu ninayofikilia naona ni nyepesi kwao, sijui wasafilishwe wapelekwe kwenye kila kisiwa cha nyoka watupwe kule
 
Baba Asimwe alikuwa na njaa kali kama ya Sudan au Gaza mganga na paroko badala ya kumpa msosi, labda walimpa "cha Arusha" , advance payment na dili la kuua mwanae, yaani I can not imagine, jinsi I love my
kids na ninavyowanunulia majezi yao ya Azam wakavaa na kupendeza, bora nife maskini kuliko utajiri wa shetani
Mkuu kama kweli huyo Baba yake na mtoto kafanya hivyo labda ana tatizo la akili au alilogwa na huyo mganga
Mimi mtoto wangu akiumwa tu najisikia vibaya, aisee nashindwa kuamini kama mzazi unaweza kumkatili mtoto wako kiasi hicho
 
WhatsApp Image 2024-06-19 at 21.14.20.jpeg




 
Back
Top Bottom