Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Aisee paroko msaidizi! Anakosa nini kutoka shirikani au jimboni? Hapa angekuwa mchungaji wa kilokole waromani katoriki wangesema makanisa ya mabati lakini huyu itasemwa kuwa asiliusishe kanisa. Hapa, kuna la kujifunza binadamu si wa kumwamini. Moyo wa msitu. Si kila kosa la mtu mmoja lihusishwe na taasisi mzima anayotokea
 
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Raia wema wanaochukia vitendo vya kinyama baada ya msako mkali kuanzia May 31, 2024 hadi usiku wa kuamkia leo June 19, 2024 wamefanikisha kukamatwa kwa Watu tisa wakiwa na viungo vinavyodhaniwa ni vya Mtoto Albino Asimwe Novart (aliyeuawa Wilayani Muleba Mkoani Kagera) wakiwa wamehifadhi katika vifungashio vya plastiki wakitafuta Mteja Mkoani Kagera.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Polisi, David Misime imesema Watuhumiwa waliokamatwa ambao wameeleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hili ni pamoja Baba mzazi wa Mtoto huyo aitwaye Novart Venant, Desideli Evarist ambaye ni Mganga wa jadi Mkazi wa Nyakahama, Elipidius Rwegoshora Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bugandika ambaye anadaiwa kumfuata na kumshawishi Baba mzazi wa Mtoto ili wafanye biashara ya viungo vya binadamu na pia anatuhumiwa kuwa ndiye aliyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga.

Watuhumiwa wengine ni Dastan Kaiza Mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman Mkazi wa Nyakahama, Gozibert Alkadi Mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Rwenyagira Burkadi Mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Ramadhani Selestine Mkazi wa Kamachumu na Nurduni Hamada Mkazi wa Kamachumu.

“Jeshi la Polisi linatoa kutoa onyo kali kwa Watu wanaoendekeza imani za kishirikina ikiwemo kupiga ramli chonganishi wakiaminishana kwamba wanaweza kupata utajiri kwa njia za kishirikina kuacha tabia hizo”
 
Mtoto analia baba baba..mama..mama..yani unaendelea tuu kushika panga sijui kisu...unapiga na kitu kizito anazimia bado nguvu unazo tuu..unaanza kukata kiungo kimoja na kingine upo tuu...hapa ndipo hata wale wanaouliza Mungu huwa yuko wapi nawaelewa...hapo ingetakiwa kutokee muujiza wa Mungu na giza totoro halafu hao watu wajikute katikati ya maji yenye mamba...
 
Sijawazungumzia hao waliokamatwa wala mtu yeyote specific ila nimezungumzia tukio kwa ujumla na uvumi unaosemwa kwamba matukio hayo husukumwa zaidi na imani za kishirikina ili mtu kujipatia utajiri au madaraka,hayo ndiyo masikitiko yangu.
Nimekuelewa
 
Back
Top Bottom