Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

SASA kADA ngoja mimi niachane na wewe maana inaonekana unaanza kukosa busara hata wadhamini wako wataanza kukushangaa mkuu

kakindo wewe kuwa against na mimi ni kama entertainment kwangu na ndio maana nishawapasha hakikisheni msije mkakimbia. hiyo ya booty camp haikuhusu wewe kabisa, bali inamhusu mgaya na anajua mwenyewe kwamba anahitajika huko booty camp ! sasa hata usiondoke, wewe kaa hapa tuhakikishe mbowe anahojiwa juu ya kauli zake !

wewe huna haja ya kwenda booty camp, anayehitajika ni huyo shahiba wako mgaya ! wanamuhitaji as fast as he can ! tena akimbie huko !
 
kakindo wewe kuwa against na mimi ni kama entertainment kwangu na ndio maana nishawapasha hakikisheni msije mkakimbia. hiyo ya booty camp haikuhusu wewe kabisa, bali inamhusu mgaya na anajua mwenyewe kwamba anahitajika huko booty camp ! sasa hata usiondoke, wewe kaa hapa tuhakikishe mbowe anahojiwa juu ya kauli zake !

wewe huna haja ya kwenda booty camp, anayehitajika ni huyo shahiba wako mgaya ! wanamuhitaji as fast as he can ! tena akimbie huko !

Kada

Suala nililokwambia kwanini Mbowe ahojiwe?

Kwani mangapi yamefanyika Tanzania na hatupati majibu yake? Kuna meremeta, kuna tangold kuna migodi kibao ambayo yanamumaliza mtanzania(mzawa). Mimi sioni kama la mbowe lingetakiwa kuwa la kwanza kuna mengi bado hayajafanyika mkuu
 
SASA kADA ngoja mimi niachane na wewe maana inaonekana unaanza kukosa busara hata wadhamini wako wataanza kukushangaa mkuu

KUna wengi wanatamani hata hakuwa upande wao huko ccm ... yaani amekuwa kama REv wright kwa Barack Obama.

Yaani mimi napenda aendelee kujiabisha yeeye na mafisadi wenzake huko ccm.
 
hata wadhamini wako wataanza kukushangaa mkuu

Originally, Kada alikuwa Chadema au upinzani, baadaye akahamia upande wa pili baada ya kuudhiwa na watu huko, sasa eti amedhaminiwa na ccm? Kwa hiyo ina maana zamani alikuwa amedhaminiwa na upinzani?
 
HIVI HAMUONI HATA MEMBE MWENYEWE ALIISHIA KUKANUSHA KAMA MTU AMBAYE AMEFUMANIWA HALAFU ANADAI 'MBONA MMETUKUTA PEMBENI YA KITANDA CHA GUEST HOUSE TUKIWA TUMEVAA NGUO, HAKIKISHENI TULIKUWA TUNAZINI ' WAKATI HUO HUO UNASIKIA HARUFU YA KONDOM ZA CHOCOLATE CHUMBANI NA MASHUKA VURURUVURUVURU!!! NA WAFUMANIWA HAWANA NGUO ZA NDANI!! UNAHITAJI USHAHIDI GANI TENA?

TATIZO MEMBE YEYE MWENYEWE NI MWANASHERIA UCHWARA. ANADHANI WOTE NI WACHWARA KAMA YEYE. INABIDI UTMIE COMMON SENSE. HIVI KWA AKILI YAKE ANADHANI UTETEZI ALIOTOA UMEONDOA SHAKA KWAMBA SERIKALI NA CCM WAMEMUUA YULE MZEE? LAZIMA UWE KICHAAA KUAMINI MEMBE AMEFANIKIWA KWA HILO.

KAMA YEYE NI MWANASHERIA KUNA KITU KINA ITWA 'RES IPSA LOQUITUR' YAANI "The facts/thing speaks for itself". kwa maana kwamba kama si mkono wa hila kile kilichotokea kisingkuwepo. Kifo cha huyu mzee hakijatokea kwa mapenzi ya mungu bali mapenzi ya CCM na serikali yake. Membe mwenyewe anajua yanaweza kumkuta ya balali akileta uzuri. Ndiyo maana unaona anatetea hata ujinga huku akijua ni ujinga.

ndo taabu ya kuwa mwanasiasa. lazima uwe mjinga. Unaweza kula mavi ukaita uji hata kama daktari akapima maabara akathibitisha kuwa ni mavi, mwanasiasa atakwambia ni uji!!
 
Prof Baregu ataka Interpol wachunguze kifo cha Ballali

Na Jackson Odoyo

SIKU moja baada ya serikali kusema kuwa hakuna sababu ya kuchunguza kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu nchini (BoT), Daudi Ballali, Mhadhiri Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwasiga Baregu amesema kuna haja ya tukio hilo kuchunguzwa.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili jana, Profesa Baregu alisema serikali inatakiwa ku kubali kufanya uchunguzi juu ya suala hilo na kama wao hawawezi watumie wataalamu wa Polisi wa Polisi wa Kimataifa (Iterpol).

Alisema suala la uchunguzi wa kifo cha Ballali bado lina umuhimu kwasababu yawezekana serikali haikuhusika, lakini watuhumiwa wengine katika suala lake wakahusika ili kupoteza ushahidi, kwa sababu walifahamu kuwa Balali alikuwa shahidi muhimu katika suala la Akaunti ya ya Madeni ya Nje (EPA).

Alisema suala hilo likipuuziwa litasababisha watuhumiwa hao wazidi kujificha kwani baadhi ya wananchi wanaamini kuwa Balali hakuchuwa fedha peke yake katika sakata hilo na amekufa kabla hajajibu tuhuma zilizo kuwa zikimkabili.

�Serikali haiko makini katika suala hili, kwa sababu kama kweli wanadai kuwa hawakuhusika, kwanini wasitoe hata historia ya ugonjwa kuanzia alipokuwa BoT hadi alipoondoka kwenda kutibiwa,� alisema Profesa Baregu

Alisema kitendo cha serikali kuendelea kuzuia uchunguzi wa kifo chake, inazidi kupoteza ushahidi juu ya suala la EPA na kwamba ikiendelea na ukimya huo itadhahirisha kuwa wanaohusika katika sakata hilo wataendelea kuneemeka na fedha hizo na hazitapatikana na kabisa .

Profesa alisema kutokana na uzito na unyeti wa suala hilo wananchi hawataacha kuhoji na kuendelea kupoteza imani na serikali yao, jambo ambalo ni hatari kwa mfumo wa utawala.

Juzi serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilitoa kauli zilizozidisha utata juu ya suala la kifo cha Balali kwamba, haina sababu ya kufanyia uchunguzi wa kifo cahe kwa kuwa alikuwa mgonjwa siku nyingi.


Nafikiri yupo sahihi..
 
Last edited by a moderator:
duh maskini Dr BALLALI,yaani almost 5days tokea amefariki watu bado wanashindana tu.
i wish atujie ndotoni wana JF sote kwa pamoja usiku mmoja na atueleze KISA NA MKASA yalomfika mpaka akafariki dunia hapo itakuwa mwisho wa maongezi
.
 
Nimejaribu bila mafanikio kuipata link ya hii post... aliyeiweka naomba ajikumbushe maana huu ndio wakati mwafaka....

WanaJF,

Nianze kwanza kwa kuwakumbusha jinsi ambavyo JF ilifanikiwa sana kwa kuwekwa barua ya Balali ya kujiuzulu hapa JF na story hiyo ikaenea kwenye vyombo vya habari Tanzania kiasi cha kufikia kina Saliva na wenzake kuchanganyikiwa na kuanza kukana hizo taarifa, habari nyingine zinazofikia vyanzo vya habari vya JF ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa Balali akafanya interview na kipindi maarufu cha uchunguzi marekani cha 60 minutes.

Ikumbukwe pia kuwa mimi binafsi nimekuwa anti-Balali mkuu katika jamvi hili na mara kwa mara nimekuwa namuombea hadharani aende hell maana ndiko wezi na mafisadi wanastahili. Pamoja na haya yote, ujio wa afisa usalama mkuu wa serikali ya Kikwete RO hapa marekani kumjulia hali Balali na yale aliyosema baada ya kuonana naye vilinifanya nibadili uamuzi wangu kwa muda na kucheza the same game inayochezwa Tanzania.

Nilijiuliza sana maswali kuwa kwa nini RO asifurahie kuendelea vyema kwa Balali na aonekane kushangaa kumuona akipata nafuu kwa haraka? Kwa nini serikali ya Kikwete ilikataa kujiuzulu kwa Balali na baada ya muda mfupi Kikwete akatangaza kwa misifa mingi kuwa amemfuta kazi Balali? Haya yote yalipelekea nimtafute Balali ili nijue kulikoni.

Kwa vile kwa sasa hairuhusiwi kusema kama Balali anaendeleaje kiafya na yuko wapi hapa US, naomba usiniulize maswali kuwa nilikutana naye wapi maana sitakujibu. Yafuatayo ni maneno ya Balali mwenyewe kuhusu ugonjwa wake na kwa nini alikimbilia hapa Marekani:

1. Balali anadai kuwa aliitwa Dodoma bila sababu maalumu
2. Anashangaa kuwa aliyoulizwa Dodoma angeulizwa hata Dar
3. Anashangaa kwa nini alisindikizwa na mkubwa toka Dodoma
4. Alishangaa sana usiri uliondelea alipokuwa Dodoma
5. Anakumbuka kuwa alikunywa na kula Dodoma na kwenye ndege
6. Anadai kuwa matatizo yake yalianza haraka baada ya Dodoma
7. Mengine ni mambo ya kitabibu......

Binafsi simuonei huruma sana Balali lakini ningefurahi kuona akitoa story yake kwenye 60 minutes. Alichokifanya Balali ni kibaya na kinastahili adhabu kubwa lakini sio ya kujaribu kutoa maisha yake ili asitoe siri ya wizi mkubwa uliofanywa wakati wa uchaguzi wa ccm na baadaye taifa mwaka 2005.

Balali anastory kubwa sana ya kutoa na ninafanya juhudi zote kwa ushirikiano na baadhi ya watu ili story yake isikiwe na watanzania woooote.

Swali kubwa ni kuwa, kwa nini kuna watu wangependa sana kumuona Balali akiwa kwenye jeneza? Nani anafaidika sana na kifo cha mtu huyu (nitamwita fisadi akipona vizuri) ?

Mtega hutegwa! Siku moja kabla ya kuanza kutapika kwa nguvu Bw. Balali inadaiwa alienda kupata msosi wa nguvu na mmoja wa viongozi wastaafu katika hali ya "kucatch up" na mambo yanayoendelea.

Ilikuwa ni baada ya kutoka huko ndiyo maumivu ya tumbo yalipoanza na kuanza kutapika. Kwa vile, ujanja ni kuwahi siyo kupata, Balali alijumlisha moja na moja na jibu likaja kuwa ni mbili, akachukua tiketi yake akaruka na kuwahi hospitali!

Kwanini hakutaka kwenda hospitali ya Taifa au yoyote nchini? Balali alihisi chochote kilichomsumbua kilitokana na chakula...Ukichanganya na madhaifu mengine aliyokuwa nayo... ilikuwa arudishe namba kiulaini kabisa! Lakini wakati mwingine dua la kuku halimpati mwewe! Jamaa amesavaivu, so far.

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kutokea.

a. Balali kudai ukimbizi ambao anatengenezewa na serikali ya Tanzania, kwa jinsi wanavyomtengeneza vibaya na hivyo akasema "fear of persecution" ambayo ni ground for political asylum.

b. Balali kutoweka ki namna. Katika ulimwengu wa plastic surgeries na Identity protection, Balali anaweza kubadilishwa sura na wajihi wake kiasi kwamba itakuwa vigumu kumfahamu ukiondoa kichwa chake ambacho jinsi kilivyoumba sidhani kama kuna Daktari anaweza kukibadilisha.

c. Kwa vile hakuna mkataba wa extradition kati ya marekani na Tanzania (sidhani kama upo?) Balali hatalazimishwa kurudishwa Tanzania isipokuwa kwa makubaliano maalum.

d. Balali anajiandaa kujibu mashambulizi na kurusha nyavu yake pana ya ushahidi na kusema nani alifanya nini. Kama kuna watu wanadhania Balali alifanya yote hayo bila kucover his behind, washtuke. Balali, anajua nani na nini kilifanyika kwani SITOSHANGAA kuna nakala za vimemo kadhaa toka kwa watu mashuhuri na baadhi ya mafaili yao yaliyokuwa BoT aliyahamisha na kuyaweka mahali fulani akijua kuwa siku moja anaweza kupata kibano
 
Na mimi naanza kukumbuka japo waligusia gusia na hii habari sehemu kubwa ya source ilikua ni JF, turudi nyuma tutaanza kupata picha angalao kidogo kidogo. Membe anapozungumza haya naona kama ANAWEWESEKA

http://www.raiamwema.co.tz/08/01/02/3.php

Afya ya Ballali bado

Waandishi Wetu
Januari 2, 2008
Yaelezwa anakula kwa mashine



HALI ya afya ya Gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Ballali, inazidi kutatanisha na kuna habari kwamba hakuwa anaweza kula chakula katika hali ya kawaida, na haijafahamika mara moja kama hali hiyo kwa sasa imetengamaa ama la.

Vyanzo mbalimbali vya habari kutoka Marekani na Dar es Salaam, vinasema kwamba hali yake ya imekuwa ya kutatanisha kabla na baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa.

Habari zinasema kwamba Ballali (65) pamoja na mambo mengine, alifanyiwa upasuaji mkubwa katika moja ya hospitali kubwa nchini Marekani iliyopo Jimbo la Massachusetts, jiji la Boston, lakini hakuna taarifa rasmi za hasa alifanyiwa upasuaji gani.

Akizungumza na RAIA MWEMA kwa simu kutoka Washington D.C, Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Ombeni Sifue, alisema jana Jumanne kwamba Balali bado yuko hospitali Boston, lakini hakuwa anafahamu ni hospitali gani aliyolazwa na wala hana taarifa za ugonjwa unaomsumbua.

"Ninavyojua yuko hospitalini Boston na hali yake inaendelea vizuri japo kwa taratibu sana. Pamoja na kuwa taarifa za ugonjwa wa mtu ni za siri, sifahamu anasumbuliwa na nini na kwa kuwa sijawahi kwenda kumuona sifahamu alifanyiwa upasuaji wa aina gani," alisema Balozi Sifue.

Imeelezwa kwamba Ballali ambaye hadi sasa kujiuzulu kwake hakujathibitishwa na Serikali, anaendelea na matibabu lakini hakuna dalili ya lini hasa atapata nafuu na kuweza kuendelea na kazi, hali ambayo ilimlazimu kuchukua jukumu la kujiuzulu nafasi yake.

Hata hivyo, habari zisizo rasmi zinaeleza kwamba Ballali alitoka hospitali na kwa sasa yuko katika moja ya hoteli jijini Boston huku akiendelea kupata uangalizi wa madaktari wa hospitali hiyo.

Imeelezwa kuwa amekuwa akila chakula kwa msaada wa vifaa maalumu, lakini Balozi Sifue alisema: "Sina taarifa za undani wa matibabu anayoyapata, lakini ninavyojua anapata nafuu pole pole."

Hadi sasa Serikali haijatoa taarifa rasmi kuhusiana na undani wa ugonjwa wa Ballali, pamoja na kuthibitisha kwamba anaendelea na matibabu katika hospitali hiyo ya Boston.

Vyanzo visivyo rasmi vinaeleza kwamba Ballali anaweza kuwa amefanyiwa upasuaji wa kichwa katika harakati za kupunguza ama kuondoa tatizo linalomsumbua kwa muda mrefu sasa na pia kwamba amefanyiwa uchunguzi wa damu.

"Upo uwezekano wa kuwa amefanyiwa upasuaji wa kichwa kutokana na matatizo yanayomsibu lakini pia wagonjwa wa aina yake wanaweza kufanyiwa upasuaji wa tumbo na kubadilishwa bandama ili kumpa afueni," kinaeleza chanzo chetu ndani ya Serikali.

Imeelezwa kwamba serikali inaendelea kugharamia matibabu ya Ballali kwa kuwa bado anatambulika kisheria kuwa Gavana wa BoT, hadi hapo Rais Jakaya Kikwete atakapokubali kujizulu kwake na kuteua mtu kushika nafasi hiyo.

Imethibitishwa kwamba Rais Kikwete hakuwahi kumtembelea Ballali alipokuwa ziarani nchini Marekani, pamoja na kuwa amekuwa akifuatilia afya yake kutumia maofisa na watendaji waandamizi wa serikali.

Rais Kikwete binafsi anaelezwa kuguswa na yanayomsibu Ballali, huku akitafakari ni nani hasa anayeweza kuchukua nafasi yake na jinsi ya kurudisha heshima ya BoT ambayo imezidi kuporomoka siku hadi siku.

Kikwete amekwisha kuziba baadhi ya nafasi nyeti zilizokuwa zikishikiliwa na watu aliowarithi kutoka kwa mtangulizi wake, Benjamin Mkapa, ikiwamo Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), Polisi, Usalama wa Taifa, na hivyo kuwapo uwezekano wa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya BoT na asasi nyinginezo kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Ballali ambaye anaelezwa kuingia BoT, Juni 1998, aliongezewa muda na Mkapa mwaka 2003, muda ambao awali ulielezwa kuwa ni wa miaka miwili tu, lakini kisheria muda huo unapaswa kumalizika Juni mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika kuadhimisha miaka miwili ya utawala wake, Jumatano iliyopita, Rais Kikwete, alikiri kufahamu kuhusu kuugua kwa Ballali, lakini alikanusha uvumi kwamba Gavana Ballali amekimbia tuhuma za ufisadi zinazoelekezwa BoT.

Inaelezwa kwamba siku Kikwete alipokutana na waandishi wa habari Ikulu, ndiyo siku ambayo barua inayoelezwa kuandikwa na Ballali ilipotumwa na kupokewa Ikulu lakini hakuna taarifa rasmi za kuthibitisha hilo ambazo zimetolewa hadi sasa.

Ballali aliondoka nchini kimya kimya na hakuna mtiririko mzuri wa taarifa za hali yake ya afya pamoja na baadhi ya watu kusema kwamba ni lazima taarifa hizo zitolewe kwa mujibu wa taratibu za ‘kiserikali.'

Nakala ya barua ambayo inaaminika kuwa ni yake kwenda kwa Rais, na ambayo Raia Mwema iliichapisha, Gavana Ballali anasema ya kuwa kutokana na "sababu za kiafya" hatoweza kuendelea na wadhifa huo na hivyo anaomba idhini ya kupumzika.

Zimekuwapo taarifa hata hivyo, kuwa baadhi ya maofisa na viongozi waandamizi wa serikalini wamekwenda kumjulia hali Gavana Ballali, akiwamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman, ambao wote wanaelezwa kuguswa na kuumwa kwake.

Mmoja wa waandamizi hao anaelezwa kumtembelea Ballali Jumapili ya Desemba 2, 2007 ambako alielezwa kuonyesha mshangao wa dhahiri wa jinsi "muujiza wa Mwenyezi Mungu" ulivyomsaidia Ballali kupambana na maradhi yanayomsumbua.

Mbali ya kuguswa na "muujiza wa Mwenyezi Mungu" mazungumzo hayo yaligusia uwezekano wa Ballali kujiuzulu ili kutoa nafasi ya kuteuliwa kwa mrithi wake, lakini pia suala nyeti la kurejea ama kutorejea kwake lilikuwa sehemu ya mazungumzo hayo.

Ballali ana nyumba yake binafsi eneo la Bethesda, Maryland Kaskazini Magharibi mwa Washington, D.C. lakini habari zinaeleza kwamba tokea alazwe hospitali hajaonekana katika nyumba hiyo.

Kuugua kwake na hatimaye kutangazwa kuwa amejiuzulu, kumekuwa na maswali mengi bila majibu na wakati wote taarifa zake zimekuwa zikitolewa nusu nusu bila kuwa na undani wa kutosha na hadi sasa Wizara ya Fedha, ambayo ndio mwajiri wake haijawahi kutoa taarifa ya wazi kuhusiana na hali yake wala kuhusu kujiuzulu kwake.

Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, aliwaambia waandishi wa habari kwamba hajapokea barua ya kujiuzulu kwa Ballali, kwa maelezo kwamba taratibu zinamtaka kuwasilisha barua kwake na si kwa Rais kama ilivyoripotiwa. Hata hivyo, Meghji alikiri kufahamu kuugua kwake.

RAIA Mwema limeelezwa kwamba Gavana Ballali alilazimika kuwasiliana na wasaidizi wake walioko Dar es Salaam, ambao waliandika barua hiyo kwa maelekezo yake na baadaye ilipelekwa Ikulu kwa faksi kabla ya barua halisi kupelekwa kwa njia ya kawaida na kupokewa.

Agosti mwaka huu Rais Kikwete alifanya uteuzi wa Manaibu Gavana watatu kama sheria mpya ilivyotaka. Walioteuliwa ni; Profesa Benno Ndullu, Lila Mkila na Juma Reli. Uteuzi wa Profesa Ndullu ndio uliogusa zaidi hisia za wengi kutokana na kutajwa kama mmoja wa wanaotajwa kuwa na uwezo wa kumrithi Ballali.

Profesa Ndullu anatajwa kuwa na historia ya utendaji mzuri tokea akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anaelezwa kushiriki katika mchakato wa kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kipindi ambacho Kikwete alikuwa Waziri wa Fedha.

Anaelezwa kwamba aliondoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1989 kwenda Nairobi, Kenya kuwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa African Economic Research Consortium kabla ya kujiunga na Benki ya Dunia akifanya kazi Dar es Salaam na baadaye makao makuu, Washington D.C kabla ya uteuzi wa kuwa Naibu Gavana.

Wengine wanaotajwa ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Blandina Nyoni, ambaye aliwahi kuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali; Dk. Natu Mwamba wa BoT; Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, ambaye alitokea BoT; Naibu Katibu Mkuu, Mipango Joyce Mapunjo, ambaye alitokea Hazina na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.

BoT imekua ikisakamwa kutokana na tuhuma mbalimbali na hivi sasa inasubiriwa ripoti ya wakaguzi wa kimataifa kutoka Kampuni ya Ernst&Young iliyokabidhiwa kazi hiyo na Serikali kupitia ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG).

Taarifa kuhusu ripoti hiyo zimetolewa zikiwa zinatatanisha baada ya Waziri Meghji kusema itatolewa wiki hii baada ya kupitiwa na CAG, huku CAG mwenyewe, Ludovick Utoh akisema kwamba ndio kwanza ameipokea Jumapili iliyopita na kwamba atamkabidhi Rais Januari, 2008.

Kuna habari kwamba pamoja na tuhuma za ufisadi ndani ya BoT kuwagusa baadhi ya watendaji serikalini na baadhi ya watu ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), baadhi ya viongozi wamekuwa wakiwakumbatia watuhumiwa hao.

Katika tukio la hivi karibuni, imeelezwa kwamba mmoja wa watu wanaotajwa sana kuhusika na upotevu wa fedha za BoT, alialikwa "kuchoma nyama" na kiongozi mmoja wa juu serikalini wakati wa Sikukuu ya Krismasi, jambo ambalo limezua maswali mengi kuliko majibu.
 
Serikali inajikanganya kifo cha Ballali - Slaa

2008-05-27 10:23:48
Na Simon Mhina

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amesema hoja za Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Benard Membe kwamba serikali haihusiki na kifo cha Dk. Daudi Ballali, hazijaisaidia serikali, badala yake zimezidi kuleta mkanganyiko.

Alisema yeye pamoja na wapinzani wengine, walijenga hoja kwamba ni kwa nini wanaihusisha serikali na kifo hicho, tofauti na Bw. Membe ambaye amekanusha bila kujibu hoja zao na wala hakutoa maelezo ya msingi.

Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alisema waziri huyo amezidisha kiwango cha wasiwasi walichonacho watanzania, pale aliposhindwa kutoa maelezo kwamba Dk. Ballali alikuwa amelazwa hospitali gani na ugonjwa gani
Alisema hoja ya Bw. Membe kwamba wanaotoa tuhuma dhidi ya serikali wanafanya hivyo kwa hisia, haina msingi na inadhihirisha jinsi waziri huyo anavyobabaika.

``Yaani ugonjwa wa mtu mkubwa mwenye tuhuma nzito kama Ballali, umefichwa, kifo chake kimefichwa, mazishi yake yamefichwa, hata Maiti yake haikuonekana, halafu anasema tuhuma zetu ni hisia? Huu ni upotoshaji mkubwa na kuzidi kujikanganya,`` alisema.

Mbunge huyo alisema kitu ambacho kingeweza kuinasua serikali katika tuhuma hizo, ni Bw. Membe kutaja sehemu aliyokuwa amelezwa Dk. Ballali.

``Tangu lini hospitali ikawa ni sehemu ya siri, kwa nini hawataki kusema?`` Alihoji.
Alisema madai aliyotoa waziri huyo kwamba mwenye vielelezo toka kwa daktari vinavyoonyesha kwamba Dk. Ballali alikufa kwa sumu avitoe, au yanaonyesha kwamba kweli kifo cha Gavana huyo wa zamani wa BoT kilipangwa.

``Mtanzania wa kawaida atawezaje kumpata daktari aliyemtibu Ballali wakati hata hospitali alipokuwa amelazwa panafichwa? Kumbe wameficha kwa makusudi ili Watanzania washindwe kupata vielelezo?`` Alihoji na kuongeza: ``Serikali haihitaji vielelezo, bali ndiyo iliyofanya njama za kuhakikisha hakuna kielelezo chochote ambacho kinahusiana na kifo hicho kinachoweza kupatikana.``

Alisema kama kweli serikali inasisitiza kwamba haihusiki, itaje hospitali ambayo Dk. Ballali alikuwa akitibiwa na ugonjwa uliomsibu.

``Bw. Membe anasema mwenye vielelezo apeleke? Kazi yake kama waziri wa Mambo ya Nje ni ipi hasa?

Yeye ndiye alitakiwa azungumze na Balozi wetu kule Marekani ili aeleze habari za ugonjwa na baadaye kifo chake, kama mtu mkubwa kama Ballali anaweza kufikwa na kifo nchi za nje bila watu kujua, sembuse mtu wa kawaida?`` Alihoji.

Dk. Slaa alisema ili serikali ijisafishe, ni vizuri ikasema ni kwa nini hata hapa mjini, matanga ya marehemu huyo yalikuwa ya siri na majirani walikatazwa kuingia huku waandishi wa habari wakifukuzwa.

``Tunataka iundwe tume huru ya kuchunguza kifo hicho, kwa vile hadi sasa serikali haijatoa maelezo yanayojitosheleza. Tunataka tume kwa vile pesa za EPA bado ziko mikononi mwa mafisadi, ambao huenda ni marafiki wakubwa wa serikali,`` alisema.

* SOURCE: Nipashe
 
Prof Baregu ataka Interpol wachunguze kifo cha Ballali

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili jana, Profesa Baregu alisema serikali inatakiwa ku kubali kufanya uchunguzi juu ya suala hilo na kama wao hawawezi watumie wataalamu wa Polisi wa Polisi wa Kimataifa (Iterpol).

�Serikali haiko makini katika suala hili, kwa sababu kama kweli wanadai kuwa hawakuhusika, kwanini wasitoe hata historia ya ugonjwa kuanzia alipokuwa BoT hadi alipoondoka kwenda kutibiwa,� alisema Profesa Baregu

Nafikiri yupo sahihi..

source: www.mwananchi.co.tz

Mkuu....Uchunguzi ni muhimu katika suala hili, lakini kuihusisha Interpol....Sidhani, kwani hakuna kipengele katika katiba ya Interpol kinachosema kuwa wanaweza kufanya hivyo; wao shughuli zao ni tofauti kulinganisha na suala la Balali lilipofikia.

Kuhusiana na serikali kutoa historia ya ugonjwa wa Balali, nayo pia sio rahisi, nina imani tuna kitu kinachoitwa "Privacy Act" serikali haiwezi kukurupuka tu na kutoa medical records za mtu kisa wanataka kujivua lawama.
But tunaweza kuishinikiza Serikali itupe zaidi ya inachotoa kuhusiana na habari hii, nina imani wanajua zaidi ya wanavyosema.....
 
Watulizane..wao wenyewe waliwahi kusema hana msaada wowote na wala hawataki kusikia...au ndio mtu akifa yanaisha yote???
 
Mamaye Ballali alindwa

na Kulwa Karedia

HALI ya ulinzi mkali imeimarishwa nyumbani kwa mama mzazi wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) marehemu Daudi Ballali.

Habari za kuaminika zilizopatikana jana nyumbani kwa mama huyo Boko, Dar es Salaam, zinasema kuwa ulinzi huo umewekwa na serikali kupitia BoT tangu kutangazwa kwa kifo cha Ballali wiki iliyopita.

“Tumesikia ulinzi huu umewakwa na serikali kwa kushirikiana na BoT kwamba hakuna mtu yeyote kuingia hapa, tunashangaa sana kuona hata sisi ambao tumekuwa naye hapa tumebaki kuwa watazamaji tu,” alisema Seif Omar, mkazi wa Boko.

Alisema kitendo kilichofanywa na serikali si cha kiungwana, kutokana na ukweli kwamba msiba huwa hauchagui maskini au tajiri wa kwenda kuzika mwenzake au jirani yake.

Tanzania Daima jana ilipofika nyumbani kwa mama huyo anayeishi nyumba namba BNJ/BOKO/1081, ilishuhudia hali ya ulinzi mkali, kitendo kilichosababisha hata mwandishi wa habari hizi kuzuiwa kuingia ndani.

Baada ya kuwasili nyumbani, mmoja wa walinzi wa Kampuni ya Regimental Security aliyekuwa getini, alikataa katakata kufungua geti hilo kwa madai kuwa amepewa maelekezo kutoka ngazi za juu serikalini na BoT.

“Nikusaidie nini, unaitwa nani na una shida gani ndugu…tafadhali nionyeshe kibali chako cha kuingia humu ndani kutoka BoT, na kama huna, nakuomba uondoke eneo hili,” alisema mlinzi aliyekataa kutaja jina lake.

Alisema yeye amepewa maelekezo hayo na maofisa wa juu wa BoT, ambao hakuwa tayari kuwataja majina na kusisitiza kuwa anatekeleza majukumu yake ya kazi.

“Nashindwa jinsi ya kuwasaidia…jamani nawaomba sana muondoke hapa,” alisema mlinzi huyo na kuendelea kufunga geti hilo, kitendo kilichoashilia kuna shinikizo kutoka juu.

Juhudi za gazeti hili kumuona mama mzazi wa Ballali ziligonga mwamba kutokana na hali ya ulinzi iliyopo.

Wakati huo huo, baadhi ya wananchi waliohojiwa na Tanzania Daima kuhusiana na kauli ya serikali juu ya kifo cha Ballali wamesema serikali inapaswa kueleza ukweli baada ya kuuficha.

“Tumeshangazwa na kauli ya serikali, tunaelewa wazi kwamba Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, atakuwa ameelewa ukweli, sasa kwa nini atufiche?” alihoji Dickson Juma.

Alisema kama kifo hicho kisingekuwa cha siri, kwanini serikali ilipata kigugumizi kusema ukweli kuanzia ugonjwa wake hadi anafariki, jambo ambalo linazua maswali mengi.

“Sisi tunasema umefika wakati sasa wa kuelezwa ukweli na kama sivyo, basi iundwe tume haraka kabla ya mambo haya hajapoa, maana tunajua yakipoa, ndiyo yamekwisha,” alisema Juma.

Naye Mwanakombo Hussein alisema kitendo cha serikali kushindwa kushiriki katika mazishi ya Ballali kinaonyesha wazi kwamba kuna matabaka ndani ya viongozi wa serikali.

Aliwataka wananchi wote kuungana na kuishinikiza serikali ili kuhakikisha inaunda tume huru kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina na majibu yatolewe haraka.

Marehemu Ballali alifariki dunia Mei 16 jijini Washington, Marekani, alikokuwa akipata matibabu tangu mwaka jana, baada ya kufukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete, baada ya kuhusishwa na ufisadi katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ambako zaidi ya sh bilioni 133 zinadaiwa kupotea.

 
Kazi kweli kweli!!!! mambo mengine moto!!!! Kudadadeki!!!!
 
tunao kesho hawa tunao!!!! sehemu ya kwanza ya kuwabana ni kesho.... whistling... wamelikoroga wenyewe.. wajiandae kulinywa!
 
tunao kesho hawa tunao!!!! sehemu ya kwanza ya kuwabana ni kesho.... whistling... wamelikoroga wenyewe.. wajiandae kulinywa!

Hapa nilipo nimeaandaa muziki utakaocheza kwenye background na sound effects zote muhimu kwa ajili ya second episode ya hii series...

muziki mupya utakuwa...

taratata ta nta tata ta ta ta.... tarantata ta nta nta tatatata....
 
BOT na serikali yao ni wapotoshaji......
hivi balali amekufa huru, hakuwa mshutumiwa wala serikali haikuwana haja nae, lakini leo nyumba ya mama yake inalindwa kwa ulinzi ulioidhinishwa na BOT ( kwa mujibu wa magazeti)....jee huyu mama ni muhimu kuliko balali mwenyewe? au ndio mama analindwa kuficha siri nyengine?
yangu macho na masikio tu!
 
Back
Top Bottom