Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Mwiba

Sasa wewe umefanya nini hebu twambie?
Mimi sasa nipo upande wa CCM ,sababu hizi longolongo wanazotupakia VU (Vyama vya Upinzani) havina mwisho wenye kuleta matumaini kwa kila Mtanzania .Ukitazama CCM wametulia na wamejipanga wanaemuona mzigo wanamwambia arudi nyuma na kama alikuwa luteni anambiwa ajiuzulu abakie koplo.
Wapinzani wanaibua kila kitu wanachoona kiwaweza kuwasaidia mbele ya kuwavutia wananchi na pia kila wanachohisi kitawafanya wananchi waikatae CCM ,lakini wapinzani wakiwa wameshika kasi na kulipuwa wanayoyaita mabomu hawajaona kuwa hakuna matunda yeyote yanayopatikana hali ni ileile.
Nikionacho mbele ni kuwa haya mabomu mwisho yatawapasukia mikononi na yatawadhuru wenyewe. CCM wametoa uhuru wa kusema utakavyo wakijua kuwa faida inayopatikana itawasaidia wao kusonga mbele na kuwa na timu kabambe.
Ili mabomu haya yawe na faida kwa wanaoyalipua ni lazima kama kufa kwanza waelekeze nguvu zao katika kudai katiba mpya na hakuna jingine litakalowasaidia.Tusidanganyane mchana kweupe.
 
Mimi sasa nipo upande wa CCM ,sababu hizi longolongo wanazotupakia VU (Vyama vya Upinzani) havina mwisho wenye kuleta matumaini kwa kila Mtanzania .Ukitazama CCM wametulia na wamejipanga wanaemuona mzigo wanamwambia arudi nyuma na kama alikuwa luteni anambiwa ajiuzulu abakie koplo.
Wapinzani wanaibua kila kitu wanachoona kiwaweza kuwasaidia mbele ya kuwavutia wananchi na pia kila wanachohisi kitawafanya wananchi waikatae CCM ,lakini wapinzani wakiwa wameshika kasi na kulipuwa wanayoyaita mabomu hawajaona kuwa hakuna matunda yeyote yanayopatikana hali ni ileile.

kama wapinzani wanaibua ufisadi wa ccm kwa nia ya kisiasa, je hao ccm wanaofanya huo ufisadi wanafanya kwa nia gani? na kama wewe uko ccm na kuna ufisadi uliokithiri, je nawe uhesabiwe kama fisadi?

Nikionacho mbele ni kuwa haya mabomu mwisho yatawapasukia mikononi na yatawadhuru wenyewe. CCM wametoa uhuru wa kusema utakavyo wakijua kuwa faida inayopatikana itawasaidia wao kusonga mbele na kuwa na timu kabambe. Ili mabomu haya yawe na faida kwa wanaoyalipua ni lazima kama kufa kwanza waelekeze nguvu zao katika kudai katiba mpya na hakuna jingine litakalowasaidia.Tusidanganyane mchana kweupe.

CCM hawajatoa uhuru wowote, wao wanasign mikataba hotelini - BUzwagi, wanasaini mikataba usiku wa maneno - RIchmonduli ya kifisadi na inapatikana kwa vile watu wamechoshwa na ufisadi.

Kinachouma hapa ni uchungu wa mali za watanzania nakama wewe hujaona hilo basi hakuna namna ya kukusaidia.
 
ngoja na huyo mama msikia amekufa kwa machungu ya mwanae!!!

Hivi Ngurumo alisema anamjua aliyempa Balali Sumu,Jina hakutaja ila alisema ni mmoja ya watu waliohusika na dili la Richmond,Ambaye naye ni Rais Kivuli..


Hivi ni Aziz au edward??Manaake aliuliza swali gumu sana Jumapili hii..Kesho nitaliamkia,Mwanakijiji Kama Vipi nipe supu hiyo ya moto mapema,gembe at jf
 
Haya ni Baadhi ya maneno ya ngurumo aliyoyatoa Jumapili katika makala yake ya Maswali magumu

Hata katika hili la sasa, mtu yule yule aliyetajwa na hayati Ballali, kwamba ‘ndiye alinilisha sumu,’ ni kigogo yule yule ambaye amekuwa anahusishwa katika mazingira na matukio mengi ya ufisadi wa kupindukia.


Yumo katika orodha ya mafisadi 11 walioanikwa hadharani na Dk. Willibrod Slaa, Septemba 15, 2007 katika mkutano wa hadhara wa Temeke Mwembe Yanga, Dar es Salaam.


Yumo miongoni mwa waasisi wa kaulimbiu ya ‘Maisha bora kwa kila Mtanzania.’ Ni mmoja wa watu ambao kwa sasa wanaangaliwa kwa macho ya chuki, kwa kuwasababishia Watanzania maisha duni.


Ni mmoja wa vinara waliofadhili na kutangaza kwa nguvu zote dhana ya ‘Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya’ ambayo imekuwa ikifupishwa kwa kuitwa ANGUKA; na kuwa kiini cha anguko la Tanzania.


Ni muasisi wa dhana iliyoangusha uchumi wa nchi na kudunisha maisha ya Watanzania, huku akiasisi dhana nyingine ya kimya kimya ya ‘Maisha bora kwa kila fisadi.’ Mtu huyu huyu aliyetajwa na hayati Ballali kwamba ndiye alimlisha sumu, yumo miongoni mwa vigogo wanaotuhumiwa kulihujumu taifa kwa kuunda mitego ya uchotaji wa pesa za wananchi kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu (EPA).



Ndiye anayetajwa kuwa mmoja wa vigogo walionufaika na pesa za Richmond; mtu ambaye inasemekana alikula njama kuchomoa mafaili ya Richmond katika kumbukumbu za msajili wa makampuni ili ‘kuiingiza mjini’ Kamati ya Bunge iliyokuwa inachunguza tuhuma dhidi ya kampuni hiyo.
Ni kigogo huyo huyo ambaye kwa wakati fulani alidhaniwa kuwa na hisa katika urais wa Jakaya Kikwete, hata ikawalazimu wanahabari kumhoji rais moja kwa moja kuhusu suala hilo.


Ni mtu huyo huyo ambaye miezi michache iliyopita, kabla ya masuala ya ufisadi kupamba moto, alikuwa akidhaniwa kuwa mfadhili na mkombozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na ambaye baadhi ya watu wanaojua jinsi awamu hii inavyofanya kazi, waliwahi kudokeza kwamba ‘ndiye rais’ wa Tanzania asiyeishi Ikulu, anayeendesha nchi atakavyo kupitia kwa rais aliyechaguliwa, anayeishi Ikulu.


Lakini kikubwa kinachomgusa na kumfadhaisha kigogo huyu ni taarifa kwamba ndiye ameshiriki kwa kiasi kikubwa kuchota mabilioni ya EPA kutoka BoT na kuyazungusha kwenye miradi yake, huku akiingiza mengine kwenye kazi za CCM, zikiwamo harakati za kampeni za uchaguzi mkuu.

Je kuna Mtu anaweza kuhisi Mtu huyu ni nani,na kama anajua kwanini serikali isimhoji ili amtaje Muuaji?ila Ngurumo amesema ipo siku kama wasipotuua tutamtaja hadharani
 
Mwanakiji Hivi hatuwezi kupata ripoti ya daktari kujua balali alikuwa anumwa na maradhi yapi?
 
He that loveth silver shall not be satisfied with silver; nor he that loveth abundance with increase: this is also vanity. When goods increase, they are increased that eat them: and what good is there to the owners thereof, saving the beholding of them with their eyes? The sleep of a labouring man is sweet, whether he eat little or much: but the abundance of the rich will not suffer him to sleep. There is a sore evil which I have seen under the sun, namely, riches kept for the owners thereof to their hurt.
But those riches perish by evil travail: and he begetteth a son, and there is nothing in his hand.
 
Kazi sana jamani mtu huyo mbona anajulikana?hivi huyoo muungwana wenu huwa hapiti humu aone uozo wao na kumkumbatia fisadi asiye na huruma kwa wa tz walio masikini?naumia sana roho yangu.....kwa ukatili wao...ila time will tell...kila mmoja atakimbia kwake na kusambaratikia huko...tunamuota shujaa ajaye na makali yasiyotabirika sio anaechekacheka hata kwenye ammbo serious ya kuangamiza nchi.....
 
Mwanakijiji kwa speculation bwana..

Mzee ukitekwa mateka hauna uhuru.. kwenda msalani lazima uombe ruhusa, chakula wanakupangia wao, kulala wanakupangia wao n.k.. Sasa taifa letu limetekwa nyara na waliotutekea wanaamua cha kufanya; hivyo lolote chini ya jua lawezekana.
 
Mkuu ES,

Uzuri wa kuishi kwingi ni kuona mengi. Tuna mifano mingi tu ya watu walio fake vifo, hivyo
ni ngumu kuamini mpaka kuwe na ushahidi wa kutosha.

Mimi swali langu ni lile lile, kafia kwenye hospitali ipi? Tukishajua hospitali, mengine tutachunguza wenyewe.

Mkuu Mtanzania,

Hii ni lazima ieleweke wazi kwani ni "point" moja muhimu sana.
 
Hoja ya Gembe na namna alivyomnukuu vizuri Ngurumo naona anaelekea kuntaja RA.
Kama ndiye mimi nitashtuka tu kidooogo.
Sijui wenzangu ninyi mtafanyaje?

Ni shuku tu na kaswali.
 
*Watoa siku 30 wahusika kujisalimisha Luganga
*Waomba serikali iwaletee mchanga wa kaburi

Na Francis Godwin, Mufindi

WAKATI mwili wa aliyekuwa gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dkt. Daud Ballali umezikwa Washington, Marekani Ijumaa iliyopita, baadhi ya wazee wa kabila la Wahehe wamekuja juu na kutoa siku 30 kwa yeyote aliyehusika kwa njia moja ama nyingine na kifo hicho, kujisalimisha kijijini Luganga, Mufindi mkoani Iringa alikozaliwa gavana huyo.

Wazee hao kutoka kijiji cha Luganga na Mtwango, wameiomba serikali ifanye uchunguzi wa kina juu ya kifo hicho na kufanya kila linalowezekana kuresha mwili huo nchini, ikishindikana ilete mchanga wa kaburi hilo ili wafanye mazishi ya kimila.

Wakizungumza na Majira jana kwa niaba ya wenzao, Mzee Samweli Kalinga (76) na Yohanes Kalinga (85), walisema wataamini kuwa mtoto wao amekufa baada ya kupata ufafanuzi wa kina kupitia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu kifo hicho.

Walisema wao kama wazee wa siku nyingi wa kijiji cha Luganga na Mtwango, wanashindwa kuamini kuwa mtoto wao amekufa, wataamini jambo hilo baada ya kuona maiti au picha yake akiwa amekufa.

Mzee Samweli alisema taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari hazitoshelezi kuamini kuwa ni kweli mtoto wao kipenzi, Dkt. Ballali amekufa hivyo ameiomba serikali kuunda tume haraka kuchunguza mazingira ya kifo cha gavana huyo wa zamani.

Alisema moja ya sababu inayowafanya waendelee kuamini kuwa Dkt. Ballali bado mzima ni mazingira ya sasa ya nyumbani kwao kijijini Luganga na nyumbani kwa baba zake wadogo eneo la Ziroziro, Mtwango.

" Nimeishi Mtwango tangu utoto wangu sijawahi hata siku moja kuona nyumba yenye msiba haina waombolezaji", alisema Mzee Samweli

Alisema kwa mujibu wa taratibu za kihehe, msiba unapotokea huombolezwa siku tatu mfululizo ama zaidi ambapo kwa muda huo, majirani hukusanyika nyumbani kwa wafiwa kuwafariji.

Alisema inawezekana ni kweli, Dkt. Ballali amekufa kama ilivyothibitishwa na baadhi ya ndugu zake lakini wao kama wazee wakihehe, wanasubiri serikali itoe taarifa rasmi ya kina ikiambatana na uchunguzi kamili wa kifo hicho.

"Tunaomba kuelezwa ugonjwa uliosababishia kifo cha mtoto wetu na jitihada zilizofanywa na serikali kuokoa maisha yake... Tunashindwa kuelewa serikali inapotoa pole wakati iliwahi kusema Ballali hajulikani alipo", alisema Mzee Samweli.

Kwa upande wake Mzee Yohanes alisema wanafanya mpango kukutana na ndugu wa marehemu kufanya tambiko la aina yake la kifo hicho na kuomba dua maalum kulaani kifo hicho kama kimetokana na 'mkono wa mtu'.

Mzee huyo, alisema wametoa siku 30 kwa watu waliohusika kwa njia moja ama nyingine na kifo hicho kujisalimisha kijijini hapo, vinginevyo watu hao hawatadumu kwenye nyadhifa zao.

Alisema iwapo kifo hicho kimetokana na mapenzi ya Mungu basi wanamshukuru kwa kutimiza matakwa yake na kama ni kwa mipango ya shetani na wanadamu, basi itashughulikiwa ipasavyo.

Pamoja na mwili huo kuzikwa Marekani, wazee hao wameiomba serikali kufanya kila linalowezekana kuurejesha nchini, ikishindikana waletewe mchanga wa kaburi lake ili wafanye mazishi kwa mujibu wa mila za kihehe, Luganga alikozikwa baba yake mzazi Mzee Timoth Ballali aliyefariki dunia Aprili 3 mwaka 2000.

" Hata kama imeshindika kuleta mwili wake basi wasafirishe mchanga wa kaburi tuje tufanye mazishi kwenye makaburi ya Luganga alipolala baba yake mzazi. Kumzika Marekani ni sawa na kumtenga na familia yake", alisema Mzee Yohana.
http://majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6779

Hii inaitwa BWANA MISOSI NITOKE VIPI. Hamna lolote wanataka kinyamazisha mdomo.
 
Back
Top Bottom