Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kuhani Mkuu: Barbarians at the Vault!!! That was the headline of the Economist a few weeks ago, nilijua labda waliandika about Bongo, kumbe walikuwa wanaandika about US market. But it was a good definition of what is happening in Bongo.
 
Pinda: Hatutachunguza kifo cha Ballali




na Mwandishi Wetu, Dodoma


ERIKALI imelikataa pendekezo la kuunda tume itakayochunguza kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Ballali kwa sababu haioni umuhimu wa kufanya hivyo.
Msimamo huo wa serikali ulitangazwa bungeni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati alipokuwa akijibu baadhi ya hoja zilizotolewa na wabunge waliokuwa wakiijadili bajeti ya ofisi yake iliyopitishwa na Bunge jana.

Hoja ya kutaka serikali iunde tume kuchunguza mazingira ya kifo cha Dk. Ballali ilitolewa na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Dk. Willibrod Slaa wakati akichangia mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu mwanzoni mwa wiki hii.

Mbali ya hilo Pinda katika majibu yake ya jana, alisema watu wenye nia ya kufahamu jinsi fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) zilivyochukuliwa, wanapaswa kufahamu hadi timu iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza itakapokamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti.

Huku akionyesha kushangazwa na ombi hilo kwa serikali, Pinda alisema kuwa pamoja na kuwa Ballali alikuwa mtumishi wa serikali, lakini yaliyotokea kila mmoja anayafahamu, na serikali haina sababu ya kuchunguza kifo hicho kwa sasa.

"Kuunda tume kuchunguza kifo cha Ballali! Eti Ballali mchawi wake ni serikali! Hilo linanipa shida. Kuendelea kumchokonoa marehemu… napata taabu sielewi kifo chake hofu iko wapi," alisema Pinda.

Alisema wanaotaka kujua sababu za kifo cha Ballali ni vema wakaomba ripoti ya uchunguzi wa mwili wake baada ya kifo (post moterm) na suala hilo linaweza kushughulikiwa na familia yake.

Pinda alisema kuwa ni kweli Ballali alikuwa mtumishi wa serikali, lakini yeye hapati raha jinsi watu wanavyokizungumzia kifo chake kwa sababu hajui msingi wa madai yanayotolewa hivi sasa kuhusu kifo hicho.

Hata hivyo, katika kauli ya mafumbo, Pinda alisema kuwa watu wanaodai uchunguzi kuhusu kifo cha Ballali wana kitu wanachokifahamu, lakini wanashindwa kukisema hadharani.

Alisema kuwa zipo hisia, na ni kweli kuwa Ballali alihusika na masuala ya EPA, lakini maadam kuna timu inachunguza suala hilo, ni bora ipewe muda kukamilisha kazi yake.

Pinda alisema hata yeye hafahamu timu hiyo imefikia wapi na jitihada zake za kufahamu zimegonga mwamba.

"Hata mimi sijui ‘what is going on’ (nini kinaendelea). Najitahidi kumuuliza (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) Mwanyika hapa, lakini ananiambia we subiri tu. Hivyo ndugu zangu tuwe na subira," alisema Pinda.

Alisema kuwa kuna hisia kuwa Ballali alihusika kwa namna fulani na EPA na ni uchunguzi unaonedelea tu ndio utakaotoa majibu ya maswali kama hayo.

Hata hivyo, alisema kuwa msisitizo wa serikali hivi sasa umewekwa katika kuhakikisha kuwa fedha zalizochukuliwa kupitia akaunti hiyo, kiasi cha sh bilioni 133, zinarejeshwa.
 
Wakuu,

Hivi unaweza kuchunguza kifo cha mtu ambaye hajafa? Labda Dr. Slaa anaogopa tu kusema, yeye angeomba serikali ichunguze utoro wa Dr. Ballali.

Eti familia itoe post-moterm, Pinda anachekesha kweli, watu ambao wameshindwa hata kusema alilazwa wapi, kweli watafika hata huko kwenye post-moterm? Toka lini gogo likafanyiwa post-moterm?

Vipi zile kanda za video, audio na mambo mengi tuliyoaambiwa hapa kwamba vitatolewa?

Mkuu Lunyungu, tangaza kazi imekushinda ili utupe mji wengine.
 
Na kweli hata jk is not ashamed of himself to commit such an awful sin to pronounced someone who is still alive hiding in one of the us supburbs in the u.s. Dead. Kweli ni dhambi

jk amebeba dhambi which atahukumiwa nao. Au shekhei yahaya anampotosha aise jamaa baala big time
 
Lowassa alitishia kama akijatwa atamleta akiwa hai. tunamsubiri.
 
Siko peke yangu karibu na Ukweli!....

Mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini, Jaji Joseph Warioba akizungumzia kifo hicho cha Dk. Ballali wiki hii, ameiambia Raia Mwema kwamba anaona unafiki wa hali ya juu katika matamshi na matendo ya wanasiasa.
"Huu ni unafiki mkubwa. Muacheni Ballali apumzike kwa amani. Kwanza walimwita ni fisadi, sasa wanasema shahidi muhimu amekufa. Katoka kuwa fisadi wakati wa uhai kuwa shahidi katika mauti," alisema Warioba katika mahojiano ya simu mwanzoni mwa wiki hii.
Aliongeza Warioba: "Amekuwa kafara. Taarifa ya Serikali kuhusu fedha za EPA ilionyesha wazi Ballali amechukuliwa hatua katika utaratibu wa kawaida wa kuwajibika. Haikumtuhumu kwamba alikuwa ameiba fedha. Fedha zile bilioni 133 ni jumla ya fedha zote zilizochukuliwa na kampuni 22 zilizotajwa katika taarifa ya Serikali.
"Ballali hakutajwa katika orodha ya kampuni hizo. Hilo Serikali inajua, viongozi wa siasa wanajua na vyombo vya habari vinajua. Lakini wote hao, kwa kipindi chote alichokuwa hai walimhukumu kama mtu aliyekuwa ameiba fedha. Lakini waliochukua fedha zile wanafahamika.
"Kwa muda wa miezi mitano Kamati (ya uchunguzi wa kashafa ya EPA) imekuwa ikiwaambia wananchi inakusanya fedha hizo kutoka kwa watu wanaoitwa. Ilipoulizwa kuhusu Ballali ilisema haimuhitaji. Maana yake hakuwamo katika orodha ya waliochukua fedha zile. Lakini sasa amefariki wimbo umebadilika. Wanasiasa na vyombo vya habari vinamwita si fisadi tena, bali shahidi muhimu wa wizi wa EPA.
"Huu ni unafiki mkubwa. Kuna visingizio kwamba ugonjwa wa Ballali haujulikani, lakini Serikali inajua kwani alikuwa analipiwa matibabu na Benki Kuu. Alikuwa Boston, Marekani, ile nchi iko wazi mtu angetaka kujua angejua. Lakini sasa wanasiasa na vyombo vya habari vinalalamika kwamba ugonjwa wake ulifanywa siri. Kumbe ni uzembe wao.
" Sasa tumeanza kutafuta mchawi huku. Na hapa ikisha kutamkwa neno fisadi tu, basi hata kama mtu hana ushahidi unakuwa fisadi. Lakini yote haya hakuna anayekuambia Ballali aliiba kiasi gani. Wamuache apumzike kwa amani, siku moja ukweli utafahamika."
Yote yalipita
 
Taarifa za kifo hapa marekani ni public info!
Na si familia inayotoa habari hizo kama wanavyodai kina Kishoka!
Habari hizo hutolewa na coroner kwenda kwenye magazet and so forth!
Na hao wenye hiyo funeral home nao wasiwasi sana kwasababu hata wao walitakiwa wawe na database yao ili tuweze kusearch watu waliokufa kama vile funeral home nyingine zinavyofanya!
Habari hizi tayari zingeshakuwa public hadi sasa!
Kwanini zinazuiliwa isivyo kawaida?
Hiyo funeral home nayo tutaichunguza tu!
progress.gif
Haya mamafia hayawezi shindwa kitu...yanaweza zika hata mbuzi yakasema ni Balali
 
Ni kweli jambo la ku-fake vifo sio geni hapa duniani. Lakini kwa hili ni vigumu sana kuamini vinginevyo. Si Balali tulikuwa tunamjua kwa sura, mliopo Washington hakikisheni hamkosi kwenye mazishi.

Hata hivyo, ni muhimu sasa kwa kuwa habari hizi zimeshakuwa wazi, watoa habari wetu hapa JF watupe source za habari zao. Hili ni muhimu kwa sababu njia za kupata taarifa ni muhimu sana katika ku-judge credibility ya hizo taarifa. Nami najiuliza yale mafumbo yote ya MKJJ wakati alijua ukweli yalikuwa ya nini hasa?

Then, kitendo cha FMES kukanusha kwa dhati kabisa habari za kifo cha Balali nacho kinazidi kutia kiwingu maana huyu bwana anaheshimika kwa kupata habari nyeti. Mimi bado naendelea kuamini kwamba huyu bwana alishaanza. Sasa kwa nini habari hizi zimetoka five days baada ya kifo hili ni swali ambalo inawezekana tusipate jibu lake milele!!
 
Back
Top Bottom