Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania


Jamani mi napenda kujua kitu kimoja:

Mzee ES ana interest gani na kuf/kutokufa kwa Balali mpaka watu wote mnang'ang'ania yeye tu?Yeye alileta ripoti kuwa Balali kafa kutoka kwa vyanzo vya kuaminika toka kwake,hata huyu Kinepi naye kaleta speculation tu (kwani hakuna uthibitishop mpaka sasa) kuwa Balali hajafa,ajabu mnamuunga mkono yeye kwa haraka zaidi bila kumtaka alete ushahidi au hamumng'ang'anii kama Mzee ES.Kilichobaki sasa ni kila mtu aamini chake kama Mwafrika wa Kike,Mtanzania walivyoamua.Kitu kimoja kiko wazi:Balali hatarudi milele Tanzania,cha muhimu kwetu ni kupambana ili tuweze kurecover kiasi kilichoibwa na kuzuia mambo haya yasijirudie tena.

Muda tunaotumia kubishana Balali kafa au hajafa ingekuwa ni busara zaidi kujiuliza kama tunaweza kurecover pesa zetu za EPA na kudili na issues nyingine za ufisadi.

By the way Mzee ES nawa mikono tu kwenye issue hii.

Hapa sikubaliani na wewe kabisa.
Ni muhimu sana kujua kama kafa au bado ili tusijefanyiwa hivyo tena na wengine. Tusipofuatilia hili, basi kila fisadi atakuwa 'anaugua' anapelekwa nje ya nchi, 'anakufa' na 'kuzikwa' huko huko! simple - watanzania wataamini tu.
Ndiyo maana mtu akifa basi hufanyika postmoterm ili kujua nini hasa kichomuua na kutafuta namna ya kudhibiti ili waliobakia wapone.
Hivyo mr. Tunatafuta ukweli ili waliobaki wasiweze kutuchezea, wajue kuwa wataumbuka tu!.
 
Ndugu wananchi,

Kufuatia utata mkubwa kuhusiana na kifo cha Ballali tumeamua kuwafahamisha yafuatayo:

Hati ya kifo ya Ballali ni namba x16789 iliyotolewa Boston au Washington na aliyeitoa ni masalakungwa mhogo mtamu namba yake ya simu ni 98810999999. Ballali alikuwa anaumwa kifaduro na mnaweza kuthibitisha hili kwa kuongea na daktari wake Mnyamani Mbuzi simu yake ni namba 777788882222. Manesi waliokuwa wanamwangalia Ballali katika hospitali ya XYZ wodi namba 555 ambayo ni ya wagonjwa wa vifaduro ni wanne na majina yao ni haya yafuatayo na pia namba zao za simu ni hizi hapa. Mganga alikuwa akimtibu Ballali aliamua kumruhusu Ballali kurudi nyumbani tarehe 101108 kutokana na sababu zifuatazo ABCD.

Kwa hiyo yeyote yule anayetaka kuthibitisha kifo cha Ballali awasiliane na daktari wake, manesi waliokuwa wanamwangalia alipokuwa amelazwa na huyo jamaa aliyetoa hati ya kifo.

Mchezo umekwisha, watu tutaingia mtamboni kuhakikisha kama kweli Ballali hatuko naye tena duniani kwa kuwatafuta hao watu ili watuhakishishie hili, lakini SIRIIIIIIIII KALIIIIIII na usanii wa hali ya juu!!!!! Wanapokuja kuomba KULA wanakuwa wanyenyekevu wa hali ya juu na hadi chungu nzima na kutunga misemo mbali mbali ili KUWADANGANYA WATANZANIA kama "uwazi na ukweli" hakuna chochote! bali tulichokiona katika awamu ya tatu ni "ufisadi, uroho wa utajiri wa haraka haraka, ubabe, kuwatusi Watanzania na matusi ya rejareja, siri kali za kuficha madhambi yao yote, na uwongo wa hali ya juu"

Awamu ya nne tukaambiwa "Maisha bora kwa kila Mtanzania" na "ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya" na tulichokiona hasi sasa ni "maisha bora kwa mafisadi", "ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya ya kuwafisadi Watanzania" na "maisha magumu kwa kila Mtanzania ambaye si fisadi" Eeh! Tanzania nchi yangu yenye milima na mabonde yenye watu wenye uungwana wa hali ya juu, yenye mito, bahari na maziwa yenye utajiri mkubwa katika rasilimali mbali mbali na zinazotafutwa kila kona ya dunia kwa udi na uvumba unaelekea wapi nchi yangu???? 🙁🙁🙁🙁
🙁
 
Jamani ya Balali tuyaache maana yanatupotezea muda. Ila tu tuendelee kumtafuta kimya kimya. Kadri tunavyopiga kelele hajafa, kafa, hajafa, kafa, kama yupo kweli anazidi kujichimbia zaidi. Lakini kama yupo kweli, Siku moja huko majuu tutakutana tu. Dunia ni kijiji siku hizi.
 
Mkuu FMES,

Basi tueleze huyo balozi Sefue aliona maiti wapi?

Mimi nilikuwa najua kwa asilimia 100 kwamba kwenye misa hakukuwa na kuona maiti. Sijui ndugu yangu FMES alipata wapi hiyo ya kusema balozi aliona maiti?

Pia FMES data zako zinasema Ballali alikufa jumapili tarehe 18, padre anasema 16.

Data za Jasusi zinasema alikufa ghafla, padre anasema aliumwa kwa muda mrefu.

Mtanzania,
Sina nia ya kurudi katika huu mjadala. Lakini hakuna mahali nimesema Daudi alikufa ghafla.

 
mchongoma huna tofauti na mwenda kuzimu, usituletee masihara watu tuna hasira za kweli. oohoo.

...aaaaaaaaaaaahhh major, acha hizo, unatishia watu wazima nyau?... kanywe maji baridi kwanza kisha;

SOMA HAPA;

Kuhusu suala la fedha za EPA, Waziri Mkuu alisema kuwepo kwa mfumo huo ni halali na makampuni yanaruhusiwa kuchukua fedha kwa ajili ya kufanya shughuli za kibiashara na baadaye kuzirejesha.

SOURCE; http://www.newhabari.com/mtanzania/habari.php?section=kitaifa&id=4161

...usiwe na hasira sana mpaka ukakataa kuuona ukweli wapi 'huwa wanatuacha' kwenye mataa.

'Balali' is a just needle in a haysack!, hujajifunza tu?
 
Duh!! hii kitu bado inaendelea...naona new twists zimejitokeza...kuna kazi!!
 
Watu wengine bwana!!! Wakiweka wao "Dataz" humu basi wanataka kila mtu azikubali. Wakiweka wengine basi wataambiwa mpaka waweke video au sound recording ndio ziaminike.

Mkuu Heshima mbele, mimi ninapoweka dataz zangu huwa nina uhakika nazo 100%, na wewe unajua wazi kuwa hazijawahi kuwa batili au za uongo ndio maana huwa sihitaji tape record, na nikizitoa within siku tatu kuna watu hapa hujitokeza na kusema wamethibitisha, kwenye hii topic nimetoa dataz nyingi ambao zote zimethibitishwa kuwa ni kweli na nimesema wazi kuwa nimeshindwa kupata jina alilokuwa analitumia Balali akiwa Hospitali, halafu bado nina utata na tarehe aliyofariki na ni kwa sababu moja tu nayo ni kwamba Mkulu Wangu Mwanakijiji bado haridhiki na tarehe, kwa sababu ninamuaminia kwa dataz ni kakubali kuwa tarehe ina utata,

Otherwise, mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kwa taifa zima la bongo kutoa dataz za alipofia marehemu Ballali, atakapozikwa, jina la Pastor wa kumzika na kanisa lake, na mpaka Hospitali aliyofia, na nikasema kwa mara ya kwanza jinsi mama wa marehemu alivyoshambuliwa na "majambazi" jinsi mke wa marehemu alivyokwenda kumuuguza, je kuna any of this dataz ilihitaji tape record?

Now ninaomba tena niseme hivi, hapa wote ni watu wazima, niaamini kuwa hakuna watoto wadogo, unapoleta dataz zinazosema kuwa eti katika nchi ya USA tena mji wa DC, kuna Pastor wa Kanisa kubwa kama la St. Stephen , kwamba huyu Pastor aliendesha misa kubwa ya marehemu a former Gorvernor wa Bank Kuu ya Tanzania, lakini toka siku ya kwanza aliyofahamishwa kuhusu kifo, mpaka kuletwa maiti kanisani na kuombewa kabla ya kwenda kuzikwa kaburini, anapotokea mtu wa kusema kuwa eti Pastor yule amesema kuwa hakuuona mwili katika anytime ya hizi shughuli, hapo wakuu tunakuwa tumefika mbali sana na hizi dataz! Eti kwamba haya yote yametendeka USA na kweli kuna watu hapa JF wanakubali hiyo as a fact, basi CCM itatawala bongo milele!

Mkuu Mtanzania,

Ninaliheshimu sana gazeti la Thisday na Kulikoni, wao wamekataa kabisa kwa sababu hawana vithibitisho vyote, na ninawaheshimu kwa kukataa ku-speculate anything, that is the way to go lakini sio kuanza kulaumu watu au kulaumu tu bila mpango na kuanza kutafuta watu uchawi wa bure, it is not fair! Kwa wale wanaomamini hajafa basi watuletee dataz nzito, lakini sio hizi nyepesi nyepesi, mimi ninaamini kuwa Balozi Sefue, aliuona mwili kwa sababu asingeuona basi bosi wake wa kazi Membe asingethibitisha kifo hicho au hata rais pia, sidhani kama hili linahitaji elumu kubwa kuelewa na hata kuelezea watu wenye akili nyingi kama hapa JF!

Mkuu Mtanzania ninaheshimu sana your stand on this ishu, na wengine wote walio pamoja na wewe, ninachosema ni kuwa kwa sisi wenye msimamo tofauti na hasa inavyoonekana ni mimi peke yangu so far na sisi pia tuheshimiwe na pia haki yetu kuuliza ukweli wa dataz za kutoka huko kwenu pia iheshimiwe kama sisi tunavyoheshimu haki yenu mkuu, ndio maana ya demokrasia tunayoidai toka kwa serikali yetu, sasa hizi name calling na accusations kama kweli tuna hoja ni za nini? Watu wakubali kuwa hawaamini lakini hawana facts, lakini logic kwenye hii ishu haziwezi kutatua tatizo, JF tunaheshimika sana na taifa kwa dataz na ukweli wa ishus muhimu za taifa letu, lakini kwenye hili wakuu tunayumba sana na tumeyumba sana, sisi siku zote huwa ni watu wa majibu tena very serious ones, sasa tatizo kwenye hili ni nini hasa?

Kama tumeshindwa kupata ukweli, basi tusubiri tutakapoupata, lakini ku-specualte kama magazeti ya kina majira na kasheshe ambao wao pia wanategemea sisi ni waste of our time, mimi ninashindwa kuyaelewa magazeti yetu, tumewapa dataz za kutosha kwenye hiii ishu toka Balali alipoondoka tu, lakini mpaka leo wanachoandika hakieleweki? Wote tunajua jinsi Mwandishi Pearly alivyokufa kule Pakistan, akifuatilia kina Osama, sasa sisi Tanzania tulishindwa nini kutuma waandishi wa kufuatilia ishu ya Balali alll that time, sasa tunaanza kutafutana uchawi?

Ndio maana nilisema kule nyuma kuwa kwenye hili la Balali wa-Tanzania wote tuko guilty kwani wote tumeruhusu kutokea bila ya kufanya anything about it, pamoja na kwamba tulikuwa na all the facts kutokana na the past kwamba this was coming, sasa tutafute ukweli wa kile tunachoamini na tukiseme hapa, kama hatuwezi tusubiri huenda siku moja kuna ukweli zaidi utatokea, lakini tusiendeele kujishusha hapa na kutafuta umaarufu wa bure wakati ukweli hatuna!

Mkuu Wa Pwani, ndugu yangu usiwe na wasi na wasi mimi, mimi sina noma kwenye kuelimishana, maana ndio hasa kinachowaketa wananchi hapa JF huwa sichoki kwenye hilo na siku zote huwa sikimbii maswali ya wananchi, ninasema nipo na nitajibu anytime ikibidi,

Mkuu Ibambasi, ahsante mkuu kwa support lakini ninakuomba next time usifanye hilo tena la kunitetea maana utashambuliwa sana hapa, mimi ninabeba masalaba wangu mwenyewe tena bila tatizo, na the buck stops here, huyu jaama anayetaka kutuyumbisha hapa JF ninamjua na nimeshamuona na niko bega kwa bega naye ninakula naye sahani moja, na ninajua mbinu zake zote, unajua huwezi kupigana na adui ambaye hujui silaha zake, ana silaha nyingi sana na ninaona tayari watu wengi hapa wameanza kuupanda mkenge wake, lakini ninasema kuwa ni ukweli tu ndio siku zote utakaosimama hapa JF, na sio uongo na ni watu wakweli tu ndio watakaodumu hapa JF, na sio wahuni na wajinga wajinga, maana sisi tulikuja hapa JF kuyakwepa magazeti ya bongo, ambayo mimi nilikuwa mtu wa kwanza hapa kusema kuwa yote yalikuwa yamenunuliwa na mtandao!

Ahsanteni Wakuu!
 
Ndugu wananchi,

Kufuatia utata mkubwa kuhusiana na kifo cha Ballali tumeamua kuwafahamisha yafuatayo:

Hati ya kifo ya Ballali ni namba x16789 iliyotolewa Boston au Washington na aliyeitoa ni masalakungwa mhogo mtamu namba yake ya simu ni 98810999999. Ballali alikuwa anaumwa kifaduro na mnaweza kuthibitisha hili kwa kuongea na daktari wake Mnyamani Mbuzi simu yake ni namba 777788882222. Manesi waliokuwa wanamwangalia Ballali katika hospitali ya XYZ wodi namba 555 ambayo ni ya wagonjwa wa vifaduro ni wanne na majina yao ni haya yafuatayo na pia namba zao za simu ni hizi hapa. Mganga alikuwa akimtibu Ballali aliamua kumruhusu Ballali kurudi nyumbani tarehe 101108 kutokana na sababu zifuatazo ABCD.



This is fantastic, kazi yako ni murua sana mkuu maana hata Ze Comedy hawajafikia, yaani kujaribu kutuzuga kwa kutumia majina? Duh kaaazi kweli kweeeeli lakini JF tuko macho sana, yalimshinda TTJ haya, wewe huyawezi haya yameshaanza kukushinda!
 
Balali saga linaendelea? Sio mchezo i love JF sababu watu wana keep up na issue, hakuna kusahau agenda hata moja.

Mimi nilishanawa mikono kwenye swala la Balali, nilikuwa sijui kama CCM wana mafia wa hali ya juu kiasi hiki. Nani anaeyewasaidia kufuta print? Maana hawajaacha fingure print zao kwenye kitu chochote.

Mtu wa kumbana ni mkewe Balali.
 
Changa la macho ilo nijuacho mimi ni kuwa kanisani mwili hufunuliwa sehemu ya kichwa kwa ajili ya kuumwagia maji ya baraka?
Labda wenzetu marekani wameadvance kiasi cha kumwagia maji ya baraka Jeneza na sio mwili.
I believe kwa 100% Balali is still alive kifo ni uzushi ili kuficha uovu wa mafisadi.
Tutaendelea kulalama mpaka kieleweke hela ya wavuja jasho watz lazima iludi..Pumbavu!!!
 
Hivi toka hili jambo lianze, kuna mtu amewahi kumsikia mtu yeyote anayesema publically kwamba aliona mwili wa Ballali?

Ballali amesaidiwa na serikali kutoroka na kwenda kuendelea kufaidi mapesa yetu aliyojichotea.

Mimi nasubiri zipite siku 40, kama hakuna hiyo dossier wanayosema aliacha, basi ndugu zake Ballali hapa JF na kwingineko should be told to shut up.

Toka September mwaka jana wamekuwa wakitumia delaying tactics kwa kutoa info kwenye media ambazo wanajua wazi zilikuwa ni uwongo na hakukuwa na njia yoyote ya kuzithibitisha.

Wakati unafika wa kuwaambia watoe hizo dossiers vinginevyo wafumbe midomo yao maana Watanzania walio wengi hawawezi kuendelea kudanganywa na huo uwongo wao.

Mara sumu, mara yuko hospitali, mara kaonana na Othman na kamshangaa kwamba bado yuko hai, mara makachero watano wanamtafuta, mara yuko Boston, mara kafia Washington DC, mara alipona ila kafa ghafla, mara dada zake kulipua bomu Dar, mara wananchi wamewaonya wasiseme, mara kuna kanda kaelezea kila kitu, mara kafa tarehe 16, mara kafa tarehe 18, mara ................

Utapeli na umafia uliozidi kiasi wa kutudanganya Watanzania. Hata kama hatuna uwezo wa kufunga kamba, wengine tutaendelea kuwazomea hapa mpaka kieleweke.
 
Hapa kila nikikuna kichwa upande wa wanaosema kuwa amekufa wanajitahidi sana kututhibitishia na wanaosema kuwa hajafa hali kadhalika inafika kipindi unashindwa kuamini kama kweli amekufa au lah.
Kazi kweli kweli hapo.
 
Balali saga linaendelea? Sio mchezo i love JF sababu watu wana keep up na issue, hakuna kusahau agenda hata moja.

Mimi nilishanawa mikono kwenye swala la Balali, nilikuwa sijui kama CCM wana mafia wa hali ya juu kiasi hiki. Nani anaeyewasaidia kufuta print? Maana hawajaacha fingure print zao kwenye kitu chochote.

Mtu wa kumbana ni mkewe Balali.


Very smart and intelligent too, mkuu Mtanganyika saaafi sana!
 
Serikali wanatakiwa watoe tamko lenye maana kuwafanya watu waamini kuwa amekufa kweli badala ya kusema tu mapenzi ya mungu watuambie aliumwa nini alilazwa wapi, alikufa lini, na mengine ambayo wananchi wanauliza otherwise watu wataendelea kuamini kuwa balali hakufa.
 
Jibu: Hapana jeneza halikufunguliwa, niliamini maneno ya ndungu za marehemu kwamba aliyeko humo kwenye Jeneza ni Balali.

Swali: Je si lazima kujua nini kipo ndani ya jeneza kabla ya kukiombea?
jibu: ni vyema ukauliza ndugu za marehemu kwa maelezo zaidi.




Hivi toka hili jambo lianze, kuna mtu amewahi kumsikia mtu yeyote anayesema publically kwamba aliona mwili wa Ballali?

Mkuu wangu Mtanzania,

Heshima mbele sana bro, mkuu kwa maoni yako ni kosa la nani kwamba hakuna aliyesema public ameuona huo mwili? Hivi siku ile si kuna wana-JF mmoja hapa alisema kuwa anaenda kwenye mazishi vipi aliiishia wapi?

Mimi mkuu siamini kuwa kifo cha Balali kinaweza kuwa ni sababu ya sisi taifa kutowashughulikia mafisadi, kwa sababu tunajua kuwa kila kitu kipo, si kamati ya mahesabu ya bunge ilishasema long time ago kuwa vitu vyote vipo, mpaka mama meghji akashikwa amezuga kwenye moja ya hizo evidence, au?
 
Mkuu wangu Mtanzania,

Heshima mbele sana bro, mkuu kwa maoni yako ni kosa la nani kwamba hakuna aliyesema public ameuona huo mwili? Hivi siku ile si kuna wana-JF mmoja hapa alisema kuwa anaenda kwenye mazishi vipi aliiishia wapi?

Mimi mkuu siamini kuwa kifo cha Balali kinaweza kuwa ni sababu ya sisi taifa kutowashughulikia mafisadi, kwa sababu tunajua kuwa kila kitu kipo, si kamati ya mahesabu ya bunge ilishasema long time ago kuwa vitu vyote vipo, mpaka mama meghji akashikwa ugoni kwenye moja ya hizo evidence, au?

Mkuu ES,

Huyo mwanaJF aliyeenda anasema hakukuwa na kuona mwili.

Wengine hawajasema publically kwasababu hawakuona mwili wa Ballali. Mtu anaweza kueneza uvumi kichinichini lakini hawezi kuharibu reputation yake kwa kusema publically kwamba kaona mwili wa Ballali wakati hakuona.

Suala la EPA bila Ballali halipo tena, si umeona report yenyewe kila kitu kinaangukia kichwani kwa Ballali?

Wakati tunaendelea na mafisadi wengi haina maana tumwache Ballali kwasababu tu kajifanya kafa.

Wizi wa BOT ukijumlisha mambo yote kuanzsia EPA mpaka Meremeta ni mkubwa kuliko ufisadi wowote ambao umewahi kufanyika Tanzania, sasa kama kinara aliyefanikisha huo wizi haguswi, unafikiri nani tena ataguswa?

Ni muhimu kwa bunge kulivalia njuga suala la RICHMOND na EPA ili japo hao waliotajwa kuhusika wawajibishwe mara moja. Waliotoroka kama Ballali waendelee kutafutwa, kama hawatafutwi basi wengine hapa JF tutaendelea kurusha vijembe ili hao waliofanikisha huo utoro wasilale salama.
 
Back
Top Bottom