Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kama ni kweli alizikwa kikatoliki kama inavyodaiwa, kuna hatua ambapo padri huwa anamfunua uso maiti na kumnyunyizia "maji ya baraka". Sijui kama padri huyo alikwepa hatua hiyo? Inapaswa aulizwe, wenye nafasi huko tusaidieni hiyo kazi. Hii kitu kama inaisha vile lakini inaibuka upya mara kwa mara!

jamani naomba huyu padri apigiwe tena simu aulizwe mambo zaidi, pengine tukagundua mengine, na vile vile huyu padri anaweza kuwa pia ni wa kuchonga. maana pesa iliyoliwa ni nyingi kiasi inaweza kufanya lolote lile,sintokaa niamini kifo hiki kamwe
 
Mkuu Mtanzania,

Na wengine heshima mbele, mimi kama Mkristo safi hii ishu nimeinawa mikono, ninaomba tena kusema ninchojua na kilichonifanya ninamini na bado ninaamini kwa 100% kuwa Balali amefariki, lakini pia ninaheshimu sana mawazo ya wale wanaoamini kuwa yupo:-

Nina uhakika kuwa alifariki Jumapili nyumbani kwake, alishughulikiwa in one way or another katika hospitali ya George Washington University Hospital lakini sio kwa jina la Balali, na hili jina la Siriani mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kulitoa, na mpaka jina la kanisa la huyu padri mimi ndiye nilikuwa wa kwanza kuyatoa, sasa ninashukuru kuwa kuna waliofuatilia kama nilivyoomba kule nyuma,

Ninaamini kuwa Balozi Sefue aliuona mwili, ndio akamuarifu rais na Membe, wakuu mimi as a Christian huu ni ushaidi tosha mbele ya Mungu wangu kuhusu kwa nini ninaamini kuwa amefariki, na ninaomba ninawe mikono hapa, lakini kwa yoyote anayetaka msaada zaidi nitampa kama nilivyowapa magazeti, katika kufanya uchunguzi zaidi, ila mimi dini yangu na Mungu wangu inanikataza kuendelea zaidi ya hapa nilipofikia na uchunguzi,

Lakini ninazisoma lines in the betweeen kwa makini sana, na ninawatakia heri wanaoendelea lakini akama kawa sina tatizo kutoa msaada kwa walio serious, pia nitoe respect kwa Majira na wengineo kwa msimamo imara wa kutoyumbishwa, that is waht we need kwa taifa letu.

Ahsante Wakuu!

kwani hata wewe unashindwa kuhongwa? usichezwe na nguvu ya pesa bana .kwani hata hapo ulipo wewe si unahangaikia mkate wako wako wa kila ?sasa ikitokea ukaupata kwa njia ya mkato zaidi utaukataa?
 
jamani naomba huyu padri apigiwe tena simu aulizwe mambo zaidi, pengine tukagundua mengine, na vile vile huyu padri anaweza kuwa pia ni wa kuchonga. maana pesa iliyoliwa ni nyingi kiasi inaweza kufanya lolote lile,sintokaa niamini kifo hiki kamwe

sawa major, mpigie basi simu huyo pa-adre !
 
Mkuu Kinepi,

Wewe unafaa kuwa mwandishi habari za uchunguzi.

Umeniacha hio na hio kazi ulioifanya...

Ndio hiki nichokisema kila siku, Tanzania hakuna press!

Gazeti limeongelea maongezi yao na Padri kana kwamba ishu hapa ni kuthibitisha kama Ballali alifanyiwa misa, au nani alimfanyia misa.

Ni mpaka Mkuu Kinepi alipopiga simu kuuliza swali husika: Je, umeuona mwili wa marehemu? Hiyo ndio ishu!

Ni investigation ya Kinepi ndio inatuambia padre anasema "mimi ndio niliombea nilichoambiwa kwamba ni maiti."

Ukisikiliza kwa makini kinachosemwa hapa, ni kwamba Padre anakubaliana na sisi, kwamba jamani eeeeh! God knows what was inside that big box! I may be a Priest, but I can't see thru wood, and I couldn't tell ya!

Ha ha ha aaaaaaaaa ........ This is just hilarious!

Again, hakuna Press Bongo! Kinepi, babu kubwa mtu wangu! LOL!
 
::Habari za Tanzania Jumatatu Juni 09, 2008

Imetolewa mara ya mwisho: 08.06.2008 1519 EAT
•
Mchungaji aliyemzika Ballali anena


*Athibitisha aliumwa kwa muda mrefu
*Aeleza alivyoongoza ibada, maziko

Na Hassan Abbas

WAKATI Watanzania wakiwa bado katika hali ya sintofahamu kuhusu ukweli juu ya kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Daudi Ballali, Mchungaji aliyeendesha misa na hatimaye maziko yake nchini Marekani amekizungumzia kifo hicho na namna maziko yalivyokuwa.

Akizungumza katika mahojiano na gazeti hili kwa njia ya mtandao, Mchungaji Klaus Sirianni wa Kanisa Katoliki la St. Stephen Martirs' lililoko District of Columbia, Washington DC, amelithibitishia gazeti hili kuwa Dkt. Ballali alikufa na yeye ndiye aliyeongoza misa na baadaye ibada ya maziko.

"Ni kweli Dkt. Daud T.S Ballali alifariki Mei 16, 2008 akiwa na baadhi ya wana ndugu zake hapa nchini Marekani," alisema Mchungaji Sirianni.

Kumekuwa na uvumi unaozidi kuenea nchini ambapo wengi wanahoji ukweli wa kifo cha Dkt. Ballali huku baadhi wakitaka kujua kama kweli kulifanyika ibada ya maziko mjini Washington kama ilivyokuwa imetangazwa.

Akithibitisha kufanyika kwa misa na ibada ya maziko ya Ballali, Mchungaji huyo ameliambia Majira Jumapili kuwa: "Misa iliyofanyika katika tamaduni za kikristo ya Dkt. Ballali ilifanyika kwenye Kanisa la St. Stephen Martyr, Washington, District of Columbia, kuanzia saa nne asubuhi, Mei 23, 2008."

Akaongeza kuwa yeye ndiye aliyesimamia misa na baadaye maziko hayo. "Aliyeongoza misa na ibada ya maziko ni mimi Mchungaji Klaus Sirianni," alisema mchungaji huyo ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa parokia ya kanisa hilo.

Katika maziko hayo Mchungaji Sirianni amethibitisha kuwa wahudhuriaji walikuwa ndugu, jamaa wa karibu na watu waliowahi kufanyakazi na marehemu huku akimtaka mwandishi kwa maelezo zaidi kuhusu sababu za kifo hicho awasiliane na wanafamilia.

"Maziko yalifanyika kwenye makaburi ya kikatoliki ya Gate of Heaven yaliyoko eneo la Silver Spring, Maryland na kwa mara nyingine mimi ndiye niliyesimamia ibada hiyo tena."


Kinepi
Baada ya kusoma habari hii, nilinyanyua simu nikampigia Padri Klaus Sirianni wa kanisa katoliki mtakatifu Stephen Martyr, Washington, District of Columbia,

Maswali na majibu yalikuwa kwa lugha ya kiingireza ila nitachapa kiswahili.

swali. padri habari za leo
jibu: Nzuri

maelezo: mimi ni kinepi Mtanzania,Nimepata taarifa kuwa wewe ndiye ulieendesha misa ya marehemu Dr. Daudi Balali

jibu: Ndio

swali: utajali kama nikikuuliza maswali kuhusu misa ile na huduma yote kwa ujumla
jibu: hapana
Ndio, Balali alifariki na mimi ndie niliyeendeshasha ibada ile mpaka makaburini akazikwa.

Swali: Padri je katika huduma yako hiyo ulipata kuuona mwili wa DR. balali ???

Jibu: Hapana.sikuuona.
Swali: Je ulipata wasaa wa kufunguliwa jeneza hata mara moja?"
Jibu: Hapana jeneza halikufunguliwa, niliamini maneno ya ndungu za marehemu kwamba aliyeko humo kwenye Jeneza ni Balali.

Swali: Je si lazima kujua nini kipo ndani ya jeneza kabla ya kukiombea?
jibu: ni vyema ukauliza ndugu za marehemu kwa maelezo zaidi.

kinepi: asante padri kwa muda wako, kwaheri.

Kutoka ubalozini wanarushiana mpira kuwa ni nani aliuona mwili.
Mpaka sasa Kifo cha Balali ni kitendawili.
Ninafanya jitihada kujua ni hospitali gani alilazwa. Nikipajua tu au mtu yeyote kama ana info tafadhali anipatie lazima ni jue Balali yuko wapi.
Majibu ya wizi wa fedha zetu ni muhimu sana.

Mara ya kwanza kabisa niliposikia Ballali yuko Marekani, ilisemekana kuwa alikuwa amelazwa katika hospitali ya "New England Medical Center" - Boston.....
 
Msihofu Atafufuka Kama Yesu Wala Hawakucheza Pele Hapa
Prof Dr Ing Rev Tumaini Geofrey Temu
 
kwani hata wewe unashindwa kuhongwa? usichezwe na nguvu ya pesa bana .kwani hata hapo ulipo wewe si unahangaikia mkate wako wako wa kila ?sasa ikitokea ukaupata kwa njia ya mkato zaidi utaukataa?

Wanaohongwa ni masikini na mafukara wa akili, unaonekana kuwa ni mmoja wao, ila samahani sio mimi,

vipi wewe unahangaika kutafuta mkate wa kila siku? Kwa hiyo unafikiri ni kila mtu? Mbona una mawazo finyu sana mkuu ya kufikiria ndani ya box lako tu? Hapa JF tunakataa haya ya kufikiria ndani ya box lako tu na kudhani ni lazima uwe ukweli wa wote wengine that is pathetic thinking!, leave a lone kuisema mbele ya hadhara duh!
 
Ukisikiliza kwa makini kinachosemwa hapa, ni kwamba Padre anakubaliana na sisi, kwamba jamani eeeeh! God knows what was inside that big box! I may be a Priest, but I can't see thru wood, and I couldn't tell ya!

Nikisema niliongea na Padri na kwamba alisema ndani ya jeneza kulikuwa na mbuzi nitakuwa ninasema ukweli au uongo? Wakuu tafuteni hoja nzito za kusimamia hoja yenu kuwa Balali yupo lakini sio hizi nyepesi nyepesi, unless kuna mwenye tape aliyomrekodi huyo Padri, hii mimi siikubali lakini sina tatizo kukubali mengine yenye more proof zaidi kuliko niliongea naye!

Kwenye hili hata hawa waandishi wanakuwa wajinga wajinga tu!

haya later......!
 
Nikisema niliongea na Padri na kwamba alisema ndani ya jeneza kulikuwa na mbuzi nitakuwa ninasema ukweli au uongo? Wakuu tafuteni hoja nzito za kusimamia hoja yenu kuwa Balali yupo lakini sio hizi nyepesi nyepesi, unless kuna mwenye tape aliyomrekodi huyo Padri, hii mimi siikubali lakini sina tatizo kukubali mengine yenye more proof zaidi kuliko niliongea naye!

Kwenye hili hata hawa waandishi wanakuwa wajinga wajinga tu!

haya later......!

Watu wengine bwana!!! Wakiweka wao "Dataz" humu basi wanataka kila mtu azikubali. Wakiweka wengine basi wataambiwa mpaka waweke video au sound recording ndio ziaminike.
 
Angalieni Thisday walivyoandika:

Ballali, who was recently reported to have died in the US, was sacked from his job in January this year by president Jakaya Kikwete after being implicated in the EPA scandal by the Ernst & Young audit report.

Ina maana hata wao hawana uhakika na kifo cha Ballali.

Hapo mkuu ES una kazi ngumu kweli!
 
samahani maelezo ya mahojiano na Padri yamechelewa kidogo.
Bali Padri kwa kinywa chake amekiri hakuona mwili wa Balali.
Simu ya kanisa ni : 202 785 0982.

Dah hii sasa kali...Mkuu Kinepi naomba usife moyo ukweli utajulikana tu kama walizika jeneza tupu tutajua tu.Endelea na kazi nzuri.
 
Katika historia ya nchi yetu na uafrika kwa ujumla. mazishi ya balali yametia fora kwa kufichwa fichwa. Alikufa wakakaa kimya mpaka waliposukumwa. Hakukuwa na maombolezo yoyote nyumbani kwake Tanzania. Mwali haukuwekwa wazi. Watu hawakuruhusiwa kushiriki mazishi. Kuna watu wamefuatilia majina ya watu waliofariki katika ile county balali alipofialakini hakukuwa na jina lolote la balali.

Kwa nini lakini watanzania tunafanywa mandondocha kiasi hiki na sisi tunakubali tu. Hata kama serikali ilikubaliana na balali aseme ukweli ili asichukuliwe hatua kitendo cha "kumpoteza" walichofanya ni cha kijinga kabisa. lakini wajue ukweli utajulikana tu, sooner than later.
 
Jamani naomba kuuliza. Hivi ndugu na jamaa zake wamefanya msiba hapo bongo??? Kweli hii haingii akilini hata kidogo. Naanza kuamini li-jamaa halijafa................ Linatanua somewhere na mapesa yetu. Nafikiri mama yake anaukweli wote na hawezi kuficha!!!!
 

Jamani mi napenda kujua kitu kimoja:

Mzee ES ana interest gani na kuf/kutokufa kwa Balali mpaka watu wote mnang'ang'ania yeye tu?Yeye alileta ripoti kuwa Balali kafa kutoka kwa vyanzo vya kuaminika toka kwake,hata huyu Kinepi naye kaleta speculation tu (kwani hakuna uthibitishop mpaka sasa) kuwa Balali hajafa,ajabu mnamuunga mkono yeye kwa haraka zaidi bila kumtaka alete ushahidi au hamumng'ang'anii kama Mzee ES.Kilichobaki sasa ni kila mtu aamini chake kama Mwafrika wa Kike,Mtanzania walivyoamua.Kitu kimoja kiko wazi:Balali hatarudi milele Tanzania,cha muhimu kwetu ni kupambana ili tuweze kurecover kiasi kilichoibwa na kuzuia mambo haya yasijirudie tena.

Muda tunaotumia kubishana Balali kafa au hajafa ingekuwa ni busara zaidi kujiuliza kama tunaweza kurecover pesa zetu za EPA na kudili na issues nyingine za ufisadi.

By the way Mzee ES nawa mikono tu kwenye issue hii.
 
masharti ya kuomba dua ya mwisho, ni lazima uone mwili au inasaliwa kutokana na imani ?? huyu padre pengine ni MAFIA TU ! sasa maiti ya nini ? kama hakuona kwa nini aliisalia ? najua alisali kutokana na imani, sasa anasema hakuuona mwili iweje aliisalia "maiti" if it was a bad idea bila ya kuiona ? hamna lolote hapa !

Mkuu maswali mazito haya, inaelekea huyu ni padre kutoka nchi za magharibi mwa Afrika...419.
 
Asante sana kinepi.
Tangu thread ya kwanza kuwa Ballali amekufa, niliandika kuwa hii ni scientific msukule au political ndondocha. Kwa faida yetu- msukule ni pale mtu halisi anafichwa na linazikwa jitu tu, labda gogo au mgomba. Ndondocha ni kama hivyo hivyo. Wanaozika wanaaminishwa kuwa wanazika mtu kumbe la.
Hii ndiyo imefanyika kwa Ballali. Ili afichwe kabisa, hospitalini yawezekana alifanyiwa plastick surgery na kubadilishwa sura. Ebu mkumbukeni Michael Jackson kabla na baada ya plastick surgery - waweza kumtambua?
Pia wana JF, ebu tukumbuke thread ya Mwafrika wa kike. Katika maelezo yake aliandika kuwa alihudhuria mazishi yale, lakini kwa asilimia 95 anaamini Ballali hajafa.
K
Mwafrika wa kike tulikuuliza maswali ya jeneza kufunguliwa hukujibu ila uliahidi kufuatilia hati ya kifo -je umekwama wapi?
 
Back
Top Bottom