Kifo cha Mwalimu Nyerere 14/10/1999, ulikuwa wapi?

Daaah... Niko darasa la nne nakumbuka ilikuwa saa nne ivi tukiwa class mwalimu akatuambia tuende Home kuna msiba mkubwa
 
hahaha kumbe wengi wadogo humu. nlikua kazini mitaa ya ohio Dar. kazini ilikua ni mwaka wa pili. chuo nlishamaliza na CPA juu.
Ipo aja ya kuifadhi id za watu humu ili utakapokuwa unabishana naye ujue ana umri gani
 
Kumbe huku % kubwa ni watoto ?,ushauri wangu ni huu,suala la umri lizingatiwe ili uweze kuwa member wa jf,pls wahusika walifanyie Kali
Na utagundua kuwa ukiandikwa uzi wa lugha ya malkia wanalalamika kweli utadhan umeandika kichina,
 
Haaaa,kwel wkt ule tulikuw tunamaliza mwezi wa9,i think,lkn nakumbuka nilikuw Primary level
 
Mi hata sikumbuki nilikua wapi ,niliona watu wamejaa kwenye tv nilivyoona watu wengi kwenye tv wanalia na kuzimia nami vimachozi vikanitoka nikawa nashangaa kweli baadae nikaenda zangu kucheza makopo sikua na muda mie
 
Nilikua shuleni darasa la5, kengele ikapigwa ya dharura tukajulishwa msiba wa taifa tukarudishwa home

Njiani tunakutana na nyimbo za maombolezo basi tukaanza na sisi kulia hasa tulivosikia vita itakuja.,.
Kumbe kakubwa wewe
 
Mlikua mnalilia nini sasa
 
nakumbuka nilikua form one tulikua break time ya saa nne tunarudi darasani mwalimu anatupa hizo taarifa bas duh kama tulinyeshewa na mvua jinsi ya masikitiko tuliyokua nayo utafikiri tumefiwa na baba zetu wa kutuzaa, hahaha kweli ujinga mzigo
 
Nilikua LA pili mudio primary tumekaa madrasa usiku stori zikaanza nyerere kafa lazima vita vitokee mi nkasema siendi mahali ntakua nalala zangu huku darasani. Miaka imesonga
Ndugu umenikumbusha mbali na hyo 'lazima vita vitokee'
 
I got my first date on this day. Fidelia akisoma hii anakumbuka nafikiri. Nakumbuka nlikuwa secondari form 5, tukatangaziwa mwl. Nyerere kafariki. Huyu dada alichelewa kureport alivyokuja akakaa next to my desk so mwandiko wake na wangu ulikuwa unafanana, baadae akaniomba nimsaidie kuandika notes, kazi niloifanya kwa uaminifu sana. Sikujua kumbe na tabia zilikuwa zinafanana, ila nlikuwa mwoga kutongoza. Rafiki yangu Michael ndo alinipelekea mpaka gest baada ya mm kuimba mashairi yakaniisha mdomoni. Siku hii ndo siku niloanza mapenzi. Mpaka leo tunawasiliana japo si kama wapenzi bali ni marafiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…