Kifo cha Sokoine: Watoto wake wataka mwili uchunguzwe kubaini kama alikufa kwa ajali au la!

Hivi siku hizi siku ya wajinga imekuwa extended na kuwa mwaka mzima?
Huyu Sokoine mbona hatukusikia mazishi yake mwaka jana? Lowassa kwenda mazishini saa saba usiku tuelewe nini?
Au ndio tambiko la kuchukua nchi mwaka 2015? Utata mtupu
 
Post mortem inawezekana hata baada ya miaka mia. Lakini ikiwa wanachakachua post mortem ya maiti mbichi, itakuwaje katika mifupa? Kwa Tanzania ya sasa, hili ombi lao limetoka mapema sana; labda mpaka CCM watoke madarakani.
 

kupima inawezekana ata kama ingekuwa miaka 100

wamtapima mifupa DNA kugundua ni yake kweli au waliìbadili?

Watapima mifupa ilivyoharibika je ni kwa kugongwa au kupigwa risasi au kulishwa sumu kabla ya ajali. Mifupa itaonesha tu

Manufaa ya uchunguzi ni kuzuia uwezekano wa kuwa na vifo vingi vya kupangwa kwani vinatishia usalama.

Ila habari iliyopostiwa ni ya kutunga tu. Kwani watoto hao wa sokoine ni nani na nani?
Wako wapi na wanashuguli gani? Waliyasema wapi haya
 
Kuna list ya utata wakikubali hayo,watajivua nguo mara nyingine tena!hawatakubali kamwe!wakubali kuwa Mungu awalaze mahala pema peponi na wapumzike salama!
 
Umepewa source kwanini usisome gazeti husika ukajiridhisha badala ya kudai ni uongo?
 
Hata watoto wa Chacha Wangwe, nao wanataka mwili wa baba yao ufukuliwe uchunguzwe upya kama kweli alikufa kwa ajali.
 
Sasa kama hakufa kwa ajali iweje? Ashakufa biashara imekwisha.
 

There is more than postmortem my friend
 

mkuu nyetk, HAPO KWENYE RED.

sayansi ya kupima kama marehemu alifariki kwa ugonjwa gani au hujuma ipo hapa duniani hata iwe ni miaka mingapi. kama ni msomi Mzuri wa historia kumbuka ugunduzi wa mwili wa farao wa kale kijana aitwae TUTANKHAMUN ambao ulizikwa karne nyingi zilizopita na kufukuliwa na ma archeologists pale the valley of kings, misri miaka kati ya 1928 - 1930s kama sikosei.

madaktari waliweza kugundua kifo chake kilisababishwa na nini na mambo mengine kadha wa kadha juu ya afya farao huyo kijana aliyetawala kipindi kifupi sana. tena madaktari wa enzi hizo mwaka 47 waliweza sembuse sasa technology imekuwa kubwa sana . kifupi hilo linawezekana kabisa mkuu.
 
Wamechelewa sana. Wametokwa imani juu ya serikali ya chama chao.
 
OOOOOOhhhhhooooo! mtatufanya tuuibe huo mwili tuwawekee mwingine!
 



Mwenyewe nimejiuliza why this?


Na naona Sokoine sasa kaibuka sana, kuliko miaka ya nyuma


I think nia ya urais inahusika hapa...kuna jambo the don anataka kutuaminisha na kupata sijui sympath ya watanzania, ila anajua yeye, sio bure.
 

1. Wakati Sokoine anafariki wanae walikuwa bado wadogo, hawakuwa na uelewa na pia hawakuwa kama ilivyo sasa.

4. Muhimu ni kujiridhisha na sababu cha kifo chake. Itasaidia kuwea historia sawa na hata inaweza kuwa fundisho kwa kizazi kijacho, kuwa uhai unathamani hivyo unapopotea /kupotezwa sio jambo la kufunika Kombe mwanaharamu apite.

Au sio chaliii
 
Post mortem inawezekana hata baada ya miaka mia. Lakini ikiwa wanachakachua post mortem ya maiti mbichi, itakuwaje katika mifupa? Kwa Tanzania ya sasa, hili ombi lao limetoka mapema sana; labda mpaka CCM watoke madarakani.


Tena washauriwe wanyamaze. Otherwise, wakifanya mchezo, hata hayo masalia ya mzazi wao kuna siku watakuta yametoweka na ndio utakuwa mwisho wa kila kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…