Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii habari inanichanganya. Nakiri kwamba sikuwahi kusikia kabisa habari za mazishi ya pili ya Ndugu Edward Moringe Sokoine hapo mwaka jana (sijui ni tarehe zip za mwezi upi?). N'nachokumbuka tu ni kwamba Moringe tulimzika katikati ya zizi la ng'ombe kijijini kwao Monduli na zizi likaendelea kutumika kusetiri ng'ombe kama ilivyo desturi yetu. Nakumbuka mengi yalisemwa baada ya kifo cha Moringe; ya kishirikina na ya kimafya kinyume kabisa na "post mortem report" ya madaktari. Leo ninapopata habari kama hii najiuliza maswali yafuatayo:
- tangu Sokoine afariki tarehe 12 Aprili 1984 hao watoto wake walikuwa wapi?
- Post mortem investigation hufainyika ili kubaini sababu za kifo cha marehemu si kwa malengo ya maelezo na kumbu kumbu tu bali pia ili kuchukua hatua kama kuna ushaidi wa kutosha kwamba kifo kimesababishwa na uzembe au makusudi ya mtu yeyote. uchunguzi huu ukifanyika sasa na ikagundulika kuna mazingira ya kuwa kifo kilisababishwa na makusudi au uzembe wa yeyote itasaida nini iwapo wasabishaji walishakufa miaka mingi?
- Mazingira mazuri zaidi ya kufanya post mortem investigation ni wakatimwili bado mbichi kikemikali. Kwa hali ya kifo hiki cha takribani miaka 29 tangu kitokee na mazingira aliyozikwa (na kuzikwa tena baada ya tetemeko) huo uchunguzi utatumia sayansi ipi?
- Uchunguzi huu unachochewa na nini sasa hivi na una maslahi gani kwa taifa na familia (kwa hao watoto wa marehemu?)
siri kubwa kuhusiana na kifo cha sokoine anayo lowassa, kwa hili hata jkn alikuwa anamgwaya sana edo! Mnakumbuka jinsi ambvyo edo alimtaka jkn aende monduli kumsafisha baada ya kumtuhumu kuwa alimchafulia jina kwa kauli zake? Captain lowassa ana mambo mengi ambayo akiamua kuyaweka hadharani watu wengi sana watabadilika kimitazamo!
Sijui kwanini ameamua kukaa kimya hata pale ambapo huwa anaonewa wazi kabisa! Kuna watu ambao hofu haziwaishi kwa kuogopa kuwa ipo siku atalipiza kisasi kwa wanayomtendea hivyo kuzidisha kasi ya kuendelea kumchafua.
...moringe aliuawa na hili halina pingamizi! Kuna watu walikuwa hawako radhi kumuona mtu anambishia jkn...walikuwa wanauwezo wa kukupoteza faster then wanaenda kumpa taarifa! Wakati mwingine jkn alikuwa anaishia kusikitika tu maana hakuwa na uwezo wa kurejesha uhai!
Natamani mwili wa balali uchunguzwe kwanza.
tangu 1984 mpaka 2013 ndio uchunguzi uanze???? hata kama ni wabaya wake watakuwa wamenusurika katika kipindi hiki cha miaka 30 iliyopita wawe hai?
kweli kabisa mkuu kuna mambo muhimu ya kuchunguza kwanza kabla ya yale ya zamani.Naunga mkono hoja, na hata wakitaka tuchangie gharama za kufanikisha zoezi la uchunguzi niko tayari kuchangia
Saa saba za usiku???!!
Katika hali ya kushangaza,watoto na baadhi ya ndugu wa aliekuwa waziri mkuu wa Tanzania,marehemu Sokoine, wanataka uchunguzi ufanyike wa mwili wa marehemu ili kubaini kama ni kweli kifo chake kilitokana na ajali au laa.
Uamuzu huo ulofikiwa mara baada ya mwili wa marhemu Sokoine kuzikwa upya mwishoni mwa mwaka jana baad ya kabuli la awali kuharibiwa na tetemeko la ardhi katika milima ya Oldonyo Lengai.
Taarifa zinasema wanafamilia hao wanakusudia kuomba kibali serikalini ili wataalamu waufanyie uchunguzi mwili huo kubaini chanzo cha kifo chake.
Kulingana na taarifa za gazeti la Tanzanian Daima la tarehe 07/04/2013,ambapo habari hii imeelezwa kwa kirefu zinasema uamuzi huo ni kutokana na hofu kuwa huenda kifo chake kilitokana na hujuma za wale waliokuwa wakimpinga hayati Sokoine katika vita vyake vya kupambana na wahujumu uchumii wakati huo.
Imeelezwa mh.Lowassa ni miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi hayo yalifanyika saa saba za usiku mwishoni mwa mwaka jana.
CHANZO:TANZANIA DAIMA ONLINE.