Kifo cha Steven Kanumba Kimedororesha Tasnia ya Filamu Tanzania

Kifo cha Steven Kanumba Kimedororesha Tasnia ya Filamu Tanzania

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
Habari za sasa wadau wa celebrities forum. ni matumaini yangu mu wazima kabisa!

Jalada lililoko mbele yenu sasa linazungumzia mustakabali mzima wa tasnia ya filamu Tanzania ambayo imepewa jina la bongo movies. tasnia hii imekuwa ni sehemu ya soko la ajira la vijana wengi ambao wamekuwa na vipaji mbali mbali vya uigizaji na hata ambao hawakuwa na vipaji lakini wamefunzwa na kuweza kumudu mikiki mikiki ya filamu kama vile Jackline wolper, ray na kajala masanja, hawa ni baadhi ya wasanii tu ambao wameingia kwenye tasnia by influence of others, lakini kwa bidii zao wameweza kumudu haswaa soko la ndani la filamu Tanzania. sijafahamu hali ya nje huko ikoje, lakini kwa upande wa ndani, kwa kiasi fulani wanasikika japo si saana!

Aidha, tasnia hii ya filamu bongo, historia iaonesha kuwa ilianza mnamo miaka ya 2000 kama sijakosea na filamu za kwanza kwanza kurushwa zilikuwa ni kama filamu ya girlfriend, filamu ambayo ilifanya vizuri kiaina fulani sokoni kulingana na hali ya kiuchumi kwa kipindi kile na watanzania waliipokea kwa mikono miwili japo awareness juu ya industry haikuwa kubwa saana kwa vile ndo kwanza watu walikuwa wanaanza.

Kadri miaka ilivyokuwa inasonga pole pole, ndivyo vijana mahiri katika tasnia walivyokuwa wanajitokeza kutoka makundi mahiri yaliyokuwa yanajihusisha na ukuzaji wa vipaji vya wasanii kama vile kaole sanaa group ambapo waliweza kuwapika wasanii manguli katika tasnia kama STEVEN KANUMBA THE GREAT na RAY THE GREATEST.

Wasanii hawa wamekuwa chachu hasa ya ukuwaji wa filamu Tanzania ambapo kwa kiasi fulani waliweza kuikuza tasnia na kuweza kupendwa katika mataifa ya nje (afrika mashariki kwa ujumla) kama kenya, uganda, rwanda drc na mataifa mengine yanayozungumza lugha ya kiswahili. mbali na hawa manguli wawili, kuna wasanii wengine pia ambao wamekuwa wasaidizi wakuu hasa katika ueneaji na upendekaji wa filamu hizi za kibongo kama vile wema sepetu, jackline wolper, irene uwoya, aunt ezekiel na wengineo kadhalika, achilia mbali wasanii wanaoigiza filamu za futuhi.

HALI YA SOKO LA FILAMU BAADA YA KANUMBA KUFARIKI DUNIA APRIL 2012.

Ni miaka miwili sasa karibia itimie toka kufariki kwa mpendwa wetu, steven kanumba, steven kanumba alikuwa muhimili mkubwa sana katika taifa hili la Tanzania katika soko la filamu kwa ujumla. SK aliweza kuitangaza nchi yetu kupitia filamu alizokuwa akifanya kwa kuwashirikisha wasanii mbali mbali wa nje kama vile wasanii kutoka nollywood (actually hawa ndio wanaoongoza kwa ubora AFRIKA) kama vile ramsey noah katika devil's kingdom na katika filamu nyingine ya dar to lagos. SK alikuwa mtu wa kujituma, haogopi challenges zilizokuwa zinamkabili, alikuwa anapambana sana na alitoa filamu zenye ubora kwa kiasi kikubwa.

Toka mpendwa wetu SK atutoke toka mwaka juzi, soko la filamu limekuwa mikononi mwa giants kama Ray, Jacob Steven, mtitu william na akina dada kama jack w. gambe, wema sepetu na irene uwoya. watu hawa ni moja kati ya mihimili ambayo tunaitegemea isukume gurudumu la filamu Tanzania toka kufariki kwa mpendwa wetu SK na hata kabla yake kwa sababu ni wajibu wao kufanya hivyo kwa sababu wao ndio wako kwenye soko kama giant producers.

Hali ya upepo wa filamu toka April 2012 imekuwa tofauti sana na sasa!!! soko la filamu limedorora sana kulingana na hali ilivyokuwa zamani. kwanini siku hizi hatuoni vitu hot na vynye ubunifu na bashahsha kama vile vya enzi za kanumba? kwanini hawa wasanii wetu wa sasa wamebweteka namna hii? najua STEVEN KANUMBA alikuwa na uwezo mkubwa saana katika soko, lakini sasa, wasanii hawa wa sasa wameshindwa nini hasa kuigwa kutoka kwa STEVEN?

Jitihada kidogo tuliziona kutoka kwa wema sepetu pale alipotaka kufanya muungano ja omotola jalade kutoka NIGERIA. wema alijitangaza sana kwamba atatengeneza filamu moja na huyu dada celebrity wa nigeria na dunia kwa kiasi kikubwa. hii ilikuwa nafasi ya dhahabu kwa wema binafsi, wasanii wengine wa filamu Tanzania, na hata taifa kwa ujumla! najua ni nafasi ndogo kiasi, lakini ni kubwa sana endapo ingefanyiwa kazi, mfano halisi labda tuone kwa diamond, kitendo cha dp kutoka kimuziki na kuwashirikisha wasanii wa nje kama davido, kimeshampa mwanya wa kutoka kwa soko la nje na kimataifa kwa ujumla! vivyo hivyo kwa tasnia ya filamu tanzania.

Mbali na wema, tunao wasanii wengine kama ray, lulu michael, jacob steven, jackline wolper, irene uwoya, aunt ezekiel, mtitu william na wengineo. ni nini hasa kinawafanya hawa wasitoke nje na kuiwakilisha nchi kisanii? kwanini wanshindwa ku -master soko la ndani kwa kuanzia tu basi, huko nje itakuwaje wadau?

Kwa kumalizia tu niseme, kufariki kwa steven kanumba, the great, kumeweka doa katika soko la filamu na filamu kwa ujumla katika nchi ya TANZANIA. hakuna msanii kwa sasa anaeonyesha jitihada zake kupeleka tasnia nchi kwa nguvu!!
filamu zetu bado ziko katika kiwango cha chini sana! tena sana! nimpe hongera mzee chillo wa pilipili entertainment kwa kuweza kuchukua tuzo ya filamu bora ya kiswahili kutoka africa magic swahili (kama sijakosea). lakini bado, bongowood sijui bongo movies badotuko nyuma sana! viongozi wanaendesha uongozi kwa unafiki, chuki na ukosefu wa elimu baina zao wenyewe!

BADO NAAMINI KUWA BONGO MOVIES ILISHIKILIWA NA STEVEN KANUMBA!

Karibuni kwa maoni.. kosoa unapoweza, jenga unapoweza!
 
yote ni sahihi kwangu kinachokosekana ni uwekezaji mkubwa na pia regulator wa hii tasnia....
 
yote ni sahihi kwangu kinachokosekana ni uwekezaji mkubwa na pia regulator wa hii tasnia....

mkuu unajua wawekezaji wakati mwingine wanavunjwa moyo na hawa wakongwe wenyewe!

hawajui kuji motivate wenyewe wasaidiwe.. sidhani kama walishawahi kuomba msaada wowote ili wasaidiwe!
 
Mkuu Excel kwa haraka haraka naweza sema ndio lakini kwa upande mwingine naweza nikapinga kichwa cha habari kuwa kifo cha kanumba kime dororesha tasnia ya filamu.

Binafsi toka Kanumba afe sijawi kununua filamu yeyote na kusema kweli nilikuwa na nunua sana hili siku za weekend nisikose m cha kuangalia ,pia nilikuwa na vutiwa na uigizaji wake.

Tasnia ya filamu tanzania ina waigizaji wazuri wengi kaama wakina Ray,JB a ambao kweli wana jitahidi kigiza hasa Jb ndio nilimtegemea ange endelea kuipaisha hii tasnia lakini cha kushangaza tasnia kweli imepoa sana tukilinganisha na kipindi alicho kuwepo kanumba.

Mimi nafikiri hawa waliobaki wamekosa ujasiri,uthubutu na ubunifu maana ina hakika kuna wanao jua kuzidi wakina Kanumba hasa niki muangalia JB.

Kwakweli tasnia himepoa sana tena sana na nina kuhakikishia miaka minne ijayo Tasnia ya filamu hitasaulika kabisa maana hakuna juuhudi za kuiendeleza.

Alaf aina za filamu wanazo zipeleka soloni hazikidhi nahitaji ya wateha na tunajua fika wateja wakubwa wa filamu hizi ni wattoto na watu wazima ambao wangependa kuangalia na familia zao.

Lakini kwa sasa ni filamu chache unaweza kukaa na watu wazima au watoto wajaangalia lasivyo utaambulia aibu maana si nzuri walahazifai kwa kuangalia na watoto au watu wenye heshimaa zao.

Hakika Tasnia ya Filamu hinahitaji mabadiliko lasivyo hikifika 2018 hakuna atakayejua kama kulikuwa na Tasnia ya filamu.
 
Last edited by a moderator:
Kanumba was a hardworking Actor........ingawa kwa vipaji wapo waliomzidi lakini ndio hivyo hawajitumi kabisa(Sijui wamerogwa)
Binafsi siwezi kusema tasnia imedorora moja kwa moja sababu kuna wasanii wazuri wanaohitaji 'kukuzwa' na sisi....
JB ni Legend ambaye huwezi kuresist kununua kazi zake na huwa hanidissapoint kwakweli....Kuna kaka(nadhani ni zao la JB)anaitwa Salim Ahmed huwa anaigiza kwa ascent ya kimakonde na pia huwa ana'act kawaida pia....ana potential sana....Movie alizocheza ni pamoja na:
-Fikra Zangu(mfanya usafi mwenzake GAI)
-Safari(Kama kijana mchawi)
-Bado Natafuta(Kinara Mkuu,Muuza Maji)
-Danija(Fundi Gari Mlemavu)

Kuna Adam Kuambiana....Very great but nadhani ni mvivu na hajitumi ipasavyo ingawa akisimamia 'Show'...you will be like 'WOW'
Na ana ung'eng'e unaoweza kumpush japo Afrika ya Magharibi hapo......Anayemjua,Amwamshe....

Kuna kazi kubwa kwa wasanii wetu wa kike.....Naogopa hata kuwagusa.
 
Wasanii wa kike monalisa hana mpinzani kama akiamua kufanya international movies, huyo jamaa anaitwa GABO, huyu jamaa ni next level..ni mbya sana na kuna mwenzie anaitwa slim omary
 
single mtambalike na JB hawa ndo hatari ila hawajajiua bado!
 
Kanumba was a hardworking Actor........ingawa kwa vipaji wapo waliomzidi lakini ndio hivyo hawajitumi kabisa(Sijui wamerogwa)
Binafsi siwezi kusema tasnia imedorora moja kwa moja sababu kuna wasanii wazuri wanaohitaji 'kukuzwa' na sisi....
JB ni Legend ambaye huwezi kuresist kununua kazi zake na huwa hanidissapoint kwakweli....Kuna kaka(nadhani ni zao la JB)anaitwa Salim Ahmed huwa anaigiza kwa ascent ya kimakonde na pia huwa ana'act kawaida pia....ana potential sana....Movie alizocheza ni pamoja na:
-Fikra Zangu(mfanya usafi mwenzake GAI)
-Safari(Kama kijana mchawi)
-Bado Natafuta(Kinara Mkuu,Muuza Maji)
-Danija(Fundi Gari Mlemavu)

Kuna Adam Kuambiana....Very great but nadhani ni mvivu na hajitumi ipasavyo ingawa akisimamia 'Show'...you will be like 'WOW'
Na ana ung'eng'e unaoweza kumpush japo Afrika ya Magharibi hapo......Anayemjua,Amwamshe....

Kuna kazi kubwa kwa wasanii wetu wa kike.....Naogopa hata kuwagusa.
Mkuu huyu jamaa ametulia sana, nilibahatika kuiona filamu yake ya bado natafuta kwa kweli iliniliza sana. hasa pale mwishoni anapomlilia mkewe Patricia na mtoto wake. ni nzuri kuangalia na familia maana hakuna mambo ya ajabuajabu .....nashukuru umenipa jina la hiyo filamu lazima niikainunue maana niliiona kwenye Basi ila nilikua siijui inaitwaje.
 
Unajua tofauti ya Kanumba na wengine ni hii. SK alikuwa akiona mbali na alikuwa na kiu sana ya mafanikio kupitia filamu.
Alitaka kufika mbali nadhani angetaka kuwa Lupita Nyong'o wa kiume kutoka East Africa kufanya kazi Hollywood.

Hawa wengine ni bora liende hawajali ubora si kitu kutoka katika mioyo yao, wala sidhani kuna mtu anafanya jitihada za kufika mbali.
Tungeanza kuona mwanga wa yoyote ila ni kama wamelala, wametosheka na mafanikio waliyopata.
 
kwanini hawa wasanii wa kibongo hawataki kwenda shule kujiongezea ujuzi, yaani ni kama vile kuna sheria inayowabana wasiende kusoma. Wengi wao wanaishia kuwa typecast, wanachoweza ni kukariri mistari ya maongezi na kuweka make up
 
Mkuu Excel kwa haraka haraka naweza sema ndio lakini kwa upande mwingine naweza nikapinga kichwa cha habari kuwa kifo cha kanumba kime dororesha tasnia ya filamu.

Binafsi toka Kanumba afe sijawi kununua filamu yeyote na kusema kweli nilikuwa na nunua sana hili siku za weekend nisikose m cha kuangalia ,pia nilikuwa na vutiwa na uigizaji wake.

Tasnia ya filamu tanzania ina waigizaji wazuri wengi kaama wakina Ray,JB a ambao kweli wana jitahidi kigiza hasa Jb ndio nilimtegemea ange endelea kuipaisha hii tasnia lakini cha kushangaza tasnia kweli imepoa sana tukilinganisha na kipindi alicho kuwepo kanumba.

Mimi nafikiri hawa waliobaki wamekosa ujasiri,uthubutu na ubunifu maana ina hakika kuna wanao jua kuzidi wakina Kanumba hasa niki muangalia JB.

Kwakweli tasnia himepoa sana tena sana na nina kuhakikishia miaka minne ijayo Tasnia ya filamu hitasaulika kabisa maana hakuna juuhudi za kuiendeleza.

Alaf aina za filamu wanazo zipeleka soloni hazikidhi nahitaji ya wateha na tunajua fika wateja wakubwa wa filamu hizi ni wattoto na watu wazima ambao wangependa kuangalia na familia zao.

Lakini kwa sasa ni filamu chache unaweza kukaa na watu wazima au watoto wajaangalia lasivyo utaambulia aibu maana si nzuri walahazifai kwa kuangalia na watoto au watu wenye heshimaa zao.

Hakika Tasnia ya Filamu hinahitaji mabadiliko lasivyo hikifika 2018 hakuna atakayejua kama kulikuwa na Tasnia ya filamu.

well said mkuu!

points ulizoongea hakika zina apply kabisa katika soko letu la bongo movie.

movie nyingi zinazozalishwa ziko irrelevant na mahitaji ya soko, japo wasanii wanajitahidi sana kustick kwenye jamii inachofanya!

lakini mkuu, jambo ambalo najiuliza, je jamii ya kitanzania ina mwamko kweli kupokea filamu za kitanzania? ama watengeneza filamu wenyewe ndio hawajawajenga watanzania kisaikolojia kupokea kazi zao?

bollywood na nollywood zimeendelea sana recently pamoja na hollywood na zimefikia hatua ya kulikamata soko la filamu duniani! je, kwa sisi tanzania, tatizo liko upande gani? wasanii? watanznania wenyewe ama serikali?
 
Mkuu huyu jamaa ametulia sana, nilibahatika kuiona filamu yake ya bado natafuta kwa kweli iliniliza sana. hasa pale mwishoni anapomlilia mkewe Patricia na mtoto wake. ni nzuri kuangalia na familia maana hakuna mambo ya ajabuajabu .....nashukuru umenipa jina la hiyo filamu lazima niikainunue maana niliiona kwenye Basi ila nilikua siijui inaitwaje.

Ni nzuri kwakweli na anapjua sana yule kaka.....
 
Mkuu Excel unamaanisha nini kusema Chillo wa pilipili entertainment?
BTW topic nzuri.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Excel unamaanisha nini kusema Chillo wa pilipili entertainment?
BTW topic nzuri.

mkuu mzee ahmed olotu a.k.a mzee chillo ana share katika kikundi cha pilipili entertainment, kama alivyonieleza mwenyewe..

thanks for accredition any way.

you can ask again if you are not enough satisfied...
 
Hongera uzi wako umechambua hii tasnia kwa upana wake na pale juu una like yangu maridadi kabisa though kuna upande naweza kuchangia katika mtazamo tofauti kidogo
Toka zamani sio mpnz kabisa wa BONGO MOVIE hii ni kutokana na wepesi ambao binafsi nauona kwny movie zao chache nlizotazama ni zile ambazo watu walizipa sifa sana and i do agree few of them ziko poa,Kanumba kifo chake ni km starting point ya downfall ya bongo movie ila kwa uhalisia tasnia yote imeoza hata wkt yy akiwa hai it is like timed bomb angekua hai naamini lingelipuka akiwepo pia.
Kudorora ni matokeo ya bongo movie kua genge la wahuni flani wasio na weledi wa kufanya movie na Kanumba kachangia maana hawa wanaosumbua leo kwa skendo za ulevi,umalaya na ukosefu wa maadili na yy alichangia kuwaletea akiangalia kigezo cha uzuri wao tu akiamini kuigiza watajua baadae ndo vile movie zikawa ni sehemu ya kuuza sura na kuonyesha magari na majumba upuuzi mtupu na leo ndio hawa kawaacha na wanaitwa waigizaji bora wa kike i reality hamna kitu kbs ni vile wana sura nzr na makalio basi.
R.I.P Kanumba kuna mchango wako pia kwny kuinua tasnia pia kwa namna moja ila wapo ambao nikiwaangalia naamini wana mchango mkubwa toka enzi za maigizo ila tasnia ikatekwa na watu wenye mtazamo wa karibu.
 
% kubwa yacc waTZ 2natatizo mapema ht km KZ ze2 hazilidhishi utakuta Movie ina Stori nzuri lkn Namna inavyochezwa igizo la jukwaani Wanaishia kujicfu na wadada kuvaa NUSU uchi kwisha Tatizo lingine kubwa nnaloliona hakuna Waalim wazuri wakuTrain waigizaji zaidi ya kukaririshwa scprit2 pia kushoot Movie kwa Camera 1 inapunguza Filling ya Scene! Ila kuna cku nilikuw safarini TANGA niliona FILM inaitwa BADO NAFUTA kuna Jamaa ailiigiza as JAMES,Honestly,RESPECT kwake naomba anihesabu kuwa mi ni SHABIKI wake!
 
% kubwa yacc waTZ 2natatizo mapema ht km KZ ze2 hazilidhishi utakuta Movie ina Stori nzuri lkn Namna inavyochezwa igizo la jukwaani Wanaishia kujicfu na wadada kuvaa NUSU uchi kwisha Tatizo lingine kubwa nnaloliona hakuna Waalim wazuri wakuTrain waigizaji zaidi ya kukaririshwa scprit2 pia kushoot Movie kwa Camera 1 inapunguza Filling ya Scene! Ila kuna cku nilikuw safarini TANGA niliona FILM inaitwa BADO NAFUTA kuna Jamaa ailiigiza as JAMES,Honestly,RESPECT kwake naomba anihesabu kuwa mi ni SHABIKI wake!

Here you go:....JAMAA anaweza ila sasa...hizo 2:....2...Sio mpango wala nini....Au vipi?
 
Back
Top Bottom