Kifo cha Steven Kanumba na hatma ya Elizabeth Michael (Lulu)

Kifo cha Steven Kanumba na hatma ya Elizabeth Michael (Lulu)

Msaniii ambaye amejizidishiwa umaarufu ndani na nje ya mipaka yetu hasa kufuatia kuhusishwa na kifo cha msanii nguri Kanumba, bibi Elizabeth Michael almaarufu kama LULU, amefikishwa leo mbele ya pirato pale mahakama ya Kisutu. Kwa mujibu wa mtoa habari, Lulu amesema ana miaka 17.. kesi imeahirishwa mpaka tarehe 23/4/2012..
Kama kuna mtu ana habari zaid ya hizi naomba atujuze kwa uzuri tu,, maana mi nimesikia ikiishia ishia..

Souce Radio One mchana huu.

Nawsilisha wakuu

Mashitaka yake ni ya kuua kwa kukusudia au bila kukusudia? Hivi murder case si mtuhumiwa ubaki kimya mpaka mahakama kuu? Kama ndio, iweje Lulu aongee mahakamani?
 
Wadau ni kwa nini Ramsey Nouh,business associate na close friend wa Marehemu Kanumba kashindwa kuja kumzika rafki yake?
 
Mhhhh..is it?Labda mimi sizijui sheria za nchi yangu,hivi mtu ili kupewa driving licence inabidi awe na umri gani?Kama kako 17 hilo gari wanalosema kalikuwa kanaendesha ilikuwa ni kwa leseni ya nchi gani?au hapa inamaanisha waliompa leseni na yeye mwenyewe wanakesi dhidi ya hili?Naipenda Tz,you can do what you want when you want to!​


nchi hii mbona mambo tambarale sana.......huyo mtoto ana mika 18 na miezi 6.....ni mtu mzima huyu....
 
wacha kaende labda katajifunza

maana asiyefunzwa na wazazi.........

hivi hako katoto kana baba kweli?

nadhani hata mamake ndo walewale
 
MUNGU ni mkubwa ukweli utajulikana tu,
Ingawa mara zote Marehemu huwa ana Makosa
Kwa anavyojulikana Lulu tabia yake atasema tu yaliyotokea usiku huo
 
sasa tunaaamini kwamba msanii wa kike kutoka ni ngumu mpaka utoe rushwa ya ngono. afanalek!!!!!!!!!!!
 
Kwa upepo unavyovuma watakachia tu haka katoto.Halafu kaongo sana kwenye mikasi kalisema kana 18 mahakamani kanasema kana 17 kanatafuta huruma ya mahakama naona.Kakitoka lazima utasikia kameokoa kimbuka kilichompitia hata kaa kamwe akasahau

lulu si mtoto aliwezaje kumbeba kitandani marehemu Kanumba, kusukuma mpaka ubongo ucheze kweli kiboko
 
Hizi habari zinachanganya kweli kweli, sasa alikataa kutoka naye lakini walikuwa all the way naked?

Wivu ulikuwa ni wa kukataliwa kitu gani?Ama wa kuongea na simu na boyfriend mwingine?

Huyu mtoto kuna mtu anamcoach namna ya kuzungumza, tatizo ni "miluzi mingi humchanganya mbwa".
 
My story baada ya kusikia stori tofauti tofauti za Lulu na Sethi, mdogo wake Kanumba, kwa mtazamo wangu inaonekana stori halisi iko hivi:

Kanumba alimpigia simu Lulu aje watoke out. Akamtaarifu na mdogo wake ajiandae. Mdogo wake akajiandaa. Lulu akaja. Akiwa hapo kwa Kanumba akapigiwa simu/ akatumiwa meseji na mwanaume mwingine (huyo mbongo fleva) akimtaka waonane. Lulu akaanza kutoa visingizio kuwa hataki kwenda tena 'club' bali anataka kurudi nyumbani. Kanumba akawa na wasiwasi ni kwa nini atake tena kurudi nyumbani wakati ashafika kwake! Mzozo ukatokea. Wakati bado wakiwa katika mzozo Lulu akapigiwa simu tena na huyo mwanaume kumtaarifu kuwa kafika hapo kumpick. Lulu akapokea hiyo simu mbele ya Kanumba lakini akaanza kuongea huku akitoka nje. Kanumba akawa ashaelewa nini kinaendelea. Akamfuata kwa hasira na kumrudisha ndani kisha kufunga mlango. Zikaanza purukushani za kugombania funguo kutoka nje. Katika hizi purukushani Kanumba akaanguka (maybe kwa kusukumwa au kuteleza). Lulu akapata chance ya kufungua mlango na kutoka. Hapo nje akamwamwambia Sethi kuwa kakako yuko kadondoka huko chumbani, kwa sababu tayari alikuwa na wasiwasi kuwa Kanumba kaumia sana. Akapanda gari lililokuwa linamsubiri hapo nje akaondoka. Sethi akaenda kumcheki kaka yake akampigia daktari. ...........
Kati ya stori zote, hii ina make sense zaidi.
Huyo "mbongo fleva" aliye "panda dau" ndo nani?
Kweli huyu mtoto wenge sana!Kama funza, hatulii?
Ni heri angeyeyusha kivingine, arudi zake home halafu huyo mbongo fleva akamchukue kutoka nyumbani anapoishi.
Swali ambalo bado najiuliza ni mazingira ya kukutwa uchi kwenye ugomvi, how possible?
Na kwanini wawe uchi wakati wa ugomvi?What was going on at the time?
 
nilimskia mwenyewe kwenye tv akisema ana miaka 18, hadi salama akawa anamtania kuwa kwahiyo sa ivi disco hakataliwi kuingia tena kama pale mwanzo akisumbuliwa na mabaunsa, leo ana 17 tena? aliona utu uzima raha eeh??? wenzake wanashusha miaka yeye akaona sifa kuongeza, haya sasa 18 iyo Mungu kamuonyesha utu uzima ulivyo na mengi.

Brother Kanumba nae alituambia kwenye kipindi cha Salama Jabir kuwa hana Mchumba wala Girl friend, na pombe huwa hagusi kabisa, ilikuwa Jack Daniel mwilini mwake? na ni pombe kali si ya kujifunzia tuseme labda alikuwa anafunza. Kweli bongo ni zaidi ya uijuavyo? Why ufiche the really u? Unajidanganya hadi wewe mwenyewe? unaudanganya mwili wako mwenyewe? then unapata nini?
Pumzika kwa amani Kanumba. Lulu ilikuwa itokee mwakani ungesema una 17 vile vile.
 
Kwa mujibu wa sheria mtu anatakiwa kushikiliwa bila kufikishwa mahakamani kwa saa 24 tuu!.

Lengo la kumfikisha mahakamani ni kumsomea tuu sababu za yeye kushikiliwa na hatatakiwa kujibu chochote. Kama ana wakili makini, ni leo leo anapewa dhamana ingawa mahakama inaweza kumkatalia dhamana kwa hoja ya kuhofi

Mkuu, hapa sijakupata vizuri "...leo leo anapewa dhamana..." hv kisheria mtu mwenye tuhuma ya mauaji ni ruhusa kupewa dhamana?!! Hebu nieleweshe kidogo hapo!
 
Huyo si under age kama amefikisha miaka 18 kwa sheria zetu anaweza kuwa na mashtaka ya jinai ndio maana amewekwa jela ya wakubwa. Ila kama yaliyoelezwa na dogo wa marehemu ndio kilichotokea ana nafasi kubwa ya kutolewa. Lakini kama katika upelelezi yatatokea mengine zaidi ambayo DDP anaweza akayajengea hoja ya mauaji ataweza kuhukumiwa kama mtu mzima tu. Tusubiri report ya daktari ndio itamtoa au kumuweka katika jinai. kwa sasa " she is innocent until proved guilty.
 
Wadau ni kwa nini Ramsey Nouh,business associate na close friend wa Marehemu Kanumba kashindwa kuja kumzika rafki yake?
Nimesikia kuwa hivi juzi alipata ajali ingawaje anaendelea vizuri, tena nimepata taarifa nyingine zikisema kuwa hawezi kuja kuuangalia mwili wa rafiki yake kipenzi kwa kuwa hataki kuamini kama amefariki.
 
Wakili wake ni Elizabeth Kaganda?

Hahahaha Nyani!!!!!, Umenikumbusha kundi lake la kina Jennifer M pale Law miaka ilee, walikuwa na vurugu hao.

But I think huyu dada atakuwa ni mwendesha mashitaka maana ni state attorney. Anyway inawezekana maana watu wanabadili majukumu kila kukicha.
 
Nimesikia kuwa hivi juzi alipata ajali ingawaje anaendelea vizuri, tena nimepata taarifa nyingine zikisema kuwa hawezi kuja kuuangalia mwili wa rafiki yake kipenzi kwa kuwa hataki kuamini kama amefariki.

Bora umemwambia yangeanza mengine!
 
Hii ndio hulka ya binadamu. Akitaka ahurumiwe, hujifanya mdogo kiumri; akitaka vya wakubwa wkt yeye ni mdogo, hujitutumua. Unakumbuka ulipokuwa ukienda uwanja wa mpira -- ndevu zilishaanza kuchipua lkn ulitaka tiketi ya mtoto. Na je ulipokuwa unataka kuingia sinema za X wkt ulikuwa ni mwanafunzi wa darasa la nne...!
 
Back
Top Bottom