Kifuatacho baada ya Job Ndugai kujiuzulu, tukae mkao wa kula

Kifuatacho baada ya Job Ndugai kujiuzulu, tukae mkao wa kula

Hiyo mihimili mingne ni kiini macho.ni mihimili yakwenye makaratasi.ndomaana namimi naunga mkono nchi kua na katiba inayijielewa.Katiba ikiyopo inamapungufu menhi ambayo hayaendani na nyakati.
Kabisaa chifu na huo ndo ukweli
 
Nadhan unajidanganya ww mwenyew,tegemeo lao kubwa lipo ktk ile katiba chakavu fullstop
Mnacheza ngoma wanayopiga wao mtaangaika sana na mtawaza na kutafakari sana ila jua CCm ni chama kinachotumia akili sana kuliko maneno na mihemko ya kisiasa

**** uliwai kufuatilia issue ya Rowasa kipindi kile anataka uraisi bas utaelewa kwa nn CCm ni chama kinachotumia akili kuliko chama chochote kile Africa

Wengi walitegemea lowasa ataiua au kuivunja ata kuizoofisha Ccm ila kilicho mkuta ata yy hakuamin alitoka akajikuta katoka pekeake
 
Swali je akiingia speaker mwingine naye pia akaonekana kuihoji serikali, je kutatokea kuombwa kungatuka madarakani
Umekwenda mbali...je atakuwa na uthubutu hata wa kuihoji serikali? Sasa washafumbwa midomo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Natumai sote tuko poa na salama, hakika Mungu ashukuriwe Kwa rehema na neema zake.

Japo nchi na raia wengi wamepokea taarifa za kujiuzulu Kwa speaker wa Bunge Kwa taharuki na mshangao. Lakini swali la kujuiliza hapa, je, nini kutafuta/nini maana ya hii move Kwa maana ya mihimili ya nchi (Serikali, Bunge na Mahakama).

Hakika wengi wanaweza muona Ndugai kama amefeli hivi, Ila ukifanya analysis ya kiuongozi na kisiasa ni kama jamaa ama make a political trap Kwa serikali iliyopo.

Ni kama amatega mtego wa kufungua hoja za kuanzishwa Kwa vuguvugu na Katiba mpya.Kwa nini nasema hivi.Ukitizama Kwa umakini na Kwa kina ni dhahiri na wazi kuwa Ndugai hakufanya kosa kama muwakilishi wa mhimili huru wa BUNGE....japo wengi wanaweza sema namna aliyotumia kuwasilisha hoja yake haikuwa sahihi,lakini swali linakuja,je kuwasilisha huko kulimuondolea ukweli kuwa yeye ni spika wa Bunge....yaani mhimili huru wa nchi.

Move hii ni dhahiri ina inaibua hoja ya je NI kweli nchi yetu ina mihimili mitatu huru yenye Uhuru wa kuhoji na kushauri mhimili mwingine bila uwoga wala kificho.

Jibu ni hapana Kwa kurejelea kujiuzulu Kwa ndugu Ndugai.Hii ni wazi kuwa mhimili mmoja Una nguvu kubwa kuliko mihimili mingine.

Hivyo basi,kifuatacho hapa ni nchi kuingia kwenye mtego wa kuhoji utendaji wa mihimili hii mitatu inayounda taifa la Tanzania.

Swali ni je,nchi itanasa kwenye huu mtego au itajinasua.

Nawasilisha.
Hilo swala la Katiba mpya, wengi wa wana CCM wamekua wakiliona kama wao haliwahusu kwa sababu wanaona linawatibulia mpango wao wa kuongoza milele. Hiki kilichotokea ni mpango wa Mungu kulipeleka Taifa kwenye kuipata Katiba Mpya. Watanzania wote bila kujali itikadi za vyama na tofauti zingine, tulione swala la Katiba Mpya ni la lazima. Katiba iliyopo ya 1977 ilikua ni ya chama kimoja cha CCM, haiwezi kukidhi matakwa ya sasa. Tupate Katiba Mpya na Bora kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
 
Inahuzunisha kama sio kushangaza kwamba watu hawaoni kosa la Ndugai lililopelekea Rais kumnanga wazi hadi akachukia uamuzi wa kujiuzuru.

Ni kweli speaker ana nafasi ya kutumia Uhuru wake wa kutoa maoni as a normal Tanzanian. Alichokifanya alitumia Uhuru wake wa kikatiba kutoa maoni yake binafsi.

Lakini tunasahau Jambo moja kwamba kila Uhuru una mipaka yake hata Katiba inatamka wazi kuhusu haki za binadamu. Unapotoa maoni yako unapaswa kuangalia na viapo vingine ulivyoapa katika utekelezaji wa majukumu yako.

Ndugai akiwa bungeni akiwa anatekeleza majukumu yake hazuiwi kutoa maoni yake na amekuwa akifanya hivyo mathalani kwenye mambo mbalimbali hata Bandari ya Bagamoyo, kuhusu mjadala wa watoto waliopata ujauzito kurudishwa shule nk.

Tatizo linakuja pale anapotoa maoni yake nje ya bunge ingali yeye ni kiongozi wa mhimili ambao umepitisha hiyo hoja akiwa amesimamia mijadala yote halafu anaibuka nje ya bunge na kuongea namna Ile.

Sasa Rais ndio head of state, pamoja Kuna separation of powers lakini Katiba hiyohiyo inatamka Rais ni head of state maana yake Ndugai anawajibika kwa president despite ya kuwa head of one of pillars of the government.

Hapa unaweza kuelewa kwamba huwezi kuita wanahabari kumpinga boss wako maana Ndugai kama spika anakuwa mtumishi wa umma by virtue ya cheo chake.

Spika akiwa bungeni anakuwa "functus officio" hivyo haina shida Ila hawezi kuongea kumcrash boss wake nje ya bunge.

Pia kwenye chama Rais ni boss wake hivyohivyo anajikuta hawezi kumcrash Mwenyekiti wake nje ya vikao vya chama.

Kawaida ukitaka kumchallenge Mwenyekiti angepaswa kuongea kwenye vikao vya chama Tena yeye ni Mjumbe wa CC wangejadili kama hiyo anachofanya Rais anakiuka ilani ya chama.

Ndio maana wanaotaka kumchallenge Mwenyekiti huwa wanajitoa kwenye chama ndio wanaongea wanayoona wapo sawa.

Mzee Lyatonga Mrema baada ya kutokubaliana na Rais mzee Mwinyi alipoamua kumpatia mfalme wa uarabuni kitalu Cha kuwinda kule Loliondo kwa miaka 99 Mrema aliona hakubaliani na yale maamuzi ndipo alijiuzulu na akajitoa CCM ndipo akaita press conference kueleza sababu za kujiuzulu.

So in my personal view, Ndugai yawezekana ana hoja ya msingi Ila amekosea protocol ya kuwasiliana maoni yake.
Hapa ume underline the fact kuwa hii mihimili haipo sawa wala huru na unathibitisha assertion kuwa katiba hii haikidhi haja...Kwani Head of State yeye anatakiwa kuja public kuubagaza muhimili ulio huru?

Simkubali Ndugai kwa tabia zake za huko nyuma lakini kwa hili no it was not right! Nani atasimama tena kuuhoji muhimili wa executive?
 
Kuondoka kwa ndugai kumenifanya nione mapungufu mengi sana kimfumo

1 . Hii nchi ina mhimili moja tu hizi zingine geresha
2. Hoja za mashiko hazipewi nafasi
3. Tunako elekea wimbo wa katiba mpya tutaimba wote ...muda ni mwalimu mzuri
Hiyo No 3 ilifaa iwe hoja ya Kitaifa muda mrefu, lakini kuna watu wamekua wakiona kama inakisumbua chama chao kisiimiliki nchi hii milele. Wanadanganywa na wanasiasa (kina Ndugai) ambao wako High Table wanakula na kusaza, huku wao hawajui mlo wa siku ya pili, wakiwa wamevalishwa mashati ya kijani.
 
Umekwenda mbali...je atakuwa na uthubutu hata wa kuihoji serikali? Sasa washafumbwa midomo.
Watu hawajui tatizo lililopo...Je kwa bahati mbaya kukitokea state capture nani ataleta balance of power? Judge Mkuu naye atathubutuje kuhukumu iwapo na yeye ni mteuliwa?

What happened is bad kwa nchi yetu kila mwenye sense of integrity hawezi kubali hili kwa hiari au kwa shari....naamini katiba mpya itakayoleta mazuio ya individuals kutumia institution power zao kuvuruga mihimili ambayo inatakiwa iwe independent and complementing each other ili kuleta unity, peace and harmony ndani ya nchi, ndiyo suluhisho ya haya mambo kutotokea tena; hakuna ziada wala pungufu...Hao wenye mihimili wame cross red line kwa usalama wa nchi yetu na tukiwa fair ni personalities zao ndiyo zimekuwa tatizo kubwa kwakua wameshindwa kujizuia kuvuruga mihimili.
 
Hahah!muwe hata mnashare Wi-fi pale bando linapokata
Hawa ndiyo wale ukiwaambia kuna umuhimu wa kupata Katiba Mpya hawawezi kukuelewa, hawaendi na wakati, wanaitaka ile ile ya 1977 ya chama kimoja cha CCM.
 
Yeye kalazimishwa kusaini tu barua, barua ya spika haiwezi kuoksa address, haiwezi kuwa na maandishi makubwa tu. Pia Taratibu za kujihudhuru hazijafuatwa. Kikubwa Mhimili mmoja umepoka madaraka kwa lazima na hapo ndiyo tutamshukuru Dkt Magufuli kwa uwazi wa kutuletea maendeleo ila ya huyu Mama ni mabaya zaidi kwa sababu huwezi kutumia state machinery kulazimisha mhimili mwingine uachie ngazi. Kitakachofuata Mama ajue that state machinery iko siku itamsumbua yeye huyo huyo tena kwa fedheha kubwa sana. Nina uhakika najua wao kazi yao ni kutekeleza kumfurahisha rais lakini haya mambo huwa yanageuka kama alivyokuwa anfanya Ndugai juu kuhoji wabunge.
Wacha Ndugai akinywee hiki kikombe pia. Amehusika kuwanywesha kikombe hicho wengine akishirikiana na JPM. Kumbuka issue ya CAG Prof Musa Assad na suala la kumfuta ubunge Tundu Lissu na kumzuia matibabu na haki zake zingine, kwa kutaja machache. Wakati wake wa kunywa hicho kikombe umefika, wacha aonje machungu waliyoyaonja wengine.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Wacha Ndugai akinywee hiki kikombe pia. Amehusika kuwanywesha kikombe hicho wengine akishirikiana na JPM. Kumbuka issue ya CAG Prof Musa Assad na suala la kumfuta ubunge Tundu Lissu na kumzuia matibabu na haki zake zingine, kwa kutaja machache. Wakati wake wa kunywa hicho kikombe umefika, wacha aonje machungu waliyoyaonja wengine.
Ni sawa but who else anafuata? We need to put this to an end and a very good end not just an end
 
Hiki ndo nilichouliza kwenye uzi wangu fulani, ile dhana ya bunge kuwa muhimili huru wa kuishauri na kuisimamia serikali itabaki baada ya ndugai kuondoka, au bunge sasa litaenda kuufyata.........litabaki kupiga makofi tu wakati chifu na madelu wakiendelea kusaka mikopo popote ilipo......
Hili bunge tangu November 2020 baada ya kuwa la chama kimoja, lilishakua la kipiga makofi. Ngoja tuwaachie hilo bunge CCM, chama "kilichoshinda kwa kishindo"

Bunge lilishaufyata muda mrefu tangu kipindi cha JPM. Angalia lilichofanya kwa CAG Prof Assad alipohoji 1.5tri.
 
Ndugai nje ya kile "kiti na lile joho" hana madhara yoyote
Hajulikani
hakubaliki
Hana mvuto kwa jamii
 
Eti political trap [emoji23] [emoji1787]
Waswahili hatuna kumbukumbu katika bongo zetu huwa zinafuta haraka sana

Hata kama una PhD bado kukumbuka ni zero

Walipodukuliwa wale walikuwa wanasema jamaa ni Mshamba
Mlikejeli sana
Ila mkasahau kuwa hata nyie mnadukuliwa kila leo

Hujiulizi kwanini baada ya kuomba msamaha akajiuzuru baada ya hapo?
Hapa ndipo ilipo point ya kujiuzulu.
 
inasemekana ile Barua ilichapwa na Vibaraka wa Mama wakaipeleka hadi Nyumbani kwa Spika wakamwambia aweke Signature yake au wamshughulikie,na Ndiyo maana barua yake inaonekana kuwa na dosari kadhaa, Tuendelee kunywa mtori
 
Mkao wa Kula au Kuliwa ?

Officially Bunge ni Rubber Stamp na hata kama ukibadilisha Katiba na Kumpa Nguvu bado atatoka kwenye hiki Chama chenye Monopoly na Kinachoendelea ndani kwao ni dhahiri tutaendelea kuliwa..., Pia uelewa na ushabiki wa Mwananchi kutokuona kwamba kuna Hitilafu ni kwamba we have a long way to go.....
 
Mkuu nchi Hii ina Mihimili mitatu, lakini Hii miwili iliyobaki yote wasimamizi wa Hii Mihimili wako under roof ya Huyo mwenzao.
1. Rais ambae ni m/kiti wa chama anapendekeza yy Jina la mtu Kuwa spika

2. Rais ambae ni mkuu wa muhimili wa Regime yy ndio anaemteua Mtu Kuwa CJ

So wote hawa wanadepend kwa hyo anaewateua

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo ni KATIBA. Tupate katiba mpya tuyarekebishe hayo.
 
Kwahiyo ndugu unataka kuniambia kuwa spika akiwa nje ya Bunge na kuongea hoja za msingi Kwa taifa hiyo inakuwa sio hoja Kwa sababu hajaisemea bungeni......na je Raisi yeye ni wapi akisemea kauli yake inakuwa ni official i.e. ni ikulu pekee au??
Spika wa bunge ni mwananchi, lakini yeye ana maamuzi.
Spika ni sehemu ya maamuzi ya serikali na ndani chama chake.
Kwa wadhfa wake wa Uspika, anakuwa mjumbe wa kamati kuu ya chama.
Bunge ni sehemu ya maamuzi ya mambo mbalimbali ya serikali.
Mkopo ulipitia bungeni, ukajadiliwa na kamati za bunge, ukaidhinishwa.
Unatoka nje ya bunge unalalamika!?
Unamlalamikia nani?
Alikuwa na uwezo wa kuukwamisha huko huko bungeni, lakini ameuidhisha, kisha unakuja kullalamika, huoni kama hakulitendea haki bunge kama kiongozi wake!!?
Hata baada ya maamuzi, kwa cheo chake anaweza kuomba kukutana na rais ili wajadiliane kuhusu mikopo na namna nzuri ya kukopa, kuipunguza au kuachana nayo.

Lakini kusimama hadharani kuiponda serikali ya chama chako na ukiwa mjumbe wa vikao vyake ni usaliti.
 
Back
Top Bottom