Tetesi: Kifuatacho: Mtafaruku wa CHADEMA na TeamLowassa kuinufaisha ACT Wazalendo, Kafulila kumfuata Zitto

Tetesi: Kifuatacho: Mtafaruku wa CHADEMA na TeamLowassa kuinufaisha ACT Wazalendo, Kafulila kumfuata Zitto

dah! siasa bhana yataka moyo maana chadema kazi mnayo awamu hii naona nondo zinatupwa kutoka upande wa pili duh!
 
Naam jicho la tatu limeshachungulia wanaChadema kindai ndaki wameshaamka sasa ni wazi wazi wantamka maneno makali yenye kuonyesha kutoridhishwa na uwepo wa Lowassa ndani ya chamn na upande mwingine wa shilingi yaani Team Lowassa wao wanajipanga na wameweza kupandikiza watu wao katika vikao vya maamuzi, naaum mbegu imepandwa na imeota sasa inamea, naaaum mmea wenyewe ni miba mikali sasa inachoma.

Kwa 'makamanda' Lowassa si tena raisi wa mioyo yao kama walivyomwita Dr.Slaa kwa miaka mitano mfululizo kabla ya kurubuniwa mwaka 2015 lakini kwa teamLowassahuwaimbii kitu. Kwa haraka haraka nyufa nyingi zimetokea kiasi kisichoelezeka na huenda 'jumba' likalemewa na kuanguka.

Naaam, 'ajizi nyumba ya njaa' kama ambavyo waswahili walivyonena..kwa sasa Zitto ameonekana kufurahiwa na 'makamanda' wakijuta sasa kumpoteza, kila mtu sasa anafutilia kauli za Zitto kwenye mitandao na mikutano na kuhakikisha zinasambaa kwa watu wengi wakati huohuo 'makamanda' wamelaani tabia ya Mbowe kuwachagulia viongozi kwenye kanda za kiutawala ndani ya chama hadi kupelekea makumi na mamia ya viongozi wa mashina kufa moyo na baadhi kujiuzuru. Kuelekea uchaguzi ndani ya chama na hata uchaguzi mkuu mwaka 2020 njia ni nyeupe na ninawaona baadhi ya wabunge wa sasa wa Chadema haswa wale wasiotokea kanda ya kaskazini na wanachama waandamizi wakihamia ACT Wazalendo na kuendelea na harakati zao kisiasa wakimsusia chama ndugu Lowassa na Mbowe.

Na chakufurahisha zaidi kafulila atagombea ubunge huko Kigoma mwaka 2020 kupitia ACT wazalendo na si Chadema ni suala la muda tu.

Nawasilisha.
Sugu anahamia chama gani?
Prof nae atakimbilia wapi?
Mbona nawaona wabunge wengi sana ambao hawajatoka Kilimanjaro na Arusha na hawana dalili ya kukihama chama hicho?
By the way,who is Zitto? Maana naona kila rejea yako ni Zitoo, na huyo Zitto alikuwa CDM mkamnunua na akajiita ni mwana mageuzi wa kweli...hata siku moja usimwamini mtu anayejiita mwanamageuzi na huku anashinda akibuni mbinu za kumaliza mageuzi....
Asante kwa post yako.
 
Tanzania vyama vya siasa viko vingi, wanasiasa waliohama vyama nao wako wengi! Katika vyama hivyo vingi, kuna vyama vichanga na dhaifu na vingine vya umri zaidi ya miaka ishirini lakini vimedumaa na pia kuna vyama ambavyo vinaendelea kumea na kustawi katikati ya "magugu", chama cha magugu (CCM). Vivyo hivyo viongozi nao wapo waliohama toka chama cha magugu na kuingia upinzani na pia toka upinzani kwenda chama cha magugu, kati yao wapo wenye nguvu na ushawishi mkubwa na pia wapo dhaifu. Hili ni jambo la kawaida sana kisiasa. Mimi nawashangaa baadhi ya watu humu kila kukicha ni kuisema Chadema tu na au Lowasa au Mbowe. Binafsi sivutiwi kabisa na uandishi wa aina hii. Sote tunajuwa Chadema na washirika wake wanaounda UKAWA nyuma yao kuna Watanzania millioni 6 waliokipigia kura kwenye uchaguzi mkuu. Idadi hii sio ya kukejeli hata kidogo. Kwa mantiki hiyo, huwezi ukalinganisha Chadema na na chama kingine dhaifu kilichopata kura chini ya laki tano halafu unakisifia chama dhaifu ! itakuwa ni wendawazimu kufanya hivyo! Kuendelea kuviponda vyama vinavyojiimarisha na kukua huku kuvisifu vyama dhaifu ni kuvidumaza vyama hivyo dhaifu.
 
Wenye akili tumekuelewa, lakini Mazuzu CHADEMA yatakupinga. Na hawaoni dalili wao ni kuongea tu bila kufikiri. Hilo nasisitiza litatokea tu. Maana Chadema sasa wamekwisha no way to go.
 
Wenye akili tumekuelewa, lakini Mazuzu CHADEMA yatakupinga. Na hawaoni dalili wao ni kuongea tu bila kufikiri. Hilo nasisitiza litatokea tu. Maana Chadema sasa wamekwisha no way to go.
Kuishabikia ccm Inatakiwa Ujipunguze Akili Kama Sivyo Hauwezi Kua Mwanachama wa ccm

Tanzania ni Nchi ya Viwanda Hapa Kazi Tu.!
Kiongozi Atakae Sema Mkoa wake una Njaa Ajiandae Kuacha Kazi.

Tanzania Imepanga Kutoa Mahindi ya Chakula tani Million 1.5

Watakaovaa Ma T-shirt Yaliyoandikwa Njaa Kukamatwa.
 
Wamemshindwa Mbowe sasa wanakimbilia Kwenye Mali zake,
Chadema ni chama cha upinzani hata mwalimu Nyerere akiona mapema kabisa bado kidogo.

Alitoa kauli hii, Sioni upinzani Tanzania labada Chadema, Hiki chama naona kina misingi kama wakiisimamia ni Chama kizuri,
Na ndio maana hata Lowassa, Kingunge , Sumae waliliona hilo.
kwahiyo kwa mbinu za kununua Upinzani utaishia kwa NCCR ya Mrema, CUF ya Lipumba sio ya Seifu siii Chadema,
Jitahidini kuchonganisha tu Mitandaoni na kwingine sii kununua Viongozi na kufanikiwa kuua chama, Chadema ni Taasisi kubwa sana,

Mnakumbuka mlimnunua nani na nini kilitokea?
Jielekeze kwenye hoja...mwambie alipe kodi
 
Kuishabikia ccm Inatakiwa Ujipunguze Akili Kama Sivyo Hauwezi Kua Mwanachama wa ccm

Tanzania ni Nchi ya Viwanda Hapa Kazi Tu.!
Kiongozi Atakae Sema Mkoa wake una Njaa Ajiandae Kuacha Kazi.

Tanzania Imepanga Kutoa Mahindi ya Chakula tani Million 1.5

Watakaovaa Ma T-shirt Yaliyoandikwa Njaa Kukamatwa.
Jikite kwenye hoja.
 
Kuna wizi mpya wa pesa za umma,Wajanja baada ya kugundua mkulu hapendi Wapinzani wameamua kubuni miladi mikubwa ya kula pesa za Umma kama Lipumba anavyozitafuna kiulaini.
Jikite kwenye hoja
 
Mbowe na Lowassa ni wasanii tu,wanawageuza wafuasi kama chapati za maji.hakuna watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama wafuasi wa chadema
 
Ndiyo maana hatupati mvua. Ni kwa sababu ya kuongezeka watu wenye mawazo ya hovyo hovyo kama huyu. Mungu hapendi haya mambo.
 
Naam jicho la tatu limeshachungulia wanaChadema kindai ndaki wameshaamka sasa ni wazi wazi wantamka maneno makali yenye kuonyesha kutoridhishwa na uwepo wa Lowassa ndani ya chamn na upande mwingine wa shilingi yaani Team Lowassa wao wanajipanga na wameweza kupandikiza watu wao katika vikao vya maamuzi, naaum mbegu imepandwa na imeota sasa inamea, naaaum mmea wenyewe ni miba mikali sasa inachoma.

Kwa 'makamanda' Lowassa si tena raisi wa mioyo yao kama walivyomwita Dr.Slaa kwa miaka mitano mfululizo kabla ya kurubuniwa mwaka 2015 lakini kwa teamLowassahuwaimbii kitu. Kwa haraka haraka nyufa nyingi zimetokea kiasi kisichoelezeka na huenda 'jumba' likalemewa na kuanguka.

Naaam, 'ajizi nyumba ya njaa' kama ambavyo waswahili walivyonena..kwa sasa Zitto ameonekana kufurahiwa na 'makamanda' wakijuta sasa kumpoteza, kila mtu sasa anafutilia kauli za Zitto kwenye mitandao na mikutano na kuhakikisha zinasambaa kwa watu wengi wakati huohuo 'makamanda' wamelaani tabia ya Mbowe kuwachagulia viongozi kwenye kanda za kiutawala ndani ya chama hadi kupelekea makumi na mamia ya viongozi wa mashina kufa moyo na baadhi kujiuzuru. Kuelekea uchaguzi ndani ya chama na hata uchaguzi mkuu mwaka 2020 njia ni nyeupe na ninawaona baadhi ya wabunge wa sasa wa Chadema haswa wale wasiotokea kanda ya kaskazini na wanachama waandamizi wakihamia ACT Wazalendo na kuendelea na harakati zao kisiasa wakimsusia chama ndugu Lowassa na Mbowe.

Na chakufurahisha zaidi kafulila atagombea ubunge huko Kigoma mwaka 2020 kupitia ACT wazalendo na si Chadema ni suala la muda tu.

Nawasilisha.
Hawa Chadema walishaambiwa toka mapema kumkaribisha Lowassa ndani ya chama ndio mwanzo wa anguko lao, nasikia hali ni mbaya ndani ya chama, hata vile viposho vya sh 50000/= vimeyeyuka, Tundu Lissu analia njaa ndio maaana anaimbuka na hoja zisizo na msingi kujaribu kutoka, lakini kila anapojaribu anakwama, dawa ni moja tu kama ni wajasiri wamfukuze LOWASSA.
 
Back
Top Bottom