Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 95,871
- 116,627
Kazi ya kuua wanaiweza sn
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yeye alienda kufanya nini hapo?Amesema mashabiki hao waliendelea kushambuliana na kuwapiga mawe askari waliokuwepo uwanjani hapo na kusababisha askari namba F.5123 D/ CPL Subira aliyekuwa na silaha aina ya AK 47 kushambuliwa sehemu ya kichwani na kuanguka chini” amesema kamanda Manyama
Tuambie namna ambayo angefanya hapa mkuu.
Tuchukulie niwewe umeangushwa chini na mawe yanamiminika na unasiraha ambayo inabidi uilinde kwa sababu kwenye huo umati sio wote ni wema mtu anaweza kupita nayo, pia ulinde uhai wako
Kumuenzi mtu ambaye hata hakuwa na mchango wowote kwenye maendeleo yaoVurugu hizo zilitokea jana Jumatatu Machi 14, 2022 saa 10 jioni wakati wa fainali ya mchezo wa mpira wa miguu wa kumuenzi Dk Living Stone baina ya timu ya Mwandiga Fc dhidi ya Kipampa Fc ya Ujiji ulioandaliwa na Shirika la Joy in The Harvest kwa kushirikiana na Chama cha Mpira wa Miguu Kigoma (KFA) na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ester Mahawe.
Hiko chombo nacho kithibitiwe na chombo kingine bila hivyo hiko chombo nacho huko mbeleni kitaleta upuuzi tuKiundwe chombo cha kudhibiti majeshi yetu hususani jeshi la polisi.......
Namna ipi tuelezeHuu Ni ujinga hakuna polisi anae ruhusiwa kutumia silaha ya Moto Tena kwa mwananchi ambae Hana silaha, hata Kama hakutii sheria bado alikua na namna nyingine ya kufanya sio kuua.
Ulikuwepo?Waha wana akili za kijinga sana.
Nadhani nimeeleweka. Polisi walikuwa wakituliza ghasia ila hao ndugu zetu wakajifanya miamba yakawakuta ya kuwakuta.
Kama askari alipiga risasi juu kuashiria watu watawanyike na wasiendelee na fujo, lakn wakakaidi na wakazidi kumshambulia askari akiwa na silaha hapo lazma silaha itumike kwa ajili ya kujihamiKupitia Twitter pia, Abdul Nondo Kaandika;
View attachment 2151568
--
Askari polisi mwenye namba F.5123 D/ CPL Subira ambaye aliyekuwa na bunduki aina ya AK 47 adaiwa kumuua Juma Ramadhani kwa kumpiga risasi na kuwajeruhi watatu wakati akiwa kwenye harakati za kujihami kwenye vurugu zilizotokea katika kiwanja cha mpira cha Lake Tanganyika mkoani Kigoma.
Vurugu hizo zilitokea jana Jumatatu Machi 14, 2022 saa 10 jioni wakati wa fainali ya mchezo wa mpira wa miguu wa kumuenzi Dk Living Stone baina ya timu ya Mwandiga Fc dhidi ya Kipampa Fc ya Ujiji ulioandaliwa na Shirika la Joy in The Harvest kwa kushirikiana na Chama cha Mpira wa Miguu Kigoma (KFA) na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ester Mahawe.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 15, 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, James Manyama amesema marehemu Juma amefariki dunia akiwa hospitalini akiendelea na matibabu.
Kamanda Manyama amesema vurugu hizo zilitokea kipindi cha kwanza wakati Mwandiga Fc iliyokuwa ikiongoza kwa goli moja liliposawazishwa na Kipampa Fc ambapo mashabiki wa Kipampa Fc kuvamia jukwaa la mashabiki wa timu ya Mwandiga na kuanza kuwazomea huku wakiwarushia chupa za maji na mawe hali iliyosababisha kuibuka kwa vurugu.
Amesema baada ya vurugu hizo kutokea askari waliokuwa wamepangwa kwa ajili ya kuimarisha ulinzi walijitahidi kudhibiti vurugu hizo lakini walizidiwa nguvu na kuomba msaada.
"Askari waliongezeka uwanjani pale kwa ajili ya kutuliza fujo na kutumia mabomu ya machozi na kishindo kuthibiti vurugu hizo lakini mashabiki hao waliendelea kufanya fujo.
“Amesema mashabiki hao waliendelea kushambuliana na kuwapiga mawe askari waliokuwepo uwanjani hapo na kusababisha askari namba F.5123 D/ CPL Subira aliyekuwa na silaha aina ya AK 47 kushambuliwa sehemu ya kichwani na kuanguka chini” amesema kamanda Manyama
Amesema askari huyo aliamua kujihami dhidi ya tishio la kunyang’anywa silaha pamoja na kutetea uhai wake kwa kufyatua risasi tisa hewani sambamba na kutoa onyo la kuwatawanya mashabiki waliokuwa wakimshambulia kwa mawe.
Amesema licha ya kupiga risasi hizo lakini mashabiki hao waliendelea kumshambulia kwa mawe akiwa ameanguka chini ndipo alipofyatua risasi tatu na moja ilimpata marehemu Juma ambaye alijeruhiwa katika paja la mguu wa kushoto na risasi ya pili ilimjeruhi Omary Amdan (35), katika unyayo wa mguu wake wa kushoto na risasi ya tatu ilimjeruhi Nasibu Moshi (35), katika mguu wake wa kushoto.
Amesema majeruhi wote walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa Maweni kwa matibabu na vurugu zilipotulia mchezo huo wa fainali uliendelea hadi mwisho.
Amesema saa 12 jioni Juma Ramadhani akiwa anapatiwa matibabu alifariki dunia huku majeruhi wawili walipatiwa matibabu na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku askari Subiri alibakia kwa ajili ya matibabu zaidi.
Amesema kutokana na tukio hilo jeshi la polisi linawashikilia watu wanne wanatuhumiwa kuwa chanzo cha vurugu hizo na upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea na watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria zaidi.
" Niwasihi wananchi wa mkoa wa Kigoma wakati wa ushabiki wa michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu washabikie kwa ustaarabu, kuvumiliana na kufuata sheria za nchi na kuacha kushabikia kwa mihemko inayosababisha vurugu,"amesema Kamanda Manyama.
Chanzo: Mwananchi
Wewe lazima utakuwa ni polisi au mtoto wa polisi hakuna raia katili namna hiiKama askari alipiga risasi juu kuashiria watu watawanyike na wasiendelee na fujo, lakn wakakaidi na wakazidi kumshambulia askari akiwa na silaha hapo lazma silaha itumike kwa ajili ya kujihami
Ni mshirikina hatari sn kila ukipanga kumfukuza unakuta unasahauZero ataunda tume. Sijui huyu baba anafanya nini ofisini
Kwani Siro alikuwepo Kigoma?IGP Sirro ni mtu wa hovyo hovyo kwa kuruhusu watu wa hovyo kutenda unyama kwa binadamu wenzeo na bado wakalindwa.
Mimi sio Polisi, ila nilipita JKT nilifundishwa hivyo. Askari unapokuwa na silaha kwa ajili ya kuimarisha ulinzi kitu cha kwanza ni usalama wako kwanza. Kwa hiyo hapo ulitaka askari apokonywe silaha na apigwe?Wewe lazima utakuwa ni polisi au mtoto wa polisi hakuna raia katili namna hii
Aliwafuata kufanya nini hao wananchi?Mimi sio Polisi, ila nilipita JKT nilifundishwa hivyo. Askari unapokuwa na silaha kwa ajili ya kuimarisha ulinzi kitu cha kwanza ni usalama wako kwanza. Kwa hiyo hapo ulitaka askari apokonywe silaha na apigwe?
Kumbe habari ujaisoma vizuri. Askari walienda pale kwa ajili ya kuhakikisha amani inakuwepo. Fujo imetokea lazima askari waende kutuliza ghasia kwa sabb wapo pale kwa sabb hiyo.Aliwafuata kufanya nini hao wananchi?
Kwa hiyo solution ilikuwa ni kuua na wakati kuna washawasha hapo?Kumbe habari ujaisoma vizuri. Askari walienda pale kwa ajili ya kuhakikisha amani inakuwepo. Fujo imetokea lazima askari waende kutuliza ghasia kwa sabb wapo pale kwa sabb hiyo.
Ajabu askari wapo pale, fujo bado inaendelea wangefanyeje sasa
Unauliza hivi na kupata sauti ya kuongea kwasababu tu hayajakukuta wewe, na Wala aliefariki hauhusiani nae.Namna ipi tueleze
Hata mimi ningeua, siwezi kushambuliwa na mawe kama mwizi ilhali nina AK-47 mkononi.Kwa hiyo solution ilikuwa ni kuua na wakati kuna washawasha hapo?
Natumai ungesikia polisi aliuwawa kwa kupigwa mawe, ungefurahi sana.Unauliza hivi na kupata sauti ya kuongea kwasababu tu hayajakukuta wewe, na Wala aliefariki hauhusiani nae.
Subiri siku polisi wafanye tukio litakalogusa familia au damu yako hapo ndipo utaelewa namna inayopaswa kutumika