Kigwangalla: Chama kimerudi kwa wenyewe

Kigwangalla: Chama kimerudi kwa wenyewe

wacha weee..wacha kazi iendelee hadi kazi yenyewe iseme " imekomaaaaa" !
 
Kuna wajinga wametumwa kusema mchuano wa siasa ni kati ya washamba na masharobaro wa mjini. Yote kupotosha wanaharamu fisadi wapite.
Siasa ni mapambano ya kitabaka kati ya wenye nacho na raia wa kawaida au ukipenda walala hoi. Hapo kati kuna tabaka la kati. Ni wafanyakazi au wafanyabiashara wadogo. Hao wanaweza kuungana na wenye nacho kukandamiza tabaka la chini au wanaweza kuunganika na walala hoi / tabaka la chini. Yote inategemea maslahi ya kila tabaka.
Tanzania tabala la chini yaani raia wa kawaida ndio kubwa. Kwa hivyo siasa za kuunga mkono maslahi ya umma hasa kuwaletea maendeleo ya kiuchumi zina nafasi ya kuungwa mkono kwa wingi.

Sio Tanzania hii chini ya utawala wa CCM. Wananchi wamesukumiwa pembeni. Wamebaki kuwa watazamaji na wategemea fadhila. Hawana sauti kwenye sanduku la kura, bungeni, kwenye mabaraza ya uwakilishi hata mahakamani.

Mapambano yaliyoruhusiwa ni kati ya makundi maslahi ndani ya chama tawala. Huko ndio kuna vita kweli kweli. Chama kile kile. Unasikia tu leo kiko kwa washamba, kesho kwa watoto wa mjini, … Wananchi wakitaka kutoa kauli bila ruhusa ya watawala wanashushiwa marungu na risasi za polisi.
 
Tabia zake chafu zinamponza, Mbona Mkapa na Nyerere hawazungumziwi hivi?
Hata Nyerere na Mkapa wangefia madarakani, watu wangefurahi na wangesema chama kimerudi kwa wenyewe!
JPM angestaafu na kupasisha uongozi kwa mwingine wasingesema chama kimerudi kwa wenyewe
Hata hivyo tunajua maCCM wengi ni maslahi binafsi ambao walinyimwa fursa za kula ndani ya chama!
 
hahahahaha mmezoea laini laini.... mmepigwa mchakamchaka chinja miaka 6 tu hapa hoi.....
 

hamisi_kigwangalla

SEKRETARIETI ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapindunzi (CCM), ikiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Komredi @daniel_godfrey_chongolo jana imehitimisha ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 na kuimarisha Chama mashinani katika mikoa ya Kagera, Geita, Kigoma, Katavi na Tabora. Pichani wajumbe wa Sekretarieti hiyo wakizungumza katika kikao cha majumuisho mkoani Tabora. Kwa hakika Chama kimerudi kwa wenyewe. CC: Komredi @shaka_hamdu_shaka. #HK #KaziIendelee #SiasaNiVitendo

View attachment 2021524
View attachment 2021525
View attachment 2021526

My take: Kwani Chama kilitekwa?
Mwambie amshukuru magufuli kampitisha alikuwa hatoboi 2025 ajiaandae kuomba ajira MLOGANZILA mchamba huyu
 
Ni hatari sana Taifa kuwa na vijana kama hawa..

Mbaya zaidi vijana hawa wapo kokote, kuanzia chama tawala mpaka vyama pinzani...

Tabia hii ni yakukemewa na watu wote....
 
Kigwangala mnafiki sana huyu mtu, kinyonga sana kwa tabia huyu, mnakumbuka wakati Mh. JPM akiwa hai, Kigwangala ndio alikuwa front line, akijifanya Sukuma gang haswa, alikuwa kumsifia JPM kila kukicha, na uwaziri juu alipewa, na hakuwahi hata kudhubutu kuonyesha dalili tu kuwa JPM aliteka Chama.

Leo hii, anaongea kuwa Chama kilitekwa, watu wa aina hii ni wa kuchunga sana, sbb wako ki maslahi zaidi na ni kuwa nao makini. Kauli kama hii angetoa Nape, bila shaka hakuna wa kupinga wala kusema ni kinyonga, ila sio Hamis, opportunist.
Huyu Kigwa mnafiki sana wakati wa Jiwe alisema chama kimerudi kwa wananchi. Sasa hivi je??
Dr. Hamis mjanja sana....anajua kubadili mitizamo kulingana na mazingira yaliyopo
 
Ni hatari sana Taifa kuwa na vijana kama hawa..

Mbaya zaidi vijana hawa wapo kokote, kuanzia chama tawala mpaka vyama pinzani...

Tabia hii ni yakukemewa na watu wote....
Huenda hiyo ndio tabia yetu Watz yaani 'unafiki'.
 
Mwache huyo sio kama wewe unaeambulia Buku saba Hamisi ameponda raha wakati wa Awamu ya Wahutu alikuwa anachukua Visichana anaenda kuvidinya huko kwenye Mbuga za Wanyamapori huku akimwambia Magufuli kuwa anawasaka Majangili.

Utadhani Majangili walikuwa wanajificha kwenye Nyapu.
Teh teh teh teh....😂😂😂...we jamaa bhana haaa haaaa haaaa 😂😂😂
 
Dr. Hamis mjanja sana....anajua kubadili mitizamo kulingana na mazingira yaliyopo

huu sio ujanja, huu ni ujinga....hatuwezi kufurahia kwa Taifa kuwa na vijana wasomi wajinga kama hawa.... sasa huyu amesoma anakuwa na tabia hizi za kigangaganga...
 
Halafu nasikia ni Daktari eti, ni kweli ? Binafsi siwezi kukubali kutibiwa na daktari low IQ kama huyo, Daktari kutwa nzima mipasho na umbea no substance, sijawahi kusikia, …
Ukiumwa kisawasawa hutochagua daktari au dawa sana sana utajali afya yako tu.
 
Kwa hiyo chama kikiwa mikononi mwa kanda za pwani kipo salama.

Chama kikiwa mikononi mwa kanda ya ziwa KIMETEKWA!

Muda wakunyenyekea mkija kanda ya ziwa myakumbuke haya maneno.
Huko kanda ya ziwa ni ngome ya Ccm.
Nakuona chawa promax wa mama unapambana
Huwezi kushindana na mama wewe masalia wa mataga.
 
Wanasiasa wa Tz ni wapumbavu sana na wajinga, wakiwa wanataka kufanikisha maslahi yao wanaongea upuuzi upuuzi tu ilikufanikisha shibe zao
 
Sio Tanzania hii chini ya utawala wa CCM. Wananchi wamesukumiwa pembeni. Wamebaki kuwa watazamaji na wategemea fadhila. Hawana sauti kwenye sanduku la kura, bungeni, kwenye mabaraza ya uwakilishi hata mahakamani.

Mapambano yaliyoruhusiwa ni kati ya makundi maslahi ndani ya chama tawala. Huko ndio kuna vita kweli kweli. Chama kile kile. Unasikia tu leo kiko kwa washamba, kesho kwa watoto wa mjini, … Wananchi wakitaka kutoa kauli bila ruhusa ya watawala wanashushiwa marungu na risasi za polisi.
Kama ndio hivi...huenda Watz ndio wametekwa.
 
Nilikuwa napatashida kuwapa watu mfano halisi wa mtu mnafiki lkn tangu magu aende vigangwala wapo kibao nahuyu ndo kubwa la manafiki akichuana na ayubu nduguyai
 
Hawa Sukuma gang ni wa kufyekelea mbali, wameambiwa waanzishe chama chao waingie frontline 2025 wana sitasita, sijui wanaogopa nini wakati wanasema ukanda wao ndio huamua Rais awe nani
Hama wewe mtabanana humohumo..who knows after samia atakuja nani?
 
Back
Top Bottom