Kijana afanya utani wa kutaka kumuua Rais Magufuli, aambuliwa kifungo cha miaka 2 jela

unajuaje alikuwa anafanya masihara?

usifuatishe vichwa vya habari vya magazeti uozo yetu haya

masihara ni utetezi wake kizimbani, ambao mahakama imeukataa...
Hivi kweli utake kumuua raisi wa nchi utangaze kama hivi?
 
Hahaha,unamtisha kumuua John ukiwa kwenye meza ya John,lazima John amuokoe John mwenzie

Huu ni ulimbukeni,ujuha na kutafuta umaarufu wa kijinga kwa baadhi ya Wabongo.
Watu mbona kila siku wanafanyaga mizaha kwenye vikao vya gahawa? Huyu kijana wamemwonea tu hasa hao waliomshtaki mwenzao kwa mapolisi.
Lakini bado hata huyu Hakimu ni chizi pia. Mtu amesha sema alikuwa anaongea kwa utani bado unampiga miaka 2 kwa kosa gani? Mtu kufanya UTANI anaweza kuhukumiwa kweli?Kama huyu Hakimu angelitaka kutenda Haki na ionekane imetendeka alitakiwa kijana apelekwe kwa Daktari aonekana kama ana akili timamu na kama kweli alikuwa ana NIA hiyo au ulikuwa UTANI tu!!Nina hakika kama ndugu zake wangelimtafutia WAKILI asingelifungwa miaka 2....! Huu ni uonevu tu.
 

Uko sahihi na naunga mkono hoja..!!
Bado nasema huyu kijana maskini(MNYONGE kwa lugha ya aliyemtania kumwua) AMEONEWA kwa 100%.Hakuna kesi hapo sanasana huyu Hakimu katumia hiyo kesi kujitangaza kwa JPM ili siku moja akumbukwe kwenye Ufalme wa Uncle Magu...!!!

Tatizo la Watz wengi hatusomi sheria wala hatuna utamaduni wa kutetea HAKI ZETU ZA MSINGI. Huyu kijana alitakiw aapatiwe WAKILI na asingelifungwa kabisa.
Hivi kijana huyu ana kosa gani la KUFUNGWA MIAKA 2 ukilinganisha na MAFISADI WALIOAMBIWA WAANDIKE BARUA ZA KUOMBA MSAMAHA NA KURUDISHA MABILIONI WALIYOKWIBA? Kwanini huyu Hakimu hakumwambia kijana aombe msamaha na kumpa ONYO kuwa asirudie tena kufanya UTANI kuliko kwenda kumrostisha miezi 12 Gerezani
 
Naona mambo yake yalikwenda haraka kwasababu pia yeye hakutaka kuisumbua Mahakama kukataa maneno yake. Ingekuwa hivyo ingekwenda hadi miaka kuja kukamirisha upelelezi.
 
Kosa halihalalishi kosa
Kama kuna kosa lilitokea na hakuna hatua za kisheria zilichukuliwa hiyo hali halihalalishi kosa kutendwa na mwingine na kunyamaziwa

Ni kama huwezi kujitetea mahakamani kwamba nimetenda kosa fulani kisa sijui kama nililolitenda ni kosa kisheria
 
Jamani, hivi kuna watu ni wanoko kiasi hicho hadi uende ukaripoti utani polisi?

Ndugu yangu yanayondelea kwenye Utawala huu yanafurahisha kama siyo kinyume chake..!!
Watanzania wengi wamejaa unafiki, chuki na hasira kwa mambo ya kijinga jinga tu...!!! Utawala wa Jiwe umezidi kudhihirisha tabia za Watz( Displaying their real colours) za unafiki.

Kwamba kwa tabia ya Rais aliyeko madarakani kwa sasa ukijikomba, ukijipendekeza na kuwachongea wenzako hasa wapinzani wa Jiwe basi UNAWEZA KUAMBULIA japo UKUU WA MKOA, WILAYA au UKURUGENZI n.k.
Usije ukashangaa huyu Hakimu aliyetoa hukumu kwa kijana huyu maskini ukasikia amepanda daraja/cheo na kuwa Hakimu Mkazi, Jaji n.k. Watu wanapata vyeo au kupanda vyeo kwa kuumiza wenzao...ni aibu!!
 
Ni kweli Mkuu, wengi sana wamepandishwa vyeo kwa kuwafanyia mbaya watu wanaosema kinyume na anavyotaka rais, lakini mkuu mimi naamini hivyo vyeo wanavyopewa kama hawa akina makonda vinakuwa havina hata raha, kwa sababu mtu nafsi yako inakuwa inakusuta kila usiku
 
Hivi kweli utake kumuua raisi wa nchi utangaze kama hivi?

ametangaza kwa sababu kutishia lazima utangaze

hajataka kumuua Rais, hakuna paliposemwa alitaka kumuua Rais

amefungwa kwa kosa la kutishia kumuua Rais

vitu viwili tofauti, kisheria makosa tofauti, adhabu tofauti...
 
ametangaza kwa sababu kutishia lazima utangaze

hajataka kumuua Rais, hakuna paliposemwa alitaka kumuua Rais

amefungwa kwa kosa la kutishia kumuua Rais

vitu viwili tofauti, kisheria makosa tofauti, adhabu tofauti...
Sijajua umesimamia upande upi, wa wale wanaoshabikia kwamba alistahiri adhabu hiyo au sisi tunaosema hakustahiri adhabu hiyo ?, kiswahili chako kigumu sana.
 
Sijajua umesimamia upande upi, wa wale wanaoshabikia kwamba alistahiri adhabu hiyo au sisi tunaosema hakustahiri adhabu hiyo ?, kiswahili chako kigumu sana.

sio Kiswahili changu kigumu, tatizo vyombo vyetu vya habari vinapotosha umma kwa upeo wao finyu wa kuripoti masuala ya kimahakama.

Kuna:

1/ Kuua

2/ Kujaribu kuua

3/ Kula njama kuua

4/ Kutishia kuua

Hakuna kutaka kuua.

Hivyo hatuwezi kuongelea suala la ni kweli alitaka kuua au hakutaka, au alitania, kwa sababu, again, hakuna kosa la kutaka kuua!

Letu hapa ni kutishia kuua. Kutishia kuua hakujalishi kama kweli ulikuwa na uwezo wa kuua au whether ulimaanisha au ulikuwa unachimba "mkwara mbuzi." In other words, ukimtisha mtu kummwaga ubongo kwa jambia wachunguzi na waendesha mashitaka hawatakwenda nyumbani kwako kuangalia je kweli unalo hilo jambia au kiwembe au msumeno. Watatafuta uthibitisho mmoja tu, wenye pembe mbili: ulitamka vitisho (actus rea), na ulinuwia kutamka (mens rea).

Amefungwa kwa sababu alitamka tishio na alinuwia kutamka, mahakama imefanya sawa.
 
Ni bora utishie kumuua Mungu utapona, lakini usijaribu kutishia kumuua John, hata ukiota ndoto tu kuwa John amekufa kaa kimya kabisa wakikusikia kuwa umeota ndoto Kama hiyo ujuwe utaishia gereza la Kisongo, Kama kuna mtu anabisha akamuulize Lema
Uko sahihi mkuuu
 
Hakuna Raisi katika historia ya taifa hili ambaye wananchi wanapenda kumuona akiwa futi sita chini ya udongo.
 
Maelezo yako ni marefu sana na yalianza kunivutia, ila ulivyomalizia umeharibu kila kitu, umejivunjia heshima Mkuu.
 
Hahah jamaa jinga

Ila ana bahati hajakaa mahabusu kabisa: kesi imekimbia balaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…