Kijana analala kwenye jeneza zaidi ya miaka 15

Kijana analala kwenye jeneza zaidi ya miaka 15

Al hamdu lillah najivunia kuwa Muislam, Uislamu ni raha sana, Uislamu ni amani, Allah anijaalie mwisho mwema!
 
Kitu cha kawaida sana hiki, sijaona jipya hapo.. 🤝🤝
 
Kila mmoja apambane kivyake kwa namna yoyote ile atakayo ona inafaa yeye kuwa na kipato......as long as tu havunji sheria za nchi wala kuumiza raia wengine. Acheni jamaa aendelee kula pesa zake anazozitaabikia yeye mwenyew.
Sawasawa
 
Sema tuache utani .......katika research yangu mjini hakuna mwenye vipesa vya kuoneka bila kupiitia kwa ndagu
 
bora huyo analala kwenye jeneza na ndan kwake mi nalala kwenye kaburi asubuh nikiamka napiga zangu mswak nakula pamba huyoo kwenye mishe kabur langu nimeweka na ac lina friji na tv kabisa kama huamin kesho asubu pita mitaa ya kino makaburin utaniona ninavyoamka na kutoka kaburn uje uandike uzi hapa mana ushamb umekuzid
SHule mnafungua lini?
 
Hapa Duniani ni watu waafrika ndiyo tunakiogopa sana kifo.

Hilo jeneza ni fenicha kama kitanda tu hakuna cha kuogopa Wala kukufuru.

Enzi zile G Nako alipoganya video ya wimbo wa "lucky me" alipata ukosoaji mkubwa sana anajitabiria kifo. Leo huyu hapa anadunda.
Ni suala tu la kubadilisha matumizi, lakini hakuna shida yoyote. Hata makanisa yanatumiwa kama baa na kasino, then Jumaoili watu watumia kuabudia.
 
Jamaa anasema alikuwa na mchumba ambaye walitaka funga ndoa ila alipomwonyesha anapolala alikimbiwa. Sasa jeneza kwa asili sio sehemu ya Kulala MTU aliye hai wewe unachukulia poa? Wewe unaweza kununua jeneza na kuwa mbadala WA kitanda tena Una Mali na nyumba Kali namna hii?
Hakuna cha ajabu hapo, ni maamuzi tu.
 
Jamaa anasema alikuwa na mchumba ambaye walitaka funga ndoa ila alipomwonyesha anapolala alikimbiwa. Sasa jeneza kwa asili sio sehemu ya Kulala MTU aliye hai wewe unachukulia poa? Wewe unaweza kununua jeneza na kuwa mbadala WA kitanda tena Una Mali na nyumba Kali namna hii?
Pengine ilikuwa ndiyo yake siku Moja akiwa nazo kitanda chake kiwe jeneza.

Mimi sijaona ubaya wowote.
 
Ni suala tu la kubadilisha matumizi, lakini hakuna shida yoyote. Hata makanisa yanatumiwa kama baa na kasino, then Jumaoili watu watumia kuabudia.
Sijui kwa nini watu wanastuka. Ni jambo la kawaida sana.
 
Kiranga Unazungumziqje hiki kisa TOA mtazamo wako.

---

Dunia ina mengi ya kushangaza ukiachana na maajabu saba ya ulimwengu lakini pia kuna maajabu ya walimwengu wenyewe, Najua umewahi kushuhudia na kusikia habari za watu kujinunulia Jeneza kwa ajili ya maandalizi ifikapo siku ya mwisho, Leo tumekutana na Kijana anayelala kwenye Jeneza kwa zaidi ya miaka kumi na tano sasa yaani hadi usiku wa leo hii kijana huyu atalala kwenye jeneza.

Kutana na Hamisi mkazi wa Dar Es Salaam kijana ambaye ameamua kuishi kwenye Jeneza badala ya kulala kitandani, Kila mtu huwa na matamanio ya kulala sehemu nzuri pale mambo yanaponyooka ila ni tofauti kwa Hamisi licha ya kuwa na Miradi pamoja na kipato kikubwa lakini amechagua kulala kwenye Jeneza.

Hamisi anasema kuwa ana amani na furaha pia suala la kulala kwenye Jeneza wala halimpi shida na haogopi kabisa kwani anaamini kuwa kuna siku atakufa hivyo hakiogopi kifo kwasasa anafurahia maisha yake na kufanya anachokitaka. Amebahatika kujenga nyumba zaidi ya moja japo anatamani sana apate mke wa kufunga naye ndoa na kupata watoto kwani aliyewahi kuwa mchumba wake alimkimbia kwa aina ya maisha aliyonayo.

Licha ya kuwa tajiri mwenye mali za kutosha lakini nyumbani kwake wanaishi watu wawili tu yeye na dada wa kazi. Dada wa kazi hutakiwa kufanya usafi nyumba yote pamoja na kumuamsha kwa ajili ya chakula, Endapo dada wa kazi akitaka kumuamsha bosi wake basi hutakiwa kugonga Jeneza mara sita na kusubiri kwa dakika tano ili bosi wake atoke nje.

Hamisi anasema kuwa haofii maneno ya watu na hata kutengwa na jamii bali anachojua yeye kuwa ana pesa na yuko huru kufanya chochote anachojisikia kikubwa zaidi anajivunia kwa kitendo chake cha kuwasaidia watu wenye mahitaji.

View attachment 2917905
Define ajabu. Ajabu ni nini. Ili kitu kiwe cha ajabu inabidi kiwe na sifa gani?
 
Screenshot_20240227-140955.jpg
Screenshot_20240227-140925_1.jpg
 
Acha maswali toa maoni yako ndo nachotaka😀
Nitatoa vipi maoni kuhusu maajabu kama mimi na wewe hatujakubaliana ajabu ni nini?

Huoni kwamba hapo tunaweza kubishana sana wakati wote wawili tunataja neno hilo hilo moja "ajabu" lakini tunamaanisha vitu tofauti?

Ajabu ni nini?
 
Back
Top Bottom