Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Yeah! Andiko limekosa mantiki baada ya kubainisha kuwa lengo la kutunza afya ni ili usipungukiwe nguvu za kiume.

Waafrika tunakuza sana hii ishu ya nguvu za kiume kana kwamba maisha kwa ujumla wake maana yake ni nguvu za kiume! NONSENSE!

Andiko Lina mantiki kubwa mno. Sema bado hujapata upeo wa kuchambua maandiko ya namna hii.
 
Haya yote kwanza kabisa maisha yawe settled alafu mpaka maisha kuwa settle ni kuanzia 40+ alafu iyo 40+ ambayo maisha yanaanza kuwa settled ndo hayo malazi yanaanza kukuandama.. katika maisha kikubwa uhai tu
Kikubwa afya,unaweza kuwa hai na maisha yakakuchapa,magonjwa yanakuandama,ukatamani bora usingezaliwaga.
 
Kwema Wakuu!

Hatufuatiliani wala hatupangiani maisha. Ila tunakumbushana huku nami nikijikumbusha pia Kwa Nia nzuri tuu. Ili baadaye tusijekujikuta katika Huzuni kuu.

Vijana tunapoambiwa tule na tunywe Kwa nidhamu sio Kwa sababu tunaonewa wivu au kuna mtu anataka kuwa juu yetu Kwa kutupa amri. HASHA! Bali ni Kwa faida yetu.

Kisukari na Presha sio magonjwa mazuri Kwa ustawi wa Ndoa zetu. Ukisikia pigo Baya basi ni kukosa nguvu za kiume. Tena Kwa miaka 40 Kwa mwanaume bado ni kijana. Na Kwa bahati nzuri miaka hiyo wengi neema ndio zinazidi kufunguka na wamesha-settle.
Sasa ume-settle alafu unajikuta huna nguvu za kiume. Asikuambie mtu inahuzunisha Sana..

Ukiona Taikon anaelezea Jambo Fulani basi kaa nalo macho, lizingatie Sana. Kwa sababu Taikon nipo kwaajili ya kujenga na wala sio kubomoa.

1. Kula na kunywa vizuri,
i. Kula Mbomboga Kwa wingi, Kula Protein Kama nyama nyeupe, maziwa, mayai, Kwa wingi,
Kula wanga kidogo Sana. Mfano unapoka maharage mengi alafu unakula na wali kidunchu, au ugali kidogo na Samaki au nyama au maharage mengi.

ii. Matunda, pendelea Kula matunda,
Kama umeoa, pendelea Ndizi zilizoiva angalau kila siku moja hasa usiku, hii itafanya uume wako kuwa na nguvu kutokana na madini ya Potassium,
Mkeo aweke Kachumburi yenye Nyanya, vitunguu, limao na pilipili hizi zinaongeza Libido.
Safisha figo Kwa Matikiti, matango, usisahau mapapai na maembe, pia machungwa huku utapata vitamini

Kula Milo miwili ukiwa age ya 25-50 iwe balanced.

iii. Kunywa maji mengi, angalau Lita mbili na nusu mpaka tatu na nusu Kwa siku.
Pombe kunywa kiasi Kwa STAREHE sio kujiumiza. Angalau kwa wiki mara moja na hakikisha usinywe mpaka ukazima.
Maji mengi ni dawa kwani yanafanya seli za mwili wako kufanya kazi Kwa ufanisi zaidi. Maji hupunguza pia sumu mwilini na kuufanya mwili wako kuwa na Nuru,
Yaani mtu anayezingatia kunywa maji ngozi yake hung'aa

Pia maji mengi husababisha mtu kutokuzeeka Kwa haraka. Na hii ni kutokana na Uzalishwaji wa seli za mwili kufanyika Kwa ufanisi


2. Fanya mazoezi,
Mazoezi hujenga mwili na kuufanya kuwa na Afya, kwani hufanya mzunguko WA damu kufanya kazi vizuri. Kumbuka Damu ndio hubeba virutubisho na kuvisafitisha mwilini. Kumbuka pia ndani ya damu ndio kuna Seli nyeupe zinazolinda mwili dhidi ya magonjwa, Seli nyekundu ambazo husafirisha hewa ya Oksijeni kuzipa Seli, tishu na ogani Uhai. Hasahasa Ubongo.

Hii ni kusema mazoezi yanaimarisha ufanyaji kazi WA viungo vya Mwili Kama vile Ubongo. Hii inafanya akili kuwa active.

Aina ya mazoezi
i. . Mazoezi ya Mwili
Haya yanalenga zaidi viungo na organ za mwili. Kukimbia, Push-up n.k.

ii. Mazoezi ya Akili/Ufahamu.
Haya yanalenga zaidi tafakuri, uchanganuzi, uchambuzi, n.k. haya ni Kwa kusoma Nyaraka na vitabu, michezo na Bangua bongo, Game zinazoshughulisha akili n.k.
Pia mazoezi ya ubongo hufanyika Kwa kujaribu kufanya vitu vipya ili kutafuta changamoto mpya. Kama ni biashara, au kazi au miradi unaanzisha ili akili ipate changamoto mpya.

iii. Mazoezi ya Kiroho na Nafsi.
Haya hulenga zaidi roho na Nafsi yako.
Kudhibiti Nafsi yako na matamanio yake, mfano Kufunga Kula na kunywa,
Kama unapenda kunywa pombe kujizuia kutokunywa Kwa muda wa siku kadhaa.
Kama unapenda Kulala na wanawake, kujizuia hata Kwa miezi sita bila kuchepuka, hayo ni mazoezi ya kiroho na nafsi.
Pia kutoa Zaka au Sadaka Ile inayouma. Ni zoezi la Nafsi au kiroho.

Hii itakusaidia kujidhibiti, pia kuzuia Nyege mshindo au ukosefu wa maamuzi.

3. Mapumziko na Burudani/STAREHE.
Angalau Kwa siku ulale masaa yasiyopungua Nane.
Starehe au burudani angalau Kwa wiki au Kwa mwezi mara moja. Hii itakufanya usiyachoke maisha na kuyaona hayana maana.

Usingizi utakusaidia kutunza Ubongo wako na hii itakusaidia nyakati za uzeeni kwani utakuwa haupotezi kumbukumbu kijinga jinga.
Kabla watu hawajaona uzee wako wewe mwenyewe utaanza kuuona Kwanza Kwa kujikuta unasahau sahau mambo, na hiyo huanza kutokea miaka 30+ kama hutokuwa mtu wa kuzingatia mapumziko.

Kijana wa sasa unapaswa ujidhibiti mwenyewe ili isijekula kwako ufikishapo miaka 40.
Hakuna kitu kibaya Kama kufikisha umri huo yaani 40+ alafu ujikute hauna pesa, alafu magonjwa Kama kisukari na Presha vikupige. Ni hatari Sana.
Kupigiwa nje nje! Yaani mwanamke wako wala hatakuwa na Woga, nawe utakuwa unajua na chakumfanya hauna.

Wale mnaolalamika andiko refu nimewasikia. Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Asante
 
Kifo kipo pale pale, hakikwepeki; tunaweza tu kuongeza siku za kuishi, lakini kifo hakizuiliki.
 
kifupi kama una kazi inayokutoa jasho kisukari utakisikia tu,kama ni mtu wa ofcn mazoezi ni muhimu sana kama ulivosema.
Aisee usijidanganye
Kuna watu nawajua kazi zao zilikuwa za kutumia nguvu na bado kisukari hakijawaacha.Yaani kazi anayofanya mtu ni ngumu kiasi hakuna haja ya mazoezi.
Labda pia life style na chakula vinachangia.
Au ni ule ugonjwa wa kurithi unakuta familia ina historia toka vizazi
 
Wanawake wa siku hizi na staili za maisha yao ni vigumu sana kuwaridhisha! Tuombe sana Mungu na kumcha pia, usimfanyie mwenzako kile usichopenda kufanyiwa [emoji1431]
 
Andiko Lina mantiki kubwa mno. Sema bado hujapata upeo wa kuchambua maandiko ya namna hii.
ROBERT HERIEL, wewe ni kijana mdogo sana, naweza kutabiri uko kwenye 20's, na ndio maana umri uliotaja wa miaka 40 unauona ni mkubwa kiasi cha kuutabiria magonjwa..

Miaka 40 ni umri mdogo sana, mimi nimeshaupita na bado naonekana mdogo,.. Sina hizo dalili za visukari sijui na vitu gani ulivyosema...

Nimeelezea hayo kwa sababu wewe unadhani mimi sijapata upeo wa kuchambua ulichokiandika..., ngoja nirudi kwenye mada..

Ulichokiandika kina uhalisia fulani, ulichoharibu tu ni kuweka msisitizo kwenye nguvu za kiume na kuchapiwa, hayo ni mawazo ya watoto wadogo, wanaowaza ''kusimamia kucha" ili usichapiwe.. Ukishafika umri wa utu uzima kama wangu, mambo hayo utayaona ni IRRELEVANT!
 
Aisee usijidanganye
Kuna watu nawajua kazi zao zilikuwa za kutumia nguvu na bado kisukari hakijawaacha.Yaani kazi anayofanya mtu ni ngumu kiasi hakuna haja ya mazoezi.
Labda pia life style na chakula vinachangia.
Au ni ule ugonjwa wa kurithi unakuta familia ina historia toka vizazi
aise tutaponea wap sasa.
 
ROBERT HERIEL, wewe ni kijana mdogo sana, naweza kutabiri uko kwenye 20's, na ndio maana umri uliotaja wa miaka 40 unauona ni mkubwa kiasi cha kuutabiria magonjwa..

Miaka 40 ni umri mdogo sana, mimi nimeshaupita na bado naonekana mdogo,.. Sina hizo dalili za visukari sijui na vitu gani ulivyosema...

Nimeelezea hayo kwa sababu wewe unadhani mimi sijapata upeo wa kuchambua ulichokiandika..., ngoja nirudi kwenye mada..

Ulichokiandika kina uhalisia fulani, ulichoharibu tu ni kuweka msisitizo kwenye nguvu za kiume na kuchapiwa, hayo ni mawazo ya watoto wadogo, wanaowaza ''kusimamia kucha" ili usichapiwe.. Ukishafika umri wa utu uzima kama wangu, mambo hayo utayaona ni IRRELEVANT!

Mkuu miaka yenu na yetu ni tofauti kabisa.
Sasa Kama kijana wa 20's anatumia Mkongo au busta yoyote Ile ili mambo yamuendee unafikiri hiyo 40+ atakuwaje.

Mpaka nimeeleza Jambo hili ujue nimeshalifanyia upembuzi na uchunguzi Mkuu.

Kama umesoma vizuri kuna sehemu nimeandika Kwa mwanaume 40 bado ni kijana Mdogo. Lakini wengi waliofikisha umri huo Kwa miaka hii wanakuwa Hoi.

Waulize wanawake watakuambia, kaa na wanawake Kwa akili watakueleza, pia jihusishe kwenye mambo ya uzazi na nguvu za kiume utakutana na wanaume wengi WA namna niliyoeleza.

Ingawaje ulichosema ukweli lakini hakuna uhalisia katika Zama hizi
 
Kama mlikuwa mmefundwa ndio haina namna itabidi Mkeo iopujakuheshimu (aende akafanyie uchafu mbali)
Kuna kipindi unajikuta una Kisukari una Presha na Moyo umeshapanuka kwa Pombe za ujanani huna mtoto huna Nyumba hela zote ulifungulia zipu Ujanani.

Unaishia kuwa mpiga mbizi mashuhuri ili kulinda ndoa isibumbuluke😂🤣
 
Back
Top Bottom