Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Wanawake wa siku hizi na staili za maisha yao ni vigumu sana kuwaridhisha! Tuombe sana Mungu na kumcha pia, usimfanyie mwenzako kile usichopenda kufanyiwa [emoji1431]

Lengo sio kuwaridhisha Bali mwanaume kuweza kujimudu na kuepuka aibu na huzuni.
 
Kuna kipindi unajikuta una Kisukari una Presha na Moyo umeshapanuka kwa Pombe za ujanani huna mtoto huna Nyumba hela zote ulifungulia zipu Ujanani.

Unaishia kuwa mpiga mbizi mashuhuri ili kulinda ndoa isibumbuluke😂🤣

Mungu aepushe😂😂😂
Ujanja wote Keisha! Kudadadeki!
 
Aisee usijidanganye
Kuna watu nawajua kazi zao zilikuwa za kutumia nguvu na bado kisukari hakijawaacha.Yaani kazi anayofanya mtu ni ngumu kiasi hakuna haja ya mazoezi.
Labda pia life style na chakula vinachangia.
Au ni ule ugonjwa wa kurithi unakuta familia ina historia toka vizazi

Wengine wanasema kisukari kinapata watu wenye vipato😂😂
 
Mkuu miaka yenu na yetu ni tofauti kabisa.
Sasa Kama kijana wa 20's anatumia Mkongo au busta yoyote Ile ili mambo yamuendee unafikiri hiyo 40+ atakuwaje.

Mpaka nimeeleza Jambo hili ujue nimeshalifanyia upembuzi na uchunguzi Mkuu.

Kama umesoma vizuri kuna sehemu nimeandika Kwa mwanaume 40 bado ni kijana Mdogo. Lakini wengi waliofikisha umri huo Kwa miaka hii wanakuwa Hoi.

Waulize wanawake watakuambia, kaa na wanawake Kwa akili watakueleza, pia jihusishe kwenye mambo ya uzazi na nguvu za kiume utakutana na wanaume wengi WA namna niliyoeleza.

Ingawaje ulichosema ukweli lakini hakuna uhalisia katika Zama hizi
Umeandika vizuri..

Ngoja na mimi nijaribu kufafanua.
Suala la nguvu za kiume ni Conspiracy, ni njama. Kuna watu wanalikuza maksudi ili wafanye biashara.

Matokeo yake watu wasio na tatizo hili wanajengwa kisaikolojia na wanadhani wanalo, wanaanza kutumia hiyo mikongo na matokeo yake wanaharibikiwa kweli, wanakuwa tegemezi wa hiyo mikongo!

Tendo la ndoa sio vita, unaweza ukaenda raundi moja tu na wewe na mwenzako mkaridhika!, Lakini siku hizi, hata anaeweza kufanya raundi mbili ndani ya usiku mmoja anataka kuaminishwa kuwa ana tatizo.., Sio kweli! Suala hili lipo kisaikolojia zaidi..

Kwa hiyo TAIKON, unaposema kuwa hili ni tatizo kubwa unaweza ukawa unasaidia katika njama labda bila hata wewe kujua. Sikatai kwamba halipo, lipo ila siyo kwa kiwango kinachosemwa.

Otherwise, umeandika vizuri mkuu!
 
Umeandika vizuri..

Ngoja na mimi nijaribu kufafanua.
Suala la nguvu za kiume ni Conspiracy, ni njama. Kuna watu wanalikuza maksudi ili wafanye biashara.

Matokeo yake watu wasio na tatizo hili wanajengwa kisaikolojia na wanadhani wanalo, wanaanza kutumia hiyo mikongo na matokeo yake wanaharibikiwa kweli, wanakuwa tegemezi wa hiyo mikongo!

Tendo la ndoa sio vita, unaweza ukaenda raundi moja tu na wewe na mwenzako mkaridhika!, Lakini siku hizi, hata anaeweza kufanya raundi mbili ndani ya usiku mmoja anataka kuaminishwa kuwa ana tatizo.., Sio kweli! Suala hili lipo kisaikolojia zaidi..

Kwa hiyo TAIKON, unaposema kuwa hili ni tatizo kubwa unaweza ukawa unasaidia katika njama labda bila hata wewe kujua. Sikatai kwamba halipo, lipo ila siyo kwa kiwango kinachosemwa.

Otherwise, umeandika vizuri mkuu!

Umeongea vizuri Sana.
Mimi sipo katika propaganda ya kukuza kuwa kuna tatizo la nguvu za kiume.

Ila naeleza kuwa ugonjwa wa kisukari na presha ukimpata mtu moja ya athari zake ni pamoja na ukosefu wa nguvu za kiume.
Ndio maana nimeandika andiko hili ili kujikumbusha na kukumbusha watu kujihadhari na mitindo mibaya ya maisha ili tusijejikuta katika magonjwa hayo.

Hiyo ya nguvu za kiume ni kidokezo au kichomekeo ili kuwafanya watu waone uhatari na unyeti wa Jambo lenyewe.

Uliwahi kukaa na wagonjwa wanaume wa Sukari au Presha?
Kama uliwahi kukaa nao basi huwezi shangazwa na nilichoandika
 
Kwema Wakuu!

Hatufuatiliani wala hatupangiani maisha. Ila tunakumbushana huku nami nikijikumbusha pia Kwa Nia nzuri tuu. Ili baadaye tusijekujikuta katika Huzuni kuu.

Vijana tunapoambiwa tule na tunywe Kwa nidhamu sio Kwa sababu tunaonewa wivu au kuna mtu anataka kuwa juu yetu Kwa kutupa amri. HASHA! Bali ni Kwa faida yetu.

Kisukari na Presha sio magonjwa mazuri Kwa ustawi wa Ndoa zetu. Ukisikia pigo Baya basi ni kukosa nguvu za kiume. Tena Kwa miaka 40 Kwa mwanaume bado ni kijana. Na Kwa bahati nzuri miaka hiyo wengi neema ndio zinazidi kufunguka na wamesha-settle.
Sasa ume-settle alafu unajikuta huna nguvu za kiume. Asikuambie mtu inahuzunisha Sana..

Ukiona Taikon anaelezea Jambo Fulani basi kaa nalo macho, lizingatie Sana. Kwa sababu Taikon nipo kwaajili ya kujenga na wala sio kubomoa.

1. Kula na kunywa vizuri,
i. Kula Mbomboga Kwa wingi, Kula Protein Kama nyama nyeupe, maziwa, mayai, Kwa wingi,
Kula wanga kidogo Sana. Mfano unapoka maharage mengi alafu unakula na wali kidunchu, au ugali kidogo na Samaki au nyama au maharage mengi.

ii. Matunda, pendelea Kula matunda,
Kama umeoa, pendelea Ndizi zilizoiva angalau kila siku moja hasa usiku, hii itafanya uume wako kuwa na nguvu kutokana na madini ya Potassium,
Mkeo aweke Kachumburi yenye Nyanya, vitunguu, limao na pilipili hizi zinaongeza Libido.
Safisha figo Kwa Matikiti, matango, usisahau mapapai na maembe, pia machungwa huku utapata vitamini

Kula Milo miwili ukiwa age ya 25-50 iwe balanced.

iii. Kunywa maji mengi, angalau Lita mbili na nusu mpaka tatu na nusu Kwa siku.
Pombe kunywa kiasi Kwa STAREHE sio kujiumiza. Angalau kwa wiki mara moja na hakikisha usinywe mpaka ukazima.
Maji mengi ni dawa kwani yanafanya seli za mwili wako kufanya kazi Kwa ufanisi zaidi. Maji hupunguza pia sumu mwilini na kuufanya mwili wako kuwa na Nuru,
Yaani mtu anayezingatia kunywa maji ngozi yake hung'aa

Pia maji mengi husababisha mtu kutokuzeeka Kwa haraka. Na hii ni kutokana na Uzalishwaji wa seli za mwili kufanyika Kwa ufanisi


2. Fanya mazoezi,
Mazoezi hujenga mwili na kuufanya kuwa na Afya, kwani hufanya mzunguko WA damu kufanya kazi vizuri. Kumbuka Damu ndio hubeba virutubisho na kuvisafitisha mwilini. Kumbuka pia ndani ya damu ndio kuna Seli nyeupe zinazolinda mwili dhidi ya magonjwa, Seli nyekundu ambazo husafirisha hewa ya Oksijeni kuzipa Seli, tishu na ogani Uhai. Hasahasa Ubongo.

Hii ni kusema mazoezi yanaimarisha ufanyaji kazi WA viungo vya Mwili Kama vile Ubongo. Hii inafanya akili kuwa active.

Aina ya mazoezi
i. . Mazoezi ya Mwili
Haya yanalenga zaidi viungo na organ za mwili. Kukimbia, Push-up n.k.

ii. Mazoezi ya Akili/Ufahamu.
Haya yanalenga zaidi tafakuri, uchanganuzi, uchambuzi, n.k. haya ni Kwa kusoma Nyaraka na vitabu, michezo na Bangua bongo, Game zinazoshughulisha akili n.k.
Pia mazoezi ya ubongo hufanyika Kwa kujaribu kufanya vitu vipya ili kutafuta changamoto mpya. Kama ni biashara, au kazi au miradi unaanzisha ili akili ipate changamoto mpya.

iii. Mazoezi ya Kiroho na Nafsi.
Haya hulenga zaidi roho na Nafsi yako.
Kudhibiti Nafsi yako na matamanio yake, mfano Kufunga Kula na kunywa,
Kama unapenda kunywa pombe kujizuia kutokunywa Kwa muda wa siku kadhaa.
Kama unapenda Kulala na wanawake, kujizuia hata Kwa miezi sita bila kuchepuka, hayo ni mazoezi ya kiroho na nafsi.
Pia kutoa Zaka au Sadaka Ile inayouma. Ni zoezi la Nafsi au kiroho.

Hii itakusaidia kujidhibiti, pia kuzuia Nyege mshindo au ukosefu wa maamuzi.

3. Mapumziko na Burudani/STAREHE.
Angalau Kwa siku ulale masaa yasiyopungua Nane.
Starehe au burudani angalau Kwa wiki au Kwa mwezi mara moja. Hii itakufanya usiyachoke maisha na kuyaona hayana maana.

Usingizi utakusaidia kutunza Ubongo wako na hii itakusaidia nyakati za uzeeni kwani utakuwa haupotezi kumbukumbu kijinga jinga.
Kabla watu hawajaona uzee wako wewe mwenyewe utaanza kuuona Kwanza Kwa kujikuta unasahau sahau mambo, na hiyo huanza kutokea miaka 30+ kama hutokuwa mtu wa kuzingatia mapumziko.

Kijana wa sasa unapaswa ujidhibiti mwenyewe ili isijekula kwako ufikishapo miaka 40.
Hakuna kitu kibaya Kama kufikisha umri huo yaani 40+ alafu ujikute hauna pesa, alafu magonjwa Kama kisukari na Presha vikupige. Ni hatari Sana.
Kupigiwa nje nje! Yaani mwanamke wako wala hatakuwa na Woga, nawe utakuwa unajua na chakumfanya hauna.

Wale mnaolalamika andiko refu nimewasikia. Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Na sisi ambao tumeanza punyeto toka Primary mpaka leo hii tupo ndani ya ndoa na tunaendeleza tufanyeje??????
 
Uzi mzuri sana! Bahati mbaya hayo magonjwa yanapiga mpaka vijana wa 30+.

Nimezika bro ile march 12 siku chache kabla ya JPM.
Yaani mnavyozungumzia haya magonjwa napata uchungu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole Mkuu
Mbaya zaidi ukute yapo kwenye familia.
Kwa upande wa baba yangu sukari ipo inatembea kizazi hadi kizazi.
Basi nasi tunajua huko mbeleni kuna tutakaokuwa nao.
Imagine familia ya watu saba watatu tu ndio hawana sukari hawa waliobaki wanapambana nao.
 
Hapa kwenyewe nina miaka 28 nina show mbovu kabisa haijawahi tokea tangu dunia iumbwe nimeshaachwa na Wanawake kama 5 hivi,nikifika miaka 40 si ndio balaa ilo.
Uzuri kiuchumi nipo vzr acha niendelee kugonga vyombo kwa kwenda mbele nguvu kizibo hata pombe nisinywe kweli ? nimeshakuwa chronic kwa kuachwa nimeshazoea
Hahahahaha!!!!
 
Back
Top Bottom