Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Kijana jitunze, kuteremkia miaka 40+ kuna zimwi linaitwa Kisukari na Presha. Mkeo atakuvumilia?

Mweee.... ndiyo kwanza nimenunua serengeti lager inavuja jasho na hili andiko lako na hii wikiendi vitu viwili tofauti kabisa mpaka nimekumbuka enzi nakua babu yangu alikuwa hataki wakati wakula na kunywa udeal na mambo mengine leo nimeelewa babu kama aliiona hii siku, anyway kachupa kamoja, mbili n.k au hata kwa siku moja si dhambi.
 
Duh!🤦🏾‍♂️Starehe ya kwanza ya masikini.😄
hiyo sio starehe ya kwanza kwa maskini, hiyo ni starehe ya kwanza kwa kila mwanaume rijali haijalishi ni billionea ama zeronea.
 
Nabii Musa alikufa na miaka mingi (80 kama sikosei) na alikufa huku macho, meno yakiwa vizuri kama teenager. Enhee hapa wasemaje
Ni miaka 120, miaka 80 ndipo alipo itwa na Bwana kwenda kuwatoa wana wa Israel kwa farao Egypt
 
Kwema Wakuu!

Hatufuatiliani wala hatupangiani maisha. Ila tunakumbushana huku nami nikijikumbusha pia Kwa Nia nzuri tuu. Ili baadaye tusijekujikuta katika Huzuni kuu.

Vijana tunapoambiwa tule na tunywe Kwa nidhamu sio Kwa sababu tunaonewa wivu au kuna mtu anataka kuwa juu yetu Kwa kutupa amri. HASHA! Bali ni kwa faida yetu.

Kisukari na Presha sio magonjwa mazuri Kwa ustawi wa Ndoa zetu. Ukisikia pigo Baya basi ni kukosa nguvu za kiume. Tena Kwa miaka 40 Kwa mwanaume bado ni kijana. Na Kwa bahati nzuri miaka hiyo wengi neema ndio zinazidi kufunguka na wamesha-settle. Sasa ume-settle halafu unajikuta huna nguvu za kiume. Asikuambie mtu inahuzunisha sana.

Presha na kisukari yatakufanya ukose Raha ya maisha sio tuu kwenye ndoa Bali hata katika ulaji wako. Utapangiwa nini ule na kipi usile. Vyakula vizuri utabaki kuvitazama tuu, utakula chukuchuku na michemsho mpaka Ulie.

Ni akheri ujipangie sasa hivi Kula Milo mizuri Kwa kufuata kanuni za Afya ya Mwili. Na ni akheri magonjwa hayo yakupate too late yaani huko miaka ya 80+ lakini sio 40+.

Ni hatari na utateseka Sana. Miaka 80+ huna ulichobakiza, hata wewe mwenyewe utakiri kuwa umekula chumvi nyingi vyakutosha. Lakini sio miaka 40-60. Hiyo ni miaka michache Sana.

Ukiona Taikon anaelezea jambo fulani basi kaa nalo macho, lizingatie Sana. Kwa sababu Taikon nipo kwaajili ya kujenga na wala sio kubomoa.

1. Kula na kunywa vizuri
i. Kula Mbomboga Kwa wingi, kula Protein Kama nyama nyeupe, maziwa, mayai, Kwa wingi,
Kula wanga kidogo Sana. Mfano unapika maharage mengi halafu unakula na wali kidunchu, au ugali kidogo na Samaki au nyama au maharage mengi.

ii. Matunda, pendelea Kula matunda
Kama umeoa, pendelea Ndizi zilizoiva angalau kila siku moja hasa usiku, hii itafanya uume wako kuwa na nguvu kutokana na madini ya Potassium.

Mkeo aweke Kachumburi yenye Nyanya, vitunguu, limao na pilipili hizi zinaongeza Libido.
Safisha figo Kwa Matikiti, matango, usisahau mapapai na maembe, pia machungwa huku utapata vitamini

Weka chumvi kiasi yenye ladha ya Kwa mbali. Usiweke chumvi nyingi. Kuweka chumvi nyingi kuna sababisha hatari ya kupata Presha "Hypertension" ambayo sio nzuri Kwa Afya yako.

Kula Milo miwili ukiwa age ya 25-50 iwe balanced.

iii. Kunywa maji mengi, angalau Lita mbili na nusu mpaka tatu na nusu Kwa siku
Pombe kunywa kiasi Kwa STAREHE sio kujiumiza. Angalau kwa wiki mara moja na hakikisha usinywe mpaka ukazima.

Maji mengi ni dawa kwani yanafanya seli za mwili wako kufanya kazi Kwa ufanisi zaidi. Maji hupunguza pia sumu mwilini na kuufanya mwili wako kuwa na Nuru.

Yaani mtu anayezingatia kunywa maji ngozi yake hung'aa

Pia maji mengi husababisha mtu kutokuzeeka Kwa haraka. Na hii ni kutokana na Uzalishwaji wa seli za mwili kufanyika Kwa ufanisi

2. Fanya mazoezi
Mazoezi hujenga mwili na kuufanya kuwa na Afya, kwani hufanya mzunguko WA damu kufanya kazi vizuri. Kumbuka Damu ndio hubeba virutubisho na kuvisafitisha mwilini. Kumbuka pia ndani ya damu ndio kuna Seli nyeupe zinazolinda mwili dhidi ya magonjwa, Seli nyekundu ambazo husafirisha hewa ya Oksijeni kuzipa Seli, tishu na ogani Uhai. Hasahasa Ubongo.

Hii ni kusema mazoezi yanaimarisha ufanyaji kazi WA viungo vya Mwili Kama vile Ubongo. Hii inafanya akili kuwa active.

Aina ya mazoezi

i. Mazoezi ya Mwili

Haya yanalenga zaidi viungo na organ za mwili. Kukimbia, Push-up n.k.

ii. Mazoezi ya Akili/Ufahamu

Haya yanalenga zaidi tafakuri, uchanganuzi, uchambuzi, n.k. haya ni Kwa kusoma Nyaraka na vitabu, michezo na Bangua bongo, Game zinazoshughulisha akili n.k Pia mazoezi ya ubongo hufanyika Kwa kujaribu kufanya vitu vipya ili kutafuta changamoto mpya. Kama ni biashara, au kazi au miradi unaanzisha ili akili ipate changamoto mpya.

iii. Mazoezi ya Kiroho na Nafsi

Haya hulenga zaidi roho na Nafsi yako. Kudhibiti Nafsi yako na matamanio yake, mfano Kufunga Kula na kunywa. Kama unapenda kunywa pombe kujizuia kutokunywa Kwa muda wa siku kadhaa. Kama unapenda Kulala na wanawake, kujizuia hata Kwa miezi sita bila kuchepuka, hayo ni mazoezi ya kiroho na nafsi.

Pia kutoa Zaka au Sadaka Ile inayouma. Ni zoezi la Nafsi au kiroho.

Hii itakusaidia kujidhibiti, pia kuzuia Nyege mshindo au ukosefu wa maamuzi.

3. Mapumziko na Burudani/STAREHE

Angalau Kwa siku ulale masaa yasiyopungua Nane. Starehe au burudani angalau Kwa wiki au Kwa mwezi mara moja. Hii itakufanya usiyachoke maisha na kuyaona hayana maana.

Usingizi utakusaidia kutunza Ubongo wako na hii itakusaidia nyakati za uzeeni kwani utakuwa haupotezi kumbukumbu kijinga jinga.

Kabla watu hawajaona uzee wako wewe mwenyewe utaanza kuuona Kwanza Kwa kujikuta unasahau sahau mambo, na hiyo huanza kutokea miaka 30+ kama hutokuwa mtu wa kuzingatia mapumziko.

Kijana wa sasa unapaswa ujidhibiti mwenyewe ili isijekula kwako ufikishapo miaka 40. Hakuna kitu kibaya Kama kufikisha umri huo yaani 40+ halafu ujikute hauna pesa, halafu magonjwa Kama kisukari na Presha vikupige. Ni hatari Sana.

Kupigiwa nje nje! Yaani mwanamke wako wala hatakuwa na Woga, nawe utakuwa unajua na chakumfanya hauna.

Wale mnaolalamika andiko refu nimewasikia. Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hilo la nyege mshindo nalo ni neno!

Mimi ni mtu mzima nina ugonjwa wa mhemko wa balekhe!

Ninatamani kuishinda hii dhambi kwa mbinu mbali mbali lakini nakumbana na vikwazo lukuki!

Nikiona mwanamke anayevutia hisia zangu, kwanza huanza kujaa mate ya ugwadu mdomoni,hali initokeayo muda nionapo acidic fruits!

Hubaki nikijiuliza: hivi kila mwanaume, tamaa zake humsumbua kama mimi au nina ugonjwa halisi?

Sasa kwa kuwa umri umesonga najitahidi kujibaraguza kama sijaona kitu ili nisiadhirike, lakini wapi bwana!

Hujikuta navunja shingo bila kutarajia ili kumfuatilia mwanamke aelekeako ili kufaidi msura wake, hiyo sasa siyo kwa hiyari ni kwa lazima.

Nikiisha kuzindukana, hujikuta naongea peke yangu kujadili kutokukubaliana na umbo la mlimbwende huyo, kwamba hawezi kuwa vile, hilo lote si kweli kuwa ni la kwake, kajaladia ama la mchina, mbona anaringa sana hasalimii wazee na mawazo tele ya namna hiyo ya kipumbafu pumbafu nk nk.

Nikaona kujiepusha na ufedhuli huu, niitint gari pia ninunue miwani tinted glass kabisa, ili haya ya dunia niyaangalie kwa shadow kupunguza maumivu ya kuona live!

Mpaka hapo kujiheshimu nimeshindwa maana shetani akinipanda kichwani hunishawishi kuvua miwani ili kuondoa "arosto", sasa ninatafuta dawa.

Ninaomba kiongozi unipe njia halisi ya kujiepusha na hii fadhaa inayotesa uzeeni.
 
One of the best thread i have met so far jn 2022.

SUBSCRIBED ikiwezekana wenye confessions waje pia for good
 
Ukiwa na "mitindo mibaya ya maisha, kula na kunywa," mwili unasusa kuzalisha insulin ?????

Answer that.
Mtindo mbaya wa maisha hupelekea seli za mwili kujenga usugu wa insulin...yaani insulin resistance.

Hii hupelekea kisukari kwa vile unakula sukari ubongo unatoa maelekezo kuwa insulin izalishwe kuzipa signal seli za mwili kutumia sukari hiyo.

kwa vile seli zimejenga usugu dhidi ya insulin basi zinagoma kuitumia ile sukari, na matokeo yake sukari inakuwa nyingi kwenye damu. Mwili unazidi kuzalisha insulin zaidi kuzishinikiza seli kutumia sukari ambayo hupelekea hyperinsulinemia.

ili kukunusuru mwili hukufanya uhisi kiu kikali ili unywe maji na kuikojoa ile sukari iliyogomewa na seli za mwili...Ndiyo maana diabetics wengi huwa na hii dalili ya kiu kikali.

Ubongo hutafsiri kuwa mtu huyo hajala kwa vile seli zake zimeshindwa ku metabolize sukari...kitendo ambacho hufanya Ubongo utoe maelekezo ya kuzalishwa homoni ya kukufanya uhisi njaa ilihali umetoka kula muda si mrefu.

Hicho ndiyo kisukari kiletwacho na usugu wa seli dhidi ya insulin na si aina ile ya kisukari kijacho kwa kongosho kushindwa kuzalisha insulin ya kutosha.
 
Hilo la nyege mshindo nalo ni neno!

Mimi ni mtu mzima nina ugonjwa wa mhemko wa balekhe!

Ninatamani kuishinda hii dhambi kwa mbinu mbali mbali lakini nakumbana na vikwazo lukuki!

Nikiona mwanamke anayevutia hisia zangu, kwanza huanza kujaa mate ya ugwadu mdomoni,hali initokeayo muda nionapo acidic fruits!

Hubaki nikijiuliza: hivi kila mwanaume, tamaa zake humsumbua kama mimi au nina ugonjwa halisi?

Sasa kwa kuwa umri umesonga najitahidi kujibaraguza kama sijaona kitu ili nisiadhirike, lakini wapi bwana!

Hujikuta navunja shingo bila kutarajia ili kumfuatilia mwanamke aelekeako ili kufaidi msura wake, hiyo sasa siyo kwa hiyari ni kwa lazima.

Nikiisha kuzindukana, hujikuta naongea peke yangu kujadili kutokukubaliana na umbo la mlimbwende huyo, kwamba hawezi kuwa vile, hilo lote si kweli kuwa ni la kwake, kajaladia ama la mchina, mbona anaringa sana hasalimii wazee na mawazo tele ya namna hiyo ya kipumbafu pumbafu nk nk.

Nikaona kujiepusha na ufedhuli huu, niitint gari pia ninunue miwani tinted glass kabisa, ili haya ya dunia niyaangalie kwa shadow kupunguza maumivu ya kuona live!

Mpaka hapo kujiheshimu nimeshindwa maana shetani akinipanda kichwani hunishawishi kuvua miwani ili kuondoa "arosto", sasa ninatafuta dawa.

Ninaomba kiongozi unipe njia halisi ya kujiepusha na hii fadhaa inayotesa uzeeni.

Nafikiri wengi tupo hivyo sema tunajizuia tuu.
Nitaanzisha thread moja kuhusu hilo.

Huo ni ugonjwa wa wengi nikiwa mmoja wao.
 
Ahsante mzee baba hii imekaa vizuri.
Inakuwaje na hawa wanaofikia huko na pressure imeanza kuonekana ananyemelea na wanawake under 30 na muda ungine kuoa kabisa...!!!!
 
Mkuu mbona unataka kupingana na baiolojia?

Ukikumbwa na "menopause" kwenye 50's bado tu utaendelea kutamani?

Au kwa kuwa siku hizi mnabwia "vinasaba"?

Naomba maswali yote niyaelekeze kwako....

Masubiria majibu.....!😊
 
Hilo la nyege mshindo nalo ni neno!

Mimi ni mtu mzima nina ugonjwa wa mhemko wa balekhe!

Ninatamani kuishinda hii dhambi kwa mbinu mbali mbali lakini nakumbana na vikwazo lukuki!

Nikiona mwanamke anayevutia hisia zangu, kwanza huanza kujaa mate ya ugwadu mdomoni,hali initokeayo muda nionapo acidic fruits!

Hubaki nikijiuliza: hivi kila mwanaume, tamaa zake humsumbua kama mimi au nina ugonjwa halisi?

Sasa kwa kuwa umri umesonga najitahidi kujibaraguza kama sijaona kitu ili nisiadhirike, lakini wapi bwana!

Hujikuta navunja shingo bila kutarajia ili kumfuatilia mwanamke aelekeako ili kufaidi msura wake, hiyo sasa siyo kwa hiyari ni kwa lazima.

Nikiisha kuzindukana, hujikuta naongea peke yangu kujadili kutokukubaliana na umbo la mlimbwende huyo, kwamba hawezi kuwa vile, hilo lote si kweli kuwa ni la kwake, kajaladia ama la mchina, mbona anaringa sana hasalimii wazee na mawazo tele ya namna hiyo ya kipumbafu pumbafu nk nk.

Nikaona kujiepusha na ufedhuli huu, niitint gari pia ninunue miwani tinted glass kabisa, ili haya ya dunia niyaangalie kwa shadow kupunguza maumivu ya kuona live!

Mpaka hapo kujiheshimu nimeshindwa maana shetani akinipanda kichwani hunishawishi kuvua miwani ili kuondoa "arosto", sasa ninatafuta dawa.

Ninaomba kiongozi unipe njia halisi ya kujiepusha na hii fadhaa inayotesa uzeeni.



Mkuu mbona unataka kupingana na baiolojia?

Ukikumbwa na "menopause" kwenye 50's bado tu utaendelea kutamani?

Au kwa kuwa siku hizi mnabwia "vinasaba"?
 
"Gender" tofauti mkuu ndiyo maana nikanyooka bila kuuma uma maneno.

Neno "kukoma" kibaiolojia sisi halituhusu, lakini nyie linawahusu na wewe unaelewa vizuri tu, ndiyo nikahoji hivyo.
 
Ukiwa na "mitindo mibaya ya maisha, kula na kunywa," mwili unasusa kuzalisha insulin ?????

Answer that.
Kadiri umri unavyoenda organs za mwili zinapungua ufanisi. Mfano zinazozalisha insulin. Sasa inabidi uzisaidie Kwa kujiangalia mwenendo wa maisha yako.
Uwezo wa figo za mtu mwenye umri wa miaka 18 sio Sawa na figo za mtu mwenye miaka 60 kuna wear and tear sasa kama umezi-abuse wear and tear inakuwa kubwa.
 
Inafikirisha sana,ukose nguvu,halafu wadada wazuri hivi na ukute una mke Mzuri,unasaidiwa,hakika utakua na msongo wa mawazo sana,tuepuke hayo magonjwa kadri tutakavyoweza,kama yakitokea,iwe bahati mbaya tu.
Niliwahi kusikia bosi mmoja,hapa Mbulu,alikua na kisukari,mkewe alikua na kashfa ya kuleta vijana toka Arusha,analala nao,na mume hakuweza kumfukuza,bilashaka kwasababu alijua ana kisukari hivyo,akawa anavunga.R.I.P mzee.
Ni yule Dr nin?
 
Kwema Wakuu!

Hatufuatiliani wala hatupangiani maisha. Ila tunakumbushana huku nami nikijikumbusha pia Kwa Nia nzuri tuu. Ili baadaye tusijekujikuta katika Huzuni kuu.

Vijana tunapoambiwa tule na tunywe Kwa nidhamu sio Kwa sababu tunaonewa wivu au kuna mtu anataka kuwa juu yetu Kwa kutupa amri. HASHA! Bali ni kwa faida yetu.

Kisukari na Presha sio magonjwa mazuri Kwa ustawi wa Ndoa zetu. Ukisikia pigo Baya basi ni kukosa nguvu za kiume. Tena Kwa miaka 40 Kwa mwanaume bado ni kijana. Na Kwa bahati nzuri miaka hiyo wengi neema ndio zinazidi kufunguka na wamesha-settle. Sasa ume-settle halafu unajikuta huna nguvu za kiume. Asikuambie mtu inahuzunisha sana.

Presha na kisukari yatakufanya ukose Raha ya maisha sio tuu kwenye ndoa Bali hata katika ulaji wako. Utapangiwa nini ule na kipi usile. Vyakula vizuri utabaki kuvitazama tuu, utakula chukuchuku na michemsho mpaka Ulie.

Ni akheri ujipangie sasa hivi Kula Milo mizuri Kwa kufuata kanuni za Afya ya Mwili. Na ni akheri magonjwa hayo yakupate too late yaani huko miaka ya 80+ lakini sio 40+.

Ni hatari na utateseka Sana. Miaka 80+ huna ulichobakiza, hata wewe mwenyewe utakiri kuwa umekula chumvi nyingi vyakutosha. Lakini sio miaka 40-60. Hiyo ni miaka michache Sana.

Ukiona Taikon anaelezea jambo fulani basi kaa nalo macho, lizingatie Sana. Kwa sababu Taikon nipo kwaajili ya kujenga na wala sio kubomoa.

1. Kula na kunywa vizuri
i. Kula Mbomboga Kwa wingi, kula Protein Kama nyama nyeupe, maziwa, mayai, Kwa wingi,
Kula wanga kidogo Sana. Mfano unapika maharage mengi halafu unakula na wali kidunchu, au ugali kidogo na Samaki au nyama au maharage mengi.

ii. Matunda, pendelea Kula matunda
Kama umeoa, pendelea Ndizi zilizoiva angalau kila siku moja hasa usiku, hii itafanya uume wako kuwa na nguvu kutokana na madini ya Potassium.

Mkeo aweke Kachumburi yenye Nyanya, vitunguu, limao na pilipili hizi zinaongeza Libido.
Safisha figo Kwa Matikiti, matango, usisahau mapapai na maembe, pia machungwa huku utapata vitamini

Weka chumvi kiasi yenye ladha ya Kwa mbali. Usiweke chumvi nyingi. Kuweka chumvi nyingi kuna sababisha hatari ya kupata Presha "Hypertension" ambayo sio nzuri Kwa Afya yako.

Kula Milo miwili ukiwa age ya 25-50 iwe balanced.

iii. Kunywa maji mengi, angalau Lita mbili na nusu mpaka tatu na nusu Kwa siku
Pombe kunywa kiasi Kwa STAREHE sio kujiumiza. Angalau kwa wiki mara moja na hakikisha usinywe mpaka ukazima.

Maji mengi ni dawa kwani yanafanya seli za mwili wako kufanya kazi Kwa ufanisi zaidi. Maji hupunguza pia sumu mwilini na kuufanya mwili wako kuwa na Nuru.

Yaani mtu anayezingatia kunywa maji ngozi yake hung'aa

Pia maji mengi husababisha mtu kutokuzeeka Kwa haraka. Na hii ni kutokana na Uzalishwaji wa seli za mwili kufanyika Kwa ufanisi

2. Fanya mazoezi
Mazoezi hujenga mwili na kuufanya kuwa na Afya, kwani hufanya mzunguko WA damu kufanya kazi vizuri. Kumbuka Damu ndio hubeba virutubisho na kuvisafitisha mwilini. Kumbuka pia ndani ya damu ndio kuna Seli nyeupe zinazolinda mwili dhidi ya magonjwa, Seli nyekundu ambazo husafirisha hewa ya Oksijeni kuzipa Seli, tishu na ogani Uhai. Hasahasa Ubongo.

Hii ni kusema mazoezi yanaimarisha ufanyaji kazi WA viungo vya Mwili Kama vile Ubongo. Hii inafanya akili kuwa active.

Aina ya mazoezi

i. Mazoezi ya Mwili

Haya yanalenga zaidi viungo na organ za mwili. Kukimbia, Push-up n.k.

ii. Mazoezi ya Akili/Ufahamu

Haya yanalenga zaidi tafakuri, uchanganuzi, uchambuzi, n.k. haya ni Kwa kusoma Nyaraka na vitabu, michezo na Bangua bongo, Game zinazoshughulisha akili n.k Pia mazoezi ya ubongo hufanyika Kwa kujaribu kufanya vitu vipya ili kutafuta changamoto mpya. Kama ni biashara, au kazi au miradi unaanzisha ili akili ipate changamoto mpya.

iii. Mazoezi ya Kiroho na Nafsi

Haya hulenga zaidi roho na Nafsi yako. Kudhibiti Nafsi yako na matamanio yake, mfano Kufunga Kula na kunywa. Kama unapenda kunywa pombe kujizuia kutokunywa Kwa muda wa siku kadhaa. Kama unapenda Kulala na wanawake, kujizuia hata Kwa miezi sita bila kuchepuka, hayo ni mazoezi ya kiroho na nafsi.

Pia kutoa Zaka au Sadaka Ile inayouma. Ni zoezi la Nafsi au kiroho.

Hii itakusaidia kujidhibiti, pia kuzuia Nyege mshindo au ukosefu wa maamuzi.

3. Mapumziko na Burudani/STAREHE

Angalau Kwa siku ulale masaa yasiyopungua Nane. Starehe au burudani angalau Kwa wiki au Kwa mwezi mara moja. Hii itakufanya usiyachoke maisha na kuyaona hayana maana.

Usingizi utakusaidia kutunza Ubongo wako na hii itakusaidia nyakati za uzeeni kwani utakuwa haupotezi kumbukumbu kijinga jinga.

Kabla watu hawajaona uzee wako wewe mwenyewe utaanza kuuona Kwanza Kwa kujikuta unasahau sahau mambo, na hiyo huanza kutokea miaka 30+ kama hutokuwa mtu wa kuzingatia mapumziko.

Kijana wa sasa unapaswa ujidhibiti mwenyewe ili isijekula kwako ufikishapo miaka 40. Hakuna kitu kibaya Kama kufikisha umri huo yaani 40+ halafu ujikute hauna pesa, halafu magonjwa Kama kisukari na Presha vikupige. Ni hatari Sana.

Kupigiwa nje nje! Yaani mwanamke wako wala hatakuwa na Woga, nawe utakuwa unajua na chakumfanya hauna.

Wale mnaolalamika andiko refu nimewasikia. Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Shukran mkuu
 
Back
Top Bottom