Kijeshi, Urusi imefeli vibaya sana huko Ukraine

Kijeshi, Urusi imefeli vibaya sana huko Ukraine

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita!

Lengo la Kijeshi la Urusi ilikuwa ni kuingia Kiev haraka, kukamata mji mkuu na kuuangusha utawala wa Zelensky. Lakini hadi leo hii takriban siku ya 60 ya kivita, Urusi imeshindwa kukamata Kiev, na majeshi yake baada ya kukutana na upinzani mkali yakakimbia(retreat) kutoka miji ya ndani na kurudi huko Mashariki ambako walikuwa wanapakalia toka mwaka 2014.

Urusi imepata hasara kubwa sana ya vifaa na askari. Vifaru vyake vilikuwa vikikaangwa kwelikweli na Javelin missiles, pamoja na drones za Bayraktaar.

Logistics za kupeleka chakula na silaha ndanindani kwa askari wake ilikuwa shida

Wakati huo vikwazo vikiendelea kuichakaza urusi kwelikweli.

Hadi hivi sasa Zelensky amefanikiwa kuilinda serikali yake, na kinachofuata sasa ni kuandaa operesheni kabambe ya kumtoa nyoka pangoni huko Mashariki, Hii itakuwa operesheni kali sana na ngumu sana lakini itawezekana.

Urusi ni Taifa kubwa lakini uchumi wake ni mdogo kuliko jimbo moja tu la Texas Marekani, haina fedha za kupigana hii vita kwa muda mrefu, itakachokifanya ni kutafuta kideal cha kizushi na Ukraine ili kuficha aibu ya uso wake!

Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano!

Mafanikio ya kijeshi ya Urusi huko mashariki mwa Ukraine katika vita hii ya Sasa wala si jambo la ajabu maana warusi walishakuwepo huko toka mwaka 2014, hakuna kitu kipya!. Ni sawasawa na kupiga bomu mochwari na kisha kushangilia kuwa umeua!
 
Toka mwanzo wa vita wenzako walikua na maneno kama hayo mara uchumi wake sio imara hawezi kupigana vita mda mrefu mara kaishiwa chakula hawezi kulisha wanajeshi wake (muda huo huo anatoa tani za vyakula kusaidia wananchi walioko ukraine) mara kaishiwa silaha zimebaki za kupambana siku 3 tu, leo ni miezi bado silaha zipo na mashambulizi yanazidi kuendelea

Sisi wachambuzi ambao hatujui masuala ya kivita tunafanya analysis kwa kufuata hisia zetu tuendelee kuwa watazamaji tu hatujui malengo ya Putin yalikuwaje na hatujui kafanikiwa au vp kwa sasa kila mtu anachukua cheo cha kuwa military analyst anachambua anavyojua yeye.

Labda unaweza kuelezea Zelensky amefanikiwaje kuilinda serikali yake? Ukiangalia kwa jicho lako la kijeshi nani kapata losses nyingi kwenye vita hii?
 
Pro NATO kwa kujifanya wajuaji hawajambo aloo. Yaani pamoja na kipigo wanachokula Kila siku hao mabwege mpaka wanajifukia kwenye mahandaki mtu Bado unapata ujasiri wa kusema eti Russia kashindwa😃😃😃😃😃😃😃😃.
Kubalini tu Putin kawavua nguo NATO mnatafuta Kila kilichojiri mbele yenu kufunika nyuchi zenu mpaka mnaokota visivyo okoteka🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Ha ha ha ha ha ha
mpaka muda huu ukraine imegawanya kati kati miji ya ya lungnsk donenk mariupol kharkiv khersan oddess imeshakuwa chini ya Mrusi.

Mpaka muda huu ukraine haina tena bahari mijai tajawa hapo juu ni miji ya kichumi kwa ukraine. Kitenda cha urusi kuiteka miji hiyo kuna uwezekano uchumi wa ukraine usiufikie hata uchumi wa hapa morogoro

Alafu hii vita ni ya urusi na nato na nato wemepigika mno mpaka makamanda wao kukamatwa

Urusi sio marekani iliyoshindwa kuiteka kamji kadogo ka mogadishu pale Somalia.

ha ha ha ha ha ha ha
 
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita...
I used to respect your contribution hapa jf, ila katika hili umefeli kufanya deep and objective analysis, malengo ya urusi sio kuteka kievi hapana ni matatu na ame achive almost 70% zerelesiky baada ya vita hawezi kua Raisi wa ukurain tena hapo ameshikiliwa na Nato pamoja na US propaganda ila wa Ukuraini wamesha kiona ni ze comedy kabisa malengo ya Urusi ni:

*Denazification of ukurain achieved 90%
*Kutenga ukurain na Nato achieved 99%
*Kuunda jamhuri mpya Donesk Republic achieved 50%
Hapo amefail wapi?.
Other achievements of Russia
  • Ameonyesha ulimwengu kwamba ni superpower
  • Amejaribisha silaha zake za siku nyingi
  • Amedhofisha marikani na kumtia aibu
*Amesababisha kuyubisha uchumi wa EU na US. NK.
 
Inawezekana unachoongea ,ila Nina hofu na mataifa ya kidictetor maana wako radhi wananchi watembee uchi na kufa njaa ilimrad watimize kile walichokusudia.

Urusi inajali dola yake kuliko wananchi, Urusi hawatakubali wadhindwe ,hata kama itagharimu uchumi kuanguka,hilo kwao halipo, kwenye serikali za kidicteta hakuna uwajibishwaji,kila mtawala anafanya anavyojua, katiba imejaa vumbi, ole wako waziri au kiongoz au media mtangaze urusi ina njaa, Uhuru hakuna, kule media yoyote hairusiwi kuongelea mambo ya serikali, bila kuomba kibali aisee Mimi udicteta siufagilii kabisa
 
Hayo ni maono yako, Mwanaume Anaeajambisha Nchi Zaidi Ya 30, Alafu Unaleta Utumbo Wako Hapa
Mmeweka Mavikwazo Lakini Bado Mnatapatapa Kila Kukicha misumari Inawaingia Wenyewe
Ukiwa Na Akili Utagundua Malengo Ya Putin Sio Ukraine, Na Hii Operation Anaiendesha Yeye Anavyotaka Sio Ukraine Wala Nato
 
Ukiitazama hii vita katika jicho la kijeshi ni dhahiri urusi imefeli!
Imefeli kwa sababu imeshindwa kufikia malengo yake ya uanzishaji hii vita!

Lengo la Kijeshi la Urusi ilikuwa ni kuingia Kiev haraka, kukamata mji mkuu na kuuangusha utawala wa Zelensky. Lakini hadi leo hii takriban siku ya 60 ya kivita, Urusi imeshindwa kukamata Kiev, na majeshi yake baada ya kukutana na upinzani mkali yakakimbia(retreat) kutoka miji ya ndani na kurudi huko Mashariki ambako walikuwa wanapakalia toka mwaka 2014.

Urusi imepata hasara kubwa sana ya vifaa na askari. Vifaru vyake vilikuwa vikikaangwa kwelikweli na Javelin missiles, pamoja na drones za Bayraktaar.

Logistics za kupeleka chakula na silaha ndanindani kwa askari wake ilikuwa shida

Wakati huo vikwazo vikiendelea kuichakaza urusi kwelikweli.

Hadi hivi sasa Zelensky amefanikiwa kuilinda serikali yake, na kinachofuata sasa ni kuandaa operesheni kabambe ya kumtoa nyoka pangoni huko Mashariki, Hii itakuwa operesheni kali sana na ngumu sana lakini itawezekana.

Urusi ni Taifa kubwa lakini uchumi wake ni mdogo kuliko jimbo moja tu la Texas Marekani, haina fedha za kupigana hii vita kwa muda mrefu, itakachokifanya ni kutafuta kideal cha kizushi na Ukraine ili kuficha aibu ya uso wake!

Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano!
Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano![emoji1534][emoji1533]
 
Mwanzo donesk na luhansk waasi walikuwa wanamiliki nusu ya majimbo.sasa ivi waasi wanamiliki zaidi ya asilimia 70 ya majimbo.Jimbo la Kharkiv nusu linamilikiwa na warusi.jimbo la Zaporizhia asilimia 80 linamilikiwa na warusi.jimbo la kherson warusi wanamiliki asilimia 100.

Sasa hapo mpaka muda huu nani kapata hasara?
 
Kikubwa nilichojifunza katika hizi vita, Moyo wa askari una nguvu kuliko silaha kali ktk mikono ya askari asiye na moyo wa mapambano![emoji1534][emoji1533]
Sio nyoo zao kua ngumu wamekua brainwashed kwa mda mrefu tena kumbuka nivijana wadogo btn 18 to 32 wana rubuniwa ni sawa sawa na wale wanao jitoa muanga kwa kujilipua
 
Wanakunywa konyagi na double kick kisha wanajizima data. Eti lengo "likikua kuikamata kiev na kuangusha serikali" then? Lengo la ukraine ni nini? Askari wake ku surrender? Kuangamizwa miji? Silaha na miundombinu? Ukraine ame archive nini mpaka sasa.?

Acheni uoga, matokeo yatakuja kwa uwazi, saizi mnafichwa na BBC na CNN. Mpaka sasa serikali ya Ukraine haina control na majimbo yote ya mashariki, kuanzia cremea, mariupol donbase nk. Hili hutoambiwa na BBC, watu wamepiga kura kujitoa ukraiane, pale zinaenda kutokea nchi 3. Stay tuned... uongo na ukweli hutengana kama mafuta na maji.
 
Back
Top Bottom