Kikao cha Dharura: Mashabiki wa team 12 (Vichwa Ngumu) zilizoanzisha "European Super League". Tukutane hapa tujadili jambo hili

Mshindi wa UEFA huwa anapata kitita cha around € Millioni 19, mshindi wa pili anapata kitita cha € Million 15.

Super League wamesema kila team itakayo kubali kujiunga na Super League kama founding member, itapewa € Billion 3 kwaajili ya kufanya maandalizi/ujenzi wa viwanja. Halafu, mshindi kwenye mashindano atapata kitita cha € Millioni 500.

Kwa hio hela ya mshindi kupokea € Millioni 500, team zitakuwa zinacheza kufa na kupona na zitatoana roho uwanjani. League hii itakua na mechi kali sana kuwahi kutokea katika historia ya mpira wa miguu (Kwanza top clubs zote za ulaya zipo, halafu hela ni ndefu sana kwa mshindi atakae beba kombe).
 
Hakika maana na wachezaji wanakuwa hawana wasiwasi wa mkataba kutokana na pesa inayoingizwa. Hii idea ingekuwa nzuri ESL ikawa na formality hii;-

European Super League na European Platnum League kwa kushirikisha vilabu 40 katika divisions mbili Super na Platnum. Kwa kuanza Ikaanza hivyo 12 Founding Members na other 5 huku zikionngezwa timu nyingine nguli na second session kukawepo na kupanda na kushuka between them.
 
Figisu kama hio aliofanyiwa Arsenal VS Barcelona na mechi nyingine nyingi ndio maana wengi walianza kuichukia UEFA, uongozi wa UEFA & FIFA wa miaka ya 1998 mpaka 2007 huko ndio ilikua vizuri. Siku hizi wanaenda kisiasa sana.

We fikiria Mwenyekiti wa UEFA siku hizi mshahara wake ni siri. Wanaficha nini kama sio ufisadi.


Safari hii watu kuanzia 16 bora, wameshapata taarifa kwamba mshindi ni PSG alie andaliwa.
 
Bonge moja la wazo hilo, la kuwa na Super League na Platinum League, kwasababu hapa watawagusa mashabiki na team zote barani ulaya na dunia kwa ujumla.

Labda watafanya hivo in time.
 
Najaribu kupiga hesabu za huu mchongo......mapositive yapo kibak na manegative yapo kibao....

Ili UEFA na Fifa waokoe hili....wafanye announcement ya kuongeza dau washiriki na mabingwa wa mashindano yao hayo......Tena liwe la kutosha
 
UEFA ni kikundi cha wahuni Kama wahuni wengine mpira siku hizi ni biashara timu zinatumia uwekezaji mkubwa kweny ujenzi wa viwanja na bei za wachezaji sikuhizi zimekua ghari sana ,timu zinatumia gharama kubwa kutibu wachezaji endapo wakipata majereha ila pesa wanayotoa UEFA ni ndogo sana na ukizingatia wanamashindano kibao ambayo wachezaji haohao inabidi watumike
 
naunga mkono hoja hata africa haiwezekani bingwa akapata bilioni ambazo hazifiki 10
 

Uefa wahuni tu wanapiga sana hela, UEFA wakithubutu kuzitoa hzo timu kwenye liga yao bhs uefa itakutana na mtikisiko wa uchumi mkubwa kutokea, kumbuka hzo tim hapo juu ndo znaongoza kwa kuwa na sponsors wakubwa ndo wanaosponsa mpaka uefa sasa wakitolewa watakosa sponsors. Hii Uefa super league itaenda kupata wadhamini wengi sana na naona jinsi tv na website zitakavonunua matangazo ya vipindi vyao. Hii ndo revolution tunayotaka
 
Mara paap timu zote sita za epl zimejitoa

Pereza ataficha wapi uso wake.....

Simkubali hata kidogo jamaa
 
Pale epl boris kauwasha moto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…