joseph1989
JF-Expert Member
- May 4, 2014
- 17,420
- 35,765
Alipewa card na refs sio UEFA...UEFA wana hali ngumu sana kwa sababu vilabu vikubwa vya dunia tayari wameshaunga mkono jambo hili bila kupepesa nadhan UEFA na FIFA bora waje matao ya chini kuwe na league 3 ukitoa zile za ndani, hiyo Champion League, Super league na Europa hapa issue kubwa ni biashara kama UEFA wameona ni changamoto basi waongeze mapato kwa hivyo vilabu na kuwa wawazi zaidi ili clubs wanachama wavunje mkataba na Super League.,
Kwa mara ya kwanza soccer linapata mtikisiko wa aina yake, na nadhan hii UEFA hawakuilalia wala kuiamkia imekuja kufumuka tu tayari watu washaingia sokoni kushawishi vilabu.,
UEFA mimi nawachukia sana mwaka 2011 Arsenal ikichecha na Barcalona ikiwa tayari Arsenal wanaitoa barcalona basi walimpa kadi nyekundu Van Parsie kwa mipango tu ili fainali lazima akacheze Barcalona na team nyengine ili wake make more money.,
Ila huu ni ufala na usaliti..siungi hii movementHabari Wana Jamii, Habari Wana Soka.
Leo ni "Afe Kipa, Afe Beki - Bukta Chanika, Boxa Vuuka - Lazima Kieleweke" limeanza amsha amsha na kuwekwa wazi kwa team vichwa ngumu barani ulaya, zilizoamua kusaliti kambi na kuanzisha League yake, hii ni baada ya kuona "UEFA & FIFA" ni wahuni na wapangaji wa matokea ya mechi juu ya meza kwa kushinikizwa na makampuni ya kucheza kamali (Betting Companies).
Team zitakazo shiriki michuano hio zitapewa € Billion 3.5 kwaajili ya kujiwekeza katika maswala mbali mbali ya team zao (Kama kuboresha viwanja n.k), nia na madhumuni ni kuwapa mashabiki wa mpira mechi zilizo bora na kali kuliko zinazochezwa katika "UEFA & EUROPEAN LEAGUE" kwa sasa hivi. Mechi ambazo pia zitachezwa katikati mwa week kama zilivyo za UEFA hivi sasa, na weekend kuachia dirisha za mechi za ligi za ndani kama ilivyo.
Ligi itahusisha team 20, 15 ambazo ni timu mama za league na nyingine kupita kwa vigezo vya nafasi watakazopata katika misimamo ya ligi za ndani.
Leo mara baada ya kutangazwa rasmi kwa kuanzishwa League hio ambayo inaonekana kuwa "TISHIO KUBWA KUWAHI KUTOKEA" hasa kwa UEFA & FIFA, taharuki imetanda baada ya tamko kutoka kwa UEFA & FIFA kukemea na kulaani kwa kuanzishwa kwa michuano hio.
Licha ya tamko la UEFA & FIFA kulaani kitendo hicho na kukiita ni ha "KIHUNI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA SOKA", walienda mbali na kusema kwamba "TEAM YOYOTE ITAKAYOSHIRIKI MICHUANO HIO BASI ITAFUNGIWA KUSHIRIKI UEFA, EUROPA NA LEAGUE ZA NYUMBANI KWAO (National League)", na kuendelea kusema kwamba wachezaji watakao shiriki michuani hio watafungiwa kushiriki "WORLD CUP na EUROPE CUP".
Jambo hili limepelekea UEFA kuahirisha kwa muda usiojulikana mechi zilizosalia za Michuano ya UEFA, ambazo ni "MANCHESTER CITY VS PSG" na "CHELSEA VS REAL MADRID". Na kusema wataitisha kikao cha dharura na kujadiliana kumpa ushindi wa mezani PSG kwenye michuano ya "UEFA CHAMPIONS LEAGUE".
Mwenyekiti wa michuano hio mipya ya "EUROPEAN SUPER LEAGUE", anaeitwa na kutambulika na "UEFA & FIFA" kama mhuni mkuu Bwana Fiorentino Pérez nae hakusita kutoa tamko ya kwamba "MKIWAFUNGIA WACHEZAJI WETU KUCHEZA WORLD CUP QATAR, SIO TATIZO KUBWA KWETU KABISA, KWANI TUTAANZISHA NA WORLD CUP YETU".
Team zenyewe ni 12, ambazo zinatambulika kama "WAASISI WA EUROPEAN SUPER LEAGUE", ni;
1) AC Milan (Italy).
2) Arsenal (England).
3) Atletico Madrid (Spain).
4) Chelsea (England).
5) Barcelona (Spain).
6) Internazionale - Inter Milan (Italy).
7) Juventus (Italy).
8) Liverpool (England).
9) Manchester City (England).
10) Manchester United (England).
11) Real Madrid (Spain).
12) Totenham Hotspurs (England).
Wadau wa soka na kubeti, nimewaita tujadiliane
Karibuni kutoa mitazamo yenu na updates kuhusu swala hili.View attachment 1757074View attachment 1757075
Borris ana nguvu gani EPL?Perez kabaki na timu kumi sasa
Nadhani umeiona nguvu ya boris pale epl hapana chezea serikali wewe sasa kwa kutulia rungu lingine linakuja kutoka kwa huyo huyo boris.....
Hana tofauti na magufuli, kutumia mabavu hata sehemu isiohitaji mabavu.Borris ana nguvu gani EPL?
Boris ametishia kufuta vibali vyote vya wachezaji wa kigeni wanaocheza vilabu vya pale uingereza, hiyo ndiyo nguvu yake?
Watu wanapinga hii league haswa Uefa sio kwasababu ni mbaya ila ni kwasababu maslahi yao ya kifedha yanaguswa, fikiria ingekuwa vipi Champions league bila hizo team 12 zilizojitenga? Maana yake ilikuwa inaenda kupoteza mvuto ama kupotea kabisa, ndio maana vitisho vimetumika sana haswa kutoka England kwasababu kwasasa Kampuni zao ndio zina haki ya matangazo ya UCL, ila kama walikuwa hawahusiki hii ishu ingeendelea.,Hana tofauti na magufuli, kutumia mabavu hata sehemu isiohitaji mabavu.
Hii league ingefungua dirisha la vijana kucheza soka, match zingekua ni kali hatari. Team zingecheza kufa na kupona. UEFA siku hizi haina hata mvuto kabisa, team zote kubwa za England zinacheza EUROPA LEAGUE na hazipo UEFA.
Watu wanaipinga kwasababu ya uoga wa kujaribu opportunity mpya, na ndio maana vijana wengi hawaendelei kwasababu ya uoga wa kujaribu mambo mapya.
Walitakiwa wairuhusu icheze hio league, kama ingetokea sio league nzuri basi ingekufa, na kama ingetokea kuwa league nzuri basi FIFA na UEFA wangejiendeleza kwa mawazo mapya kufufua league zao.
Watu ni waoga wa competitors kibiashara. Ni ujinga na upuuzi huo watu waliokua nao kwa kuishi maisha kwa kukariri.
Kuna tetesi team za England zimepewa dau zito na UEFA kujitoa katika hio league, hii ni sawa na rushwa. Soon time will tell scandle nyingine katika soka, kama ilivyokua scandle ya Platini kupokea mpunga mrefu kutoka kwa Qatar ndani ya FIFA WORLD CUP.
Wanafiki haswa, Perez anadai hii project imefanyiwa kazi kwa miaka 3 na hivyo vikao vilikuwa vinaendeshwa na directors wa hizo club ila walivyokuja kugeuka ni kama walikuwa hawajui kilichokuwa kuna endelea.,Perez alijisahau kuwa alikua anapanga mipango na jopo la wanafik
Perez amesema hii league ni kwasababu ya kuokoa mpira wa miguu;Wanafiki haswa, Perez anadai hii project imefanyiwa kazi kwa miaka 3 na hivyo vikao vilikuwa vinaendeshwa na directors wa hizo club ila walivyokuja kugeuka ni kama walikuwa hawajui kilichokuwa kuna endelea.,
Halafu ni mashabiki wa team za England tu ndio ninaona wanalia sana sijui shida yao ni nini haswa, ila Spain na Italy sijaona hiyo shida.
Walionekana waliwashika vibaya SANA Uefa, jana nimeona interview ya Rais wa UEFA akiulizwa kama game za nusu fainali zitaendelea ama laa jamaa akasema uwezekano wa kutokuchezwa ni mdogo sana kwa kuwa walikuwa wameshaingia makubaliano tayari na wadau, so zile mara PSG atapewa ushindi zilikuwa ni kelele tu na panic kutoka kwa maafisa wa UEFA., jamaa walipata moto utadhani kuna raia wameuwawa.Perez amesema hii league ni kwasababu ya kuokoa mpira wa miguu;
1) UEFA inauwa mpira wa miguu, na siku hizi haina ladha wala mechi kali kabisa (Mechi kali zinaanza robo fainali). Wao wanataka Super League match kali zianzie group stage mpaka fainali.
2) Hakuna mtu aliojitoa mpaka sasa hivi kwenye Super League, kwasababu kuna kipengele cha kutokujitoa pindi utakapo sign mkataba wa kujiunga Hivo wote team 12 badi zipo kwenye hio league (Waliweka hivyo kwasababu ya kukwepa wanafiki watakao geuka geuka).
3) Super League haijafa bado, ipo standby kupisha kelele na figisu zinazo fanyia Europe.
Akili za waingereza na wabongo tofauti ni kidogo tu.Wanafiki haswa, Perez anadai hii project imefanyiwa kazi kwa miaka 3 na hivyo vikao vilikuwa vinaendeshwa na directors wa hizo club ila walivyokuja kugeuka ni kama walikuwa hawajui kilichokuwa kuna endelea.,
Halafu ni mashabiki wa team za England tu ndio ninaona wanalia sana sijui shida yao ni nini haswa, ila Spain na Italy sijaona hiyo shida.
Akili za waingereza na wabongo tofauti ni kidogo tu.
Wanafiki haswa, Perez anadai hii project imefanyiwa kazi kwa miaka 3 na hivyo vikao vilikuwa vinaendeshwa na directors wa hizo club ila walivyokuja kugeuka ni kama walikuwa hawajui kilichokuwa kuna endelea.,
Halafu ni mashabiki wa team za England tu ndio ninaona wanalia sana sijui shida yao ni nini haswa, ila Spain na Italy sijaona hiyo shida.
Hata hazitofautiani Mkuu,. Menno I meengi kila mtu ni mjuaji, huko soka mpaka viongozi wa kisiasa wanaingilia, huko Spain sijasikia tamko lolote za kiongozi wa kisiasa zaidi ya wadau wa soka., ndio maana sioni tofauti ya Waingereza na Wabongo.Akili za waingereza na wabongo tofauti ni kidogo tu.
Perez alichokuwa anataka ni namna ya kuongoza wigo wa mapato ndani ya club, anaona kama Uefa wanawanyonya sana ndio maana alitaka kujinasua huko.Chakushangaza kabisa ni kuwa ni kama watu ambao hawakujiandaa na hilo jambo, Perez alishajiripua na yupo tayari kwa lolote litakalotokea. Sasa wao sijui walitegemea mambo yatakwenda kilainilaini hivi? Nashindwa kuwaelewa kabisa.