Kikao cha mwisho tulikubaliana kuwa tutauza umeme nje, kulikoni sisi ndo tunanunua tena?

Kikao cha mwisho tulikubaliana kuwa tutauza umeme nje, kulikoni sisi ndo tunanunua tena?

Upekuzi101

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
221
Reaction score
542
Kikao cha mwisho tulikubaliana kuwa bwawa likikamilika hatutahangaika tena kuhusu umeme, zaidi tutakuwa na umeme wa kutosha hadi tutauza kwa majirani. Ghafla mama akiwa Same amesema itabidi tununue umeme Ili kuzuia umeme kukatika Kanda ya kaskazini.

Kwaiyo mheshimiwa Samia tukuamini kwenye lipi?
Je tuamini bwawa litamaliza tatizo la umeme au tuamini mpango wako mpya wa kununua umeme nje ndo utamaliza tatizo la umeme kaskazini?

Je swala la sisi Tanzania kuuza umeme ndo limekufa hivo au sisi ndo hatukuelewa vizuri uliposema tutauza umeme nje? au ulimaanisha baada ya bwawa kukamilika tutanunua umeme nje ?
Mtangulizi wako alikuwa bingwa wa kusema na KUTEKELEZA, wewe ni bingwa wa kusema na kuja kubadilisha ulichokisema baadae.

Hizi hotuba hawa jamaa wanakuchomekea tu unakuja kukutana nazo wakati wa kusoma tu au umedhamiria tu kutudanganya danganya kama watoto?

Mama Samia kuwa makini, watanzania tunakuangalia tu ila tushakuelewa kuwa wewe ni bora liende, maana haiwezekani tupambane kuzalisha umeme megawatt 2000 alafu Leo uje utuambie eti unapanga kununua tena umeme, isije ikawa washakuchomekea Ile mipango ya RICHMOND, ESCROW NA MEREMETA. Mambo ya kusema nyeupe Leo kesho unasema nyeusi yanatutia mashaka.

Je tutauza umeme, au tunauziwa umeme
 

Attachments

  • IMG-20250310-WA0023.jpg
    IMG-20250310-WA0023.jpg
    128.6 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0018.jpg
    IMG-20250310-WA0018.jpg
    51.6 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0014.jpg
    IMG-20250310-WA0014.jpg
    99.9 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0013.jpg
    IMG-20250310-WA0013.jpg
    88.3 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0006.jpg
    IMG-20250310-WA0006.jpg
    76.8 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0003.jpg
    IMG-20250310-WA0003.jpg
    47.6 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0002.jpg
    IMG-20250310-WA0002.jpg
    85.4 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0004.jpg
    IMG-20250310-WA0004.jpg
    13.3 KB · Views: 1
  • IMG-20250310-WA0000.jpg
    IMG-20250310-WA0000.jpg
    107.8 KB · Views: 1
Hata mimi nakumbuka minutes za kikao cha mwisho tulikubaliana sisi tutauza umeme nje ya nchi baada ya ule mradi mkubwa wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kukamilika. Nashangaa inakuaje tena tununue Ethiopia. Watupe ufafanuzi kwakweli
 
Hata mimi nakumbuka minutes za kikao cha mwisho tulikubaliana sisi tutauza umeme nje ya nchi baada ya ule mradi mkubwa wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kukamilika. Nashangaa inakuaje tena tununue Ethiopia. Watupe ufafanuzi kwakweli
Ndivyo ilivyokuwa, hivi vinavyotokea ni vioja
 
ʰᵃᵖᵒ ⁱᵗᵃᵏᵘʷᵃ ᵏᵘⁿᵃ ᵏᵃ ᵐᵖᵃⁿᵍᵒ ʷᵃᵐᵉᵏᵃᶠᵃⁿʸᵃ Τεηα ...υjυε νισηgσzι ωετυ hυωα ωαηατεsτ mιταmbσ κωαηzα τhεη ωασηε rεαcτιση κυτσκα κωα residents
 
Kikao cha mwisho tulikubaliana kuwa bwawa likikamilika hatutahangaika tena kuhusu umeme, zaidi tutakuwa na umeme wa kutosha hadi tutauza kwa majirani. Ghafla mama akiwa Same amesema itabidi tununue umeme Ili kuzuia umeme kukatika Kanda ya kaskazini.

Kwaiyo mheshimiwa Samia tukuamini kwenye lipi?
Je tuamini bwawa litamaliza tatizo la umeme au tuamini mpango wako mpya wa kununua umeme nje ndo utamaliza tatizo la umeme kaskazini?

Je swala la sisi Tanzania kuuza umeme ndo limekufa hivo au sisi ndo hatukuelewa vizuri uliposema tutauza umeme nje? au ulimaanisha baada ya bwawa kukamilika tutanunua umeme nje ?
Mtangulizi wako alikuwa bingwa wa kusema na KUTEKELEZA, wewe ni bingwa wa kusema na kuja kubadilisha ulichokisema baadae.

Hizi hotuba hawa jamaa wanakuchomekea tu unakuja kukutana nazo wakati wa kusoma tu au umedhamiria tu kutudanganya danganya kama watoto?

Mama Samia kuwa makini, watanzania tunakuangalia tu ila tushakuelewa kuwa wewe ni bora liende, maana haiwezekani tupambane kuzalisha umeme megawatt 2000 alafu Leo uje utuambie eti unapanga kununua tena umeme, isije ikawa washakuchomekea Ile mipango ya RICHMOND, ESCROW NA MEREMETA. Mambo ya kusema nyeupe Leo kesho unasema nyeusi yanatutia mashaka.

Je tutauza umeme, au tunauziwa umeme
Boss kasema...hahahaaa, hii ndiyo Tanzania. Nchi haina dira, ni vile kiongozi akiamka anaongea anavyo ona itafurahisha hadhira anayohutubia. Kama haya mambo ya umeme yapo kwenye mpango mkakati wa wizara, ni wazi inajulikana aidha tutauza umeme au tutanunua. Jibu liwe moja tu na ibaki kuwa hivyo kwa kipindi tulichojiwekea mkakati.
 
Watu wote hatuko sawa. Huwezi kumpa any old Joe or Jasmini kazi ya Rais.

Mtu hajawahi hata kujaza fomu ya maombi ya Urais, unajuaje anataka hayo majukumu ya kukaa anafikiria fikiria matatizo ya nchi ?

Achilia mbali uwezo, hata nia hajawahi kua nayo. Hajawahi kuomba hayo ma kazi kwa saab anajua kuna watu wengine wanaomzidi qualification, asingepita.

Bahati mbaya alipoingia akakuta Watanzania wenyewe ni push overs, unawasukuma kama walevi, wazee jeshini na kwingineko wanainama kumsujudia na kuponda vichwa vya wenzao wanamhoji huyu Mama.

Akaona, aaah, hii misakala ya Tanganyika nisotoke mvi bure, ngoja nijilie niondoke.

Kazi yeyote ambayo unaifanya bila accountability, haina bosi, na sio ya mtaji wa mfukoni kwako, na hujali legacy yako, huwezi kuumiza kichwa.
 
Ushaambiwa umeme wa ethiopia ni wa bei nafuu usiochoelewa ni nini? We ni bure kabisa
 
Boss kasema...hahahaaa, hii ndiyo Tanzania. Nchi haina dira, ni vile kiongozi akiamka anaongea anavyo ona itafurahisha hadhira anayohutubia. Kama haya mambo ya umeme yapo kwenye mpango mkakati wa wizara, ni wazi inajulikana aidha tutauza umeme au tutanunua. Jibu liwe moja tu na ibaki kuwa hivyo kwa kipindi tulichojiwekea mkakati.

Ethiopia ni karibu kuliko bwawa la Nyerere ARUSHA to RUFIJI 806km ARUSHA to ETHIOPIA 1935km. Sisi ndo tutakuwa hatujui hesabu 😁🫣
🤔🤔🤔🤔
 
Ushaambiwa umeme wa ethiopia ni wa bei nafuu usiochoelewa ni nini? We ni bure kabisa
Kwani si tulikubaliana baada ya kukamilika ujenzi wa bwawa la Nyerere, umeme utakidhi mahitaji ya nchi nzima! Na utakaobaki tutauza nje!!

Sasa inakuwaje tena kununua umeme wa Ethiopia, ili kuunganisha na grid ya Kaskazini? Ni kwamba Ethiopia ni karibu zaidi kuliko lilipo bwawa la Nyerere? Na inakuwaje umeme wa Ethiopia uwe bei nafuu kuliko umeme wa kwetu?

ccm acheni kuwaona wananchi hawana akili ya kufikiria bhana! Kama mna ajenda yenu ya siri iwekeni tu wazi ili wananchi wajue.
 
Kwani si tulikubaliana baada ya kukamilika ujenzi wa bwawa la Nyerere, umeme utakidhi mahitaji ya nchi nzima! Na utakaobaki tutauza nje!!

Sasa inakuwaje tena kununua umeme wa Ethiopia, ili kuunganisha na grid ya Kaskazini? Ni kwamba Ethiopia ni karibu zaidi kuliko lilipo bwawa la Nyerere? Na inakuwaje umeme wa Ethiopia uwe bei nafuu kuliko umeme wa kwetu?

ccm acheni kuwaona wananchi hawana akili ya kufikiria bhana! Kama mna ajenda yenu ya siri iwekeni tu wazi ili wananchi wajue.
ESCROW, RICHMOND NA MEREMETA ndo style zao
 
Wame mislead Bi Mkubwa hizi Hotuba Kachomekewa tu kwa kweli, Lakini swala Nyeti kama Nishati Kwanini asiwe aware kiasi Icho?

Ufafanuzi wa Msigwa ndio umekuja Kuharibu kabisa
 
Wame mislead Bi Mkubwa hizi Hotuba Kachomekewa tu kwa kweli, Lakini swala Nyeti kama Nishati Kwanini asiwe aware kiasi Icho?

Ufafanuzi wa Msigwa ndio umekuja Kuharibu kabisa
Hawa lao moja sema ni vile tu Mungu anajua kuumbua watu mapema. Yani tueekeze kwenye megawatt 2000 bwawa la Nyerere alafu sasahivi mtuambie mnanua umeme? Au mnaamua kujifanya mnanua umeme nje baada ya bwawa kukamilika Ile mle ela za bure kumbe hamna umeme wowote mnanua maana kimsingi TANZANIA haiitaji kununua umeme nje, zaidi labda kuuza.
 
Hawa lao moja sema ni vile tu Mungu anajua kuumbua watu mapema. Yani tueekeze kwenye megawatt 2000 bwawa la Nyerere alafu sasahivi mtuambie mnanua umeme? Au mnaamua kujifanya mnanua umeme nje baada ya bwawa kukamilika Ile mle ela za bure kumbe hamna umeme wowote mnanua maana kimsingi TANZANIA haiitaji kununua umeme nje, zaidi labda kuuza.
Kabisa Mkuu hakuna sababu ya msingi ya Kununua umeme Nje period, Hio Msigwa kusema wanakwepa transmission Losses je huo umeme Ukisafiri kutoka Ethiopia mpaka Tanzania hakutakuwa na izo Losses?
 
Kabisa Mkuu hakuna sababu ya msingi ya Kununua umeme Nje period, Hio Msigwa kusema wanakwepa transmission Losses je huo umeme Ukisafiri kutoka Ethiopia mpaka Tanzania hakutakuwa na izo Losses?
Hawa Wana jambo lao na tutalijua soon
 
Back
Top Bottom