Kikatiba, Waziri Mkuu ndiye Msimamizi wa Mawaziri wote. Sasa Lukuvi na Kabudi watasimamia Mawaziri vipi?

Nani asiye jua lukuvi,na kabudi ni watu potential !?, ameona kuwaacha hawa watu italeta mijadala mirefu ,so ameamua kutuliza hali ya hewa! Binafsi nimekuelewa kuwa ,hao wameachwa Kama washauri wakuu wa rais !! yaani kwa lugha ya mtaani watakuwa ni wakuda ,yaani wanaangalia wazr gani,au katibu yupi hawajibiki kikamilifu ,wanamshauri rais afanye Jambo !!! ila sijajua mishahara yao itakuwa na reflection ya idara gani.yote juu ya yote ,ametumia busara ku settle Mambo!!
 
Nimejifunza kuwa kuna mtu anawekwa Kando kinamna. Amesema "kuwasimamia vizuri hawa Mawaziri waweze kutenda. Yaani hawa vijana nilioapisha Leo wanahitaji usimamizi mzuri". That was a very strong indirect message to someone who was playing behind the back of her Excellency. Open the code!!!!
 
Hapa ndio umuhimu wa katiba mpya. Katiba iseme categorically idadi ya wizara na majina yao. Maana sasa hao watalipwa kwa nafasi zipi?
 
Katiba haijamtaja Rais kama mjumbe katika baraza la mawaziri!
 
Wasaidizi Maalum wa rais kuhusu utendaji wa Mawaziri.
 
Lukuvi sawa lkn siyo kwa kuboronga kwa Kabundi
 
PM ametengwa kimtindo? Huyu kumwondoa lazima serikali ivunjike; ni mtu mzito pengine mama asingependa kwenda to that extent kaamua kutumia Plan B. Let's wait and see!
Mimi naona waziri.mkuu anasafishiwa njia na kuwa waziri asiepatwa na uchafu.nahic kuna jamba mbele yake.

Kama unakumbuka waziri mkuu alipokwa madaraka yake tangu pale TAMISEMI iliporudishwa ofisi ya Rais.

Kuanzia pale waziri.mkuu ameachwa huru na hakua na kazi ya kufanya na kwa kua hakua na kazi ya kufanya na kama hana kazi ya kufanya utamchafuaje!!

Hivyo ninachokiona hapa huko baadae hata akiandaliwa kupeperusha bendera itakua lahisi kwake.
 
+ 'majukumu hayo hayapo kwenye muudo".
Mjinga ndio tu atachelewa kushtuka
 
... ungetusaidia kama ungetuwekea sababu na utaratibu wa Rais kumuondoa PM.
Kwa katiba ya sasa hakuna utaratibu ulioanishwa wa kumuondoa waziri mkuu, mawaziri, wakuu wa mikoa n.k pia kwa katiba hii Rais hahiitaji kutoa sababu zozote kuwaondoa viongozi au watumishi katika mhimili wake isipokuwa CAG tu.
 
PM aanze kukaa mguu sawa!
 
... hatoki kirahisi Mkuu! Ni process fulani ndefu tofauti na mawaziri wa kawaida ambao taarifa za kuondolewa kwao wanaweza kuzipatia bar. Pengine ndio maana mama hakutaka maprocess marefu kaamua atumie shortcut fulani hivi.
Na hiv pm ana mvuto kwa watu na wanasiasa ..bas imekua tabu kwelkwel
 
Naona mama katumia lugha ya kidiplomasia zaidi ila Nia ni kuwafanya washauri Wake binafsi
 

Atavimbiwa sana PM na Hao Mawaziri kwenye Cabinet usishangae mpake 2024 akawa hana Hamu na Icho cheo Kabisa
 
Mama kaamua kusawazisha hali ya hewa.
Binafsi naiona hii kama mbinu ya mama kuwabana lukuvi na kabudi ktk harakati zao za kumuangusha mama kwenye mbio zake za urais 2025. Maana hawa kabudi na lukuvi walikuwa ni key players wa sukuma gang
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…