Kikosi cha Timu ya Taifa kufuzu AFCON Chatangazwa

Kikosi cha Timu ya Taifa kufuzu AFCON Chatangazwa

Sio una wasiwasi bali ni kweli hao wanaocheza ligi za nje ya Africa ukimuacha Samatta na Dismas wana uraia wa nchi nyingine lakini wana uwezo wa kuchezea timu ya taifa bila shida maana inaruhusiwa kwenye mpira...
Nimewahi kusema hata wachezaji tunaowaleta kucheza ligi yetu, tukitambua wale wazuri sana halafu hawana rekodi za kuchezea timu za taifa huko watokako, tuwape uraia chap kwa haraka.

Mimi sina shida na kuwapa uraia wachezaji wenye asili ya Tanzania walioko huko nje, swali langu la msingi, wamekana uraia wao wa huko nje kama matakwa ya sheria zetu za uhamiaji zinavyotaka?

Kama tumeamua kufumba macho, kwa nini sasa tusibadili sheria za uhamiaji kama tumeona suala la uraia pacha lina faida. TFF hawana mamlaka ya kuvunja sheria za nchi.
 
Ni kweli kabisa. Halafu nina wasiwasi baadhi ya hawa wachezaji wana uraia wa nje pia, au tufumbe macho kwa kuwa ni jambo la kitaifa?
Kwa mfano Kamungo siyo raia wa Tanzania kwa sasa hivi. Alizaliwa kambi ya wakimbizi Nyarugusu halafu akapewa makazi ya Kudumu Marekani akiwa na miaka kumi na nne. Sasa hivi yeye ni mmarekani siyo Mtanzania wala Mrundi tena.

1686839669603.png



1686839777533.png


Hata hivyo ndiyo maana kuna haja ya kuruhusu uraia pacha.
 

Attachments

  • 1686839757190.png
    1686839757190.png
    175.5 KB · Views: 3
Kwa mfano Kamungo siyo raia wa Tanzania kwa sasa hivi. Alizaliwa kambi ya wakimbizi Nyarugusu halafu akapewa makazi ya Kudumu Marekani akiwa na miaka kumi na nne. Sasa hivi yeye ni mmarekani siyo Mtanzania wala Mrundi tena.

Hata hivyo ndiyo maana kuna haja ya kuruhusu uraia pacha.
Na hautasikia mtu analihoji hili.
 
wamekana uraia wao wa huko nje kama matakwa ya sheria zetu za uhamiaji zinavyotaka?
Suala la kuchezea timu ya taifa ipo hivi,unaweza bila shaka ukachezea timu ya taifa X wakati huohuo una utaifa wa taifa Y,kwa mfano pierre Aubameyang ni raia wa ufaransa lakini anaichezea Gabon achana na suala la utaifa pacha yeye prior nationality yake ni mfaransa kwa mambo mengine yote ukiachana na Football

Sheria za Fifa zinataka pia usicheze mechi za mashindano zaidi ya mbili za kimataifa kabla ya kuswitch to another national mfano Diego costa alichezea Brazil mechi mbili kabla ya kuhamia Spain..

Kwa hapa Tz miez michache iliyopita TFF walitoa waraka na special permission kwa ushirikiano na uhamiaji kwamba wale players Diaspora wote wanaotaka kuwakilisha Tz wanaruhusiwa kutuma taarifa zao watapewa kibali maalumu cha kuwakilisha Tz hata kama wana uraia wa nchi nyingine bila kuukana(FIFA inalikubali hili suala) hata kibu Dennis aliiwakilisha Tanzania akiwa na utaifa wa Burundi kama utakumbuka kabla ya kupewa uraia na kamishna wa uhamiaji kwa infuence ya simba sc..
 
Suala la kuchezea timu ya taifa ipo hivi,unaweza bila shaka ukachezea timu ya taifa X wakati huohuo una utaifa wa taifa Y,kwa mfano pierre Aubameyang ni raia wa ufaransa lakini anaichezea Gabon achana na suala la utaifa pacha yeye prior nationality yake ni mfaransa kwa mambo mengine yote ukiachana na Football

Sheria za Fifa zinataka pia usicheze mechi za mashindano zaidi ya mbili za kimataifa kabla ya kuswitch to another national mfano Diego costa alichezea Brazil mechi mbili kabla ya kuhamia Spain..

Kwa hapa Tz miez michache iliyopita TFF walitoa waraka na special permission kwa ushirikiano na uhamiaji kwamba wale players Diaspora wote wanaotaka kuwakilisha Tz wanaruhusiwa kutuma taarifa zao watapewa kibali maalumu cha kuwakilisha Tz hata kama wana uraia wa nchi nyingine bila kuukana(FIFA inalikubali hili suala) hata kibu Dennis aliiwakilisha Tanzania akiwa na utaifa wa Burundi kama utakumbuka kabla ya kupewa uraia na kamishna wa uhamiaji kwa infuence ya simba sc..
Jambo la msingi ulilosema ambalo sikuwa na taarifa nayo ni hiyo para ya mwisho uliposema uhamiaji walitoa ruhusa maalumu kwa hao wachezaji ambayo imewaruhusu kupewa uraia wa Tanzania bila kuukana huo walionao (sidhani kama ni kibali kama ulivyosema bali ni uraia wa Tanzania).

Lakini mfano wako wa kwanza hauna mantiki sana hapa kwa sababu Gabon na Ufaransa wote wanaruhusu uraia pacha.
 
Wachezaji wa makolo kaz kuchoma tu
Na shabalala angeachwa tu
 
Back
Top Bottom