Kikwete afanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri - Aprili 2012

Kikwete afanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri - Aprili 2012

Hata hawajaanza kazi mumeanza kulalamika, mulitaka muchaguliwe nyinyi akina pro-Hitler? Hebu angalia hiyo swastika uliyoweka hapo kaburu weeee.

Bibi bitimkongwe hiyo quotation ya Katiba Mpya umeipata wapi? Maana huyu jamaa ni shabiki namba moja wa JK, sijui alitaka ateuliwe yeye au alikuwa na watu wake? Maana naona kuna mahali anasema wamemshauri, hakusharika ... kaazi kweli kweli!

Tume ya katiba naona ushauri wenu ulikuwa fake au inawezekana hao mliowapendekeza hawafai au ni mabomu zaidi. Maana kupata watu waadilifu ni shughuli pevu. Sophia Simba alishasema ndani ya CCM hakuna msafi.
 
Lowasa ana Uwakilishi Mzuri sana ndani ya Baraza la Mawaziri. Ame Kweli Lowasa ni "Yupo ambaye Hayupo"
 
Kutokana na madiliko ya baraza la mawaziri, Dr Hussein Mwinyi ameteuliwa kuwa Waziri wa afya. Dr Mwinyi ni mbunge toka Zanzibar na hii wizara siyo ya Muungano, inashughulika tu na afya upande wa Tanzania bara.
Zanzibar wanayo wizara yao ya afya

Hebu tuangalie hii changamoto!
Usishangae yupo sahihi kabisa.Jurisprudential nature ya muungano wetu ni unique sana na hii ndio imeufanya udumu muda mrefu na watu wengine kupenda kujifunza kwetu.Tanganyika ili surrender power zake zote kwenye serikali ya jamhuri ya muungano na ilifutika na hakuna serikali duniani kwa sasa inayoitwa Tanganyika.kwa mimajili hiyo watanganyika wote baada ya muungano walibadilika kuwa raia wa Tanzania na sii raia wa tanganyika wala Zanzibar.Kwa upande wa zanzibar walisurrender some of their power to the union goverment.ndio maana kuna serikali ya mapinduzi ya zanzibar.hivyo mzazibari ni raia halali wa zanzibar na ni raia halali wa Tanzania.kwa kuwa serikali ya Tanganyika haipo hivyo mzanzibar ana dual citizenship.Hivyo basi mzazibari yoyote ana haki zote tanzania ikiwemo ya kuwa waziri hata kwenye wizara ambazo sio za kimuunganokwani zanzibar nayo ni Tanzania lakini mbunge wa TAnzania bara hawezi kuwa waziri zanzibar kwa sababu watanzania wote sio wazanzibari ila wazanzibari wote ni watanzania
 
Ni vigumu kuamini kama hili ndilo baraza la kufufua CCM! Nyalandu atakuwa na ubavu mbele ya yule Kamran wa Pakistan? Na akiungana na Pius Msekwa au Kinana huko maliasili kuna kitu kitabakia kweli? Adam Malima na Kilimo wapi na wapi kama sio utani? Makama ana ujuzi gani kwenye science & technology kama sio kulinda maslahi ya wakubwa-vodacom ili waendelee kukwepa kodi?

Kwenye wizara ya fesha ndio nimechoka kabisa. CHADEMA wajipange maana hii penalti iko wazi.
ulitaka apewe mchaga au mpare ndo uridhike?
 
Jamani mm natokea moshi vijijini huyu chami kwanza anaogopa wananchi wake haswa wa old moshi, kuna wakati alikuja huku na polisi akasema alijua tutamfanyia vurugu. so mi ningeshauri wamwondoe kbsa hata ikiwezekana ubunge.
 
Rais Jakaya Kikwete wa
Tanzania amewafuta kazi
mawaziri waandamizi katika
baraza lake la mawaziri. Katika
mabadiliko hayo, waziri wa
fedha Mustapha Mkullo ni
miongoni mwa waliowekwa
kando.
Mawaziri wapya waliochukua
nafasi mpya kuwapisha
walioachwa ni kama ifuatavyo
(walioachwa majina kwenye
mabano), Waziri wa Nishati na
Madini - Profesa Sospeter
Muhongo (William Ngeleja),
Waziri wa Fedha - Dr William
Mgimwa ( Mustapha Mkullo),
Waziri wa Uchukuzi - Dr
Harrison Mwakyembe (Omar
Nundu), Waziri wa Maliasili na
Utalii - Khamis Kagasheki
(Ezekiel Maige), Waziri wa
Afya na Ustawi wa Jamii - Dr
Hussein Mwinyi (Dr Haji
Mponda) na Waziri wa
Viwanda na Biashara - Dr
Abdallah Kigoda (Dr Cyril
Chami).
Ubadhirifu
Kabla ya kusoma orodha hiyo
mpya, Rais Kikwete alisema
majadiliano ya kina
yamefanyika na wenzake kabla
ya kuikamilisha, "Tumeona
wawili kati ya wale tunaweza
kuwahamishia katika wizara
nyingine, lakini tukitazama
baraza zima kwa ujumla wake,
tumewapanga hapa na pale
kuwabadilisha baadhi ya wizara
ili kuimarisha utendaji.
Hatujabadili idadi ya wizara,
tulikuwa na mjadala mkali
kidogo na wa kina kidogo - ipo
rai kuwa wizara hiyo imekuwa
kubwa mno".
Hatua hiyo ni sehemu ya
utekelezaji wa mapendekezo
yaliyotolewa na mdhibiti na
mkaguzi mkuu wa hesabu za
serikali ambaye alibainisha
hitilafu kadhaa za ubadhirifu
wa fedha za umma kwenye
wizara hizo.
Fedha za umma
Sura nyingi mpya zipo katika
nafasi za manaibu waziri.
Miongoni mwao ni January
Makamba anayechukua unaibu
waziri kwenye Wizara ya
Mawasiliano na Teknolojia,
akina mama wawili Saada
Mkuya Salum akiwa naibu
waziri wa fedha kutokea
Zanzibar bega kwa bega na
mwenzake mpya Janet Mbene
anayesimamia wadhifa huo huo
kwa upande wa Tanzania bara.
Vile vile Rais Kikwete kwa
mara ya kwanza amewateua
manaibu waziri wawili
kusaidiana majukumu kwenye
Wizara ya Nishati na Madini.
Mabadiliko hayo yamekuwa
yakisubiriwa kwa muda tangu
mjadala mkali ulipozuka
bungeni kuwahusu mawaziri
ambao wizara zao zilituhumiwa
kuhusika na ubadhirifu wa kiasi
kikubwa cha fedha za umma.
Hata hivyo Rais Kikwete
amewaeleza watanzania kuwa
kuanzia sasa, uwajibika wa aina
hiyo utawahusu maaafisa
waandamizi wote katika
wizara husika.
ORODHA YA MAWAZIRI NA
NAIBU MAWAZIRI
MAWAZIRI
1. OFISI YA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
(Mahusiano na Uratibu)Ndugu
Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
(Utawala Bora)Ndugu George
Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
(UTUMISHI)Ndugu Celina
Kombani, Mb.,
2. OFISI YA MAKAMU WA
RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Makamu wa Rais
(MUUNGANO)Ndugu Samia H.
Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Makamu wa Rais
(MAZINGIRA)Dr. Terezya P.L.
Huvisa, Mb.,
3. OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu (Uwekezaji na
Uwezeshaji)Ndugu Mary M.
Nagu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu (TAMISEMI)Ndugu
Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,
4. WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa
Afrika Mashariki Ndugu
Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa Ndugu Shamsi
Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa UjenziDr. John P.
Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa
Jamii Dr. Hussein A.H. Mwinyi,
Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo
ya Ufundi Dr. Shukuru J.
Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto Ndugu
Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa
Kimataifa Ndugu Bernard K.
Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na
Sheria Ndugu Mathias M.
Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani
ya Nchi Ndugu Emmanuel
Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya
Mifugo na Uvuvi Dr. David M.
David, Mb.,
Waziri wa Kazi na
Ajira Ndugu Gaudentia M.
Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano,
Sayansi na Teknolojia Prof.
Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Prof.
Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa MajiProf. Jumanne
Maghembe, Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara
Maalum Prof. Mark
Mwandosya, Mb.,
Waziri wa Kilimo, Chakula na
Ushirika Eng. Christopher
Chiza, Mb.,
Waziri wa UchukuziDr.
Harrison Mwakyembe, Mb.,
Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Dr.
Fenella E. Mukangara, Mb.,
Waziri wa Maliasili na
Utalii Ndugu Khamis
Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na
Biashara Dr. Abdallah O.
Kigoda, Mb.,
Waziri wa FedhaDr. William
Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na
Madini Prof. Sospeter
Muhongo, Mb.,
5. NAIBU MAWAZIRI
OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI
6. OFISI YA MAKAMU WA
RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu
wa RaisNdugu Charles
Kitwanga, Mb.,
7. OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa,
Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,
8. WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na
AjiraDr. Makongoro M.
Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo,
Chakula na UshirikaNdugu
Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya NchiNdugu Pereira A.
Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na
BiasharaNdugu Gregory G.
Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya
Mifugo na UvuviNdugu
Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa
KimataifaNdugu Mahadhi J.
Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya
Makazi,Ndugu Goodluck J.
Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na WatotoNdugu
Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya UfundiNdugu
Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano
wa Afrika MasharikiDr. Abdulla
Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na
UtaliiNdugu Lazaro Nyalandu,
Mb.,
Naibu Waziri wa UjenziNdugu
Gerson Lwenge, Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na
Ustawi wa Jamii,Dr. Seif
Suleiman Rashid, Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na
MadiniNdugu George
Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano,
Sayansi na TeknolojiaNdugu
January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa UchukuziDr.
Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari,
Vijana, Utamaduni na
MichezoNdugu Amos Makala,
Mb.,
Naibu Waziri wa MajiEng. Dr.
Binilith Mahenge, Mb.,
Naibu Waziri Nishati na
MadiniNdugu Stephen Maselle,
Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na
SheriaNdugu Angela Jasmine
Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa FedhaNdugu
Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa FedhaNdugu
Saada Mkuya Salum, Mb.,
Wataapishwa Jumatatu tarehe
8 Mei, 2012 saa 5.00 asubuhi
katika viwanja vya Ikulu
 
Hilo baraza ni kama mazingaumbwe, hamna jipya, ni sawa na kupasha kiporo!!!!!
 
vyizi umesahau yakua uteuzi unabase sana kwa kujuana na siyo sifa za utendaji. huyu bibie ni shemeji yake


Rais ameteua kwa kuangalia vigezo gani:baby: Mtu kama Hawa Ghasia ambaye hana uwezo wa kujibu hoja za maandamano ya wafanyakazi unamuweka wizara yenye matatizo makubwa kama TAMISEMI nini kitatokea, ushauri wa bure ulikuwa ni kumpandisha Agrey kuwa waziri kamili hilo ni Jembe.
Acha tuone hilo baraza lililosukwa kama litatusaidia.
 
Last edited by a moderator:
Uswahiba huu wa jk na mkuchika ni hatari kwa Taifa, hivi madudu yoote yaliyofanywa kwenye halimashauri imekuwaje waziri huyu akabaki Ktk baraza la mawaziri?. Nasikitika sana hata Jumanne magembe kabaki! Kwa kweli nihatari! Huku kwa walala hoi unga kg 1 ni sh 1200! haijawahi tokea tangu tupate uhuru! Huku mahindi yakiozea kwenye ghala la taifa.

Wadau je wamestahili kubaki?
 
Mkuu haikusaidii chochote wewe kama mwislamu kuwa na waziri mwislamu mwenzako mbambaishaji na asiyeweza kazi. Ndo maana unaona ameamua kumrudisha Kigoda na kuwaacha ndani Shukuru Kawambwa na Malima kupunguza pengo upande huo hauna watu. Tukitoka kwenye dini tutahamia kwenye ukabila. Mimi wasukuma wenzangu wawili wamepigwa chini nami nianze kulalamika? Hapana! Walikuwa wezi na wa mali za umma kwahiyo let them go. Tunataka maendeleo kwa waTZ wote.

Mawaziri wengi wa kisukuma huwa ni mabwege,sehemu zingine za nchi kama uchagan lami na umeme hadi vijijin,wenyewe wakipata uwaziri misifa kibao! Wabadilike,eneo lote la usukuman lingekuwa juu kimaendeleo kuliko sehemu yoyote tz hii! Raslimali kibao ziko kule.
 
Siamini kama aliyekuwa waziri wa TAMISEMI bado wanapeta....Ni kweli kuwa mtandao ule......unawahusu wengi. Nani amfunge mwenzake kengele.
 
Shabaasshhhh, kweli kazi ipo, na kama mtu anaweza piga mkwala wa hata watu wasitoke nje ya DSM halafu anakuja na utumbo wa kiasi hiki kweli tumeisha. Mwinyi Waziri wa Znz, wizara isiyo muungano, Hawa Ghasia, ni ghasia kweli kuanzia issue za B'moyo na kutokuwa na hoja, hapa labda kama issue ni urafiki. Kigoda... mgosi huyu yuko kwenye kundi la watafunaji na watia sahihi mbovu, malima... kwani lazima awe kwenye baraza. Hakuna watu... ataenda tena kuibiwa hotelini akiwa na vocha za pembejeo... Nyalandu... American boy... ndo atauza kabisa hao chui na tembo kuliko aliyekuwepo, hana msimamo ni bendera na mr... misifa. Waziri asiye wizara maalum, ni ujing uliobaki kwetu tu... hili tulikatae, na hii iwe moja ya ajenda za CDM kwa maandamano, maana hapa bado hakuna badiliko kwa hiyo kujiuzulu kwa raisi asiye ona hali halisi iwe ndo ajenda.

Hawa wabunge walioteuliwa bila kuapa... Wenye upeo wa kisheria tupeni mwanga, vinginevyo kweli kuna umuhimu wa kipengele cha kumshtaki rais anapo--abuse--madaraka aliyopewa. Nonsense;Nonsense; Nonsense... kichwa hoi kabisa.
Mapambano yaendelee bila kuweka silaha chini maana tumeuzwa.
 
Langu jicho na sikio! Da lkn mtu kama wasira wanaendelea kumwacha hapo kwa vigezo gani!
 
yaani Mwanri kelele zote hizo bado ni Naibu Waziri? January angepewa Uwaziri wa ardhi na Nyumba ili awatetee wanyonge. Anyway huko Mawasiliano anaweza akapaweza.
 
Back
Top Bottom