Kikwete alikuwa genius wa uchumi, Magufuli itabidi akajifunze kwake kama kweli ana nia ya kurudisha uchumi wa Tanzania kwenye reli

Kikwete alikuwa genius wa uchumi, Magufuli itabidi akajifunze kwake kama kweli ana nia ya kurudisha uchumi wa Tanzania kwenye reli

Kwanza inabidi ukajifunze "elementary" economics;
Ukitaka ku-import hizo pesa utatoa wapi? Ongelea wewe mwenyewe ukitaka kununua vitu lazima uwe na pesa na wewe kuwa na hiyo pesa lazima ukafanye kazi. Nchi ndiyo hivyo hivyo, lazima watu wafanye kazi nchi ipate pesa. Au watu hao wauze mazao nje ili mpate fedha ya kigeni muagize hayo mafuta. Kama pesa hakuna hapo nchini au mfukoni mwako lazima ukakope. Kwa Tanzania kwa sasa lazima ijikite kwenye export oriented economy na infrastructure investment. Hata kama unakopa na una invest kwenye infrastructure italipa, Tanzania bado inatakiwa ikue. Usikope kulipa mishahara.
Sasa jiulize mwenyewe hizo sectors ambazo Tanzania inaweza kujiimarisha iwe na export oriented economy ni zipi? Pamba isiuzwe, nguo zishonwe ziuzwe ulaya au Marekani, Food processing, fruits etc etc

Hizo data ulizotoa namba zake ndogo sana, huwezi kujenga uchumi kwa namba kama hizo. Unajua Tanzania biashara yake kidunia ni "negligible" ukilinganisha na nchi zingine? Yaani mapato ya Coca Cola cmpany kwa mwaka huwezi kulinganisha na Tanzania. Magufuli anachofanya yupo kwenye right track. Ila utekelezaji wake uwe flexible. Requires agility; yupo too "rigid".

Usianze kumwosha yule mwizi wenu JK kwa propaganda za "ukilaza"; Magufuli is by far the right man, ajirekebishe tu kwa hayo anayokosea, hasa dictatorship.
Miradi ya magufuli ikiisha italipa.
Una mengi ya kijifunza ndugu.. inawezekana huelewi background ya vitu nikivyovieleza.

Naona urudi shule kwanza ndo uje tubishane kwa hoja
 
Kipindi cha Mh. Kikwete ndicho kipindi ambacho kulikuwa na ushiriki wa asilimia kubwa kati ya sekta binafsi na serikali na raia wa kawaida wakaweza kufaidi mapato mazuri kutoka serikalini kupitia shughuli kadha wa kadha.

Kiuchumi haikuwa jambo baya sawa sababu hapo tunaita kuna fair distribution ya wealth na ni economic inclusion ya level nzuri.

Changamoto ya awamu ya kikwete ni usimamizi mbovu wa sheria za kulinda masilahi ya taifa na maadili ya viongozi. Watu waligeuza serikali ni mali yao binafsi na kufanya wanachotaka.

Hii aikuwa nzuri hata kidogo, kulitakiwa kuwapo na staha katika uongozi na adabu kwa katiba ya nchi. Watu walikuwa ni miungu watu na walivimba hata wakaota pembe.

Mh. Rais wa sasa naweza mpongeza katika eneo la kurejesha nidhamu ya uongozi na hofu kwa kiasi fulani ingawa sasa ameanza kuharibu kwa ubabe wa kimaamuzi na kuwa na vipaumbele binafsi.

Pia ameharibu zaidi kwa kuua ule ushirikiano uliokuwapo na sekta binafsi ambayo kwa nafasi kuwa walikuwa ndio daraja la kupitisha tija na masilahi ya kiuchumi kwa wananchi wa kipato cha kati na kuwafikia wale wa kipato cha chini.

Sekta binafsi ni nyeti sana kwa taifa kama letu ambalo serikali imefeli sana katika kutumia rasilimali zilizopo kujipatia mapato.
Bila sekta binafsi si ajabu hadi leo gesi tungekuwa hatuijui tungekuwa bado tunatumia mkaa na majiko ya mafuta. Gesi yote kwa 100% ingeuzwa nje kama malighafi ila shukurani ziwaendee makampuni binafsi leo hadi bibi yangu anatumia gesi kule mkoani na ikiisha analalamika kabisa kuwa hataki tumia mkaa.

Sekta binafsi ni chachu ya mambo mengi sana. Kuiuwa ni mwanzo wa kuifanya uchumi ushuke ufanisi na mzunguko wa pesa kuanza kufeli.

Serikali ya awamu hii ya walipwa mishahara wasiojua maana ya kutafuta kwa jasho imekazana kutengeneza makanuni n amasheria yasiyokuwa na uhusiano na uhalisia na kuwa changamoto.

Kimsingi raisi wa sasa angejikita katika kuboresha na sio kusimamia sheria za sasa za mamlaka mbali mbali na kuiacha sekta binafsi ikue then tungekuwa mbali sana.

Ila kwasababu ya uzito wa kufikiria wao wapo busy tu na kushikana mashati na kukomoana.

Anyways, ngoja amalize muda wake tujipange upya, kujikwa sio na kuanguka sio mwisho wa safari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu ni mchaga wa kishumundu unadhani utaongea nini kuhusu JPM zaidi ya kuponda! Watu wa huku Kilimanjaro na Arusha mna ukabila na ukanda wa kishenzi sana ilihali sisi huko makwetu mnaishi tu bila ubaguzi.

Nasema wazi Rais huyu wa sasa angekua ni Mchaga,Mmeru,Mmasai wala maingekua na ujinga wa makelele yasiyo na maana kama jinsi mlivyo maana tunakujueni vyema.

Hakuna Rais anayeingia mamlakani pasi MUNGU kupenda hivyo na isitoshe kazi anayofanya JPM ni mna macho lakini hamuoni,mna maaikio lakini hamsikii..mpo mpo tu kama ndondocha
 
Mimi siyo mchumi lakini ninajiuliza hivi kuwekeza kwenye Long term investments ambazo zinatumia Government spending ambazo tunategemea kupata mult plier effect kwenye uchumi na sekta ya kijamii kuna shida gani? Pia keep in mind serikali imewekeza sana kwenye sekta ya elimu,afya,maji,umeme etc je hiyo siyo social investment by implication etc ? Inategemea kwenye analysis yako unatumia theoretical/ economic approach ipi na kwa mtizamo na models zipi kupima mafanikio ya sasa.
Inawezekana kuwekeza lakini inabidi kutazama at who's expense!

Mfano ninaoweza kukupa ni wa mtu na mkewe wanapopanga maswala ya maendeleo ya familia yao.

Wanaweza kuamua kuanza kufanya maendeleo kabla ya kuleta watoto kwa kuwekeza katika biashara na miradi ili muda wakaianza kupata watoto wawe na akiba ya kutosha ya kulisha na kuhudumia watoto kwa vitu kama elimu, mavazi na entertainment mbali mbali bila kuathiri mingapo yao ya maendeleo.

Lakini pia wanaweza kupata watoto kwanza kisha wakati watoto wanakua na mahitaji yao yanaongezeka hapo hapo wakawa na changamoto ya kubalance pesa na muda kuhudumia watoto na hapo hapo kufanya maendeleo. Hapa kuna hatari ya kufeli kwa baadhi ya mambo sababu ya maandalizi mabovu, watoto wanahitaji pesa kuwatunza ila with no return, ujenzi unahitaji pesa but with no return. Ila biashara zinahitaji pesa kwaajiri ya mtaji ili zilete returns kwenye familia.

So kwa mfano huo, nikurejeshe katika uhalisia. Sisi ni kweli tunahitaji miundo mbindu ila katika baadhi ya maeneo na sio kwa uharaka wa hivyo.

Sasa kulikuwa na haja gani ya kununua ndege zote zile kwa haraka as if ni lazima. Pia kuna haja gani ya kujenga reli ambayo hatujaelewa itabeba nini kwa sasa ikielekea huko inapokwenda....?!

Kuna vitu huwa inafika muda utasikia raia wenyewe wanakwambia wanataka kitu fulani. Na sio wewe useme tunatakiwa kuwa na kitu fulani.....

Jambo jingine ni kwamba kuelekeza nguvu kufufua mashirika ya serikali ambayo management yake ni ya watu wenye elimu ya juu ila wasio na ufanisi wa wanachofanya plus rushwa na uhujumu juu hii ni kupoteza sana pesa, hizo pesa wangepewa vijana wa Tanzania wachache wenye ambition ya biashara wangeshafika mbali sana kimaisha na kutoboa.

Serikali inatakiwa kuwekeza katika kuongeza idadi ya mabilionaire na mamilionaire hapa nchini na kila mkoa...... Unapokuwa na raia wenye kipato kidogo hata msawala ya maendeleo ya viwanda ni ndoto isiyokuja kutimia.... Sababu nani atanunua, gari, nguo, simu nzuri kama hakuna hela..... Nani atapanda ndege aache basi....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fresh Natombe..!!
Mnaweza msingizia mambo mengi Kikwete. Lakini epukeni kumsingizia kuwa alikuwa Genius. Huko ni kumkebeh.

Lakini wewe inawezekana hujui maana ya neno genius. Ungejua usingelitumia hili neno kwa mtu kama kikwete.

Kwa kauli hizi naona ni bora Magufuli aendelee kuongoza. Maana kama bado kuna watu wana akili kama zako ni hatari kwa taifa.

Kikwete aliiharibu hii nchi pakubwa sana.
 
Kweli kabisa mtu unajiita naa ntombe? Hata kama ni mwanamke huwezi jiita jina hilo.
 
Apendae kujifunza huwa bora zaidi na upunguza chance ya kukosea. Kujifunza sio ujinga kwan Hakuna ajuaje KILA kitu
 
Back
Top Bottom