Elections 2010 Kikwete awateua Meghji na Nahodha ubunge

Elections 2010 Kikwete awateua Meghji na Nahodha ubunge

2.jpg
 
Msijaribu kupotosha umma, huo ni uongo na ufisadi. Hivi mnapata raha gani mnaposema uongo?? Kwanini tunashindwa kujadidi issue na ukweli wenyewe. Tuwache udini na chiku zisizokua na msingi!!


Kwa hiyo tuogope kusema kama tunaona kuna chembe za rasilimali za taifa kutumika kunufaisha watu kifamilia zaidi? Kwani unafikiri ni siri kwamba Mama Meghji ni mkwe?

Hebu niambia kama kweli meghji na mwanamke mchapakazi kwani nini kwa zaidi ya miaka 35 haendi jimboni kugombea? Kwa nini asubiri kutunukiwa ubunge?

Mbona Halima Mdee kaenda jimboni? Mbona wana Kawe wamemtosa mgombea wa CCM na NCCR na kumpa mwanadada Halima Mdee? Tena jimbo la Kawe lenye changamoto nyingi?

Kwanini Meghji asiende kugombea jimboni? Kweli miaka 35 ya kuwa mbunge wa kutunukiwa hajapata ujasiri wa kwenda kugombea?

Au kuna kingine ambacho watanzania hatukijui na hatukioni ambacho Mkuu wa Kaya anakiona? Na vipi kuhusu uhusiano wake na kigogo mmoja mkubwa? Je uteuzi wake umefuata merits? Hicho ndo tunachokijadili hapa!!
 
- Well, kwa kweli kwenye siasa ni lazima ku-comment kwa chochote kinachotokea hasa wakati huu wa mwisho wa uchaguzi na hasa uchaguzi wa mwaka huu,

- However: my take ni kwamba huu uteuzi ni non-effect kwa taifa kwa sababu kwa wale mnaojua vizuri functions za wabunge na effect zao bungeni, Wabunge wa Viti Maalum na wabunge 10 wa kuteliwa na Rais huwa hawana nguvu kabisaa na hata Mawaziri huwa hawawasikilizi kabisaa.

- Otherwise, Mh. Nahodha akiwa Visiwani hakuharibu na amekua royal asiye na makundi, pia ni mchapa kazi kwa hiyo hapa naona akipewa u-Waziri wa Muungano. Mama Meghji, ameshiriki sana kwenye kampeni za majuzi na ni mtu wa karibu sana na "Kigogo" mmoja na yeye namuona akirudi Cabinet, huyo mwingine namuona akiwa mbunge tu!

- Ninaamini ni uteuzi wa kisiasa za Muungano zaidi kuliko 2015, ingawa kama Mama Meghji atarudi tena Cabinet, baada ya kuondoka kwa kashfa italeta maswali valid ya commitment ya uongozi wa hiii awamu kwa wananchi, hasa ukiheshimu matokeo ya uchaguzi ulioisha, siamini kwamba CCM watafanya makosa hayo, maana itakua ni kuanza kujichimbia mapema kaburi la 2015.

- CCM imefika mahali sasa ni lazima tuambiane ukweli tena bila kuogopana wala kuoneana haya hizi tabia za kuwazungusha viongozi wale wale na hasa walioharibu tayari na huku tukiacha vijana wengi waliochaguliwa majuzi tena wengi wao ni Ma-Doctors wa kweli, itakatisha tamaa sana, maana comes 2015 hawa vijana wataishia kuingia Upinzani kwa hili ninasema hivi iwapo tu huyu Mama atapewa tena U-Waziri, ni matumaini yangu kuwa Mwenyekiti wa CCM taifa ataheshimu matokeo ya uchaguzi wa majuzi na kumuacha huyu mama bungeni tu, au ikibidi kumpa nafasi hukooo kwenye mambo ya Muungano tu!

- Wananchi tumechoshwa na hawa viongozi walioharibu tayari, sasa wapewe wengine wapya, maana wapo wengi sana!



William.


Kwa mara ya kwanza mkuu umeongea pointi. Thx.
 
Hiki kipindi ni cha lala salama, hiyo ya maam'kwe ni cha mtoto subiri all stars watangazwe:deadhorse:
 
huyo mwingine ni mpya katokea wapi? Prof Makame mnyaa Mbarawa, nani ana cv yake?

Makame Mnyaa Mbarawa
mechanical engineer, researcher

Location: Pretoria
Country: South Africa
Makame Mnyaa Mbarawa is recognized in Marquis Who's Who.:tape:
 
Kwa hiyo tuogope kusema kama tunaona kuna chembe za rasilimali za taifa kutumika kunufaisha watu kifamilia zaidi? Kwani unafikiri ni siri kwamba Mama Meghji ni mkwe?

Hebu niambia kama kweli meghji na mwanamke mchapakazi kwani nini kwa zaidi ya miaka 35 haendi jimboni kugombea? Kwa nini asubiri kutunukiwa ubunge?

Mbona Halima Mdee kaenda jimboni? Mbona wana Kawe wamemtosa mgombea wa CCM na NCCR na kumpa mwanadada Halima Mdee? Tena jimbo la Kawe lenye changamoto nyingi?

Kwanini Meghji asiende kugombea jimboni? Kweli miaka 35 ya kuwa mbunge wa kutunukiwa hajapata ujasiri wa kwenda kugombea?

Au kuna kingine ambacho watanzania hatukijui na hatukioni ambacho Mkuu wa Kaya anakiona? Na vipi kuhusu uhusiano wake na kigogo mmoja mkubwa? Je uteuzi wake umefuata merits? Hicho ndo tunachokijadili hapa!!

Wewe na wenzako ndio mliosema kuwa zakia ni mama mkwe, sasa unaruka ruka nini?? Wewe ulichojadili ni kuleta uongo kuwa Zakia ni mkwe, sijaona wapi umejadili kingine. Ingekua jambo la hekima kama ungeweza kusema ukweli uliodanganya, au kuthibitisha madai yako. It is that simple!
 
Makame Mnyaa Mbarawa
mechanical engineer, researcher

Location: Pretoria
Country: South Africa
Makame Mnyaa Mbarawa is recognized in Marquis Who's Who.:tape:

Kwenye uchaguzi wa mwaka huu;wapiga kura wamemnyang'anya Rais JK na CCM yake majimbo zaidi ya 20 ya Uchaguzi waliyokuwa wanayashikilia;na sababu moja wapo kubwa ni hii ya ukubwa wa serikali yake lkn BADO HAJASIKIA NA ANAENDELEA KUITANUA SERIKALI!

Kuteua hata Mbunge mmoja tu ni kuiongezea serikali gharama kubwa za uendeshaji ZISIZO NA ULAZIMU WOWOTE lkn yeye hadi sasa kateua watatu na likely atazidi kuteua zaidi;Mwaka 2015 huu ni ushahidi mwingine kama CCM bado hawajifunza kwa kichapo cha mwaka huu!
 
Wewe na wenzako ndio mliosema kuwa zakia ni mama mkwe, sasa unaruka ruka nini?? Wewe ulichojadili ni kuleta uongo kuwa Zakia ni mkwe, sijaona wapi umejadili kingine. Ingekua jambo la hekima kama ungeweza kusema ukweli uliodanganya, au kuthibitisha madai yako. It is that simple!

Inawezekana siyo kweli kwa mila zetu huwezi kumpa mkweo bega...au hapa alikuwa hajaoa maana huyo jamaa kushoto sasa hivi mvi kuliko EL

jk+2.JPG
 
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,

THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Wabunge watatu (3) kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kama ilivyorekebishwa na kupewa mamlaka ya kuteua Wabunge 10.

Wabunge walioteuliwa ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa na Ndugu Zakia Hamdan Meghji.

Rais atateua wengine waliosalia siku zijazo.

Rais Kikwete ameshawasilisha majina ya wateule hao kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda (Mb) kwa ajili ya hatua zipasazo.

MWISHO
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dodoma
17 Novemba, 2010

ivi hii directorate sijui takataka gani ya ikulu, hii kuchanganya kiswahili na kiingereza ndo nn?? juu kiingereza chini kiswahili kwani hawawezi weka kiswahili koote??au ndo sheria??ovyoooo!!!!
 
ivi hii directorate sijui takataka gani ya ikulu, hii kuchanganya kiswahili na kiingereza ndo nn?? juu kiingereza chini kiswahili kwani hawawezi weka kiswahili koote??au ndo sheria??ovyoooo!!!!

Halafu barua ilikuwa ina mwadress nani? Umma au ofisi ya RAIS?Hata kuandika barua tumeshasahau jamani?
 
Inawezekana siyo kweli kwa mila zetu huwezi kumpa mkweo bega...au hapa alikuwa hajaoa maana huyo jamaa kushoto sasa hivi mvi kuliko EL

jk+2.JPG

Safari, najua kwa mila zetu mtu mzima kukubali makosa inakua kazi kidogo. Tuachie hapo!! Ahsante kwa picha
 
Prof Makame Mbarawa, Associate Professor at the Department of Mechanical Engineering, Faculty of Engineering and the Built Environment, recently returned to home soil after spending five months on sabbatical leave at the Combustion and Laser Diagnostic Laboratory of the Seoul National University in Korea. In the course of his visit to Korea, he also spent time working at the Combustion Laboratory of the Donkook University, also in Seoul.

Prof Mbarawa’s main focus was to examine the effects of various gaseous additives on soot formation in laminar diffusion flames, using a laser light scattering/extinction technique. During his visit, he also read three papers at various international conferences.

Prof Mbarawa said he would like to use the knowledge he gained during the trip and compare it to the current teaching approaches in the Department, and identify and apply best practices. He added that he would also apply the quality of good supervision principles that he observed on postgraduate students.

The Seoul University’s Mechanical and Aerospace Department comprises 1 300 students, 600 of whom are involved in postgraduate studies.

He explained that the research group he worked with had consisted of one post- doctorate, six doctorate and five master’s students. The group met every week for two hours to discuss problems, find solutions and give feedback on the previous meeting’s problems. This “buddy” approach between the students made a lasting impression on him, Prof Mbarawa added.

“I was amazed by the Korean people’s dedication, culture and way of work. A typical workday during the week starts between 09:00 and 10:00 and lasts until 22:00. On Saturdays, the workday is up to 14:00.

He admitted that it was tricky to become accustomed to the chopsticks and highly spiced Korean dishes, but once he had adapted, he even enjoyed kimchi, a traditional Korean dish of fermented vegetables (mainly cabbage) seasoned with chili peppers and salt.
:A S cry: so, tumtarajie kuwa waziri wa sayansi teknolojia na elimu ya juu??
 
Mkuu tazama list hii
1. Dkt Mwakyembe
2. Prof. Kapuya
3. Prof. Mwandosya
4. Prof. Maghembe
5. Prof. Msolla
5. Dkt. Burian
6. Dkt. Shein
7. Dkt Bilal
8. Prof. Lipumba
9. Dkt. Slaa
10. Prof. Mwakyusa
11. Prof. Mwalyosi
12. Prof. Tibaijuka
13. Dkt. Ishengoma
14. Dkt. Migiro
15. Dkt. Kawambwa
16. Dkt. Magufuli
17. Dkt. Mwinyi
18. Dkt. Wanyancha
19. Dkt. Lucy Nkya
20. Dkt. Chami
.........
.........
.........

HAWA BWANA WANAKIMBIA NJAA HUKO VYUONI WALIKOKUWA WANAFUNDISHA AU WANAKOSTAHILI KWENDA KUFUNDISHA KASORO WA 9. HUYU NI MTUMISHI WA KWELI WA WANANCHI
umesahau wengine

Dkt JK
Dkt Mkapa
Nk
 
- Well, kwa kweli kwenye siasa ni lazima ku-comment kwa chochote kinachotokea hasa wakati huu wa mwisho wa uchaguzi na hasa uchaguzi wa mwaka huu,

- However: my take ni kwamba huu uteuzi ni non-effect kwa taifa kwa sababu kwa wale mnaojua vizuri functions za wabunge na effect zao bungeni, Wabunge wa Viti Maalum na wabunge 10 wa kuteliwa na Rais huwa hawana nguvu kabisaa na hata Mawaziri huwa hawawasikilizi kabisaa.

- Otherwise, Mh. Nahodha akiwa Visiwani hakuharibu na amekua royal asiye na makundi, pia ni mchapa kazi kwa hiyo hapa naona akipewa u-Waziri wa Muungano. Mama Meghji, ameshiriki sana kwenye kampeni za majuzi na ni mtu wa karibu sana na "Kigogo" mmoja na yeye namuona akirudi Cabinet, huyo mwingine namuona akiwa mbunge tu!

- Ninaamini ni uteuzi wa kisiasa za Muungano zaidi kuliko 2015, ingawa kama Mama Meghji atarudi tena Cabinet, baada ya kuondoka kwa kashfa italeta maswali valid ya commitment ya uongozi wa hiii awamu kwa wananchi, hasa ukiheshimu matokeo ya uchaguzi ulioisha, siamini kwamba CCM watafanya makosa hayo, maana itakua ni kuanza kujichimbia mapema kaburi la 2015.

- CCM imefika mahali sasa ni lazima tuambiane ukweli tena bila kuogopana wala kuoneana haya hizi tabia za kuwazungusha viongozi wale wale na hasa walioharibu tayari na huku tukiacha vijana wengi waliochaguliwa majuzi tena wengi wao ni Ma-Doctors wa kweli, itakatisha tamaa sana, maana comes 2015 hawa vijana wataishia kuingia Upinzani kwa hili ninasema hivi iwapo tu huyu Mama atapewa tena U-Waziri, ni matumaini yangu kuwa Mwenyekiti wa CCM taifa ataheshimu matokeo ya uchaguzi wa majuzi na kumuacha huyu mama bungeni tu, au ikibidi kumpa nafasi hukooo kwenye mambo ya Muungano tu!

- Wananchi tumechoshwa na hawa viongozi walioharibu tayari, sasa wapewe wengine wapya, maana wapo wengi sana!



William.

William, nimekusoma. Lakini naomba uwe mkweli katika mjadala. Sio kweli Zakia aliondoka kwa kashfa, kama ulivyoweka hapo juu. Jaribu kuwa mkweli....wewe ni CCM kama sikosei. Wewe uko kundi gani??? Kwanini chama chenu kinakosa nguvu sasa ? Je ni uchu wa madaraka sababu moja wapo? Ni uongozi mmbovu wa katibu na mwenyekiti wake?
 
Wewe na wenzako ndio mliosema kuwa zakia ni mama mkwe, sasa unaruka ruka nini?? Wewe ulichojadili ni kuleta uongo kuwa Zakia ni mkwe, sijaona wapi umejadili kingine. Ingekua jambo la hekima kama ungeweza kusema ukweli uliodanganya, au kuthibitisha madai yako. It is that simple!
:nono: Kwani kuna siri, nani hajui? kamwulize Mama Meghji au JK atakueleza. Is is such a shame
 
Back
Top Bottom