Pasco,
..kwani EL na JK wamekosana?
..nadhani JK is doing all that he can kijinusuru yeye na hawa maswahiba zake.
JokaKuu, JK na EL hawajakosana, na wala hawajakutana barabarani hivyo ni wale wale they are one and only, tofauti yao ni sisi tunaowatazama, umdhanie ndiye, siye!, na umdhaniye siye, ndiye!. Kuna mmoja kati yao anayeonekana mchafu, kumbe ndiye msafi, ila uchafu ni kweli ameubeka ili mwenzake aonekane msafi!
Kwa wenye kumbukumbu ya 2005, JK na EL walichgukua fomu pamoja na kuzisainisha pamoja, walikodi ndege moja kwenda kuzirudisha fomu zao kwa pamoja kule Dodoma, na baada ya Mkapa kupitishwa, walifanya press conference ya pamoja na JK akalalamikia kupigwa zengwe!.
Ben baada ya kushinda, akashauriwa na sytem enzi za Abson, ambao ndio hao hao kina EL na RA, kuwa ni lazima awatumie kwenye cabinet yake, ili kuwaconsole wafuasi wao, kama walivyompa umakamo wa rais, Dr. Bilal, lengo ni kuwapooza tuu wafuasi wake kule Zanzibar ili wasipige kura ya chuki dhidi ya Shein ili kuiadhibu CCM.
Kwa vile hawa ni mafahali wawili, mara tuu baada ya kuingia cabinet, wakaamua wakiendelea kupigana, ziumiazo ni nyika, hivyo wakatengeneza mtandao wa "the winning coalition" kujiandaa kwa 2005 na kuamua iwe isiwe, lazima mmoja kati yao ateuliwe. Yeyete aliyeonekana anaweza kuwa kikwazo, alishughulikiwa ipasavyo akiwemo Magufuli, na Mwandosya, wenye kumbukumbu mtakumbuka makambora ya scandali baada ya scandali za dhidi yao zilivurumishwa.
EL na JK walijiwekea their own secret accord, (Hawakukutana barabarani), wakakubaliana JK ndie achukue fomu na EL asichukue, kwa ahadi kuwa EL atakuwa PM na baada ya zamu ya JK, EL ndie angefuatia automatically!.
CCM ilipobakiza wagombea watatu, JK , Dr. Salim na Prof. Mwandosya, zengwe lililovurumishwa kwa Dr. Salim mnalijua, mpika zengwe mnamjua na shukrani kwa wapakuaji wa hilo zengwe mnajua walivyozawadiwa!. Mtu wa ajabu kabisa kwenye CCM ni Mkapa, anajua wazi kabisa ukweli kuhusu Dr. Salim na uwezo wa JK ukimlinganisha na Mwandosya, lakini Mwenyekiti wa CCM, kama zuzu vile ( naamini teknolojia ya Mlingotini ilitumika!), alijiunga na kambi ya JK , tena sio tuu kwa mwenyekiti ku take side, bali kuwa kuwadi wa JK kwa kumpigia kampeni za wazi kuwaambia wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM, wamchague mtu aliyetoka mbali na CCM!. Kitendo cha Prof. Mwandosya kuonekana ni mtu wa principles na Mkapa aliyajua madudu yake aliyofanya pale Ikulu, ilionekana Prof. anaweza kumtundika msalabani, bora zimwi likujualo, wakamchinjia Prof. Baharini na JK akapeta na ndio ikatoka ni mpaka magogoni!.
Kweli JK aliitimiza ahadi, EL Waziri Mkuu!.
Dili la Richmond lilivyokuja, ni dili la mzee mzima mwenyewe!, hata vile vimemo vya EL yeye alikuwa ni mjumbe tuu au tarishi wa mwenye mali! dili Richmond lilipobackfire, ndipo RA na EL wakatumia Dowans kumnusuru muzeiye! Sitta anajua, na kwa vile na yeye 2015 alijipanga kuingiza karata yake, kupitia vijana wa TISS, wakafanya utambuzi yakinifu na kupata ushahidi wa vimemo vya EL. Sitta akamtumia Mwakyembe kumtundika msalabani EL na kumsulubisha moja kwa moja bila kumuuliza chochote!.
Kwa vile l;engo lilikuwa ni kumsulubu EL, wakati wote wa uchunguzi, EL na RA hawakuwa na wasiwasi wowote, kwa vile walijiaminisha, maadam game ni la muzeiye, basi muzeiye akalipumch na kuzuia lisifumke, ndio maana kina Hosea walikuwa na viburi vya ajabu!. Kabla ripoti haijatoka, JK alishaiona, EL alishaiona na aliyeipeleka kote huko ni SS, JK alitoa go ahead EL akaangwe ili CCM inusurike, vingenevyo SS angeliomgoza bunge kwenye impeachment!. Hivyo EL akatolewa kafara, muzeiye akapona, CCM ikapona na hapo sasa ndipo vita mpya ikaanza!.
The King Maker (RA), akajiapiza, lazima atawashughulikia vimbembele wote kwenye kamati ya Mwakiembe wakianzia na SS, na kusema ukweli, faranga ilitembezwa, waliosalimika kama SS ameponea tundu la Sindano la huruma ya JK na walijiundia safe heaven ya CCJ ili watimkia kule, milango ikafungwa, SS akapiga magoti CCM ndia salama yake, hata huo uspika akapigwa chini, Selelii kilichomkuta mnakijua ilimradi ni piga ua!.
Baada ya JK kuridi 2010, akamshukuru Mwakyembe kwa kumnusuru, na asanye SS kwa kuto mu impeach, akijiaminisha EL ataendelea kunyamaza, na infact EL aliamua kunyamaza kimya kabisa!. Kilichomtibua ni vuvuzela la kile kitoto kijinga jinga ambacho kinapuliza vuvuzela la ufisadi as if hakijua nani ndio mafisadi halisi ndani ya CCM!, nawahakikishia mwisho wake ni uchaguzi wa CCM mwakani!.
Sasa kinachoendelea, nadhani RO ni implant ya RA pale TISS hivyo they are not sure EL atanyamaza mpaka lini!, hivyo the only way ni au wamshughulikie au wampe anachotaka ambacho ni urais 2015!. JK ni powerless with nothing to do maana EL ndio kashika mpini mtake msitake, mkubali msikubali
El in this game, "this (EL) is the name of the game!.