KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,147
Hata hii inaweza kuwa club,Wako wapi kina Es na mwanakijiji,mbona pamepooza hapa club..ni sawa sawa club siku asipokuwepo jenerali na balozi ami au chenge inavokua doro ati,kuna watu wameumbwa hivyo uwepo wao unakua ni a million dollar!
Hauna haja ya kujisikia mpweke. Cha kufanya uheshimike, lipa ada yao ya mwaka, ambayo ni kubwa sana, kitu kama laki tano au milioni moja. Pili, jitengenezee mazingira upate cheo serikalini au kwenye taasisi kubwa au nyeti nchini, na kama hilo haliwezekani, ongeza juhudi uwe mjasiriamali ili uwe na uwezo mzuri wa fedha utakaokupa heshima mbele ya wanachama wenzako. Ukifanikiwa kufanya hayo, taratibu utaanza kualikwa kwenye hafla zao za usiku wa manane huko kwenye nyumba za kukodi maeneo ya Mbezi, na kusubur Toyota Hiace iwaletee mabinti wa boarding sekondari, lakini sana sana mabinti wa vyuo vyetu vikuu, kisha muwachezee watoto wa watu, huku mkiwa mnatembea uchi wa mnyama na vilevi vyenu mikononi, mkibadilishana binti kwa binti na kusisitiza sera ya uwazi, sio sera ya wivu, huku pia mkiwalazimisha watoto wa watu wafanye ngono wao kwa wao nyie mkipiga makofi na miluzi, mkiongozwa na 'prince to be', Fred Edward Ngoyai Lowassa na kundi lake, kisha kuwarudisha watoto wa watu kabla ya jua kuchomoza, kwa hiace mliyokodi, wakiwa wamelewa, na wachovu, bila ya senti, kwa ahadi kwamba mtawarudia tena, kwani nyinyi ndio wenye nchi.
Ndio maana nimeweka msisitizo wa neno "TETESI."
wala usiogope hizi ni propaganda tu hamna lolote,mleta mada alimuandalia mazingira jamaa aje atoe habari,ni strategy lakini ili kuielewa inabidi utumie akili kidogo...ila huyu ni mkali kuliko kina wale wawili watatu tuliowazoea kuichezesha jf ngoma ya lowassa,huyu amejipanga na sidhani kama alipanga peke yake,it seems ni jopo lililokaa haswa,unajua hii pamoja na kuwa na watu elfu sita lakini inaogopwa sana na bwana mkubwa asiwaambie mtu,zipo jitihada za makusudi zimekuwa zikisukwa bila mafanikio kujaribu kubadili muelekeo humu ndani before uchaguzi mkuu wa ccm,hili ninalijua na nina uhakika nalo na aliyekabidhiwa jukumu hilo namfahamu sawasawa,ni mwanafunzi wa zamani wa ununio zamani akiijiita mbongo hapa lakini ukimtazama haonekani kuwa hivyo!
uliwezaje kununua kinywaji wakati pale bill inatakiwa kwenda kwa member aliye kuleta? au siku hizi wamelegeza masharti? kwamba yeyote tu anaweza kwenda? si patajaa kama swazi na kuharibu usalama wa nji!Siku ya kwanza nilipelekwa na member, siku ya pili nikajiendea mwenyewe, wanakuona kama sio mwenzao, you don't belong!. Kwa mfano wewe kama ni mtu wa kujichanganya hivi vibaa vya uswazi, siku ukizikamata, hebu nenda kanywee ile bar pale Kempinski, utawakuta wabongo of a certain class, hata ukijikalia counter ili ujichanganye, utaishia kujistukia hauchanganyiki!. Ile Tanzania Nyerere aliyoiacha ya Classless society haipo tena!, sasa ni silent classes za wenye nacho na wasio nacho!.
Mtoahabari.
Nimepigwa na Butwaa!! "Nambie unafurahisha Baraza" Yani yote haya mada ni hii ya Mtandao Hatari??
Kijana anatuletea za Balasconi! Mwambieni hapa sio Utaliani, Kisha amwangalie Nzi atapata somo "Kama yeye ajua wa mbele, wenzie wajua wa nyuma." Tena kazi mbaya si mchezo mwema.....................
Mkuu.
Tetesi tafsiri yake si Lisemwalo lipo?
ama uzi huu si wa mchezo, embu tupeni bac huo ujio wa chama kipya, kitaitwaje? kadri uzi unavyoendelea na kama mengi yasemwayo ni kweli, si ccm, wala cuf ama chadema wanaofaa kuongoza hili taifa, moyo unauma sana nikifikiria wakina sie tunaokubari wanayotuambia na kuamini wanavyotuongoza, kumbe yote si kweli wanayapanga na kucheza na akili zetu. kuna watu wamepoteza maisha kwenye chaguzi mbalimbali kwa ajili ya mapenzi ya vyama vyao, sie twachinjana kumbe wao wanapangiana. mtoahabari yote umesema lakini hilo la vyama vya upinzani navyo mpaka kumegewa pesa na hao tunaowaita mafisida, aisee nimechoka na kuchoka, kweli usilolijuwa dah
Mkuu T R,
Mimi nilikuwa na hisia kuwa Mtoa Mada ( Hutaki Unaacha) na Mtoa habari ni Mtu na Kivuli chake!! Nadhani unanielewa? Angalia huu mjadala ulivyopoteza Afya. Isipokuwa siamini kuwa unahusiana na uchaguzi wa CCM mwakani.
Jamaa yuko maandishi yake yako very technical,ukiingia kichwa kichwa utacheza ngoma ya lowassa bila kujielewa,si unasikia kuna watu wanakwambia kesho maofisini na kwenye barza za kahawa wataipata?hapo lengo la "mleta mada" hutaki unaacha litakua limetimia au halijatimia kwa watz wa kawaida ambao wanapenda sana kuhadithiwa ili wakahadithie kama walikuwepo mahali husika?si unajua wabongo wanavyopenda kuonekana ni watu wa usalama wa taifa kwa kuhadithia story za "hatari" huko uswahilini kwetu?tuwe makini.
Leo utaambiwa Rashid othman kwa kuwa ana undugu wa damu na jaji wetu mkuu na ro inasemekana alichaguliwa na Lowassa na rostam nae pia kawekwa na hao japo hawakuwako madarakani jaji mkuu akichaguliwa,lakini wabongo kwa kupenda stori wanakubali bila kuchallenge,leo utaambiwa lowassa na rostam wana miguvu mpaka ya kutishia watu wasizungumze kwenye vijiwe lakini ukiuliza jamani eeeh hawa watu wakubwa kuliko chama na serikali walioshika kila sehemu nyeti si waliapa jimbo la igunga litaenda upinzani sasa imekuwaje bila msaada plus hujuma zao ccm imeshinda igunga?hawakujibu utaambiwa aidha hutaki unaacha au tulikua tunatoa taarifa tu,basi ili mradi sarakasi za maneno zisizoisha lakini wabongo wa wengi wa humu bado wako usingizini,hawahoji hoja za wazi kama hizi zinazohitaji ufafanuzi zaidi,wanataka stori zaidi za kwenda kutishia watu mitaani!
uliwezaje kununua kinywaji wakati pale bill inatakiwa kwenda kwa member aliye kuleta? au siku hizi wamelegeza masharti? kwamba yeyote tu anaweza kwenda? si patajaa kama swazi na kuharibu usalama wa nji!
The Romantic,taarifa zako zimejaa vitisho unajaribu ku create fear ili watu wasimjadili lowassa kwa kuwaogopa kina davis mosha,we kama unawaogopa shauri yako kaka,lakini kiukweli hawana lolote wale ni misifa jazz band,huyo lowassa mwenyewe pengine wanazisikia tu habari zake,wadau niwaambie kitu kwanza hakuna mtu muoga kama lowassa,mnajua kwanini siku hizi ananywea whisky zake nyumbani wakati alikua member mwenzetu mzuri tu kwenye kikao chetu cha jioni?anadai eti ana maadui wengi nae anaogopa kuuawawa kama huyu jamaa anaetuletea taarifa anavyotaka na sisi tuogope tuanze kunywea vyumbani kama jamaa!nyie endeleeni kusikiliza hivyo vitisho visivyokuwepo,taarifa za huyu jamaa zinataka kuwanyang'anya uhuru wenu wazee wenu walioudai kutoka kwa muingereza kwa niaba yenu,mtoa taarifa waambie waliokupa hizi taarifa wanadhani zinaweza kumtisha mtu kama jenerali ulimwengu,ami mpungwe,kleist sykes,wendo mwapachu n.k.,muulize lowassa,kwanini siku hizi haji club?mbona chenge anakuja?
EL na RA kuikosa igunga katika uchaguzi mkuu mdogo, na badala yake JK na watu wake kuibuka kidedea...,JK na watu wake kushindwa kwenye uchaguzi wa wabunge wa viti maalum UVCCM, na badala yake EL na RA kubeba viti vyote, yote ni sehemu ya mapambano. Kuelezwa jinsi gani EL anafanya kazi mitaani sio kutishwa, bali kupewa tahadhari. Mtu anaye threat ni yule anaye inspire fear or dread kwa wenzake kuhusu jambo fulani, lengo likiwa kuwafanya wafuate maelekezo yake ili wasipate madhara. Mtu anaye toa tahadhari, ni yule anaye elezea mwenzake/wenzake juu ya hatari fulani iliyopo, ili wenzake hao waifahamu na hivyo kuikwepa. Ninachofanya sio kuwaeleza wenzangu wafuate maelekezo yangu na waache matendo yao kulipigania taifa lao, bali kuwaeleza wenzangu juu ya hatari iliyopo katika mapambano yanayoendelea kulikomboa taifa lao, ili waifahamu hatari hiyo, na hivyo waikwepe, na kujizatiti zaidi, bila ya kuacha mapambano. Vinginevyo mpaka baina na threat na caution ni mwembamba sana mithili ya uzi wa kushonea, hivyo kupelekea taarifa zangu kuonekana kama vile zinaangukia pande zote. Lakini wa kuelewa wanaelewa.
Mtoahabari,
Nimekuelewa vizuri hapo unaposema wewe ni mtoa taarifa tu. Kwani taarifa si lazima iwe sahihi ama la. Ni mpaka hapo hapo itakapotokea ndio itakuwa sahihi. Kama nilivyosema huko nyuma ni jukumu letu wana JF kufanya our own independent assessment ili kabla ya kufikia kwenye final solution. "mtaohabari" katimiza wajibu wake kwa sisi watanzania tuliosoma. Nasi basi tutumie akili zetu (za kuzaliwa + darasani/vyuoni) tufikie mwisho. Na ndio hapo kila mmoja wetu ajitokeze kuplay his/her part.
Ushauri mzuri wa wahenga wetu naona upo valid kabisa katika hili "ILI KUMUUA NYOKA LAZIMA UENDE KICHWANI". Hivi sasa namkumbuka sana marehemu E. MZENA, yule kamanda alikuwa jasiri na hana uoga, kama angalikuwapo huyu EL angeshakuwa history na wafuasi wake waliobakia inakuwa rahisi kuwadhibiti. Unfortunately, operations specialists waliopo chini ya RO ni gutless and cowards! Mmebakia ma-Analyst mnaona upuuzi wote unaoendelea bila kujua la kufanya. Kuna kitu wenzetu wanaita true sons of the country they are sucrificed for the benefits of the future generations. Sijui sie kitu kama tunacho mtaohabari?
Natamani uniruhusu nianze kukunukuu andishi moja hadi lingine katika yale yanayoleta shaka ya vitisho zaidi na yanayomjenga jamaa na kuonyesha kujaribu kuonyesha kwamba kuchagua kupambana nae ama kumdhibiti kama nguvu ya umma ni kuchagua kifo na kwamba hakuna njia ya kumzuia?japo sipendi sana tuiteke ionekana ni mpambano wa mimi na wewe bali kila mwenye lake aliweke