Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Ogah, Nyerere alikuwa mjamaa kwa imani, maneno na matendo!. Hawa waliopo ni wajamaa kwa maneno tuu lakini matendo ni tofauti!. Ni katika utofauti huo Lowasa ndie mwenye afadhali!. Kama Nyerere angefufuka leo na kuwashuhudia waliotangulia wale wafanya biashara tuliowapangisha Ikulu na hawa waliopo wanavyo najishi mahali patakatifu pale na kupageiza ni pango la walanguzi!. Angemshika mkono na kumsafisha japo mwizi lakini mambo yanakwenda kuliko mijizi mingine inakwiba na hakuna kinachoendelea!

Mwizi ni mwizi tu, hakuna mwizi mwenye afadhali. Huwezi kusema mwizi X ana afadhali kwa kuwa eti akienda kuiba hauwi victim.
 
Nitabaki kuwa Tomaso kwenye hilo kwa kuwa naona kampeni za kuleta Chaguo Jipya la Mungu inarudi kiaina.

Wengine wanasema jamaa ana UTHUBUTU na sasa naona anaitwa MKOMBOZI.

Hata JK tuliambiwa ni mtu wa watu, hana makuu, kimbilio la wanyonge, angeboresha maisha ya walalahoi na mambo mengine kibao.

Masikini ndio wanazidi kuwa choka mbaya. Kila kukicha unakuta ni afadhali ya jana.

Nakumbushia tu. Huyu si ndiye aliyetaka kutuletea dili ya mvua ya Thailand. Bahati nzuri fisadi mwezake huko Thailand akapinduliwa kabla ya kukamilisha dili lao.
 
Nakumbushia tu. Huyu si ndiye aliyetaka kutuletea dili ya mvua ya Thailand. Bahati nzuri fisadi mwezake huko Thailand akapinduliwa kabla ya kukamilisha dili lao.
Mkuu ile report ya jamaa mmoja aliyekuwa akijiita Kasori au Kisori, katibu mkuu serikali ya Nyerere aliishia wapi nakumbuka naye hakurudi kuimalizia. Kwa kukumbusha tu huyu jamaa aliandika jinsi Nyerere alivyomtoa EL ktk wagombea urais, kisha EL akamtuma nadhani Kawawa kwenda Butiama kumwambia Nyerere alisafishe jina lake ili apate kugombea Ubunge... Ile habari ilikuwa nzito sana lakini jamaa akaingia mitini...

2. Hivi wale wote waliokuwa Tume ya Mwakyembe wapo bado hai au madarakani, nakumbuika Seleli alipigwa chini wale wengine Je?..
 
Mtandao

Ninachozungumzia hapa ni kundi kubwa na hatari linaloaminika kuongozwa na Edward, Rostam, Othman, Apson, Karume na Shein na Mkapa. Ninakufahamu vizuri sana na ungekuwa uwezo wako, hawa wote ungeweza kufanya uwezalo ili kumweka madarakani mtu unayemtaka kwa maana ya Asha au Nahodha. Huu ni mtandao unaofanya kazi kwa umakini wa hali ya juu sana. Ukitaka kuamini, jiulize swali la kipuuzi sana kuwa kwanini kila plans unazofanya (zisizo na faida) kwa kundi hili zote zimefail?

1. Shein ni nani?

Nataka nikukumbushe ''issue'' ya Omar Juma. Huyu alikuwa threat kubwa kwa kundi lenu kwa ajili ya 2005. Mtandao wake ukibebwa na Mkapa ulikuwa ni hatari sana. The only way ilikuwa ni ''kumwondoa'' na hilo liliwezekana.
Siku nikiwa na muda nitaeleza mchezo wote ulivyofanyika. Wakati jina limeletwa tukiwa hotel moja maarufu hapa Dar, nakumbuka hukuweza kumfahamu Shein wala kulitamka jina lake vizuri. Ulikosea mara tatu kulitamka. Tukacheka wote. Hatimaye Shein akawa makamu wa rais.

Baada ya wenzako kukuweka madarakani (mgombea ndani ya CCM), kosa ambalo Shein hataweza kukusamehe katika maisha yake (Mimi sio Mungu, kwani anaweza kukusamehe vilevile) ni pale ulipo-attempt kumfanya Zakhia kuwa makamu wa rais. Asingekuwa Edward, Rostam, Mkapa na Karume, leo hii Shein angekuwa mwenyekiti wa TPDC au TANAPA
Kwenye Hayo maandishi hapo juu kabla ya kusema "sitaki na kuacha" ama "nataka na kuyameza" kidogo yanahitaji ufafanuzi maana kuna contradiction ya hali ya juu,nilitoa muda jamaa arudi lakini hajafanya hivyo nimaeamua kukichambua kilichopo katika maandishi yake komoja baada ya kingine:

Tunaaminishwa kwamba marehemu Dr.Omari ali juma alikua threat kwa genge la jakaya,lowassa na rostam,sitta na wengine kwa kuwa mtandao "wake" (dr.omari)ulioongozwa na mzee mkapa ulikua "hatari" sana,mpaka hapa tunaona kwamba kuna makundi mawili "hatari" kwa jinsi alivyoonyesha mleta thread,yani kundi la kina jk,lowassa,rostam na sitta na kundi la mkapa,dr omari na apson!Lakini hapohapo jamaa anatumbie tena APSON,MKAPA,LOWASSA,ROSTAM wako kwenye kundi moja dhidi ya kikwete!hili linahitaji ufafanuzi zaidi..tujue kwanza kundi lililompoteza dr omari ni lipi kati ya hayo mawili,hii itatusaida kwenda mbele zaidi na kujua kundi hatari la mkapa lililokua na dola liliishia wapi baada ya dr omari "kupotea"

Jambo lingine ni suala la jk baada ya kupitishwa kugombea jamaa anatueleza alitaka kumuweka zakia kuwa mgombea mwenza wake lakini mtandao ukamgomea,hapa sijaelewa ni mtandao upi kati ya wa akina kikwete,lowassa na rostam ama wa mkapa,maana ni wazi mkapa hakua kwenye mtandao wa kina kikwete lowassa rostam na sitta,ndio maana hata kwenye issue ya kuteaua waziri mkuu jakaya alihitilafiana na "wazee" kina mkapa ambao hawakumtaka lowassa awe pm,hili nina (ushahidi nalo)mpaka jakaya alipopandisha mashetani ya kikwere na kuwaeleza kinaga ubaga kama hawezi tena kukubali wamchagulia waziri mkuu na yeye anataka kufanya kazi na swahiba wake lowassa,ikumbukwe hapo mwanzo "wazee" walishamchagulia watu kadhaa nyeti akiwemo mwanasheria mkuu!

otherwise tuache propaganda watz wa sasa wanakumbu kumbu nzuri ya kilichotokea nyakati za mwanzo za utawala wa kikwete na mtandao wake pamoja na wazee wa nchi!japo kutokana na ushabiki wapo baadhi watajifanya wamesahau na kukubali ulaghai wa kwamba mkapa,rostam na lowassa walikua mtandao mmoja!ingekua hivyo mkapa asingemkataa lowassa kuwa waziri mkuu mpaka jk alipopandisha mashetani ya kwao ndio wakanywea!na wala kina rostam hawakutaka shein awe mgombea mwenza,walika na mtu wao kutoka unguja na sio pemba!
 
There you are!......na ENL alipojua hayo kupitia vijana wake alifanya nini akiwa kama kiongozi...........mbona huendelezi/humalizii?......wee unafikiri Nyerere (RIP) alikuwa zuzu?..........

usicheze na shekeli hata Yuda alimuuza Yesu, na usicheze kukaribishwa british legion, ndio maana unasikia jamaa alikwenda pale bila support ya member , akaona afadhali aishie uswazi!
sasa hivi naona kampeni za waandishi kununuliwa ahead of 2015 zinaongezeka
 
Mkuu ile report ya jamaa mmoja aliyekuwa akijiita Kasori au Kisori, katibu mkuu serikali ya Nyerere aliishia wapi nakumbuka naye hakurudi kuimalizia. Kwa kukumbusha tu huyu jamaa aliandika jinsi Nyerere alivyomtoa EL ktk wagombea urais, kisha EL akamtuma nadhani Kawawa kwenda Butiama kumwambia Nyerere alisafishe jina lake ili apate kugombea Ubunge... Ile habari ilikuwa nzito sana lakini jamaa akaingia mitini...

2. Hivi wale wote waliokuwa Tume ya Mwakyembe wapo bado hai au madarakani, nakumbuika Seleli alipigwa chini wale wengine Je?..

Mkandara,

Waraka wa Mzee Kasori kwenda kwa Lowassa uko hapa hapa JF, juzi juzi tena naona ulikuwa kwenye page ya juu kabisa. Sina hakika kama Hamis Kasori aliingia mitini, nadhani ujumbe wake ulikuwa umekamilika. Yeye kwa mtazamo wake alichokoza na alikuwa akisubiri tu Lowassa ajiweke kwenye kilengesho. Ila kwa kuwa Lowassa ni mjanja wa kufunika uvundo, alikaa kimya bila kujibu na hivyo ule waraka ukawa umepotezewa kiaina.

Wajumbe wa Kamati Teule ya Dr. Mwakyembe wote bado wako hai.
Dr. Mwakyembe ndio huyo ambaye anaendelea kuugua huku akiwa Naibu Waziri wa ujenzi
Eng. Stella Manyanya bado ni Mbunge wa Viti Maalum na majuzi alipewa ulaji wa Ukuu wa Mkoa wa Rukwa.
Ndugu yangu Lucas Selelii ndo huyo yuko Nzega akiuguza kupigwa chini na wapiga kura wake.
Habib Mnyaa bado ni Mbunge kupitia CUF.
Herbert Mntangi bado pia yuko Bungeni.

Kwa hiyo mjumbe pekee aliyepoteza ulaji ni Lucas Selelii.
 
Kwenye Hayo maandishi hapo juu kabla ya kusema "sitaki na kuacha" ama "nataka na kuyameza" kidogo yanahitaji ufafanuzi maana kuna contradiction ya hali ya juu,nilitoa muda jamaa arudi lakini hajafanya hivyo nimaeamua kukichambua kilichopo katika maandishi yake komoja baada ya kingine:

Tunaaminishwa kwamba marehemu Dr.Omari ali juma alikua threat kwa genge la jakaya,lowassa na rostam,sitta na wengine kwa kuwa mtandao "wake" (dr.omari)ulioongozwa na mzee mkapa ulikua "hatari" sana,mpaka hapa tunaona kwamba kuna makundi mawili "hatari" kwa jinsi alivyoonyesha mleta thread,yani kundi la kina jk,lowassa,rostam na sitta na kundi la mkapa,dr omari na apson!Lakini hapohapo jamaa anatumbie tena APSON,MKAPA,LOWASSA,ROSTAM wako kwenye kundi moja dhidi ya kikwete!hili linahitaji ufafanuzi zaidi..tujue kwanza kundi lililompoteza dr omari ni lipi kati ya hayo mawili,hii itatusaida kwenda mbele zaidi na kujua kundi hatari la mkapa lililokua na dola liliishia wapi baada ya dr omari "kupotea"

Jambo lingine ni suala la jk baada ya kupitishwa kugombea jamaa anatueleza alitaka kumuweka zakia kuwa mgombea mwenza wake lakini mtandao ukamgomea,hapa sijaelewa ni mtandao upi kati ya wa akina kikwete,lowassa na rostam ama wa mkapa,maana ni wazi mkapa hakua kwenye mtandao wa kina kikwete lowassa rostam na sitta,ndio maana hata kwenye issue ya kuteaua waziri mkuu jakaya alihitilafiana na "wazee" kina mkapa ambao hawakumtaka lowassa awe pm,hili nina (ushahidi nalo)mpaka jakaya alipopandisha mashetani ya kikwere na kuwaeleza kinaga ubaga kama hawezi tena kukubali wamchagulia waziri mkuu na yeye anataka kufanya kazi na swahiba wake lowassa,ikumbukwe hapo mwanzo "wazee" walishamchagulia watu kadhaa nyeti akiwemo mwanasheria mkuu!

otherwise tuache propaganda watz wa sasa wanakumbu kumbu nzuri ya kilichotokea nyakati za mwanzo za utawala wa kikwete na mtandao wake pamoja na wazee wa nchi!japo kutokana na ushabiki wapo baadhi watajifanya wamesahau na kukubali ulaghai wa kwamba mkapa,rostam na lowassa walikua mtandao mmoja!ingekua hivyo mkapa asingemkataa lowassa kuwa waziri mkuu mpaka jk alipopandisha mashetani ya kwao ndio wakanywea!na wala kina rostam hawakutaka shein awe mgombea mwenza,walika na mtu wao kutoka unguja na sio pemba!

Mkuu The Romantic,

Mimi nilivyomwelewa mtoa mada ni kwamba Dr. Omar A. Juma alikuwa ni threat kwa mtandao kwa sababu kubwa mbili, alikuwa ni clean [hana uchafu wa kumchafua nao] na kwa kuwa alikuwa ni Makamu wa Rais na anatokea upande wa pili wa Muungano then it was easy kujenga hoja ya kuwa mteule wa kugombea nafasi ya urais. Moja, kwa kutumia u-Zanzibari [kwamba baada ya Mkapa wa bara then angefuata wa Visiwani]. Pia hakuwa na tuhuma zozote chafu. So, the best way ya ku-deal naye ilikuwa ni kumwondoa njiani [if at all kifo chake kilitokana na hilo].

Hapo inabidi ukumbuke kwamba wana Mtandao walikuwa wana-deal na yeyote yule aliyekuwa anaonekana kwamba anaweza kuwa kizuwizi kwao. Ndio maana wale ambao walikuwa na "tuhuma" za ukweli au za majungu, tayari walishaandaliwa njia ya kuwamaliza kiaina.

JK, Lowassa, RA, Sitta, Membe na wengineo wengi tu walikuwa kundi moja la mtandao. Ingawa baada ya uchaguzi ndipo yalipozaliwa makundi mawili, mtandao original na mtandao matumaini [wale ambao hawakuambua kitu cha maana pamoja na ku-toil sana kwenye kampeni za mtandao]. Hao akina Apson walikuwa recruited along the way. Mkapa alikuja kuingizwa kwenye kundi la mtandao dakika za mwisho. Mkapa kwa kujua kwamba hilo lilikuwa ni kundi la opportunists, hakuwa na uhakika wa usalama wake wala mali zake na ndipo mtandao walipolambishwa EPA ambayo inawahenyesha mpaka leo na ndio maana akina Kikwete na Pinda wanaendelea kumtetea Mkapa mpaka leo hii kwamba mwacheni apumzike.

Zakhia Meghji alikuwa ni mwana mtandao. So, waliomgomea hawawezi kuwa wana mtandao, bali watakuwa ni wazee wa CCM kwenye Kamati Kuu. Ubaya wa kupendekeza Mgombea Mwenza ni kwamba mgombea Urais hupendekeza jina na ndipo wazee walafi wa CCM hujadili hilo pendekezo na kukubaliana na ndipo huenda kutangazwa kwenye Mkutano Mkuu wa Chama. Kwa hiyo kama ni kugoma, watakuwa waligoma akina Mkapa na wengineo walio kwenye CC. Wakati huo mgombea mteule huwa hana final say na inawezekana CC inaweza kuibuka na jina tofauti kabisa na lile lililopendekezwa na mgombea mteule.

Kwenye swala la Waziri Mkuu, CC wala Rais aliyetangulia huwa hawana nafasi kwa kuwa Rais mteule anakuwa na uhuru wake wa kupanga safu ya watendaji bila kukishirikisha chama chake. Ndio maana JK alikuwa na jeuri ya kuwagomea. Ni ngumu kugoma kwenye uteuzi wa mgombea mwenza kwa kuwa kila kitu kinafanywa na chama kwa kuwatumia wale "ma-think tank" wao walio kwenye CC.
 
Mkandara,

Waraka wa Mzee Kasori kwenda kwa Lowassa uko hapa hapa JF, juzi juzi tena naona ulikuwa kwenye page ya juu kabisa. Sina hakika kama Hamis Kasori aliingia mitini, nadhani ujumbe wake ulikuwa umekamilika. Yeye kwa mtazamo wake alichokoza na alikuwa akisubiri tu Lowassa ajiweke kwenye kilengesho. Ila kwa kuwa Lowassa ni mjanja wa kufunika uvundo, alikaa kimya bila kujibu na hivyo ule waraka ukawa umepotezewa kiaina.

Wajumbe wa Kamati Teule ya Dr. Mwakyembe wote bado wako hai.
Dr. Mwakyembe ndio huyo ambaye anaendelea kuugua huku akiwa Naibu Waziri wa ujenzi
Eng. Stella Manyanya bado ni Mbunge wa Viti Maalum na majuzi alipewa ulaji wa Ukuu wa Mkoa wa Rukwa.
Ndugu yangu Lucas Selelii ndo huyo yuko Nzega akiuguza kupigwa chini na wapiga kura wake.
Habib Mnyaa bado ni Mbunge kupitia CUF.
Herbert Mntangi bado pia yuko Bungeni.

Kwa hiyo mjumbe pekee aliyepoteza ulaji ni Lucas Selelii.


Hii ni sehemu ya waraka wa mzee kasori kwenda kwa Lowassa!
Kwa mapenzi mema na nchi yetu na mwana (CCM) napenda niwape mfano hai wa Bwana Lowasa asivyo muadilifu na asivyopenda kuwajibika kichama CCM na kiserikali. Tanzania nzima mtakumbuka kuwa huyu mheshimiwa Edward Lowasa alikuwa ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais mwaka 1995 na akaenguliwa kwa hoja nzito ya kutokuwa muadilifu na marehemu Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere, kwa ukweli (wala sio tuhuma) kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa kipindi kifupi ndani ya CCM na Serikali.Muda mfupi alikuwa ni mtumishi wa CCM, muda mfupi kama Mkurugenzi wa kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha.

Mfano hai wenyewe uko hivi; tufuatane kwa kuusoma tafadhali:-
Mara baada ya kurudi Butiama, 1995, baada ya kuenguliwa kugombea nafasi ya urais, siku moja mapema asubuhi Bwana Lowasa alinipigia simu na kusema yafuatayo:

"Bwana Kasori, naomba uende kumwambia Baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, aende Monduli kusaidia kusafisha jina langu ili nisikose ubunge kutokana na yale aliyonisema Dodoma'. Nilishikilia mkono wa simu (TTCL) kwa zaidi ya nusu saa tukiwa tunazungumza na hatimaye mimi nilipata ujasiri wa kumwambia Bwana Lowasa kuwa siwezi kwenda kusema maneno hayo kwa Baba wa taifa na kwamba akitaka aje Butiama na nitamruhusu waongee ana kwa ana. Nikanyamaza na hatimaye yeye akawa wa kwanza kukata simu. Hiyo ikawa itifaki njema kwangu!

Kesho yake tena asubuhi nilipokea simu, safari hii akawa ni mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa maneno yake alisema "Bwana Kasori,jana ulizungumza na Edward Lowasa; naomba ufikishe ombi lake kwa Baba wa taifa tafadhali".

Kutokana na heshima ya Mheshimiwa Mzee Kawawa, nilikubali na nikaenda na kabla ya hapo nilimuomba Mzee Kawawa akae karibu na simu ili nimpe jibu muda si mrefu.

Nilimueleza Baba wa Taifa kuwa "Mheshimiwa Edward Lowasa kupitia kwa Mhe. Mzee Rashidi Mfaume Kawawa anaomba usaidie kusafisha jina lake kule jimboni kwake Monduli ili asikose ubunge kutokana na yale uliyomsema katika Kamati Kuu ya CCM Dodoma". Jibu la Baba wa Taifa alilonipa ni kuwa "Nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa"!

Watanzania wote, leo March19, 2008, nawaomba radhi kuwa jibu hilo kwa uzito wa maneno hayo kuwa "Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa" kweli kwa kuzingatia heshima kati ya wazee hao wawili; "Kawawa sikumwambia hivyo"! Badala yake nilimdanganya (nawaomba radhi tena watanzania) jibu nililompa Mzee Kawawa ni kuwa juma lililokuwa linafuata tungekuwa Dar es Salaam na kwamba aje Msasani aongee na Baba wa Taifa. Mhe. Kawawa alikubali.

Nikarudi kwa Baba wa taifa kusema uongo (naomba radhi tena) kuwa "Mzee Kawawa ameomba mzungumze tatizo la Lowasa tutakapofika Dar es Salaam". Baba wa taifa alikubali na akaagiza nimuombe Mhe. mzee Kawawa kuwa Lowasa na Guninita na wapambe wengine wa Lowasa wote wafike Msasani.

Siku ya siku ikafika. Tukawepo Msasani na Mhe.mzee Kawawa akaja. Lowasa hakuwepo! Sababu anazijua mwenyewe.(muulizeni maana nasema ukweli). Mkutano ulipoanza mzungumzaji wa kwanza nikawa mimi, kueleza lengo la mkutano. Mzungumzaji wa pili alikuwa Baba wa Taifa na swali la kwanza ni kuuliza Lowasa yuko wapi?.

Bila kupoteza wakati Mwalimu alisema "Rashidi , huyu Kasori ananiambai eti niende Monduli nikasafishe jina la Mhe. Lowasa eti asikose ubunge kwamba nilimchafulia Dodoma katika Kikao cha Kamati Kuu ya CCM. Kutokana na ombi lako nilimtuma akuambie usiwe mjinga kama Lowasa. Kasori alikuambia eh?"

Oneni , huko nyuma tayari nilishasema uongo kwa kutosema maneno hayo kwa Mhe. mzee Kawawa. Kweli hilo kurudiwa na Baba wa Taifa kwa Mzee Kawawa mbele yangu lilisababisha kalamu yangu kuanguka, nikatetemeka na nikatokwa na jasho jingi mbele ya hao wazee!!! Bila kutegemea na kwa mshangao mkubwa Mhe. mzee Kawawa alikubali kwa kuitikia "NDIO ALINIAMBIA". Mwalimu akacheka sana!!!! Sababu sijui hadi leo kwa nini alicheka sana.

Kwa kuendelea, Mwalimu alimwambia Mzee Kawawa kuwa "Kasori ana umri mkubwa kuliko Lowasa. Kasori alipata taabu sana kufikisha kwangu ombi la Lowasa na aliniambia kuwa jana yake alikuwa amekataa ombi la Lowasa. Sasa nasema kuwa kwa umri wangu mimi mzee, Lowasa ni mtoto wangu tena mdogo sana. Kwa heshima mliyonayo kwangu na kwa chama cha Mapinduzi mtanishangaa sana mkisikia niko Monduli eti nipo kwenye majukwaa nasafisha jina Bwana Lowasa asikose ubunge.

Kweli Lowasa ni jasiri sana kusema maneno hayo. Hayo ningeambiwa na Kasori tu ningesita kumuamini. Lakini kwamba hata wewe Rashidi ulitumiwa kusema maneno hayo! Huyu Lowasa ni jasiri sana!!. Lakini kwa nini hajatuambia ukweli kuhusu mali hizo ambazo ni nyingi kuliko mimi ambaye nimekuwa Rais wenu kwa kipindi kirefu? Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mhe. Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowasa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu. Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda,umesikia eh?"

Mkutano ukaisha hapo Msasani. Hadi uchaguzi 1995, unafanyika na kumalizika Baba wa Taifa hakwenda Monduli. Alichukia sana tabia za Lowasa na alimfahamu kama mtu muongo na mwenye kiburi. Hadi Baba wa Taifa anafariki,sikuwahi na hata niandikapo makala hii sijasikia wala kusoma popote ambapo Lowasa anakanusha alivyolombikiza mali akiwa mtumishi wa CCM na serikali kwa muda mfupi kiasi cha kumzidi Rais wa Kwanza !!!


Samwel. H. Kasori
Katibu mstaafu wa J.K.Nyerere
0754 372141
 
usicheze na shekeli hata Yuda alimuuza Yesu, na usicheze kukaribishwa british legion, ndio maana unasikia jamaa alikwenda pale bila support ya member , akaona afadhali aishie uswazi!
sasa hivi naona kampeni za waandishi kununuliwa ahead of 2015 zinaongezeka
August, nakuomba uamini sio kweli watetezi wote wa Lowassa humu wamelipwa!. Just amini hivyo!.
Mimi Pasco (wa jf) ni mmoja wa watetezi wa Lowassa ateuliwe kuwa mgombea wa CCM nikiwa sina chama wala sijapewa senti tano ya mtu awaye yote!.
 
mijadala kama hii huwa inaniogopesha...imekaa kimafia mafia
Ipo siku, mtandao wa wananchi uta shinda....
 
kama mpaka Pasco ame convert....basi una haki ya kukata tamaa......
honestly huwa najiuliza hii nchi ina walakini gani?
mbona we cant finds men with balls kwenye siasa zetu?
decent men???????
The Boss, kuna msemo wa Kiswahili usemao "Usiogope kugombana na nduguyu/rafikiyo katika jambo ambalo mtakuja kupatana!".

Kwa utetezi wangu kwa Lowassa bora tugombane tuu kwa sasa akishateuliwa tutapatana tuu!.

Kwa wale mnaonifahamu na kunikubali kuhusu misimamo yangu katika baadhi ya issues, natoa wito tuungane mikono tumsafishe Lowassa awe mgombea wa CCM, tumeshasema mara mia humu kama dhambi kuu ya Lowassa ni zigo la Richmond, kwenye sakata hilo Lowassa alikubali tuu kulibeba ili CCM iokoke kama Bwana Wetu Yesu Kristo alivyobeba dhambi zetu na kwa kuteswa kwake sisi tumeponywa vivyo hivyo kwa kuteswa kwa Lowassa CCM imeokoka maana laiti mngelimjua mwenye zigo lake halisi!, I can't imagine kama Lowassa angehojiwa na kuusema ukweli ingekuwaje!.

Lowassa ni mtu shupavu na jasiri sana, just imagine mpaka leo bado anaendelea kulibeba hili zigo kwa uvumilivu mkubwa na ustahimilivu wa hali ya juu!. Nani mwingine kwenye CCM angeweza kuvumilia yote hayo bila kumtaja mwenye zigo lake!.

Zawadi pekee anayostahili sasa ni kutunukiwa ugombea kwa tiketi ya CCM tena nawaombeni sana sana sana tuungane katika hili!.
 
Lol...sasa naweza kusema kwa uhakika kabisa hata mzee wa vijisenti nae 'tulimwonea'...maana ni kweli vilikuwa 'vijisenti'! Pasco, honestly, hivi kumtetea kote huku EL ni kwa maslahi ya nchi yetu ya Tanzania? Kweli!?
SMU, tangu thread ya Vijisenti nimesimama nae, wanamuonea tuu kwani kuiukweli zile fedha alizokutwa nazo ni kweli kabisa ni 'vijisenti' tuu!.

Uwingi au uchache ni relative na terns of comparison. Kwa mfano mishahara ya juu nchini Tanzania ni Milioni mbili!. Hiyo ndio mishahara ya wakurugenzi, makatibu wakuu, wakuu wa wilaya, mikoa, majaji na wabunge. Kwenye benki ya ADB, hizo milioni 2 ndio kima cha chini, watu wanalipwa mpaka zaidi ya milioni 30 pm!.

Pesa alizokutwa nazo Mzee wa Vijisenti ni peanut ukilinganisha na migawo wenzake waliopata!. Kosa lake ni kutuhifadhi tule tujisenti twake ile benki ya kule Virgin Island hatimaye tukaonekana!. Wenzake wamehifadhi fedha kweli kule Credit Sussie hivyo hazijaonekana!.

Hivyo Chenge was right kuviita vijisenti maana kwenye ule mgao yeye ndie amemegewa fungu dogo!. Jee laiti mngelijua waliovuta fungu nene ni kina nani?. Mngeshindwa hata kushangaa mgebaki midomo wazi!. Mnajua ni kwa nini licha ya ushahidi huo hajashitakiwa?!. Amini nawaambieni hahashitakiwa kwa sababu ni heri aachwe ajikalie kimya asije kushitakiwa na kuwataja washirika wake ambao kwa kwa macho ya kawaida ni 'Watakatifu'!.

SMU nakuhakikishia asilimia 100% kwa 100% utetezi wangu kwa EL ni kwa maslahi ya taifa!. Sina maslahi binafsi yoyote na sijapokea hata senti tano ya yeyote!
 
Pasco,
Anaekamatwa amebeba, si ndie Mwizi?

Jujuman ni kweli anaekutwa na ngozi ndie aliyeiba ng'ombe!. Lakini wakitokea watu waliomshuhudia mwizi halisi wa ng'ombe na kumshuhudia akimchinja na kumchuna ngozi aliyoibwaga hapo chini na yeye kusepa na nyama huku nyuma masikini wa watu kajionea ngozi iliyotupwa na kujiokotea ili ikamfae ndie sasa ahukumiwe kwa wizi wa ng'onbe!. Jee hii ni haki?!. Jee hii ni halali?.
Kwenye sakata la Richmond, Lowassa amekutwa tuu na ngozi siye aliyeiba ng'ombe!.
 
August, nakuomba uamini sio kweli watetezi wote wa Lowassa humu wamelipwa!. Just amini hivyo!.
Mimi Pasco (wa jf) ni mmoja wa watetezi wa Lowassa ateuliwe kuwa mgombea wa CCM nikiwa sina chama wala sijapewa senti tano ya mtu awaye yote!.
Mkuu Pasco hebu jifikirishe kidogo.tunaambiwa juzi Lowasa amemvua nguo mkuu wa Kaya kwa kuonesha lile zigo si lake lakini kwa alivyonukuliwa akizungumza alisema alimpigia mkuu akiwa nje ya nchi akitaka kuifuta Richmond! Hivi Pasco kweli lowasa anajua kampuni ya mkuu wa kaya alafu ampigie kumwambia naifuta!toka awali hii Richmond ilibebwa na Lowasa bila kujua zigo la nani? Tunaaminishwa Lowasa alishirikishwa mwishoni kuokoa jahazi,mwisho gani? Pale akina mwakyembe walipoanza uchunguzi? Au kuwajibika kwakwe haraka ndio kumuokoa Mkuu wa Kaya? Tunaambiwa mkuu alisoma ripoti ya Richmond kabla haijaenda bungeni alafu akaruhusu isomwe! Dili lake alafu ajiumbue vile! Hiyo kampuni toka inaingia Tz inaitwa Richmond na hilo jina ENL analitumia hata sasa kwenye biashara zake ni coincidence tu? Wakuu nisaidieni kunitoa kwenye hili lindi la maswali lisilo na majibu! Kweli Richmond isiwe zigo la ENL liwe la Mkuu wa Kaya? Inafikirisha sana!
 
Keil,

Mkuu wangu sijui nianzie wapi. Maana umesema sana na upo sahihi kabisa. Bado namtetea Lowassa, naamini vyama vya upinzani havijakomaa na sio instutionalized kama CCM.
CUF = Maalim
CDM = Mtei, Ndesa, Mbowe, Makani
NCCR = Mbatia

Kwahiyo mgombea urais wa CCM ndio atashinda na CCM ndo chama huru ANGALAU.

Tukubaliane kutokubaliana mpaka nitakapomshawishi Mkandara akija bongo naye anisaidie namna ya kuelezea kuhusu Lowassa.

Ila bado naamini ELairline ndo airline pekee inayostahili kuwa NATIONAL carrier wa kuanzia 2015.
 
Mkuu Pasco hebu jifikirishe kidogo.tunaambiwa juzi Lowasa amemvua nguo mkuu wa Kaya kwa kuonesha lile zigo si lake lakini kwa alivyonukuliwa akizungumza alisema alimpigia mkuu akiwa nje ya nchi akitaka kuifuta Richmond! Hivi Pasco kweli lowasa anajua kampuni ya mkuu wa kaya alafu ampigie kumwambia naifuta!toka awali hii Richmond ilibebwa na Lowasa bila kujua zigo la nani? Tunaaminishwa Lowasa alishirikishwa mwishoni kuokoa jahazi,mwisho gani? Pale akina mwakyembe walipoanza uchunguzi? Au kuwajibika kwakwe haraka ndio kumuokoa Mkuu wa Kaya? Tunaambiwa mkuu alisoma ripoti ya Richmond kabla haijaenda bungeni alafu akaruhusu isomwe! Dili lake alafu ajiumbue vile! Hiyo kampuni toka inaingia Tz inaitwa Richmond na hilo jina ENL analitumia hata sasa kwenye biashara zake ni coincidence tu? Wakuu nisaidieni kunitoa kwenye hili lindi la maswali lisilo na majibu! Kweli Richmond isiwe zigo la ENL liwe la Mkuu wa Kaya? Inafikirisha sana!
MTAZAMO, naomba tusiendelee kuandikia mate ilhali wino upo!. Vuta subira kidogo tuu and time will tell!.
 
Mkuu The Romantic,

Mimi nilivyomwelewa mtoa mada ni kwamba Dr. Omar A. Juma alikuwa ni threat kwa mtandao kwa sababu kubwa mbili, alikuwa ni clean [hana uchafu wa kumchafua nao] na kwa kuwa alikuwa ni Makamu wa Rais na anatokea upande wa pili wa Muungano then it was easy kujenga hoja ya kuwa mteule wa kugombea nafasi ya urais. Moja, kwa kutumia u-Zanzibari [kwamba baada ya Mkapa wa bara then angefuata wa Visiwani]. Pia hakuwa na tuhuma zozote chafu. So, the best way ya ku-deal naye ilikuwa ni kumwondoa njiani [if at all kifo chake kilitokana na hilo].

Hapo inabidi ukumbuke kwamba wana Mtandao walikuwa wana-deal na yeyote yule aliyekuwa anaonekana kwamba anaweza kuwa kizuwizi kwao. Ndio maana wale ambao walikuwa na "tuhuma" za ukweli au za majungu, tayari walishaandaliwa njia ya kuwamaliza kiaina.

JK, Lowassa, RA, Sitta, Membe na wengineo wengi tu walikuwa kundi moja la mtandao. Ingawa baada ya uchaguzi ndipo yalipozaliwa makundi mawili, mtandao original na mtandao matumaini [wale ambao hawakuambua kitu cha maana pamoja na ku-toil sana kwenye kampeni za mtandao]. Hao akina Apson walikuwa recruited along the way. Mkapa alikuja kuingizwa kwenye kundi la mtandao dakika za mwisho. Mkapa kwa kujua kwamba hilo lilikuwa ni kundi la opportunists, hakuwa na uhakika wa usalama wake wala mali zake na ndipo mtandao walipolambishwa EPA ambayo inawahenyesha mpaka leo na ndio maana akina Kikwete na Pinda wanaendelea kumtetea Mkapa mpaka leo hii kwamba mwacheni apumzike.

Zakhia Meghji alikuwa ni mwana mtandao. So, waliomgomea hawawezi kuwa wana mtandao, bali watakuwa ni wazee wa CCM kwenye Kamati Kuu. Ubaya wa kupendekeza Mgombea Mwenza ni kwamba mgombea Urais hupendekeza jina na ndipo wazee walafi wa CCM hujadili hilo pendekezo na kukubaliana na ndipo huenda kutangazwa kwenye Mkutano Mkuu wa Chama. Kwa hiyo kama ni kugoma, watakuwa waligoma akina Mkapa na wengineo walio kwenye CC. Wakati huo mgombea mteule huwa hana final say na inawezekana CC inaweza kuibuka na jina tofauti kabisa na lile lililopendekezwa na mgombea mteule.

Kwenye swala la Waziri Mkuu, CC wala Rais aliyetangulia huwa hawana nafasi kwa kuwa Rais mteule anakuwa na uhuru wake wa kupanga safu ya watendaji bila kukishirikisha chama chake. Ndio maana JK alikuwa na jeuri ya kuwagomea. Ni ngumu kugoma kwenye uteuzi wa mgombea mwenza kwa kuwa kila kitu kinafanywa na chama kwa kuwatumia wale "ma-think tank" wao walio kwenye CC.

nimesoma maandishi yako naona hayana chembe ya shaka na ndicho ninachokijua mimi,kama umesoma sawasawa nilichoandika nilikua namchallenge mtoa tetesi ama mleta thread,kwamba katuchanganya aliposema kwamba DR. alikua tishio kwa mtandao wa kina lowassa na rostam(kikwete,sitta etc)kutokana na kuwemo kwenye mtandao aliouita "hatari" wa mkapa na apson ambapo kama umemuelewa ilibidi aondolewe duniani,hapa ni wazi kama mtandao wa lowassa ndio ulihusika kumuondoa mtu wa mtandao "hatari" wa mkapa na apson kulitokea kutoelewana kwa mitandao hii miwili,sasa ilikuwaje tena mtandao wa kina lowassa uungano na mtandao wa mkapa kumshinikiza mtu wa mtandao wao amchukukue mtu wa mtandao wa mkapa?nakataa kusema mkapa alikua mtandao mmoja na kina lowassa wakati wa kumtafuta mgombea mwenza wa kikwete,ingekuwa hivyo angekua anaujua mkakati mzima wa kumuweka lowassa kuwa waziri mkuu na wala asingemtoa jasho kikwete na kulia kwamba wamemchagulia mgombea mwenza,wamemchagulia mwanasheria mkuu na sasa wanataka kumchagulia waziri mkuu ambae alikua huyu pinda na hiyo hawezi kukubali tena!Lengo langu ni kueleza aliyembeba lowassa mbele ya wazee wa nchi ambao walikua hawamtaki ni kikwete japo pengine baadae alikuja kujuta au bado anajuta...

unajua jk asingeleta ubishi kwa kina mkapa pale mwanzo haya matatizo yatokanayo na lowassa yasingekuwepo,na pia kumtosa mangula kwenye sekretariet licha ya tofauti zao kwenye mchakato(mangula hakumtaka jk wala genge lao) na kumuandama kuhakikisha haingii nec kupitia uenyekiti wa mkoa ccm iringa lilikua kosa pia
 
Nakumbushia tu. Huyu si ndiye aliyetaka kutuletea dili ya mvua ya Thailand. Bahati nzuri fisadi mwezake huko Thailand akapinduliwa kabla ya kukamilisha dili lao.

.......alikuwa ANATHUBUTU!.........
 
Usicheze na kitu inaitwa love of shekeli.....The root of all evils!

"Extreme Ukosefu" wa Shekel ndio root ya all evil. Tatizo la ulafi wa EL lazima tukumbuke alipoanzia ni ile decade (1979/80-1989) alikuwa na njaa ya ajabu. Si ajabu aliwahi kukosa pesa ya matibabu ya watoto! na huo ndio kuwa mwanzo wa kuapa kuhakikisha akipata mwanya basi aendelee kuchoto. Alipofikia hivi sasa ni kama depression/addiction au kama si hivyo ni pathological related issues ambazo zinahitaji matibabu. Ni very rare kuona mtu asiyeridhika kwa kiwango chake.

Ndugu yangu Pasco unanitisha kwa jinsi ulivyo "up the ante" kumtetea "ELAirline"...Mkandara tafadhali mkumbushe rafiki yako kwenye mazungumzo yenu awe makini asitake kukutana naye huyo "mgombea wake" kwani (kwa mujibu wa mabandiko yaliyopita) mwenzie inasemekana kafudhu techniques za ku-unlock wanaume wenzie. Sio vizuri kuanzisha ugomvi kati yako na "PS" wa EL kisha tukaishia kukufungulia thread humu kwani JF ni kiboko!
 
Back
Top Bottom